Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g93 9/8 kur. 16-19
  • Shule Mpya Katika Afrika

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Shule Mpya Katika Afrika
  • Amkeni!—1993
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kusudi la Shule Hiyo
  • Mazoezi ya Pekee
  • Maelezo Kutoka Shambani
  • Ni Nani Anayestahili?
  • Shule ya Mazoezi ya Kihuduma—Mlango Mkubwa Unaoongoza Kwenye Utendaji
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Shule Ambayo Wahitimu Wake Wanawafaidi Watu Ulimwenguni Pote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Kuwazoeza Wahudumu wa Ufalme
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Hatua Kubwa Nyingine Katika Elimu ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1993
g93 9/8 kur. 16-19

Shule Mpya Katika Afrika

Na mleta habari za Amkeni! katika Nigeria

KATIKA Julai 1990 kulisomwa barua ambayo ilisababisha msisimko mkubwa miongoni mwa wafanyakazi wa kujitolea zaidi ya 400, Mashahidi wa Yehova, wanaoishi na kufanya kazi katika ofisi ya tawi ya Watch Tower Society katika Igieduma, Nigeria. Ile Shule ya Mazoezi ya Kihuduma, iliyoanzishwa katika United States katika 1987, ilitazamiwa kuanzishwa Afrika, na madarasa ya kwanza yangefanyiwa katika Igieduma!

Miezi iliyofuata, familia ya Betheli ilifanya matayarisho ya darasa la kwanza.a Wanafunzi na wafunzi wangehitaji makao. Vyumba vya wageni vilivyoko havingetosha; vyumba 15 zaidi vilihitajiwa. Kwa hiyo Mashahidi walianza kugeuza vyumba vya kuhifadhia vitu kuwa vyumba vyenye kupendeza vya makao. Hilo lilitia ndani kuweka vigae sakafuni, kupaka rangi kuta, na kuweka mapazia. Duka la useremala lilitengeneza na kuweka vitanda, makabati, na madawati. Hatimaye, viti, taa za kusomea, na rafu za vitabu zililetwa. Rafu hizo zilijazwa vichapo vya kitheokrasi.

Kwa kuongezea, chumba cha kubarizi cha familia kiligeuzwa kuwa darasa na maktaba kwa wanafunzi. Kimojapo chumba cha wagonjwa kilikuwa ofisi ya muda ya wafunzi na kiliwekwa madawati, meza, na vifaa vingine vya ofisi. Huko nyuma, habari za shule iliyopaswa ianzishwe zilipojulishwa kote nchini kwenye mikusanyiko na makusanyiko ya Mashahidi wa Yehova, mamia ya maombi yalianza kufika kutoka kwa waliotazamiwa kuwa wanafunzi.

Kufikia juma la kwanza la Februari 1992, kila kitu kilikuwa tayari. Wafunzi wawili, Michael Purbrick na Peter Nicholls, kutoka Uingereza walifika ili kufundisha darasa la kwanza. Pamoja na wanafunzi 22, walimu watatu waliotarajiwa kufundisha, Isaiah Mnwe, Isaiah Olabode, na Pius Oparaocha pia walikuja. Hao walikuwa Mashahidi Wanigeria ambao walipaswa wazoezwe kufunza madarasa ya baadaye.

Kusudi la Shule Hiyo

Katika Betheli yote, kulijawa na hisia za matazamio na msisimko. Kwa nini? Kwa sababu ya athari inayofaa ambayo shule hiyo ingeleta kwa kazi ya kufanya wanafunzi katika Nigeria. Zamani sana Yehova alitabiri kwamba angetoa ‘zawadi katika namna ya watu.’ (Zaburi 68:18, NW) Alifanya hivyo katika nyakati za mitume, hata kama vile mtume Paulo alivyoandika kwenye Waefeso 4:8-11. Leo, Yehova pia anatoa zawadi katika wanaume. Shule ya Mazoezi ya Kihuduma ni uandalizi wenye upendo wa kuwawezesha baadhi ya wanaume hao wachukue madaraka zaidi ya tengenezo.

Katika nchi hiyo, kuna Mashahidi zaidi ya 160,000 katika makutaniko zaidi ya 3,000. Baadhi ya makutaniko hayo yana mzee mmoja au wawili tu na watumishi wa huduma wachache. Makutaniko mengine yana maeneo makubwa sana ambako habari njema hazijahubiriwa sana. Hivyo, kuna uhitaji mkubwa kwa wanaume wenye kustahili si kuongoza katika kazi ya evanjeli tu bali pia kulichunga kundi na kufundisha makutaniko.

Kusudi la Shule ya Mazoezi ya Kihuduma ni kuzoeza akina ndugu watunze madaraka hayo. Baada ya kuhitimu, baadhi ya wanafunzi hao huchukua kazi ya upainia wa pekee au kazi ya kusafiri, maeneo ya utumishi ambayo yana uhitaji mkubwa katika Nigeria. Wengine hurudi kwenye makutaniko yao ili kutoa msaada na kitia-moyo kwa akina ndugu wenyeji. Wanaume hao waliostahili vizuri ni baraka kama nini kwa makutaniko wanayotumikia!

Mazoezi ya Pekee

Ingawa Shule ya Mazoezi ya Kihuduma ni upanuzi wa Watch Tower Bible School of Gilead, ambayo huzoeza wamishonari kwa ajili ya utumishi wa kigeni, utaratibu wayo ni wa pekee. Wakati wa shule ya majuma manane, wanafunzi hufanya funzo la Biblia lenye kina kirefu sana. Wanachunguza kwa uangalifu kiwango kikubwa cha mafundisho ya Biblia, kutia ndani shauri la madaraka ya uchungaji na miongozo ya kushughulikia matatizo katika maisha ya Kikristo. Pia wanajifunza yale ambayo Maandiko yanasema juu ya usimamizi, mambo ya kihukumu, na ya kitengenezo. Wanapokea mazoezi ya kipekee katika kusema hadharani na wanapokea uangalifu wa kibinafsi kutoka kwa wafunzi wenye kujali, ambao huwasaidia katika maendeleo yao ya kiroho.

Kwa ujumla, mwanafunzi wa kawaida hupokea migawo 45 ya darasa, na kunufaika kutokana na saa 256 za maagizo ya darasani. Kwa kuongezea, yeye hutumia saa 140 akifanya masomo ya kufanyia nyumbani na saa 14 akifanya mitihani.

Ijapokuwa kitabu kikuu cha mafundisho ni Biblia, wanafunzi huombwa walete nakala zao za kibinafsi za vitabu vingine 16 shuleni, vya msaada wa Biblia vilivyochapishwa na Watch Tower Society. Wakati wa shule, wanafunzi pia hufanya utafiti wa kina kirefu katika vichapo vinginevyo vilivyoko kwenye maktaba yenye vitabu vingi ya Betheli. Kwa wazi, wanahitaji kuwa wasomaji wazuri.

Zaidi ya kazi ya shule, wanafunzi hufanya kazi dakika 45 kila siku katika mojapo idara nane za Betheli: usafi, chumba cha kulia chakula, utunzaji wa bustani, utunzaji wa nyu-mba, jikoni, usafishaji nguo, upakizi na usafirishaji. Wao hubadilishana kazi ili kwamba kufikia mwisho wa majuma manane ya masomo yao, kila mmoja wao awe amepata maarifa katika idara hizo zote. Mwanafunzi mmoja alisema kwa mshangao: “Kufanya kwangu kazi katika idara mbalimbali kulinifanya nielewe kwamba Yehova ndiye msimamizi wa kazi hiyo.” Mwingine alisema: “Waangalizi wako tayari kurekebisha na kufundisha kwa upendo.” Na mwingine alieleza: “Kazi ya Betheli ni jambo ambalo kila mtu anapaswa kujaribu na kuona kwamba ni jema.”

Akina ndugu waliyaitikiaje mazoezi waliyopokea? Mmoja alisema: “[Ilikuwa] shule bora kuliko shule zote.” Mwingine alisema kwa idili: “Ni mpango bora zaidi kama nini!” Mioyo yao ikiwa imejaa shangwe na uthamini, wanafunzi wa darasa la kwanza waliandika katika barua moja: “Azimio letu ni . . . kuweka maisha zetu katika ujumbe wa habari njema.”

Maelezo Kutoka Shambani

Wakati wa sehemu ya kwanza ya 1992 na ya 1993, madarasa ya kwanza manne ya Shule ya Mazoezi ya Kihuduma katika Nigeria yaliongozwa. Katika barua ya uthamini iliyoandikiwa Baraza Linaloongoza, wanafunzi wa darasa la pili waliandika: “Kwa kweli, hatujawahi kuhudhuria shule nzuri zaidi ya hii. Mtaala huo wafaa zaidi kuliko programu ya chuo kikuu. Hivyo basi twaona ikiwa rahisi kukubaliana na William Phelps kwamba ‘ujuzi wa Biblia bila masomo ya chuo ni yenye thamani zaidi kuliko masomo ya chuo bila Biblia.’ Katika yote hayo, kupendezwa kwenu nasi kikweli ni dhahiri. Kwa hiyo tumeazimia kufanya kazi ya wakati wote kuwa kazi-maisha yetu.”

Wahitimu wamepokewaje katika migawo yao mipya? Mwangalizi asafirie aliandika barua kuhusu wahitimu wawili wa darasa la kwanza wanaotumikia wakiwa mapainia wa pekee hivi: “Mikutano sasa inavutia, inatia moyo, ni yenye kufurahisha, na yenye umaana. Utendaji katika utumishi wa shambani unaongezeka . . . Kutaniko linafurikwa na shangwe . . . Nilipohoji ndugu kadhaa juu ya mapainia hao wa pekee, mwangalizi msimamizi alijibu kwa machozi ya shangwe, akisema: ‘Twamshukuru Yehova na tengenezo lake kwa kupeleka wasaidizi wenye utimamu na wenye matokeo kwenye kutaniko letu.’”

Ni Nani Anayestahili?

Kuhudhuria Shule ya Mazoezi ya Kihuduma katika nchi yoyote ile ni pendeleo ajabu la utumishi, baraka ya kustaajabisha kutoka kwa Yehova. Bila shaka, mazoezi hayo husaidia wanafunzi waongeze hali yao wakiwa watu wa kiroho na kuwasaidia watumiwe kikamili zaidi na Yehova.

Kwa kueleweka, matakwa ni ya hali ya juu. Ili kustahili, wenye kujaza maombi lazima wawe wametumikia wakiwa wazee au watumishi wa huduma katika kutaniko la Kikristo kwa angalau miaka miwili. Nafasi ya kwanza hupewa kwa wale walio kwenye utumishi wa painia wa kawaida. Wote wanapaswa kuwa waseja na wenye umri wa kati ya miaka 23 na 50. Hawapaswi kuwa waliokaripiwa au kutengwa wakati wa kipindi cha miaka mitano iliyopita. Wenye kujaza maombi wanapaswa kuweza kusoma, kuandika, na kuongea Kiingereza vizuri, na wanahitaji kuwa na afya nzuri, wasiohitaji utunzi au chakula cha pekee.

Jambo lenye kutokeza ni kwamba, wale wanaojitolea wapaswa kuwa tayari, wenye nia, na wenye uwezo wa kutumikia popote watakapohitajiwa. Hili lahitaji tamaa si ya kufanya tu mapenzi ya Mungu bali pia roho ya Isaya, ambaye alijitolea kwa hiari kufanya kazi ya pekee, akisema: “Mimi hapa, nitume mimi.”—Isaya 6:8.

Je! wewe una roho kama hiyo? Je! umo katika hali ya kufikia pendeleo hili la utumishi? Wale ambao wamefanya hivyo hawana masikitiko. Mhitimu mmoja wa shule hiyo ambaye sasa anatumikia akiwa mwangalizi wa mzunguko aliandika hivi: “Kwangu mimi, Shule ya Mazoezi ya Kihuduma ilikuwa zawadi isiyokuwa na jambo la kuilinganisha. Imethibitika kuwa kilele cha maisha yangu ya kiroho. Kama ningekuwa na fursa ya kuishi maisha yangu tena, nisingalichagua kamwe njia tofauti ya maisha.”

[Maelezo ya Chini]

a “Betheli,” kutokana na Kiebrania humaanisha “nyumba ya Mungu,” ni jina linalopewa kwa kila kao la tawi la Watch Tower Society.

[Picha katika ukurasa wa 16, 17]

Wafunzi Isaiah Mnwe na Pius Oparaocha

Mafunzo ya darasani

Kikundi cha mazungumzo darasani

Kufanya utafiti katika maktaba

[Picha katika ukurasa wa 18]

Kufanya kazi katika Ufuaji Nguo na Idara ya Upakizi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki