Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 1/1 kur. 21-24
  • Kuendeleza Uchumba Kuwa Wenye Kuheshimika

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuendeleza Uchumba Kuwa Wenye Kuheshimika
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UCHUMBA UMEPASWA UTIMIZE NINI?
  • MWENENDO WA KUHESHIMIKA KATIKA UCHUMBA
  • Matembezi ya Wavulana Pamoja na Wasichana na Uchumba
    Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Jinsi ya Kuwa na Uchumba Wenye Mafanikio
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
  • Kutayarisha Kwa Ajili Ya Ndoa Yenye Mafanikio
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Maoni ya Mkristo Juu ya Uchumba
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 1/1 kur. 21-24

Kuendeleza Uchumba Kuwa Wenye Kuheshimika

BIBLIA inasema hivi: “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi.” (Ebr. 13:4) Je! si jambo la akili kwamba kinachotangulia ndoa katika nchi nyingi​—uchumba​—nacho kimepaswa kiendelezwe kuwa chenye kuheshimika ikiwa kitampendeza Mungu?

Katika sehemu nyingine kijana wa kiume anaruhusiwa kuwa pamoja na msichana mchanga wakati tu anapokuwapo angaa mzazi mmoja au mtu mwingine mzee. Lakini, katika nchi nyingi za Ulaya na Amerika, mara nyingi huenda vijana hao wakawa pamoja pasipo mwangalizi. Kwa hiyo, ulizo ndilo hili ambapo uhuru huo ulio mwingi zaidi unaporuhusiwa, je! uchumba wawezaje kuendelezwa kuwa wenye kuheshimika? Kijana wa kiume au wa kike aweza kufanya nini ahakikishe kwamba kwa upande wake uchumba utaongoza kwenye ndoa yenye furaha kweli kweli na yenye kufanikiwa?

Sikuzote uhuru unafuatana na madaraka. Kwa hiyo, ikiwa hili ndilo ulizo unalokutana nalo sasa, ingekuwa vema uikumbuke kanuni njema iliyoandikwa katika Wagalatia 5:13. Bila shaka, hapa mtume Paulo alikuwa akizungumza juu ya uhuru ambao Ukristo uliwaletea wale walioukubali. Lakini kanuni yatumika kwa namna yo yote ya uhuru, zaidi ikiwa twataka kuutumia ulete matokeo mema na kibali cha Mungu. Mtume anaandika hivi: “Maana ninyi, ndugu, mliitwa mpate uhuru: lakini uhuru wenu usiwe sababu ya kuufuata mwili, bali tumikianeni kwa upendo.” Upendo wa kweli, kwa Mungu na kwa jirani yetu, kutia na mtu ambaye huenda tunamchumbia​—utatusaidia kuepuka kutumia uhuru wo wote tulio nao kwa njia ya kichoyo, yenye kudhuru.

UCHUMBA UMEPASWA UTIMIZE NINI?

Ili uwe wenye kuheshimika, wapaswa uchumba uendelezwe mradi wake ukiwa ndoa. Kwa hiyo, haupaswi uanze mbele ya mtu kuwa tayari kutwaa madaraka ya ndoa. Bila shaka, huwezi kujua pale pale mwanzoni kama wataka kuoa au kuolewa na mtu ama sivyo. Ni busara kutofanya haraka mno katika kukaza fikira zako juu ya mtu mmoja ye yote. Lakini hii siyo sababu ya kuendeleza “uchumba” wenye maongezi ya kucheza tu.

Hata ikiwa “unapendezwa” na fulani, ungekuwa mwenye hekima kujaribu kwa kitambo kushirikiana na huyo kama sehemu tu ya kikundi, katika mambo yafanywayo na kikundi cha watu. Kwa sababu gani? Kwa maana, katika hali hizo, mara nyingi waweza kupata maoni bora ya namna mtu alivyo hasa. Hii ni kwa sababu sote twaelekea kutenda tulivyo hasa wakati tunapokuwa hatujisikii kwamba mtu fulani anatuangalia sana. Lakini wakati watu wawili wanapojitenga na kikundi hicho, maelekeo ya kawaida tangu wakati huo ni kuwa namna ambavyo yule mwingine anakutaka uwe, hata kuonyesha unayapenda anayoyapenda na kuchukia anayoyachukia. Na nyakati nyingine huenda hili likasingizia utu wa mtu hasa. Wakati watu wanapoachwa wakiwa wawili, wanaweza vile vile kufikiriana kwa kutumainiana mema peke yake. Ikiwa watu wawili wanaoana kwa kuvutwa na maono hayo ya moyoni, mara nyingi wanaelekea kuzinduka vibaya sana. Ni afadhali zaidi kutofanya jambo mpaka ulifikiri kwanza.

Kwa jumla, mwanamume ndiyo anayeanzisha uchumba, kwa kuonyesha kupendezwa na mwanamke. Ikiwa yeye ni mwaminifu na anamaanisha hivyo, mwanamke anayo haki ya kuamini kwamba yeye (mwanamume) anafikiria ndoa. Halafu? Basi, mwanamke ndipo anapokuwa na daraka la kujiuliza kama anaamini anaweza kufikiria kuolewa naye. Ikiwa mwanamke ana hakika kwamba asingemfikiria yeye kama atakayekuwa mumewe, basi ungekuwa ukatili kwake kumruhusu mwanamume akuze kupendezwa kwingi naye. Wasichana wengine wamekubali mtu fulani awachumbie ati wazidishe hali yao ya kupendwa na watu wengi au ya kufaa, wakitumaini kwamba vijana wengine wa kiume watawaona. Vijana wengine wa kiume wamefanya lilo hilo, wakidhani wanaweza kufanya ujanja, wakiwa wanafurahia mambo kisha watoroke mbele ya mambo kuwa mabaya mno. Lakini matumizi hayo ya kichoyo ya uhuru wa mtu yanaweza kudhuru sana, kuleta madhara ambayo huenda yakamalizika ikiisha kupita miezi mingi au hata miaka.​—Linganisha Mithali 26:18, 19.

Ni kwa kutumiwa kwa njia isiyo ya kichoyo tu uhuru wa kuchumbia uwezavyo kuleta faida. Unaweza kutoa nafasi ya kufahamiana zaidi na mtu ambaye unafikiria kuishi naye maisha yako yote. Ikitegemea namna ambavyo kila mmoja alivyo mwaminifu kwa mwenzake, mwaweza kuja kujua mapendezi ya kila mmoja na mambo asiyoyapenda, kanuni, tabia na matumaini, ndiyo, na hamaki na nia na anavyotenda akipatwa na magumu. Kwa haki wataka ujue mambo kama vile: Je! yeye ni mwenye fadhili mwenye ukarimu na mwenye kufikiria watu wengine? Namna gani juu ya heshima kwa wazazi na wazee? Je! kuna ushuhuda wa kutosha juu ya adabu na unyenyekevu, au mtu huyo ni mwenye kujisifu, mwenye kiburi? Je! naona kujiweza na usawa au, mahali pake, naona udhaifu na utoto, pengine kununa au hata hasira za ghafula? Kwa kuwa sehemu kubwa ya maisha ni kazi, namna gani juu ya dalili za uvivu, uzembe au hali ya kutumia fedha ovyo ovyo? Namna gani juu ya mipango ya wakati ujao? Je! jamaa yatamaniwa au anapendezwa na shughuli fulani ya pekee? Katika makala yenye kichwa “Dalili za Hatari katika Uchumba” mwandikaji anasema hivi: “Uchunguzi wetu wa watu waliochumbiana na waliooana ambao ni wenye furaha na huzuni uligundua wale waliooana lakini wenye huzuni hawapatani sana katika miradi ya maisha na mafaa.”​—Medical Aspects of Human Sexuality, Novemba 1970, ukurasa wa 43.

Zaidi ya yote, imekupasa utake kujua yule mwingine anathamini kwa kadiri gani makusudi ya Mungu katika mapendezi yake na mipango Ndiyo, umalizapo uchunguzi wote, ninyi mwafaana kiasi gani? Ikiwa mambo fulani yanahitilafiana kwa uzito, usijidanganye ukifikiri kwamba ndoa itayaondoa tu yenyewe. Huenda ikaleta ugumu zaidi wa kuhitilafiana.

MWENENDO WA KUHESHIMIKA KATIKA UCHUMBA

Katika nchi ambako watu wanaruhusiwa wazazi kushirikiana bila ya mtu wa kuwaangalia, watu wanaochumbiana mara nyingi wanajitia katika vionyesho vya upendano kama vile kushikana mikono, kupigana busu, hata kukumbatiana. Je! hili lafaaje? Je! Biblia inatupa mashauri yo yote juu ya mambo hayo?

Biblia haitoi kanuni zo zote za wazi juu ya mambo haya. Bila shaka, wazazi wanayo haki ya kuwaagiza wana wao na mabinti ni kanuni gani wanazotaka wajiongoze kwazo. Wajapokuwa wazee katika kundi hawawezi kuweka kanuni hizo, wanaweza kuelekeza fikira za vijana kwenye kanuni zifaazo za kuongozea zinazopatikana katika Neno la Mungu, na ye yote atakaye kufuata mwendo wa hekima kwa uaminifu katika maisha atayatii mashauri hayo kwa kupenda na kwa furaha.​—Mit. 1:7-9; 2:6-9.

Bila shaka, Biblia inakataza waziwazi mambo kama vile uasherati. Lakini vile vile inaonya juu ya mwenendo mwingine mchafu ambao huenda usiwe mzito kama uasherati. Watu wo wote wawili wanaotii maonyo haya watajiepusha na huzuni nyingi nao hawatajihatirisha na kusumbuka wakumbukapo mwenendo fulani mpotovu wa wakati uliopita.​—Efe. 5:3-5.

Kushikana mikono kwaweza kuwa wonyesho safi wa upendano kati ya watu wanaotazamia kuoana. Kweli, kunachochea, lakini hili ni jambo la kawaida nalo si baya kwa lazima. Kwani, kumwona tu yule ambaye mtu anayetazamia kuoa au kuolewa naye huenda vile vile kukachochea, ‘kuufanya moyo upige kwa kasi zaidi.’ (Wim. 4:9, NW) Hata hivyo, yatupasa tukumbuke kwamba mgusano wa mwili unaongezea “mvuto” wa nyege kwa kuwa ndiyo hali ya kibinadamu. Vile vile ni jambo la uhakika kwamba namna ndogo za mgusano zinaporudiwa-rudiwa yale maono ya raha yaliyoletwa nazo kwa kawaida yanapungua. Hii yaweza kukufanya utafute kitu kingine chenye kuchochea zaidi sana. Lakini waweza kuendelea kwa kadiri gani bila ya kuhatirisha uhusiano safi? Kwa sababu ya kuiona hatari inayoweza kutokea, watu wengine wanapendelea kujizuia kabisa wasiwe na mgusano wo wote wa kimwili wakati wa uchumba, na hakuna mtu anayepaswa kuidharau hali yao ya dhamiri.​—⁠Linganisha Warumi 14:5, 10, 22, 23.

Kupigana busu vile vile huenda kukawa wonyesho safi wa upendano kati ya watu wanaofikiria ndoa​—au huenda kusiwe. Kwa kweli ulizo ni, Ni kwa kadiri gani nyege zinavyohusika? Namna fulani za dansi ni safi na zisizo na nyege; nyingine si safi. Ndivyo ilivyo na kupigana busu, au hata kukumbatiana. Lakini hata ukiwa safi, kila mmoja wa wonyesho huu unaonyesha hatua mpya imechukuliwa. Zikichukuliwa mapema wakati wa uchumba​—pengine hata mbele ya kuchumbiana​—zinaweza kuudhoofisha ukamatano wa wale watu wawili ukawa kutosheleza nyege tu, zikiwafanya waingie katika mwenendo mchafu, ikiwa si uasherati.​—Kol 3:5, 6.

Yatupasa tuwe wanyofu. Ikiwa hatuna kujiweza kwenye nguvu katika mambo haya, basi haitupasi tuuhatirishe wakati wetu ujao au ule wa mwingine. Je! wewe ungeendesha motokaa katika barabara ya mtelemko yenye kupinda-pinda ukijua breki zake ni mbaya? Wakati wa kukata maneno na kutafakari mambo haya ni mbele ya kuanza, si nyuma ya kuanza. Mara tamaa za mwili zianzapo kusisimka, kwa kawaida ni vigumu sana kuzizuia zisiendelee. (Yak. 1:14, 15) Wale wanaoacha nyege zikue ndani yao hata kutamanl kufanya ngono​—na hali hawaistahili hii kwa kuwa hawajaona​—wanajiweka katika wasiwasi, kuvunjlka moyo na maumivu. Ni kama kusoma kitabu chenye kusisimua​—mwishowe kuja kugundua sura ya mwisho imekatwa.

Wale wanaoufanya ukamatano wao katika uchumba wenye kuheshimika sana watafanikiwa zaidi katika ndoa kuliko wale wanaouruhusu ukamatano wao upoteze heshima kwa urafiki unaoongezeka polepole kuwa mwingi sana. Msichana atamheshimu namna gani mtu ambaye inampasa yeye (msichana) ‘azidi kumzuia’? Lakini kijana wa kiume aonyeshaye nguvu za kuvumilia na kujizuia kwenye kuheshimika anaheshimiwa. Ndivyo ilivyo na kwa msichana. Na zaidi yeye amepaswa ajue kwamba, hata ingawa huenda maono yake yakachukua muda kuchochewa, mara nyingi sivyo ilivyo kwa mwanamume,​—Mit. 25:28.

Kushindwa kujizuia na wonyesho unaoongezeka wa nyege kwaweza kuelekeza kwenye ndoa ya mapema mno isivyofaa. Kitabu Adolescence and Youth (ukurasa 288) kinasema hivi: “Hatua za kwanza za uchumba mara nyingi ni zenye mahaba. Wakati huo ndoa yaweza kumfanya mtu atazamie mengi zaidi katika ndoa hiyo kuliko ambayo yaweza kutoa. Kwa kawaida uchumba uliorefushwa unaleta kufahamiana kuzuri zaidi na yule mtu mwingine hata ndoa yaweza kuwa yenye mapatano.” Kujizuia lazima kutumiwe kwa uchumba huo mrefu zaidi​—ama sivyo huenda nguvu za nyege zikakua mapema sana hata kuwa hatari sana.​—Linganisha 1 Wakorintho 9:27.

Vile vile huenda mashaka mazito na shuku zikasitawi mkiisha kuoana ikiwa nyege ziliachiliwa ziwe zenye nguvu wakati wa uchumba. Huenda wale watu wawili wakaanza kushangaa, Kweli tulioana kwa sababu tulipendana? Au tulinaswa tu na nyege? Ulikuwa uchaguzi wa hekima? Vile vile huenda msichana akaelekea kutilia mashaka ukweli wa upendo wa mumewe, akishangaa kama yeye (mumewe) hakumwoa yeye kwa sababu tu ya mwili wake wala siyo kwa sababu ya alivyokuwa na alivyo kama mtu.

Ili ujilinde mwenyewe na furaha yako ya wakati ujao, epuka hali zinazovuta nyege. (Zab. 119:101, 104) Mahali pasipo na watu na giza havitakusaidia kuuendeleza uchumba kuwa wenye kuheshimika. Wala hali ambapo wakati unaelekea kuwa mwingi mno na kuonekana hakuna la kufanya ila kujitia katika wonyesho wa upendano. Lakini raha nyingi iliyo safi yaweza kupatikana katika utendaji kama vile kucheza mchezo fulani, kula chakula pamoja katika hoteli au kutembelea nyumba fulani ya makumbusho (museum) au mahali pa kwenu panapopendeza. Hata ingawa mnajisikia kufurahia faragha kwa sababu hamko karibu na watu mnaofahamiana nao, mngali mna ulinzi wa kutokuwa mbali kabisa na watu wengine.

Vile vile, kuliko kuwaza juu ya “unayoyakosa” tu kwa kuonyesha kujizuia, wazia yale unayoyatayarisha kwa wakati ujao. Ndipo, miaka yote itakayofuata, utaweza kutazama nyuma kwenye uchumba wako, si kwa kuchukizwa au kujuta, bali kwa furaha.​—Rum. 13:13, 14.

Ndiyo, uchumba waweza kukujaribu kweli juu ya ulivyo kama mtu, mambo uliyo nayo moyoni mwako, namna ulivyo mwaminifu. Neno la Mungu haliweki mipaka kamili kwa kila upande wa shauri hili. Lakini kanuni zifaazo, mashauri ya hekima na viongozi vyenye manufaa vipatikanavyo katika Neno la Mungu ni msaada wa kutosha kwetu kudumisha usawa, kukaa ndani kabisa katika mipaka ya mambo yaliyo safi na yenye afya kwa adili. Hivyo wonyesho wetu wa upendano kwa anayetazamiwa kuwa mwenzi hautamdhuru huyo hata kidogo, moyoni au kiroho. Kwa hiyo, ukija kuingia uchumbani, kwa kila hali uendeleze kuwa wenye kuheshimika. Utafurahi sikuzote kwamba ulifanya hivyo.

[Picha katika ukurasa wa 22]

Ikiwa uchumba wa mtu unakuwa mfululizo wa wonyesho wenye nyege kujizuia kukiwa kuchache zaidi na zaidi, hii itapasaje matumaini ya ndoa yenye kufanikiwa?

[Picha katika ukurasa wa 23]

Kuna furaha nyingi sana iliyo safi iwezayo kuonwa na inayolinda pia wenzi wawili wasijitenga kabisa na wengine

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki