Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g95 6/22 uku. 3
  • Matabiri ya Mwisho wa Ulimwengu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matabiri ya Mwisho wa Ulimwengu
  • Amkeni!—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Kuna Maonyo Mengi Bandia?
    Amkeni!—1993
  • Je, Mwisho wa Dunia Uko Karibu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
  • Sababu ya Wengi Kuamini Ulimwengu Utakwisha
    Amkeni!—1995
  • Je, Unapaswa Kuogogopa Mwisho wa Ulimwengu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1995
g95 6/22 uku. 3

Matabiri ya Mwisho wa Ulimwengu

“Kwa maelfu ya miaka manabii wa giza wamekuwa wakitabiri kwamba ulimwengu ulikuwa karibu kwisha.”—Premonitions: A Leap Into the Future.

KATIKA mwaka 1033, miaka 1,000 tu baada ya kifo cha Kristo, wakazi wa Burgundy, Ufaransa, walikuwa na hofu kubwa kwa sababu ilikuwa imetabiriwa kwamba ulimwengu ungekwisha mwaka huo. Matazamio ya mwisho wa ulimwengu yaliongezwa wakati idadi isiyo ya kawaida ya mvua ya radi na njaa kali vilipotukia. Umati mkubwa ulijiingiza katika wonyesho wa hadharani wa toba.

Miongo kadhaa mapema, mwaka wa elfu moja kutoka kuzaliwa kwa Kristo ulipokaribia (kulingana na kronolojia iliyokubalika wakati huo), wengi waliamini mwisho wa ulimwengu ulikuwa karibu sana. Utendaji wa kisanaa na kitamaduni katika makao ya watawa ya Ulaya wasemekana kuwa ulikuwa karibu kukoma. Eric Russell alionelea hivi katika kitabu chake Astrology and Prediction: “‘Kuona kwamba mwisho wa ulimwengu ulikuwa ukikaribia sasa’ kulikuwa utaratibu wa kikawaida katika mawasia yaliyofikilizwa wakati wa nusu ya pili ya karne ya kumi.”

Martin Luther, ambaye alianzisha Marekebisho Makubwa ya Kidini ya Kiprotestanti katika karne ya 16, alitabiri kwamba mwisho wa ulimwengu ulikuwa karibu katika siku yake. Kulingana na mamlaka moja, yeye alitaarifu hivi: “Kwa upande wangu, nina hakika kwamba siku ya hukumu itakuja karibuni sana.” Mwandikaji mwingine alieleza hivi: “Kwa kulinganisha matukio ya kihistoria na unabii wa Biblia, Luther alikuwa aweza kutangaza ukaribu wa msiba wa mwisho.”

Katika karne ya 19, William Miller, ambaye kwa kawaida husifiwa kwa kuanzilisha Kanisa Adventist, alitabiri kwamba Kristo angerudi wakati fulani kati ya Machi 1843 na Machi 1844. Kama tokeo, wengine wakati huo walitarajia kuchukuliwa mbinguni.

Katika nyakati za karibuni zaidi, dini fulani yenye chanzo katika Ukrania iitwayo Great White Brotherhood ilitabiri kwamba ulimwengu ungeisha Novemba 14, 1993. Katika Marekani, mwevanjelisti wa redioni, Harold Camping, alisema mwisho wa ulimwengu ungekuja katika Septemba 1994. Kwa wazi, matabiri haya ya tarehe za mwisho wa ulimwengu hayajawa sahihi.

Je, hili limesababisha watu wasiamini zaidi kwamba ulimwengu utakwisha? Kinyume cha hilo. “Ukaribio wa mileani mpya katika mwaka wa 2000,” lilionelea U.S.News and World Report la Desemba 19, 1994, “unafungulia unabii mwingi mno wa siku ya mwisho wa ulimwengu.” Hilo gazeti liliripoti kwamba “karibu asilimia 60 ya Wamarekani wanafikiri ulimwengu utakwisha wakati fulani ujao; karibu thuluthi yao wanafikiri utakwisha mnamo miongo michache.”

Kwa nini kumekuwa na matabiri mengi kuhusu mwisho wa ulimwengu? Je, kuna sababu nzuri kuamini ulimwengu utakwisha?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki