Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g94 3/8 kur. 10-11
  • Ule Muhula Mpya wa Halisi Utakujaje?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ule Muhula Mpya wa Halisi Utakujaje?
  • Amkeni!—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Ni Suluhisho Halisi?
  • Biblia—Kitabu cha Majibu
  • Je! Wewe Utakuwako?
  • Ile Harakati ya Muhula Mpya Ni Nini?
    Amkeni!—1994
  • Harakati ya Muhula Mpya Ipendwayo na Wengi
    Amkeni!—1994
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—1994
  • Je! Mungu Anajali?
    Je! Mungu Anajali?
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1994
g94 3/8 kur. 10-11

Ule Muhula Mpya wa Halisi Utakujaje?

MTUNGAJI wa kike wa vitabu vya Muhula Mpya Shirley MacLaine alitoa maoni ya kawaida sana alipoandika hivi: “Mimi nilijikuta nikifikiria sana kasoro iliyokuwa ikitendeka ulimwenguni. Huwezi kuepuka kufikiri uonapo kwa kweli ule ufukara, kule kufa njaa, ile chuki iliyopo. Mimi nilianza kusafiri nilipokuwa na umri wa miaka kumi na tisa, na sasa, nikiwa na miaka 45 hivi, ningeweza kusema kwa uhakika kwamba mambo yalikuwa yamezidi kuzorota.”[1]

Vivyo hivyo, watu kila mahali wamechoshwa na unafiki na uwongo wa kidini. Wametatanishwa na kutojali na kutofaa kwa serikali. Wanashtushwa na ile mitazamo wanayohisi kuwa ni kutojali mambo na makosa ya kizembe yanayofanywa na uwanja wa tiba. Na wengi hudhulumiwa na upendeleo wa rangi ya ngozi au wa jinsia fulani za watu na maoni ya ushupavu.

Je! Ni Suluhisho Halisi?

Hakuna shaka, sisi twahitaji sana ulimwengu mpya. Lakini je! matumaini ya Muhula Mpya ni halisi? Au harakati hiyo yauonyesha wakati ujao kwa njia iliyo kama zile sinema za sayansi bandia tu ambazo huigizwa Hollywood? Je! yaonekana kuwa busara kutia imani katika unabii mbalimbali ambao msingi wao ni mapokeo yaliyokwisha sahauliwa zamani, ngano za kale, na mambo ya kudhania tu?

Kwa wazi, mengi ya mawazo yaliyochaguliwa na harakati ya Muhula Mpya huenda yakaendeleza hali njema ya kiakili na kimwili kwa njia ndogo. Lishe njema, mazoezi, burudiko, na kuhangaikia mazingira, yote hayo ni mambo yafaayo maishani. Labda wanatiba wangepata mafanikio mazuri zaidi kama wangeangalia zaidi mahitaji ya kihisiamoyo ya wagonjwa wanapotibu maradhi yao ya kimwili. Lakini muda si muda kila mtu huwa mgonjwa, na hata walio na afya zaidi hufa hatimaye. Hatuwezi kufurahia maisha kikamili na huku tunatazamia kuwa wagonjwa na kufa. Je! watetezi wa Muhula Mpya hutoa suluhisho lifaalo kwa matatizo hayo?

Watu zaidi na zaidi ni wenye huzuni na wameshuka moyo, na ile harakati ya Muhula Mpya haiwezi kusaidia sana. Gazeti International Herald Tribune la London lilisema: “Ikiwa karne ya 20 ilileta Muhula wa Wasiwasi, basi kuondoka kwayo kunashuhudia pambazuko la Muhula wa Kushuka Moyo.” Gazeti hilo liliongezea kwamba “uchunguzi wa kwanza wa kimataifa juu ya mshuko mkubwa wa moyo wafunua kuzidi kuongezeka kwa ugonjwa huo ulimwenguni pote.”[2]

Harakati ya Muhula Mpya, ikiwa na dalili zayo za uanadini bandia, haijazii utupu wa kiroho ulio katika jamii ya ki-siku-hizi. Msaada wowote ule wa kiroho iutoao ni wa muda tu. Kwa kukiri wazi, dini ya tangu jadi, hasa Jumuiya ya Wakristo, haijapunguza kufa njaa kiroho kwa ujumla. Gazeti moja lilishutumu wazi “kushindwa kwa Kanisa kujitahidi kuwafikia wale wanaohisi wakiwa peke yao, wasiotendewa kwa huruma, wasiopendwa.” Gazeti hilo lilieleza dini ya ki-siku-hizi kuwa ya ulegevu, “yenye kuondolea mtu hisia yoyote ya uhusiano wa moja kwa moja pamoja na Mungu.”[3]

Biblia—Kitabu cha Majibu

Jumuiya ya Wakristo imetohoa kweli za Biblia na kupunguza uzito wazo. Vilevile, mafundisho mengi ya Muhula Mpya ni kinyume cha mafundisho ya Biblia. Kwa kielelezo, chukua lile wazo la Muhula Mpya kwamba wanadamu wanaweza kuleta suluhisho kwa matatizo ya dunia. Biblia hutaarifu wazi kwenye Yeremia 10:23: “Njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu.” Andiko jingine husema: “Wokovu una BWANA [Yehova, NW].”—Zaburi 3:8.

Biblia haifundishi kwamba wanadamu wana nafsi isiyokufa ambayo huishi ikiwa kitu chenye kujitegemea, kilicho kando na mwili. Kulingana na Maandiko, nafsi hufa, na kifo huwa ndio mwisho wa mawazo na utendaji wote. (Hesabu 23:10; 35:11; Mhubiri 9:5, 10) Hiyo yaondolea mbali lile wazo la Muhula Mpya la mtu kuzaliwa upya akiwa na umbo tofauti.

Zaidi ya hilo, haiwezekani kuwasiliana na wafu. Kulingana na Biblia, wowote usemwao kuwa ni uwasiliano pamoja na wafu kwa kweli ni uwasiliano pamoja na mashetani—roho walio adui za Mungu na wanadamu. Kwa hiyo, Sheria ya Mungu ililifanya zoea la uwasiliani-roho, kutia na kila namna ya uaguzi, unajimu, na upitishaji wa habari zitokazo kwa roho waovu, kuwa adhabu ya kifo.—Mambo ya Walawi 19:31; 20:6, 27; Kumbukumbu la Torati 18:10-12.

Biblia ndiyo chanzo cha uponyaji wa kweli wa kiroho. Ina fungu la mafundisho ambayo husaidia Wakristo kujifahamu jinsi walivyo kwa ndani na kugeuza utu wao. (Warumi 12:2; 2 Wakorintho 13:5; Waefeso 4:21-24) Hiyo hufundisha nidhamu ya kibinafsi, utimamu wa akili, staha kwa mtu binafsi na wengine.

Biblia hutupa ufahamiano na nguvu iliyo ya juu zaidi katika ulimwengu wote mzima, Muumba, ambaye, kwa kweli, “hawi mbali na kila mmoja wetu.” (Matendo 17:24-28) Na Biblia huandaa majibu ya kuridhisha kwa maswali kama vile: Kwa nini tupo hapa? Kwa nini twazeeka na kufa? Hutukia nini baada ya kifo? Kwa nini Mungu ameruhusu mateso mengi hivyo? Ni nani wale watu wenye nguvu walio katika makao yasiyoonekana? Je! wao ndio huleta mengi ya yale yaitwayo matukio mabaya yasiyo ya kawaida?

Kuhusu wakati ujao, Biblia huahidi afya kamilifu na uhai wa milele na ulimwengu mpya wa amani na upatano, wenye mazingira safi, papa hapa duniani. (Isaya 33:24; 2 Petro 3:13) Katika ulimwengu mpya huo, bila shaka wanadamu wataongeza ujuzi wao na, chini ya mwelekezo wa Mungu, wafumbue mafumbo mengi juu ya mwili wa kibinadamu, sayari yetu, na sehemu ile nyingine yote ya ulimwengu wote mzima. Yote hayo yatatimizwa na nguvu ya Yehova, Mungu apendaye wanadamu.

Je! Wewe Utakuwako?

Hata hivyo, Biblia hufundisha pia kwamba mibaraka hiyo yapatikana kwa wale tu waishio kupatana na sheria za Mungu. Sheria hizo si za kuonea. Lakini ni lazima zitiiwe. (Mithali 4:18, 19; 1 Yohana 5:3) Haiwezekani kuunga mkono wazo lisilo la Kimaandiko la Muhula Mpya na wakati uo huo kuiamini Biblia.—1 Wakorintho 3:18-20; 10:18-22; Yakobo 4:4.

Kwa hiyo, Wakristo wa kweli huepuka kufungamana na ile fikira isiyo ya Kimaandiko ya harakati ya Muhula Mpya. Utimamu wa kuamua mambo na kiasi vyahitajiwa. Yapasa iangaliwe kwamba kile kibandiko “Muhula Mpya” kimekuja kutumiwa mahali pengi kutaja mambo ambayo hayakuanza na harakati ya Muhula Mpya na ambayo huenda yasiwe ni yasiyo ya Kimaandiko. Iko hivyo hasa katika nyanja za afya, lishe, sanaa, na muziki. Kwa hiyo ni lazima Wakristo watumie utambuzi na usawaziko wa akili huku wakihakikisha kujitenga na chochote ambacho hukatazwa katika Biblia. Kwa kufaa, Mithali 14:15 hushauri hivi kwa hekima: “Mjinga huamini kila neno; bali mwenye busara huangalia sana aendavyo.”

Ndiyo, Biblia ndiyo ufunguo wa kuangaziwa nuru ya kweli. Upuuzaji wa Maandiko ambao Wana-Muhula-Mpya huwa nao kwa ujumla waweza kuleta giza zaidi tu ulimwenguni. Lakini Biblia hutoa nuru ya kiroho na tumaini la ulimwengu mpya kama ilivyoahidiwa na Mungu: “Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita. Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.”—Ufunuo 21:3-5.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki