Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g91 12/8 kur. 20-23
  • Ulimwengu Usio na Udhibiti

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ulimwengu Usio na Udhibiti
  • Amkeni!—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mivuto Mibaya
  • Kifaa cha Kukinza Mwenendo Huo
  • Kufuata Mifano Mizuri
  • “Naitaka Sasa!” Muhula wa Utoshelezo wa Papo Hapo
    Amkeni!—1991
  • Je, Biblia Inakataza Kufurahia Ngono?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Kwa Nini Watu Hawana Subira?
    Amkeni!—2012
  • Ulimwengu Usio na Uhalifu Waja Karibuni!
    Amkeni!—1998
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1991
g91 12/8 kur. 20-23

Ulimwengu Usio na Udhibiti

Ufuatiaji usio na subira wa binadamu wa kupata utoshelezo wa papo hapo umetokeza kukosa kwake kudhibiti mambo. Hebu angalia mifano michache:

Kimazingira: Mwanadamu anaangamiza mazingira. Baada ya muda mrefu, madhara yatakuwa ni msiba; ingawa, kwa wakati huu kupunja dunia mali ya asili yayo na kufanya jitihada kidogo tu ili kukomesha uchafuzi kwamaanisha pesa kwa viwanda na serikali. Kwa hiyo, upunjaji huo waendelea, kujapokuwa kuteta kwa wanamazingira.

Kiuchumi: Mataifa mengi kuzunguka ulimwengu hukopa pesa zaidi na zaidi, yakiweka rundo la madeni kwa ajili ya mahitaji ya kiuchumi ya sasa. Kwa moyo mwepesi wao hupuuza maonyo makali ya wanauchumi—kwamba riba ya madeni hayo yote yaweza kuongezeka kuwa mzigo usiobebeka baadaye au kwamba uchumi wa ulimwengu unaotegemezwa na deni ya ulimwenguni pote ni hafifu sana na waweza kuanguka iwapo nchi maskini zikatae kulipa madeni yao.

Maadili: Watumiaji wa dawa za kulevya na wanywaji pombe kupita kiasi, wacheza kamari, wahalifu wa aina yoyote ile, wazinzi, waasherati—ni nani awezaye kukana kwamba hesabu zao zinaongezeka leo? Ni kikundi chenye hitilafu kilicho na jambo moja linalofanana: Wanakitaka kitu chenyewe SASA! Kama hicho “kitu chenyewe” ni ngono, pesa, mamlaka, au kulewa kidogo tu, wengi wana nia ya kutupilia mbali ndoa, familia, dhamiri, ulinzi wa kifedha, afya bora, jina zuri, hata uhai, kwa raha hizo za muda mfupi.

Si kutia chumvi hata kidogo kusema kwamba ulimwengu wa leo umekosa udhibiti, ukiongozwa na pupa iliyo karibu kama ya kitoto. Wengine hupinga kwa unyofu hali ya kukosa mwono wa mbali ambayo ni kawaida sana ulimwenguni. Lakini nguvu zenye uwezo zaidi zisizotuwezesha kuona madhara ya baadaye na zisizoweza kutusaidia sisi sote kujidhibiti, ndizo zimeenea zaidi.

Mivuto Mibaya

Mwanadamu wa ki-siku-hizi, hasa katika mataifa yaliyoendelea zaidi kiviwanda, huwa mara zote yumo katika propaganda zinazoenezwa kupitia vyombo vya habari. Utoshelezo wa papo hapo huenezwa kwa ustadi iwe ni kupitia televisheni, redio, sinema, magazeti, au magazeti ya habari.

Utangazaji wa biashara katika vyombo vya habari, hukutia moyo ununue, ununue, ununue—na kujaribu kujipatia kadi za mkopo ili uweze kununua, sasa, sasa, sasa. Baadhi ya bidhaa zilizotengezwa ziko tayari karibu nawe kwa kupiga simu. ‘Usijali kulipa sasa!’ matangazo hayo yaonekana yakisema kwa kutuliza. Matangazo hayo huwa yamebuniwa kwa ustadi wa kuchochea hisia za mtu. Fungua ukurasa katika gazeti, na wimbi la marashi lakupiga. Fungua redio, na mlio wa matangazo hayo walia kichwani mwako bila kukoma kwa siku kadhaa. Fungua televisheni, na picha zayo zenye kuvutia zakuduwaza. Katika mtindo wa muziki wa video, picha huenda kwa kasi ili kunasa akili hata kwa muda mfupi tu.

Televisheni hufanya mengi zaidi ya kutangaza utoshelezo wa papo hapo. Huueneza wazi. Kuifungua tu hivi, inatokeza tamaa ya kutumbuizwa. Mara nyingi hutumbuiza kwa kuonyesha watu wakitosheleza tamaa zao. Mtu wa vitendo hugeukia ujeuri ikiwa washindani wake ‘wanastahili kutendewa kijeuri.’ Mtoto mtundu huaibisha wazazi wake kwa michezo ya mizaha yake. Wenye tamaa ya kimahaba hukubali mara moja uzinzi au ngono ya kabla ya ndoa. Mara nyingi televisheni huwa haikatai watu hao kwa ajili ya ukosefu wao wa kujidhibiti; huwatukuza, ikiwapa utukufu wa kutazamisha au kuwashangilia kwa vicheko vya kujifanya tu.

Vivyo hivyo, makala moja ya hivi karibuni katika The Atlantic Monthly ilisema kwamba sinema za Hollywood za siku hizi ni “kioja ambacho kimebuniwa kwa ustadi ili kiridhishe katika kila dakika,” huku “kila sinema baada ya sinema ikilia kwa sauti, ‘Waweza kuvipata vyote!’” Inaonekana, hakuna kitu kingine chochote kiwezacho kutosheleza watazamaji zaidi kushinda jeuri. Makala hiyo yashtaki kwamba sinema za zamani “zilikandamiza maoni ya watazamaji ya kujiunga na ubaya,” huku “kwa kutofautisha, jeuri ya sinema sasa inatumiwa kualika mtazamaji afurahie ile hisia ya kuua, kupiga, kulemaza.” Kwa hakika, vitendo na jeuri vimejaa sana kuliko hadithi na maongezi hivi kwamba maandishi ya sinema za ki-siku-hizi huwa mafupi kwa kuandikwa kwa asilimia 25 kushinda miaka ya 1940, hata ingawa sinema zenyewe zina urefu ule ule.

Dini za ulimwengu zimo katika hali nzuri ya kuinua jamii ya kibinadamu kutoka huu ‘ukichaa wa sasa’ uliopotoka. Na bado, wengi wa viongozi wa kidini huonekana kama wanakwama kwa hali yao wenyewe ya kujitafutia utoshelezo wa papo hapo. Je! ni mara ngapi sisi husoma juu ya kutafuta kwao mamlaka na umashuhuri katika uwanja wa kisiasa, au wakijipendekeza wenyewe na wafuasi wao waliopotoka kwa kupunguza viwango vya adili, au hata kutumia Biblia kama wonyesho wa haki kwa nje na huku nyuma wakifanya wapendavyo kwa unafiki? Badala ya kufichua utoshelezo wa papo hapo kama vile ambavyo huwa hasa—sehemu ya uvutio wa dhambi—wamejiunga na wengine wa ‘viongozi wa maadili’ katika kupunguza wazo la dhambi, wakiielezea kwa maneno matamu na yasiyochukiza yenye uzuri kama vile ‘matatizo ya kurithiwa’ na ‘mitindo ya maisha ya badala.’

Kifaa cha Kukinza Mwenendo Huo

Kukiwa na hali kama hiyo duniani, twawezaje kujikinga? Twawezaje kufanya maamuzi bila kuegemea upande wa uvutio wa utoshelezo wa papo hapo? Huenda jibu likakushangaza: Biblia yaweza kusaidia. Kinyume cha vile wengi huenda wakafikiri, Biblia haipingi raha. Haiendelezi kujinyima mno mambo au kukataa vitu vyote. Badala ya hivyo, Biblia hutufunza jinsi ya kuishi maisha yenye furaha, raha ikiwekwa mahali panapofaa.

Biblia huelezea Muumba kuwa “Mungu ahimidiwaye [mwenye furaha, NW]” ambaye ‘huyafurahia matendo yake.’ (1 Timotheo 1:11; Zaburi 104:31) Kwa upande wa wanadamu, Mhubiri 3:1 inasema: “Kwa kila jambo kuna majira yake, na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.” Hiyo inatia ndani, kulingana na mistari inayofuata, wakati wa kucheka, wakati wa kucheza, wakati wa kukumbatia, na wakati wa kupenda. Mithali 5:18, 19 hata inahimiza uzuri wa raha ya kingono kati ya mtu na mke wakati iwaambiapo waume: “Umfurahie mke wa ujana wako.” Kwa wazi basi, utoshelezo wote si mbaya, wala si lazima namna zote za utoshelezo zikataliwe eti zinakatazwa na sheria. Hata hivyo, udhibiti ndio mara nyingi jambo linalokosekana.—Wagalatia 5:22, 23.

Ni lazima tuweke raha zetu mahali pa kuzifaa. Twahitaji kutanguliza mambo yafaayo. Kumpendeza Mungu lazima kuje kabla sana ya raha zetu; ni lazima kuwe kwanza katika maisha yetu. Kisha kunafuatwa na upendo wemye kuongozwa na kanuni kwa mwanadamu mwenzetu. (Mathayo 6:33; 22:36-40) Ikiwa kweli twapenda Mungu na jirani, basi tutafurahia kuweka utoshelezo wetu nyuma ya mambo hayo mawili ya kutangulizwa.

Mambo ya kutangulizwa yenye msingi wa Biblia yatatusaidia kukataa kabisa utoshelezo ikihitajika tufanye hivyo. Tutawachia mbali ulevi, uzinzi, uasherati, kucheza kamari, pupa, utumizi mbaya wa dawa za kulevya, na jeuri. Dhambi hizi huleta utoshelezo wa papo hapo kwa njia zazo tofauti tofauti, lakini zinachukiza Mungu na kuumiza mwanadamu mwenzetu. Sheria za Mungu dhidi ya dhambi hizo ni ishara ya hakika ya upendo wake kwetu, kwa sababu mwishowe, dhambi huumiza zaidi yule mwenye kuitenda. Matokeo yaweza kuwa maradhi, nyumba iliyovunjika, au umaskini. Huenda ikawa ya kukata maneno kama kifo au yenye msiba kama maisha mapungufu na yasiyotimizwa.

Kufuata Mifano Mizuri

Mungu ataka tuishi maisha yenye furaha, yenye kujaa maana; Neno lake limejaa mifano ya wanaume na wanawake ambao waliishi hivyo. Katika visa vingi imani yao na upendo wao kwa Mungu uliwasukuma waahirishe utoshelezo wao. (Ona Waebrania, sura ya 11.) Musa ni maarufu katika jambo hilo. Akiwa amelelewa kama mwana wa binti ya Farao katika Misri ya kale, alikuwa na maisha ya utoshelezo mbele yake. Mamlaka, umashuhuri, mali, na bila shaka nafasi tele za ngono, zote zingekuwa zake iwapo angebaki kati ya watu wa nyumba ya Farao. Badala ya hivyo, alijiunga na taifa la Israeli, lililodharauliwa na kutiwa chini ya utumwa. Kwa nini?

Waebrania 11:25 inajibu kwamba alichagua “kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha katika dhambi kwa kitambo.” Musa aliuona utoshelezo wa papo hapo jinsi ulivyo hasa. Wa papo hapo. Wa muda tu. Wa kuisha upesi. Hivyo, badala ya kukazia akili mambo ambayo yangemletea raha ya wakati huo tu, alikaza fikira kwenye wakati ujao wenye furaha. Kama vile Waebrania 11:26 inavyosema: “Aliyatazamia hayo malipo.” Malipo hayo yalikuwa halisi kwake, kama vile Mpaji wa malipo alivyokuwa halisi kwake. Mstari wa 27 wasomeka hivi: “Alistahimili kama amwonaye Yeye asiyeonekana.”

Huenda wengine wakadharau uchaguzi uliofanywa na Musa. Wengine huenda wakasema kwamba wao wangalichagua mali, mamlaka, sifa. Lakini fikiria hili: Ikiwa Musa angalifuatia njia ya utoshelezo wa papo hapo, je! hata tungemjua leo hii? Je! jina lake la Kimisri lingeokoka likiwa mwandiko wa kutumia herufi za picha-muundo kwenye jiwe moja lililopasuka katika chumba cha ukumbusho fulani, likiwa halina maana na kujificha lijulikane tu na waakiolojia wachache? Au, kwa uwezekano zaidi, halingeweza kulala likiwa limezikwa chini ya ardhi na kusahauliwa chini ya vumbi na mchanga kwa karne 34? Na vipi juu ya malipo yake? Je! Musa alikuwa na uhakika wa kuwa katika kumbukumbu la Yehova ikiwa angalichagua njia rahisi ya kujifurahisha mwenyewe?

Jina la Musa linatia nguvu mamilioni ya watu leo. Wakati wake ujao ni wa hakika. Wakati ujao wako pia waweza kuwa wa hakika vivyo hivyo. Wewe pia waweza kuwa kitia moyo kwa wengine. Unapofanya maamuzi yako katika maisha, tokea makubwa hadi madogo, usidanganywe na propaganda ya ulimwengu huu kwamba ni lazima upate unachotaka SASA! Hebu jiulize, ‘Je! ninachotaka kinapatana na kile ambacho Muumba wangu angenitakia? ‘Je! kufuatia ninachotaka kwaweza kumaanisha kuweka miradi ya kiroho mstari wa nyuma? Je! nahatarisha zawadi yangu kwa njia yoyote ile? Ni mfano wa aina gani ninaowekea marafiki na familia?’

Usichague mwono mfupi wa ulimwengu huu badala ya hekima ya Mungu ionayo mbali. Usibadilishane furaha ya muda mrefu na raha ya muda mfupi, ile ya milele kwa ile ya muda tu. Na hata hivyo, Muumba wetu atutolea utoshelezo kwa njia ya hali ya juu iwezayo kuwazika. Ni kama vile Zaburi 145:16 inavyosema juu yake: “Waufumbua mkono wako, wakishibisha kila kilicho hai matakwa yake.” Baadhi ya matoshelezo hayo ni ya papo hapo; lakini mengine yahitaji wakati na subira. Maisha katika utumishi kwa Yehova yamejawa na raha—mazuri ya uumbaji, uchangamfu wa urafiki, shangwe ya kazi ngumu yenye kuthawabisha, furaha ya kujifunza majibu ya maswali ya maisha yanayotatanisha zaidi. Zaidi ya hayo, Muumba atutolea maisha ambayo yatatosheleza milele.—Yohana 17:3.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki