Njoo, Usikilize Hotuba ya Watu Wote Bila Malipo:
“Fuata Nuru ya Ulimwengu”
Wanadamu wanahitaji nuru ya kuangaza njia yao kama vile ambavyo gari huhitaji taa zayo za mbele katika barabara yenye kujipinda ya milimani wakati wa usiku. Nuru ya kiroho yaweza kulinganishwa na taa za mbele za gari zilizo nzuri sana, zinazoangaza barabara ili watu waweze kuona vizuri wanakoenda. Ni nini kilicho chanzo cha nuru hiyo ya kiroho? Na ni nani anayeimulika leo?
Hayo ni maswali yatakayojibiwa katika hotuba ya watu wote itakayotolewa kwenye mamia ya “Wachukuaji Nuru” Mikusanyiko ya Wilaya ya Mashahidi wa Yehova itakayofanywa kuanzia Oktoba 30, 1992 hadi Januari 3, 1993. Wewe unaalikwa kwa uchangamfu uhudhurie.
Programu ya mkusanyiko itakuwa pia na mazungumzo yenye msaada kuhusu mambo halisi ya maisha na pia drama ya Biblia yenye mavazi kamili. Nenda kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova katika eneo lako ili ujulishwe ni wapi na lini mkusanyiko utafanywa karibu na nyumbani kwako, au uandikie watangazaji wa gazeti hili.