Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w76 9/15 kur. 415-417
  • Kichwa Cha Nyumba Yako ni Nani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kichwa Cha Nyumba Yako ni Nani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • WATOTO WAKALI SANA, KWA SABABU GANI?
  • JAMBO GANI LIFANYWE?
  • JAMBO LA MAANA
  • Ubora wa Kutia Adabu katika Upendo
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Wazazi—Wazoezeni Watoto Wenu Kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Kulea Watoto tangu Uchanga
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
w76 9/15 kur. 415-417

Kichwa Cha Nyumba Yako ni Nani?

LEO hilo si ulizo la upuzi. Toronto Star lilisema hivi juu ya maneno ya mtaalamu mmoja alipokuwa akisema juu ya daraka la watoto na wazazi katika chuo kimoja: “Kuna ongezeko la kushangaza sana katika hesabu ya watoto walio na vichwa vikubwa wakitaka mamlaka katika Amerika ya Kaskazini ambao wanatawala na kuongoza maisha za wazazi wao.”

Sasa, namna gani nyumba yako? Angalia kwamba mtaalamu huyo hakusema kwamba wazazi wanataka iwe hivyo, wala kwamba wao wanakubali watoto wawaongoze. Lakini ikiwa watoto “wanatawala na kuongoza maisha za wazazi wao,” ni nani hasa kichwa cha nyumba?

Kwa mfano, huenda watoto wakapata vitu wanavyotaka kwa kulia kwa sauti kubwa na kukasirika-kasirika. Pengine hawatafanya hivyo kila wakati, lakini watafanya hivyo mara nyingi hata wasiache. Katika jamaa nyingine watoto wana mamlaka ya kukubali au kukataa mambo wanayofanya wazazi wao, hata kuamuru wazazi ni wakati gani wao (wazazi) wamepaswa kuja na kwenda.

Kama ndivyo mambo yalivyo katika nyumba yako au sivyo, kutokea sana kwa mambo hayo kwalazimisha kila jamaa kuyafikiria. Kwa sababu gani kwanza ugumu huo unatokea? Wawezaje kuondolewa au kuzuiwa katika nyumba yako, na kwa matokeo gani?

WATOTO WAKALI SANA, KWA SABABU GANI?

Ni nini kinachoweza kufanya mtoto ajaribu kuwa “kichwa” cha nyumba? Sababu kubwa ni kwamba yeye si mkamilifu, kama vile watu wazima wasivyo wakamilifu. Biblia inataja hilo, ikisema: “Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto.” (Mit. 22:15) Na mambo mengine kama haya yanaongeza maelekeo hayo ya kutokamilika:

Mtoto anachukua hatua ya kwanza ya kuwa “kichwa cha jamaa” wakati wazazi wanapojaribu kumhonga ndiyo awe na adabu njema, kama kumwambia hivi, ‘Ukiwa na adabu njema dukani, nitakununulia peremende.’ Sivyo, kwa kufanya hivyo wazazi wasingekuwa wakimpa zawadi tu, kitu cha kumwonyesha upendo na ukarimu. Kwa kumhonga hivyo wanamtia mtoto katika hali ya kuwaongoza wao kufanya vile anavyotaka wafanye. Je! wewe wadhani mtoto haoni anapohongwa?

Kwa njia hiyo watoto wengi wanajifunza njia ya kuongoza wazazi wao, kwa kuwatisha kwamba watafanya jambo fulani baya wasipopewa wanachotaka. Kivulana mmoja alisema hivi, “Mimi hupata ninachotaka kwa kuendelea kumwonyesha mama nitaharibika asiponipa ninachotaka.” Naam, kivulana huyo ndiye huongoza mama yake. ‘Lakini,’ huenda mtu akawaza, ‘je! mtoto hajifunzi kuwa na adabu njema kwa njia hiyo?’ Tofauti na hivyo, kivulana huyo aliendelea kusema: “Bila shaka, yanipasa kuharibika mara nyingi kutosha niweze kumsadikisha hanipi bure vitu ninavyotaka.” Kwa hiyo, ni nani hasa anayeongoza mwingine?

Sababu nyingine ni mazingira ya mtoto. Huenda akawa anaona watoto wengine wakipiga ubwana juu ya wazazi wao, na hivyo yeye ajaribu kufanya hivyo pia. Ikiwa wewe u mzazi, uonapo dalili za kwanza mtoto wako akijaribu kukuongoza wewe na uwe macho umchukulie hatua kwa imara lakini kwa upendo, hivyo umsaidie aone kwamba yeye siye kichwa.

Katika Ulster, Ireland, watoto wengi huingia katika magenge ya watoto wenye kutupia watu mawe na kutumia mamlaka nyingi sana shuleni na katika ujirani. Kwa vyepesi jambo hilo huja kufanywa nyumbani; wanataka kutawala huko pia. Ripoti ya karibuni juu ya hali katika Ireland ilisema hivi:

“Wazazi wengine wanaelekea kuogopa watoto wao. Mama mmoja mwenye kivulana wa miaka 11 alisema, ‘Yeye ni mwenye nguvu kuliko mwanamume mzima. Ndiyo sababu nilimpeleka kwa daktari mkuu. Aliniogofya.’”

Tena, huenda mtoto akajaribu kuwa “bwana-mkubwa” nyumbani kwa sababu anashindwa kujua ni nani anayeongoza jamaa. Pengine wazazi wake hubishana na kupigiana kelele wanapotaka mambo yafanywe. Baba hutoa sauti ya nguvu kwamba yeye ndiye bwana-mkubwa, kisha mama anapiga kelele ya kutokutii na ya ukali. Jambo hilo lamwacha mtoto katika hali gani? Huenda akatumia hali hiyo ya kutopatana kugonganisha wazazi, na hivyo asimamie mambo kwa kadiri ya kumfanya kichwa.

JAMBO GANI LIFANYWE?

Ingawa sababu na matatizo yanayofanya watoto wajitwalie ukichwa ni mengi. bila shaka matokeo ni mabaya. Mtoto hawi mwenye furaha​—⁠-hupatwa na matatizo na ukuzi wake huharibika.

Ripoti ya Israeli ilionyesha hivi: “unaotumiwa na watawala hao wakali ndani ya jamaa unawaacha wakiwa na wasiwasi wa kupatwa na mabaya zaidi huko nje. . . . Wanaogopa kwamba hawatakuwa na mtu wa kuendea wakiwa na shida.”

Jibu ni nini basi? Si fundisho jipya wala uvumbuzi wa karibuni wa daktari wa kuangalia akili za watoto. Hasa. ni matumizi ya mashauri yaliyoandikwa miaka mingi iliyopita katika Biblia.

Sehemu ya mashauri ya Muumba yaonyesha tuone mtoto katika jamaa kama sehemu ya mpango ambao kichwa chake kilichowekwa ni baba. Yeye si mtawala mkali, bali ni kichwa chenye upendo na huruma kwa mke na watoto pia. (Kol. 3:18-21) Kwa wazi, ili mtoto auone na kuuheshimu ukichwa, lazima baba atimize madaraka yake. Pia, yampasa mama aonyeshe kwa kawaida kwamba anaheshimu na kushirikiana na mpango huo.

Ubora wa wazazi wote wawili kujitahidi kufanya hivyo unaweza kuonekana kutokana na yanayotukia wasipofanya hivyo. Kitabu Between Parent & Child kinataja nyumba ambako baba huepuka daraka lake naye mama anakuwa ndiye mwamuzi wa mwisho wa mambo yote ya maana.

“Mume katika nyumba kama hiyo huelekea kuepuka kuwa kichwa cha nyumba. Humtaja mke wake waziwazi kuwa ‘bibi-mkubwa.’ Watoto wake wanapomwomba awafanyie uamuzi, mara nyingi yeye husema ‘Kamwulizeni mama.’ Katika nyumba hizo, watoto hukua bila kuheshimu sana wala kupendezwa sana na wanaume. Vivulana na visichana pia humchukua baba vile wanavyoambiwa yuko na mama yao: mwanamume asiye na akili, mzembe aliyeumbwa vizuri kwa asili.”

Tofauti na hivyo, Neno la Mungu hushauri hivi: “Akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.” (Efe. 6:4) Naam, baba ndiye kichwa cha jamaa na yampasa asimamie na kushiriki katika malezi ya watoto wake. Je! ndivyo ilivyo katika jamaa yako?

Biblia yaonyesha pia vile msaada wa mama katika jamaa ulivyo wa maana. Akiheshimu ukichwa wa mumewe, anaweza kufanya kazi naye kwa umoja waongoze watoto. Mithali 14:1 yasema: “Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.”​—⁠Linganisha Mithali 1:8; Mambo ya Walawi 19:3.

Hivyo yamaanisha kwamba mtoto asipewe nafasi ya kutumia akili yake mwenyewe au kutoa maoni? Sivyo. Lakini wazazi wanaweza kumpa daraka fulani na uhuru na bado ajulishwe siye kichwa. Badala ya mama kuuliza, ‘Wataka kuamsha kinywa na nini?’ aulize, ‘Leo tutakunywa vya moto. Wataka uji, chai au kahawa?’ Kwa hiyo mtoto anapewa uhuru kadiri fulani na uchaguzi lakini anajulishwa pia kwamba siye kichwa cha jamaa.

JAMBO LA MAANA

Ili watoto wajue kwamba sio walio kichwa cha nyumba wanapaswa kutiwa adabu. Wazazi wengine hukataa jambo hilo. Kwa sababu wazazi hukataa nao watoto hukataa. Lakini, angalia maelezo ya daktari wa uchunguzi wa akili ya watoto Wayne Weisner:

‘Watoto wanahitaji kutiwa adabu ili wastaarabike. Hata wanataka watiwe adabu. Wanakubali kutiwa adabu kwa vyepesi wanapotiwa na wazazi walio imara, lakini wenye kufanya hivyo kwa njia nzuri sikuzote. Lakini wazazi wote wawili wakubaliane kabisa juu ya adhabu itakayotolewa, ama sivyo kutopatana kwao ndiko atakakofikiria mtoto, na hiyo itampa maelekeo ya kutokutii.’

Bila shaka, maoni hayo yanarudia tu yale ambayo Mungu aliandikisha zamani kuonyesha mwendo bora wa kufuatwa na wazazi: “Kusahihishwa na kutiwa adabu ni kwema kwa watoto. Mtoto akifuata njia yake mwenyewe, atamwaibisha mama yake.”​—⁠Mit. 29:15, Today’s English Version.

Ni wazi kwamba katika nyumba nyingi watoto ndio vichwa, wakiamuru na kuongoza wazazi wao. Lakini nyumba hizo hazina furaha. Wazazi hawana furaha. Watoto hawana furaha, wala hawatakuwa nayo. Neno la Mungu laonyesha wazi kwamba matokeo bora na furaha hupatikana wakati baba mwenye upendo anapotumia ukichwa kwa kupatana na mke mwenye heshima, mwenye kushirikiana naye. Mpango huo unaleta hali ya usalama na uongozi imara ambao kwao watoto hukua wakawe watu wazima wenye kiasi, waliokomaa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki