Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g97 2/8 uku. 31
  • Umaskini—‘Dharura Isiyojulikana’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Umaskini—‘Dharura Isiyojulikana’
  • Amkeni!—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Wafungwa wa Umaskini
    Amkeni!—1998
  • Jitihada za Kumaliza Umaskini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Umaskini Unaoongezeka—Tisho kwa Wote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1997
g97 2/8 uku. 31

Umaskini—‘Dharura Isiyojulikana’

“TWASIKIA sana kuhusu dharura kubwa za kuongezeka kwa joto duniani na tabaka za ozoni na uchafuzi wa bahari,” alisema mshauri wa Umoja wa Mataifa Dakt. Mahbub Ul-Haq, lakini aliongeza: “Kuongezeka kwa joto duniani na dharura nyingine nyingi zilizo kubwa bado hazijaua mtu yeyote [huku] dharura zisizojulikana husababisha vifo vingi katika nchi zinazoendelea kila siku.” Dakt. Ul-Haq alitoa maelezo juu ya moja ya dharura hizo zisizojulikana. “Umaskini,” alisema, “kwa kweli ndio muuaji mkuu zaidi.” Kwa njia gani?

Kwa wengi wa watu bilioni 1.3 duniani kote ambao wanaishi kwa dola moja au chini kwa siku, umaskini hugeuka kuwa msiba wenye kufisha. Kufikia watu milioni 18, laripoti gazeti UN Chronicle, hufa kutokana na “visababishi vinavyohusiana na umaskini” kila mwaka. Idadi hii inatisha! Kwa mfano, ebu wazia uangalifu utakaopewa kichwa cha habari ikiwa wakazi wote wa Australia, karibu milioni 18, wangekufa kutokana na njaa kwa mwaka mmoja! Hata hivyo, vifo vya mamilioni hayo maskini, likaeleza tangazo la Redio ya Umoja wa Mataifa, “havizungumziwi sana.” Kwa kweli, huu ni, ‘msiba usiojulikana.’

Kuvunja kimya hicho, wawakilishi kutoka nchi 117 waliohudhuria Mkutano wa Ulimwengu wa Maendeleo ya Jamii, ambao ulikuwa ndio mkutano wa kwanza kabisa kufanywa, walizungumzia njia za kupambana na tatizo la ulimwengu la umaskini. “Miaka 150 iliyopita ulimwengu ulianzisha vita dhidi ya utumwa,” alikumbusha James Gustave Speth, mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo. “Leo ni lazima tuanzishe vita ya ulimwengu dhidi ya umaskini ambao umekumba wengi.” Kwa nini kuna hangaiko hilo? Umaskini, alionya, “unatokeza kuvunjika moyo na ukosefu wa uthabiti na unaharibu ulimwengu wetu.”

Walakini, hata wajumbe walipokuwa wakizungumzia njia za kumaliza umaskini, ‘saa ya umaskini,’ ikiendelea kuonyesha idadi ya watoto wazaliwao katika familia maskini kila siku, ilionyesha kwamba hali ya umaskini duniani kote iliendelea kuwa mbaya. Saa hiyo, iliyoonyeshwa katika mahali pa mkutano, ilionyesha kwamba wakati wa mkutano huo uliochukua juma moja, karibu watoto 600,000 waliongezwa katika idadi yenye kuongezeka ya watoto maskini. Mwishoni mwa siku ya mwisho ya mkutano huo, saa ya wonyesho ilizimwa; lakini kihalisi, kama Speth alivyoonyesha, “tatizo la umaskini laendelea kukua.” Swali sasa ni hili, Je, tatizo la umaskini litapata uangalifu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki