Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g97 1/8 kur. 9-10
  • Ulimwengu Usio na Pupa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ulimwengu Usio na Pupa
  • Amkeni!—1997
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Tatizo la Elimu?
  • Mwingilio wa Mungu
  • ‘Kuwaangamiza Wale Wanaoiangamiza Dunia’
  • Je, Kweli Kuna Mtu Anayeweza Kuubadili Ulimwengu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Mtu Fulani Anajali Kikweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Pupa—Inatuathirije?
    Amkeni!—1997
  • Mamilioni ya Walio Hai Sasa Hawatakufa Kamwe Wamalizike Katika Dunia Yetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1997
g97 1/8 kur. 9-10

Ulimwengu Usio na Pupa

“BILA mageuzi makubwa katika njia ambayo wanadamu wanafikiri, hakuna chochote kitakachoboresha hali ya wanadamu, na msiba ulio mbele ya ulimwengu . . . hautaweza kuepukika.”—Václav Havel, rais wa Jamhuri ya Cheki.

Watu wengi hutambua kwamba utaratibu wa sasa wa ulimwengu hauwezi kuendelea kuwapo. Wengine, kama Václav Havel, waona badiliko kubwa katika kufikiri kwa wanadamu na katika matendo kuwa ndilo suluhisho la pekee. Kwa mfano, mchunguzi mmoja wa hali ya sasa ya ulimwengu, asema: “Kwa mamia ya mamilioni ya walio maskini hohehahe, hali ya chakula na vitu vingine vilivyo muhimu kwa maisha haitakuwa bora . . . ila tu mataifa ya ulimwengu yachukue hatua ya mara moja na kubadili hali zinazoendelea sasa.”—Food Poverty & Power.

Hata hivyo, je, inafaa tuweke tumaini letu la kuendelea kuishi kwa aina fulani ya badiliko kubwa la asili ya binadamu? Je, kwa uhakika twaweza kutumaini serikali ‘zichukue hatua ya mara moja ya kubadili hali zinazoendelea’? Wengine hufikiri hivyo. ‘Mungu alitupa hiari, na ni juu yetu kubadili mambo,’ wao wasema. Lakini ukweli mtupu wa historia wazusha maswali mazito kuhusu tamaa na uwezo wa mwanadamu wa kufanya mabadiliko ambayo yanahitajika. Maoni haya si ya kutazamia mabaya, bali ni halisi. Je, ungetumainisha uhai wako kwa daktari-mpasuaji fulani ukijua kwamba wagonjwa wote waliotangulia ambao aliwashughulikia walikufa?

Ni Tatizo la Elimu?

“Tatizo ni la elimu,” asema Ted Trainer, katika Developed to Death—Rethinking Third World Development. Asema kwamba watu wasipofundishwa ili waone kwamba badiliko la msingi ndilo linalohitajika, “hatuwezi kutumaini kufanya badiliko la kupata utaratibu mzuri wa ulimwengu.” Bila shaka kuna uhitaji wa kufundisha watu umaana wa kufanya badiliko katika mitazamo na matendo ikiwa ulimwengu utaokoka. Hakika hiyo ni muhimu, na Biblia yasema juu ya programu kama hiyo ya elimu. Inasema kwamba dunia “itajawa na kumjua BWANA.” Kisha, hakuna mtu ‘atakayedhuru wala kuharibu’ mahali popote duniani.—Isaya 11:9.

Lakini hakuna kiasi cha elimu, hata ile programu ya elimu ya Mungu, ambacho chenyewe kitaondolea dunia watu wenye pupa ambao hudhuru sana na kusababisha uharibifu mwingi. Elimu hiyo itatokeza badiliko kwa watu tu wanaotaka kubadilika, watu wanaotaka kujipatanisha na viwango vya Mungu. Kulingana na Yesu Kristo, wao ni wachache. (Mathayo 7:13, 14) Hivyo, Biblia haitegemezi ahadi yayo ya badiliko kwenye tumaini fulani bandia kwamba siku moja wanadamu wote watatambua kwa ghafula ukubwa wa tatizo hilo na kubadili njia zao. Inasema kwamba Mungu atachukua hatua ya moja kwa moja ya kuondoa watu wenye pupa duniani.

Mwingilio wa Mungu

Wengi huona wazo la mwingilio wa moja kwa moja wa Mungu kuwa ndoto au mazigazi tu. “Maendeleo makubwa ya elimu katika karne ya 18 yalitulazimisha kuondoa wazo lenye kufariji kwamba Mungu mwenye kuingilia mambo angeingilia mambo na kurekebisha hali,” chasema World Hunger: Twelve Myths. Lakini je, tuamini mabishano na falsafa za kitaalamu za wale ambao hawana tumaini katika “Mungu mwenye kuingilia mambo”? Je, masuluhisho yao si madanganyo tu?

Ni jambo la hekima kutegemeza tumaini letu la kuokoka kwenye unabii usiokosea unaopatikana katika Biblia ambao hutaja mwingilio wa Mungu. Si “wazo la kutuliza” tu kuamini ahadi za Mungu—hilo ndilo tumaini halisi la pekee la kuokoka ambalo tunalo!

‘Kuwaangamiza Wale Wanaoiangamiza Dunia’

Mungu anaahidi nini hasa? Jambo moja ni kwamba yeye anaahidi kuondoa kutoka duniani wale wanaochafua na kuharibu mazingira. Ufunuo 11:18 yatangaza kwamba ana “wakati uliowekwa rasmi” wa “kuwaleta kwenye uangamizi wale wanaoiangamiza dunia.” Hilo litamaanisha nini? Hilo litamaanisha mwisho wa wale wote ambao sasa wananyanyasa walio maskini na dhaifu. Mungu “atawahukumu walioonewa wa watu, atawaokoa wahitaji, atamseta mwenye kuonea.” Yeye ataondoa wenye pupa na kuruhusu wahasiriwa wasio na hatia kupata ufanisi. “Atamkomboa mhitaji aliapo . . . Atawakomboa nafsi zao na kuonewa na udhalimu.”—Zaburi 72:4, 12-14.

Hilo litaleta badiliko lililoje! Kulingana na mtume Petro, badiliko hilo litakuwa kubwa hivi kwamba litatokeza “mbingu mpya na dunia mpya.” (2 Petro 3:13) Katika “dunia mpya” hii, kila mtu atafurahia kiasi kitoshacho cha mazao ya dunia. (Mika 4:4) Hata sasa, kuna chakula tele cha kutosha kila mtu. Tatizo ni kutosambaza chakula ifaavyo. “Imekadiriwa kwamba tunaweza kutokeza chakula cha kutosha kuweza kulisha watu bilioni 38-48 katika eneo la dunia liwezalo kufanyiwa ukulima,” asema Anne Buchanan, katika kitabu Food Poverty & Power.

Dunia hii itaokoka. Muumba wayo “hakuiumba ukiwa, aliiumba ili ikaliwe na watu.” (Isaya 45:18) Hatua ya Mungu dhidi ya watu wenye pupa itamaanisha “dhiki kubwa” ya kipindi kifupi. (Mathayo 24:21) Kisha waokokaji wa dhiki hiyo watafurahia dunia iliyo paradiso, ambayo imekaliwa na watu ambao hawana pupa hata kidogo. (Zaburi 37:10, 11; 104:5) Itakuwa kama Biblia inavyoahidi: “Bwana MUNGU atafuta machozi katika nyuso zote.”—Isaya 25:8.

Unaweza kuwa mmojawapo watu wenye kunufaika na hatua ya Mungu ya kuondoa pupa kutoka duniani. Ikiwa kweli unataka kufanya mapenzi ya Mungu, tumia msaada wote unaoandaliwa ili kukusaidia uendelee kuishi sasa katika ulimwengu wenye pupa. Chukua hatua ya kuokoka “dhiki kubwa.” Mashahidi wa Yehova wako tayari kukusaidia kujifunza mambo unayohitaji kujua. Basi uwe huru kuwasiliana nao kwenye Jumba la Ufalme la kwenu au andika kwa kutumia anwani iliyo karibu zaidi ambayo imeorodheshwa kwenye ukurasa 5.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki