Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g90 6/8 kur. 10-12
  • Je! Wewe Unamwabudu Mungu Aliye Hai?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unamwabudu Mungu Aliye Hai?
  • Amkeni!—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wewe Utaabudu Nani?
  • Wenye Ujitoaji kwa Mungu-mwanadamu kwa Nini?
    Amkeni!—1990
  • Mungu ni Nani?
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • “Mungu wa Pekee wa Kweli” Ni Nani?
    Amkeni!—2005
  • Mungu—Yeye Ni Nani?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1990
g90 6/8 kur. 10-12

Je! Wewe Unamwabudu Mungu Aliye Hai?

INGAWA Tadashi Ishiguro alizaliwa baada ya Vita ya Ulimwengu ya Pili—baada ya ukanushaji wa kihistoria wa maliki wa Kijapani kuwa yeye si mungu—yeye bado aliamini kwamba maliki alikuwa mungu. “Yeye hangelipaswa kukanusha uungu wake,” akasema Tadashi.

Hata hivyo, ndugu yake alisababu naye juu ya jambo hilo: ‘Maliki, kama vile watu wale wengine, huzeeka na kuwa mgonjwa. Hawezi kuepuka mwisho wa watu wote: kifo. Yeye hawezi kujiokoa mwenyewe, achilia mbali watu wengine.’ Baada ya mazungumzo hayo, ambamo ndugu yake alirejeza kwenye Biblia, Tadashi aliamua kuchunguza kwa uangalifu imani zake.—Mhubiri 3:19; Warumi 5:12.

Baada ya muda, alianza kuona hekima ya kitia-moyo cha Biblia: “Msiwatumainie wakuu, Wala binadamu.” Kwa nini? Kwa sababu, kama Biblia inavyosema, “hakuna wokovu kwake. Pumzi yake hutoka, huurudia udongo wake, Siku hiyo mawazo yake yapotea.” (Zaburi 146:3, 4) Kweli kweli, kuwatumaini wanadamu wanaoweza kufa kuwa miungu mwisho wake ni kutamaushwa, hata msiba!

Kikundi cha visiwa vya Japani chadhaniwa kuwa kiliumbwa na matone ya maji yakianguka kutoka kwenye mkuki wake Izanagi, baba ya mungu-mke-jua Amaterasu Omikami. Lakini imani hii haina msingi halisi. Vipi, basi, juu ya imani ya kwamba maliki Mjapani ni mzao wa kibinadamu wa mungu-mke huyo na kwa hiyo yeye ni mungu? Je! hiyo pia si hadithi ya kitamaduni isiyo na msingi? Kwa sababu waliabudu kitu ambacho hawakujua kweli kweli, maelfu ya Wajapani walidhabihu maisha zao kwa niaba ya mmoja ambaye hangeweza kuwasaidia. Inasikitisha kama nini!

Kama matokeo ya mazungumzo pamoja na ndugu yake, ikawa wazi kwake Tadashi kwamba dunia yetu yenye kupendeza, na pia uhai juu yayo, ni kutoka kwa Muumba mwenye nguvu na mwenye upendo. (Waebrania 3:4) Kulingana na Biblia, Mungu wa kweli ni wa “tangu milele hata milele.” (Zaburi 90:2) Yeye yuko hai milele. Maisha yake si ya kipimo cha miaka 70 au 80, wala yeye hategemei ushauri wa washauri wake.—Zaburi 90:10; Warumi 11:34.

Tofauti na hilo, Biblia inasema juu ya Muumba: “Hufanya kama atakavyo, katika jeshi la mbinguni, na katika hao wanaokaa duniani; wala hapana awezaye kuuzuia mkono wake, wala kumwuliza, Unafanya nini wewe?” (Danieli 4:35) Jinsi alivyo tofauti na wanadamu ambao huenda wakachukuliwa kuwa miungu lakini wasiweze kutimiza hata mapenzi yao wenyewe!

Tadashi alipoendelea kujifunza Biblia, imani yake katika Mungu ambaye aliivuvia ilikua. Huyu si mungu wa hadithi ya kitamaduni. Badala yake, yeye ni halisi, Mtu asiyeonekana. Katika Biblia, ambayo Mungu alivuvia wanadamu waiandike, anatuambia kwamba jina lake ni Yehova. (Zaburi 83:18) Pia anatuambia juu ya yale ambayo amefanya, juu ya anayokusudia kufanya, na juu ya jinsi anapaswa kuabudiwa. Hata hivyo, unawezaje kuwa na uhakika kwamba Yehova ni Mungu aliye hai ili imani yako kwake isiwe ya bure?

Katika kutangaza ukuu wake juu ya wengine wote, Yehova alisema: “Mimi ni Mungu, wala hapana mwingine; mimi ni Mungu, wala hapana aliye kama mimi; nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.”—Isaya 46:9, 10.

Kwa hiyo, Uungu wake unathibitishwa na uweza wake wa kutabiri wakati ujao na kuhakikisha kwamba mapenzi yake mwenyewe yanatimizwa. Yeye aweza kulinda na kuokoa watumishi wake, tofauti na wanadamu wanaoabudiwa kama miungu lakini hulindwa na raia zao wenyewe. Kwa hiyo, muda si muda, Tadashi akaja kumwabudu Mungu wa Biblia, akajiunga na nduguye katika kumtumikia Yehova Mungu akiwa mmoja wa Mashahidi Wake.

Wewe Utaabudu Nani?

Miungu mingi inaabudiwa leo, kutia ndani binadamu ambao watu wanawapa sifa ya nguvu za mungu. Biblia inasema: “Wako waitwao miungu, ama mbinguni ama duniani.” (1 Wakorintho 8:5) Kwa kielelezo, katika Athene, mji wa kale wa Kigiriki, madhabahu ilitengenezwa ambayo juu yayo yalikuwa maneno: “KWA MUNGU ASIYEJULIKANA.” (Matendo 17:23) Kwa hiyo Waathene walikuwa kati ya wale walioabudu kile ambacho wao walikubali hawakukijua kikweli.

Kwa hiyo kuna uwezekano kwamba sisi leo tungeweza kuhusika katika kuabudu tusichojua. Mamilioni ya Wajapani walijihusisha katika ibada hiyo, wakadanganywa na mawaziri walioendeleza imani ya kwamba maliki alikuwa mungu. Hata maliki alihusika na udanganyi huo. Kwa hiyo jifunze somo: Uhakika wa kwamba wazazi wetu wanaamini jambo fulani au kwamba mawaziri wanasema jambo fulani ni kweli hilo peke yake halifanyi jambo hilo liwe hivyo. Tunahitaji kuchunguza ili kuhakikisha kwamba sisi tunajua kikweli tunachoabudu.

Waathene wa kale, au Wajapani walioishi kabla ya Vita ya Ulimwengu ya Pili, sio peke yao walioabudu kitu ambacho hawakukijua kikweli. Hata leo mamilioni ya watu katika Jumuiya ya Wakristo wanaabudu Utatu. Ikiwa wewe ni mtu kama huyo, jiulize: Je! kweli mimi namjua Mungu ninayeabudu? Jina lake ni nani? Yeye awezaje kuwa watu watatu katika Mungu mmoja? Chanzo cha imani hiyo ni nini?

Wanaoamini Utatu yawezekana wanadhania kwamba Yesu Kristo na mitume wake waliufundisha na kwamba hilo ni fundisho la Biblia. Lakini sivyo. New Catholic Encyclopedia inakubali: “Ubuni huu ‘Mungu mmoja katika Watu watatu’ haukuwa na msingi imara, kwa uhakika haukuwa kabisa sehemu ya maisha ya Kikristo na dai lao la imani, kabla ya mwisho wa karne ya 4 [mamia ya miaka baada ya Yesu na mitume wake kuwa duniani]. . . . Kati ya Mababa wa Kimtume, hakukuwako lolote hata lenye kukaribia kidogo wazo au maoni hayo.”

Kwa upande mwingine, mamia ya miaka kabla ya Yesu Kristo kuja duniani akiwa mwanadamu, fundisho la utatu lilikuwa limetia mizizi sana kati ya watu ambao dini zao zilikuwa zinategemea hadithi za kitamaduni. Kwa kielelezo, Wamisri wa kale waliabudu utatu wa Osirisi, Isisi (mkeye) na Horasi (mwanae). Nao Wahindu, hata mpaka leo hii, wanaabudu utatu wenye kufanyizwa na Timurti wenye vichwa vitatu wa Brahma, Vishnu, na Siva.

Kwa hiyo badala ya kufuata na kuabudu kwa njia ile ambayo wale wanaokuzunguka wanaabudu, chunguza ili uhakikishe kwamba kweli kweli unajua unachoabudu. Waathene, waliokuwa wakiabudu kitu wasichokijua kikweli, waliambiwa kwamba Mungu “hawi mbali na kila mmoja wetu,” na kwamba angeweza kupatikana na yeyote anayemtafuta kwa bidii. Kwa hiyo, tunaweza kuwa na uhakika kwamba tukitafuta kwa bidii Mungu wa kweli aliye hai, tutampata.—Matendo 17:27.

[Picha katika ukurasa wa 10]

Tadashi aliamua kuchunguza kwa uangalifu imani zake

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki