Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g93 11/22 kur. 8-10
  • “Sisi Hatunyimwi!”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Sisi Hatunyimwi!”
  • Amkeni!—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Amua Kumwabudu Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—1994
  • “Kwa Nini Sisherehekei Krismasi”
    Amkeni!—1994
  • Chukua Msimamo Upande wa Ibada ya Kweli
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1993
g93 11/22 kur. 8-10

“Sisi Hatunyimwi!”

Maoni yametolewa na walimu na wengineo kwamba watoto wa Mashahidi wa Yehova hunyimwa furaha kwa kutoruhusiwa kujiunga katika sherehe za shule za Krismasi, Ista, na Halowini. Yafuatayo ni maoni machache ya watoto ambao ni Mashahidi wa Yehova, wakieleza katika barua sababu inayowafanya wao wenyewe wakatae kuwa na sehemu yoyote katika kusherehekea sikukuu hizo.

“INGAWA niliwaeleza wanashule wenzangu sababu iliyofanya nisisherehekee mambo hayo, bado wao walihisi nilikuwa nikinyimwa furaha. Lakini sivyo! Waona, sikuzote iliwabidi wangoje hadi Krismasi au sikukuu fulani nyingineyo ili kupata zawadi ilihali mimi nilikuwa nikipewa zawadi na kwenda kwenye karamu katika mwaka wote. Najua napendwa si na familia yangu tu bali na kutaniko na Yehova pia, na jambo hilo ni la pekee kwangu zaidi ya sikukuu yoyote.”—Becky, umri wa miaka 13.

“Najua kwamba sikukuu hizo zote zina mwanzo mbaya. Yesu hakuzaliwa siku ya Krismasi. Familia yetu hailazimiki kufanya chochote ili kulipia sikukuu hizo. Sikuzote familia yetu ipo tayari kunisaidia wakati wowote ninapoihitaji. Hiyo yapita zawadi nyingine yoyote ambayo wao waweza kunipa.”—Josh, umri wa miaka 15.

“Krismasi. Mimi sinyimwi furaha kwa sababu hiyo [sikukuu] kwa vyovyote si ya Kikristo. Ni afadhali nijue wazazi wangu walinipa zawadi kuliko Baba Krismasi fulani wa kifumbo. Ista. Kwa habari ya Ista ni vigumu kwelikweli kwa kuwa watu watasema ni kwa ajili ya ‘Yesu na ufufuo’ au ni ‘kwenda kutafuta mayai,’ tu. Lakini mayai na Yesu yana uhusiano gani hasa? Hata jina Ista latokana na kijimungu kike cha kale. Halowini. Wazo la msingi la Halowini halinivutii hata kidogo. Mizuka na wachawi, PUUU!”—Katie, umri wa miaka 10.

“Nikiwa kijana sijapata kuhisi mtamauko kwa sababu ya kutosherehekea sikukuu za kilimwengu. Sijaambiwa na wazazi wangu kwamba ‘huwezi kufanya hili au lile kwa sababu wewe ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova,’ lakini nimefahamishwa Biblia na maoni ya Yehova juu ya sikukuu hizo. Kwa habari ya zawadi hizo, nyumbani mwetu, kupeana zawadi ni jambo la mwaka wote.”—Ryan, umri wa miaka 17.

“Kila sikukuu yasherehekea jambo lisilofaa na yakazia mambo yasiyofaa. Watoto walio wengi nijuao husherehekea sikukuu kwa ajili ya peremende na zawadi. Jambo nililo nalo, ambalo ni bora kuliko sikukuu ni tengenezo la Mashahidi wa Yehova lililo zuri ajabu. Badala ya kuendelea kwa siku moja, kama vile sikukuu, Neno la Yehova Mungu ni ujumbe wenye furaha udumuo milele.”—Brooke, umri wa miaka 14.

“Sababu zinazonifanya nisitamani sikukuu: 1. Biblia husema hazifai. 2. Mimi sijali juu yazo. 3. Mama na baba hunipa zawadi.”—Brandi, umri wa miaka 6.

“Mimi sihisi nimenyimwa furaha. Mimi sijali juu ya sikukuu. Mimi hupata zawadi, na sisi hucheza michezo na kuwa na karamu. Mimi hupata vitu vingi bila kulazimika kusherehekea sikukuu. Hata nifanye nini, nataka niendelee kuwa Shahidi na hakuna jambo linaloweza kunizuia.”—Brianne, umri wa miaka 9.

“Naenda darasa la tano na sisikitiki kukubali kwamba mimi ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Wakati mmoja mvulana mmoja aliniambia kwamba ni lazima niwe nahisi vibaya kwa sababu sikupata zawadi zozote wakati wa Krismasi, lakini nilisema mimi hupata zawadi mwaka wote. Halafu akasema kwamba nilikuwa na bahati. Nafikiri hakupaswi kuwa na Shahidi wa Yehova anayehisi sikitiko kwa sababu ya kuwa Shahidi wa Yehova.”—Jeff, umri wa miaka 10.

“Dadangu nami tulifanya kusherehekea ukumbusho wa ndoa ya wazazi wetu kila mwaka kuwa sikukuu yetu wenyewe ya familia. Nilipata shangwe nyingi zaidi kwa sababu ya kupanga kuwa na zawadi na kadi na vitu na kusaidia wazazi wangu wapange mambo ili kushtuana kuliko vile nilivyopata kupokea zawadi kutoka kwa yeyote. Kutoa ni bora kuliko kupokea.”—Rachel, umri wa miaka 16.

“Nilipokuwa mchanga zaidi, sikukuu fulani zilikuwa ngumu kwangu. Lakini baadaye niling’amua kwamba sikukuu hizo zaweza kusababisha pupa, mabishano, na huzuni. Kunapokuwa nyakati zilizowekwa za kutoa, wewe hupati kushtuliwa na zawadi. Ni afadhali nipate zawadi za pekee wakati wowote mwakani. Kusherehekea au kutosherehekea ni sehemu ndogo tu ya uamuzi mkubwa zaidi: kama utajiweka wakfu kumtumikia Yehova au la. Nifikiriapo jambo hilo kwa njia hiyo, chaguo lifaalo huwa wazi.”—Ben, umri wa miaka 13.

“Kuna nyakati nilipokuwa mdogo ambapo nilihisi kwamba nilikuwa nikinyimwa furaha, lakini baadaye nilicheka nilipofikiria jinsi mayai, Yesu, na sungura wa Ista walivyokuja kuwa pamoja wote. Nilipokuwa na umri mkubwa zaidi na wazazi wangu wakanieleza jinsi vifananisho hivyo vyote vilivyoanza, niliiona kuwa yenye kuchukiza. Niliudhika kufikiri jinsi Yehova na Yesu wanavyohisi kwa kuhusianishwa na mawazo hayo ya kipagani.”—Alexa, umri wa miaka 18.

“Wakati wa Krismasi, kuwa shuleni kwaweza kukushusha moyo sana na kwaweza kukufanya uhisi umeachwa nje. Halafu nikang’amua kwamba kusherehekea Krismasi hakuwezi kusuluhisha matatizo yako, hakuwezi kuleta familia yako pamoja, na hakuwezi kukufanya uwe mwenye furaha. Ni kuishi tu kwa viwango vya Biblia kwamba hilo lawezekana.”—Joe, umri wa miaka 15.

“Badala ya kuwa na Krismasi au sikukuu nyingineyo, tuna Siku Kubwa ya Vitu vya Kuchezea. Twapata zawadi ya pesa za kutumia katika chochote tupendacho. Mwaka mmoja nilitoa hotuba kwa darasa langu juu ya dini yangu. Badala ya kufuata kijia cha ulimwengu, mimi nina kijia changu mwenyewe ili kuhudhuria mikutano, kwenda katika utumishi wa shambani, na kufanya sala kuwa sehemu ya maisha yangu. Nitabatizwa kwenye kusanyiko linalokuja.”—George, umri wa miaka 11.

“Mimi hupenda kupata zawadi, nami huzipokea muda wote wa mwaka. Kwa habari ya karamu, mimi sihisi kukosa mambo mengi. Namfurahisha Yehova nichukuapo msimamo kwa ajili ya kweli. Yachekesha kuona baadhi ya wanadarasa wenzangu ambao si Wakristo, bali ni Wahindu, Wayahudi, na kadhalika, wakisherehekea Krismasi na kupata zawadi lakini hawajui maana ya sikukuu hiyo.”—Julia, umri wa miaka 12.

“Nilipokosa sikukuu shuleni, sikujuta. Watoto hufanya mambo mengi ya kiajabu-ajabu, kama vile kuvaa kwa ajili ya Halowini. Mimi siitamani hata kidogo. Mimi huwaambia jinsi wazazi wangu huninunulia vitu katika mwaka wote. Wao huniambia juu ya kanisa lao na jinsi liwatoavyo miayo, nami huwaambia juu ya mikutano tufanyayo kwenye uwanja, nao huona wivu wakati mwingine. Lakini mimi sioni wivu juu yao. Kwa kumalizia, nasema fanya marafiki na wale tu wanaostahi itikadi zako na usiache kamwe mwanafunzi au mwalimu akulazimishe kufanya lolote lililo kinyume cha mapenzi ya Yehova.”—Justin, umri wa miaka 12.

“Je! nahisi nimenyimwa? La, kwa sababu sisi huwa na karamu nyinginezo, na wakati watu washerehekeapo Krismasi, watoto hufikiria hasa Baba Krismasi, au wakati wa Ista wao hufikiria sungura wa Ista, lakini najua watokana na dini za kipagani. Napenda utumishi wa shambani kwa sababu huo hunisaidia nikazie fikira kwenye kweli.”—Sharon, umri wa miaka 8.

“Naweza kusema kwa haki kwamba sijapata kuhisi kutoridhika kwa sababu ya kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Familia yetu nami huwa na mambo mengi yenye kufurahisha. Kunapokuwa karamu shuleni mama yangu hunichukua kwenda nje kwa chakula cha mchana. Wazazi wangu huniletea vitu vizuri shuleni bila sababu yoyote ya pekee na watoto wote wajua kwamba tuna furaha. Niko karibu sana na wazazi wangu na watoto wanaponiuliza mbona sisherehekei sikukuu mimi huwaambia kwamba husherehekea kila siku. Shahidi yeyote angewezaje kuhisi ameachwa nje?”—Megan, umri wa miaka 13.

“Halowini. Watoto wakivaa kama mashetani, waigizaji wa vitabu vya ucheshi—kwa nini? Watoto huzurura mitaani wakienda nyumba kwa nyumba kupata mifuko iliyojaa peremende. Au kutupa mayai kwenye nyumba, kutanda karatasi za choo juu ya miti, na jambo lililo baya zaidi ni kwamba wazazi walio wengi huunga mkono jambo hilo.”—Zachary, umri wa miaka 10.

“Hainibidi kungoja siku ya pekee ili kupata zawadi. Wakati wote mama na baba hunipa vitu vingi vya kuchezea. Halowini ni ibada ya mizuka. Haifai. Mungu pekee tupaswaye kuabudu ni Yehova.”—Nicholas, umri wa miaka 6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki