Kujifunza Kuishi Kulingana na Biblia
◆ Kijana Myahudi mwanamume aliyekuwa akiishi katika mji ulio kati ya Ulaya na Asia alikuwa akitiwa moyo na waalimu wa dini wa eneo hilo apate mazoezi ya ualimu wa dini. Wao walimtia moyo ayapate ijapokuwa walijua alikuwa mfisadi. Alipokuwa akifikiria maombi yao, Mashahidi wa Yehova walimfikia. Ingawa aliyajua sana Maandiko ya Kiebrania, alikubali kujifunza nao Biblia. Karibuni akajua kwamba kujua tu yanayofundishwa na Biblia hakutoshi bali kwamba kuyazoea ni kwa maana pia. Aliposoma makala katika Mnara wa Mlinzi juu ya maoni ya Mkristo juu ya uchumba, alisadiki kwamba njia yake ya maisha haikumpendeza Mungu. Aliwaendea waalimu wake wa dini akawaonyesha walikuwa wameshindwa kumfundisha ubora wa kuishi kupatana na Maandiko Matakatifu. Waalimu hao hawakuweza kumpa majibu ya kumtosheleza.
Aliamua kwamba Mashahidi wa Yehova walikuwa wakiishi kupatana na dini ya kweli, zaidi ya kuifundisha. Kwa hiyo aliendelea kujifunza Biblia akithamini zaidi akaanza kubadili maisha yake. Hata alitembelea wasichana wote aliokuwa akifanya uasherati nao, akaketi wazungumze na kuwasomea makala ya uchumba. Sasa wawili kati ya wasichana hao wanaeleza wengine kweli ya Biblia kwa bidii, na yeye mwenyewe amekuwa mwanafunzi aliyebatizwa wa Yesu Kristo.