Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g92 6/8 kur. 20-23
  • Uwezo Ambao Kweli Inao wa Kurekebisha Tabia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwezo Ambao Kweli Inao wa Kurekebisha Tabia
  • Amkeni!—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi Ukweli Ulivyonibadili Nisiwe Mhalifu Niwe Mkristo
    Amkeni!—1990
  • Simba Angurumaye awa Kondoo Mpole
    Amkeni!—1999
  • Utoro Wangu Kuelekea Kweli
    Amkeni!—1994
  • Biblia Inabadili Maisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1992
g92 6/8 kur. 20-23

Uwezo Ambao Kweli Inao wa Kurekebisha Tabia

“Mvunjaj-nyumba mmoja, aliyefunguliwa mapema, alifanya uvunjaji mara 500 katika miezi saba. Mnajisi, aliyefunguliwa miaka minne kabla ya kifungo chake kisichopungua miaka kumi alimnajisi na kumwua mwanamke mmoja. Muuaji aliyeachiliwa kwa ahadi ya kutotoroka alivunja nyumba na kuuwa watu watatu.”—Reader’s Digest, Novemba 1990.

“Karibu asilimia 63 ya wafungwa waliofunguliwa kutoka magereza ya majimbo walifungwa kwa uhalifu mbaya katika muda wa miaka mitatu, Idara ya Hukumu ikasema katika uchunguzi uliotolewa leo.”—The New York Times, Aprili 3, 1989.

“Wazo la kwamba gereza ni mahali ambapo wahalifu wanaweza kurekebishwa si la kweli. Gereza ni mahali pa mchanganyiko wa ‘nyumba za hifadhi’ na ‘shule za uhalifu.’”—Toronto Sunday Star, Machi 20, 1988.

Mlinzi katika Kisiwa cha Rikers, jela ya New York City, asema: “Kijana huja hapa, mwenye umri wa miaka kumi na tisa, alikuwa mlinzi wakati wa wizi. Atokapo hapa, hatakuwa mlinzi wakati wa wizi. Wakati utakaofuata, atakuwa mtu atakayefyatua risasi.”—gazeti la New York, Aprili 23, 1990.

“Milango ya gereza imekuwa kama milango ya kuzunguka: karibu theluthi mbili ya wafungwa wote hufungwa tena katika kipindi cha miaka mitatu ya kufunguliwa kwao.”—gazeti Time, Mei 29, 1989.

HAKUNA yoyote ya yaliyo juu iliyo habari mpya. Ni mambo ya kawaida: Magereza hayarekebishi tabia. Kweli inafanya hivyo. Mfano unaothibitisha jambo hilo ni: Ron Pryor.

Ron huanza kila siku kwa kusoma andiko la Biblia na familia yake. Ndoa yake ni yenye amani na upendo. Makao yake ni yenye utaratibu na safi. Wana wao wawili walikuwa wanafunzi wazuri—bila dawa za kulevya, bila kileo, bila matata. Kwa sasa wako peke yao wakishughulika na utendaji wa Kikristo. Ron na mke wake, Arlynn, ni wenye shughuli katika jamii yao wakifanya kazi ya kujitolea wakiwa Wakristo. Maisha yenye maana wakitumikia wengine.

Hata hivyo, katika 1970, Ron Pryor alikuwa gerezani akingojea kuhukumiwa kwa ajili ya uuaji. Alipatikana kuwa na hatia, akadhibitishiwa kosa lake, na akaanza kutumikia katika gereza la jimbo. Ulikuwa upeo wa kazi-maisha ya muda mrefu ya uhalifu ambao ulimpeleka gerezani mara nyingi. Lakini acha Ron aeleze habari yake.

“‘Kifungo’ cha kwanza ninachokumbuka kilikuwa kifungio kilichounganishwa na kamba hadi kwenye kizingiti cha kamba za kuanikia nguo. Nilipokuwa na miaka mitatu au minne, nilikuwa na tamaa ya kutembea. Ningezunguka huko na huko, nipotee, nichukuliwe na polisi na kurudishwa nyumbani. Mwishowe, mama yangu aliniambia kuwa ikiwa sitaacha tabia hiyo, angepiga simu kwenye makao ya mayatima waje wanichukue na kunifungia. Nilikaa katika uwanja nikilia, nikiwangojea waje. Hawakuja. Badala yake, mama yangu alinifunga kwenye kizingiti cha kamba ya kuanikia nguo.

“Kadiri nilivyoendelea kuwa mkubwa, nilikuwa naingia kwenye matata, na jeuri ikawa ndio jibu la kila shida yangu. Nilihisi nikiwa nimevurugika, nimetatanika, nimeachwa. Sikuwa nikitambua lililo zuri na lililo baya. Niliacha hisi zangu, si dhamiri, ziwe mwongozo wangu. Shuleni nilipitishwa kutoka darasa moja hadi darasa lingine kwa sababu walimu walifurahi kuniondoa. Niliachia darasa la saba na nikatoroka nyumbani. Nilijiunga na mashirika mabaya, na kweli kupatana na onyo la kimandiko, kuliniongoza katika shida zaidi.—1 Wakorintho 15:33.

“Shule za kurekebishia tabia upesi zilichukuwa mahali pa kamba za kuanikia nguo. Hazikunirekebisha tabia. Ningekimbia na kushikwa. Nikitoroka kutoka shule moja Virginia, niliiba gari dogo la mizigo na nikashikwa. Nilipokuwa mbele za hakimu aliyeitwa Jenkins juu ya mashtaka ya uibaji-gari, niligundua kwamba lilikuwa gari la hakimu Jenkins ambalo nilikuwa nimeiba! Nilikuwa na umri wa miaka 16 tu, lakini nilitangazwa kuwa mkaidi na nikahukumiwa kama mtu mzima. Niliwekwa ndani kwa miaka miwili.

“Baada ya kufunguliwa kutoka gerezani katika miaka yangu ya 20, nikawa na pikipiki. Nilichochewa na hisi ya uwezo iliyonipatia, lakini hilo halikutosha. Nilijiunga na Pagans—genge la pikipiki ambalo kila mara lilikuwa likizungukazunguka likitafuta matata, likiwa na tamaa ya kuanzisha ghasia wakati wote. Nilifaana nalo sawa sawa.

“Baadaye, nilikuwa dereva wa kilori kidogo nikisafirisha mazao kutoka Florida. Sikuwa tena pamoja na Pagans, lakini nilipokuwa nikija kutoka Virginia wakati huu, katika 1969, nilikutana na baadhi ya wenzangu wa zamani wa Pagan. Tukaanza kusherehekea—kunywa divai, kulewa kwa dawa za kulevya. Fujo ikaanza, ikaongezeka na katika mapigano hayo yenye ghasia nyingi yenye kuchochewa na kileo na dawa za kulevya, nilipiga mtu risasi na kumwua. Matokeo zaidi ya mashirika mabaya! Baadaye, niliulizwa maswali na wapelelezi wawili, na nikakubali kuwa niliuwa. Hilo lilitukia katika 1970.

“Nilikuwa jela nikingojea kuhukumiwa na bado nikiwa mfanya ghasia mwasi. Kwa mfano, asubuhi moja mtunzi akaja na kahawa. Walikuwa kwa kawaida wanakupatia kikombe cha ziada cha baadaye. Asubuhi hiyo, nilikitia kikombe changu chini ya mdila, lakini akasema ‘hakuna ziada.’ Lililomaanisha kwangu ni kwamba aliamua kumpa mtu mwingine. Kwa hivyo nikasema, ‘Kwa hivyo mna upungufu wa kahawa asubuhi hii, eh?’ Akasema, ‘Ndiyo.’ ‘Basi, chukua hii yangu.’ Nikamrushia usoni. Nilifungiwa nikiwa peke yangu.

“Kwa hiyo ninatembea nikizungukazunguka katika hilo shimo la futi nane kwa kumi ambalo halina madirisha. Kwa mara ya kwanza maishani mwangu, nikaanza kufikiria. Nilijawa na maswali. ‘Kwa nini maisha yangu kila mara yako katika vurugu namna hii? Kwa nini niko kwenye shimo hili? Kwa nini naishi? Kwa nini? Kwa nini? Kwa nini?’ Maswali haya yalizidikuja bila majibu. Halafu nikajiambia: ‘Mimi nimefikia mwisho wangu. Hakuna mahali pa kwenda. Isipokuwa—ikiwa kuna Mungu—Mungu ambaye huniona mimi, anayejua kwamba naishi, anayenielewa—jambo ambalo nashindwa! Mungu ikiwa uko, ikiwa unajua niko, ikiwa kuna kitu ninachoweza kufanya—niambie tu kitu fulani, kitu chochote!’

“Kulikuwa na Biblia hapo ndani. Nikafikiria, ‘Hilo ndilo mwanzo.’ Nikaanza kuisoma. Sikumbuki nililosoma. Nakumbuka tu nikiisoma, bila kuelewa kitu. Katika muda wa juma moja nilikuwa katika chumba cha jela. Chumba kimoja kilifunguliwa, vitanda vyake viwili vilikuwa vitupu. Waliniweka ndani, na baada ya siku mbili wakaleta mfungwa mwingine ndani. Nilikuwa nikiisoma Biblia wakati huo, niking’ang’ana nayo. Aliniona nikiisoma na akaniuliza: ‘Ungependa kuelewa Biblia?’ ‘Ndiyo!’ ‘Nitakupatia kitabu ambacho kitakusaidia.’ Aliwasiliana na mmoja wa mashahidi wa Yehova—walio kuwa wamejifunza naye wakati mmoja—na upesi akanipatia kitabu chenye kichwa Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele. Hilo lilikuwa katika Julai 1970.

“Nikaanza kukisoma, na nikakisoma kuanzia jalada hadi jalada. Sikuelewa kila kitu, lakini kilileta umaana. Kadiri mashahidi wa Yehova walivyokuja kujifunza na mimi, maswali yote niliyokuwa nayo kifungoni yalianza kujibiwa. Kwa mara ya kwanza maishani mwangu, nikapata kuona kindani lile lilikuwa jema na lililokuwa baya. Kadiri nilivyokuwa nikitumia chakula hiki cha kiroho, nikaanza kukaribia kuwa kama ‘wale ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mbaya.’ (Waebrania 5:14) Dhamiri yangu ilikuwa ikisisimuka, ikaanza kuamka!

“Hili pato la ukweli wa Biblia la ghafula lilifanya geuzo kubwa la hali ya akili yangu. Nilikuwa nimekisoma kitabu kwa saa 24. Usiku wote nilienda kutoka mwisho huu hadi mwisho ule mwingine. Nilikuwa nimeazimia kuwafanya wafungwa wenzangu waone kweli nilizokuwa nikijifunza. Nilifikiri kila mtu angechochewa juu yazo kama vile mimi. Hawakuchochewa. Nilikuwa matata kwa wafungwa wengine mbeleni; sasa nilikuwa chanzo kikubwa hata zaidi cha usumbuo—jambo ambalo hakuna aliyefikiria ingekuwa hivyo! Lakini kadiri Mashahidi walivyokuja kujifunza nami kwenye gereza, nikawa mwenye ustadi zaidi katika kuhubiri.

“Nilifanya mabadiliko mengi, na katika miezi miwili nikawa mdhamini. Hata waliniacha niende nje, jambo ambalo halikuwa la kawaida kwa sababu ya rekodi yangu iliyopita na sababu niliyokuwa hapo. Kanuni nilizokuwa nikijifunza katika Biblia zilikuwa na matokeo yayo. Maji ya kweli kutoka kwa Neno la Mungu yalikuwa yakifanya kazi yake ya kusafisha, kama yalivyofanya katika siku za mitume. Uwezo wayo wa kurekebisha unaonyeshwa kwenye 1 Wakorintho 6:9-11, kama ifuatavyo:

“‘Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi. Na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa.’

“Mwishowe nikaja kuhukumiwa. Walinipa miaka 20 kwa uuaji. Katika 1971, nikapelekwa kwenye gereza lenye ulinzi mkali. Ilikuwa ni hapo ndipo funzo langu na Mashahidi wa Yehova lilipoanzishwa tena. Mwenendo wangu ulikuwa umebadilika kabisa. Upesi katika gereza hili jipya, walinifanya mdhamini na wakaanza kunipa ruhusa za kupumzika. Katika pindi moja, niliuliza Shahidi niliyekuwa nikikaa naye: ‘Ni nini kinachonizuia nisibatizwe?’ Alichunguza kupitia kundi la wenyeji wa hapo na jibu likaja: ‘Hakuna.’ Katika 1973, mapema jioni, nikabatizwa kwenye kidimbwi cha ng’ombe katika shamba lililokuwa karibu. Nilisali nilipokuwa nikiingia kwenye maji, kwa kuwa hivyo ndivyo Yesu alifanya alipokuwa akizamishwa ndani ya Mto Yordani na Yohana Mbatizaji.

“Baada ya hilo, maendeleo yangu ya kiroho yalikuwa ya haraka. Nilijiunga na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi iliyoongozwa katika kundi la hapo—nikihudhuria bila kuwapo, pasipo shaka. Nilipata migawo yangu ya shule na nikaiweka kwenye kaseti, na ikasikilizwa na kundi. Kiongozi wa shule alirudisha shauri la kunifanya nifanye maendeleo. Tulikuwa na mikutano ya kila juma gerezani ambapo wafungwa wengine walikaribishwa kuhudhuria.

“Wakati wote huo nilikuwa nikiongezea maandiko mengi katika maarifa yangu ya Biblia. Yalikuwa kama mawe ya kukanyagia yakiniongoza kutoka kwenye adili iliyotatanika ambayo nilikuwa nikiishi kwa wakati mwingi wa maisha yangu, mpaka nilipothamini badiliko alilozungumzia mtume Paulo kwenye Wakolosai 3:9, 10: “Mmevua kabisa utu wa kale, pamoja na matendo yake; mkivaa utu mpya, unaofanywa upya upate ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba.”

“Katika 1978 kusikilizwa kwa mara ya tatu mbele ya baraza la kutoa ruhusa kulikuwa kunakaribia. Nilikataliwa mara mbili kwa sababu ya uhalifu mbaya sana. Wakati huu baraza lilipokea barua 300 kutoka kwa Mashahidi na wengine wakionyesha mabadiliko niliyofanya.

“Nafasi zangu za kufunguliwa zikionekana kuwa nzuri, nilifikiria juu ya uwezekano wa kuoa. Arlynn, mjane mwenye watoto wawili, alikuwa akiniandikia nilipokuwa gerezani. Alinitembelea akiwa na wavulana wake wawili. Nilimpenda naye alinipenda. Nilifunguliwa Februari 1, 1978. Tukaoana Februari 25, 1978. Sasa, miaka 13 baadaye, bado tuna ndoa yenye furaha. Mmoja wa wavulana wetu ameoa na mwenye bidii akiwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Mvulana yule mwingine anatumikia kwa wakati wote kwenye makao makuu ya ulimwenguni ya Mashahidi wa Yehova huko Brooklyn, New York.

“Sala zangu zimejibiwa. Nawashukuru ndugu na dada ambao wamekuwa wakinisaidia. Furaha yangu yote ni kwa Mungu mwenye furaha, Yehova.—1 Timotheo 1:11.

“Hata hivyo, najuta sana kwa dhambi zangu za zamani. Nauchukia mwenendo wangu wa zamani. Nimesali mara nyingi kwa Yehova anisamehe, na nahisi kwamba amenisamehe. Natumaini pia kwamba watu niliokosea zamani wanaweza kunisamehe. Na natumaini kwamba mtu niliyeuwa atapata nafasi ya kufufuliwa na kuishi milele katika Paradiso ya Mungu duniani. Hilo lingefanya furaha yangu itimilike!”

Yale ambayo vifungo vya gereza na vifungo vya upweke vilishindwa kufanya, kweli ya Biblia ilifanya. Ilimfanya Ron Pryor kuvua utu wake wa zamani wa uhalifu na kujivika utu mpya wa Kikristo. Kwa nini? Kwa sababu “Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu,” kutia ndani nguvu ya kurekebisha tabia.—Waebrania 4:12.

[Blabu katika ukurasa wa 21]

Nilikuwa nimeiba kilori cha hakimu Jenkin!

[Blabu katika ukurasa wa 22]

Kulikuwa na Biblia katika kifungo cha upweke. Nikaanza kiusoma

[Blabu katika ukurasa wa 22]

Walinihukumu miaka 20 kwa uuaji

[Picha katika ukurasa wa 23]

Ron Pryor na mke wake, Arlynn, leo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki