Wakati Wako Ujao—Waweza Kuwaje?
UCHUNGUZI wa jenomu wa binadamu tayari wafunua mengi kuhusu maradhi ambayo huenda hatimaye yakampata mtu. Lakini vipi kuhusu uwezekano wa kutokeza madawa na matibabu na hata uzuiaji wa magonjwa kama hayo?
Kadiri watafiti wanavyojifunza zaidi kuhusu jenomu za mimea, wanyama, na wanadamu, ndivyo kunavyokuwa na uwezekano mkubwa zaidi wa kukuza madawa na tiba ili kutibu maradhi, kwa uchanya lasema The Times la London. Hata hivyo, kama vile gazeti la Industry Week laripoti, wanasayansi watoa tahadhari fulani kwa sababu taratibu hii “ingeweza kukawia kabla ya uchunguzi kwa miaka 20 hadi 50.” Hali hii, kulingana na mwanabiokemia profesa Charles Cantor, humwacha mtu “kwa wazi . . . bila tumaini.” Lakini hilo halipasi kuwa hivyo.
Kwa wazi Biblia yaahidi mwisho wa maradhi yote. “[Mungu] atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena,” Ufunuo 21:4 lataarifu. Je, wanajeni watafanya hili liwe kweli kwa kile gazeti la The Christian Century huita “uumbaji mpya wa jeni”? Utimizo wa ahadi za Biblia hautegemei kukamilishwa kwa Mradi wa Jenomu ya Binadamu, yoyote ya “uumbaji mpya wa jeni,” ama, kwa kweli, uboreshaji wa polepole wa mazingira yetu. Badala yake, uhakika wazo hutegemea kikamili kani tendaji ya Mungu, roho yake takatifu.
Kukabiliana na Urithi na Mazingira
Karibu miaka elfu tatu iliyopita, mfalme fulani Mwisraeli alisema hivi: ‘Nimefanywa kwa jinsi ya ajabu ya kutisha.’ Ingawa Daudi hakujua lolote kuhusu Mradi wa Jenomu ya Binadamu wa leo, aliimba kwa sifa ya Mungu hivi: “Macho yako yaliniona kabla sijakamilika, chuoni mwako ziliandikwa zote pia.”—Zaburi 139:14, 16.
Mfalme huyu wa kale alijuaje kwamba ukuzi wake akiwa kijusu ndani ya mimba ya mama yake ulifuata maagizo “yaliyoandikwa”? Daudi mwenyewe alikubali hivi: “Roho ya BWANA ilinena ndani yangu, na neno lake likawa ulimini mwangu.” (2 Samweli 23:2) Naam, kani tendaji ya Muumba, roho takatifu, iliongoza uandikaji wa Daudi.
Je, hapa si kunalo funzo ambalo watu wengi leo hulipuuza au, angalau, huchelewa kulifikiria? Ingawa urithi na mazingira kwa kiasi fulani hutufanyiza tulivyo, roho takatifu ya Mungu yaweza kutuathiri kwa nguvu sana, hata kushinda vutano zile nyingine.
Ebu fikiria kisa cha Ian. “Nilikuwa kivulana kisisimukaji sana,” yeye aeleza. “Baba yangu nyakati fulani husisimuka kupita kiasi, na sasa vivulana vyangu vyafanana kabisa naye. Nilipokuwa mchanga zaidi, nilikuwa mwepesi mno wa hisia. Singeliweza kusema lolote bila kugugumiza na kubabaika, na ndipo nilianza kutumia kileo kama suluhisho. Kilinituliza, ndivyo nilivyofikiri. Kwa kweli, kulewa kulizifanya hisia zangu ziwe mbaya sana.” Ian alipoanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova, aling’amua kwamba ilimpasa kuacha kutegemea alkoholi ili kudhibiti hisia zake. “Nilihisi kwamba hiari yangu mwenyewe ilitosha, na kwa hakika niliacha kulewa kwa mwaka mzima. Lakini,” yeye alikubali, “singeliweza kukaa bila kulewa.”
“Siku moja,” yeye aendelea, “nilikuwa nikitembea kwa barabara katika mvua nikifiri kwamba ningetembea hadi nife. Nilikuwa nimeacha na kurudia kulewa mara kadhaa. Ndipo niling’amua kwamba nilikuwa nikijaribu kushinda tatizo langu la kulewa kwa njia yangu, si kwa njia ya Yehova. Basi nilianza kusali nilipokuwa nikitembea, nikisema kwa Yehova, kama tokeo, sasa nitafanya mambo kwa njia yake, nikimwomba anipe roho yake takatifu ili kunitia nguvu.” Hiyo ilikuwa karibu miaka kumi iliyopita. Sasa Ian yukoje?
“Bado nahitaji kujitahidi ili kudhibiti udhaifu wangu,” yeye akubali, “na nimejifunza kumtegemea Yehova kabisa ili kuendelea.” Kufikia hapo Ian afikiria mafanikio yake yalitokana na nini? “Nakumbuka mgawo wangu wa kwanza wa kusoma Biblia baada ya kurudi kwenye kutaniko la Mashahidi wa Yehova. Ulikuwa Zaburi 116, ambayo huanza hivi: ‘Nampenda BWANA kwa kuwa anaisikiliza sauti yangu na dua zangu.’ Katikati ya zaburi hiyo, nasoma hivi: ‘Nimrudishie BWANA nini kwa ukarimu wake wote alionitendea?’ [mstari 12] Hiki kilikuwa kama kikanyagio kilichonisaidia kurudia ukawaida fulani wangu.” Sasa Ian ashauri yeyote aliye katika hali kama hiyo hivi: “Usijidanganye mwenyewe.” Yeye aongezea hivi: “Hatimaye nilipofanyia kazi tatizo langu na kusali kwa ajili ya roho takatifu ya Yehova ili kutia nguvu azimio langu, nilianza kufaulu.”
Ian, pamoja na Mashahidi wa Yehova wengine karibu milioni tano, hutegemea roho takatifu ili kumsaidia kufuata njia iliyoelezwa katika kitabu cha maagizo kilicho muhimu zaidi, Biblia. Acha Mashahidi wa mahali pako wakufahamishe ujumbe wayo ulio wazi, rahisi, sahili—ule wa Ufalme wa Mungu, serikali yake ya kimbingu mikononi mwa Kristo Yesu aliyefufuliwa. Mwakilishi huyu karibuni ataondoa kila alama ya hitilafu ya jeni na ataandalia jamii ya binadamu mazingira ya paradiso ambayo katika hayo wataishi milele. Waweza kuwapo pia!