Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g91 3/8 uku. 13
  • Barua ya Shukrani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Barua ya Shukrani
  • Amkeni!—1991
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Sijapata Kusoma Cho Chote Kinachofanana Nacho’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Itikio la Wasomaji kwa Kitabu ”Young People Ask”
    Amkeni!—1991
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—2003
  • Kitabu cha Danieli Chafafanuliwa!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1991
g91 3/8 uku. 13

Barua ya Shukrani

KILA mwaka Mashahidi wa Yehova huchapa na kutawanya makumi ya mamilioni ya nakala za Biblia na za vitabu vinavyosaidia kuielewa Biblia. Hivi majuzi, mwanafunzi wa Biblia mmoja kutoka Texas, U.S.A., alipokea kutoka kwa mpwa wake wa miaka 20 barua ya shukrani kwa ajili ya nakala za vichapo hivyo ambavyo alikuwa amempa. Yafuatayo, kwa sehemu, ni maelezo yake kuhusu vitabu hivyo:

“Mpendwa Shangazi Irene na Familia,

“. . . Sasa ni saa 7:00 asubuhi, kwa hiyo sina hakika barua hii itakuwa na urefu gani, lakini nitajaribu kusema ninayotaka kusema, na hasa yangu ni kukushukuru!

“Vile vitabu ulivyoniletea ni vizuri ajabu! Kwa kweli hivyo ni zaidi ya niliyotazamia. Vinaongeza ladha kwenye kila jambo; kile kijambo kinachofanya ipendeze na istahili jitihada ya kusoma.

“Life . . . by Evolution or by Creation ni kivuta-fikira kweli kweli! Watungaji wa kitabu hiki wanahitaji pongezi ya mkono! Maelezo ni ya lugha rahisi kabisa, yenye akili, na yenye kueleweka. Mstari niupendao zaidi katika kitabu hicho ni ‘Kufanyizwa kwa uhai na aksidenti kwalingana na kutokezwa kwa kamusi kubwa na mlipuko katika duka la uchapaji.’ We! hilo limeelezwa vizuri kama nini!

“Paradiso [Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani] ni kitabu kingine kilichoandikwa vizuri. Hiki kinafanya muhtasari wa mambo mengi ambayo nimekwisha soma lakini chafanya hivyo kwa uzuri na uhakika zaidi kushinda habari nyingineyo. Bado sijamaliza kitabu hiki.

“Kutoa Sababu [Kwa Kutumia Maandiko] ni kamusi ambayo nimekuwa nikiitaka sikuzote. Utoaji sababu wenye akili juu ya dhana za msingi ambazo hapo mbele nimeshindwa kushika; maoni ya Kibiblia juu ya vichwa vya kisasa. Lo! ni cha kustaajabisha kama nini! Hakika ni kitabu cha kuchunguzwa; lazima nikushukuru tena.

“Questions [Young People Ask—Answers That Work] ni kitabu ambacho imetukia leo kikawa msaada. Nilikitumia kushauri rafiki yangu mpendwa ambaye ana matatizo mengi ya kufanya matembezi ya kutafuta mahaba. Aliyaelewa kweli kweli yale majibu ya akili. Pia mimi binafsi nimekiona kuwa msaada katika kujielewa vizuri zaidi. Asante.

“Na mwisho lakini bila shaka sicho cha mwisho, New World Translation. Tafsiri hii ni rahisi zaidi kuielewa kushinda KJV [King James Version] yangu hivi kwamba najikuta nikiirejezea mara nyingi zaidi ya ile nyingine . . . Mungu akubariki kwa ajili ya zawadi hizi zenye thamani! . . .

“Bila vitabu ulivyonipelekea yawezekana bado ningekuwa nimelemewa na kujihurumia, lakini sasa nina vyombo vya kushughulika na hali yangu, na hilo ni jambo ambalo ni vigumu kulipia. Yesu angekuonea fahari. Mimi pia nakuonea!

“Nimejifunza mengi sana kwa muda mfupi sana, inasisimua we! Sikudhani kamwe kwamba Biblia ingeweza kuwa yenye kupendeza na kusisimua hivyo. Sasa nina sababu zenye nguvu za kukazana kulipita tope la maisha ambalo Shetani amenitupia, nami nataka kuzishiriki na ulimwengu. Asante!

“Tafadhali wape familia salamu zangu. . . .

“Nasali kwa ajili yenu nyote!

Nasema asante,

Michael”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki