Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g97 4/22 uku. 31
  • Njaa ya Kiroho Katika Rumania

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Njaa ya Kiroho Katika Rumania
  • Amkeni!—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Mikusanyiko ya Rumania Yafanywa Japo Upinzani
    Amkeni!—1997
  • Kanisa Othodoksi la Kigiriki—Dini Iliyogawanyika
    Amkeni!—1996
  • Bucharest—Jiji Lenye Majengo ya Kale na ya Kisasa
    Amkeni!—2009
  • Nilijifunza Kweli ya Biblia Katika Rumania
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1997
g97 4/22 uku. 31

Njaa ya Kiroho Katika Rumania

RIPOTI ya Shirika la Habari la Associated Press kutoka Brasov, Rumania, ilisema kwamba karibu asilimia 90 ya watu milioni 23 wa Rumania ni washiriki wa Kanisa Othodoksi, ambalo liliruhusiwa kutenda wakati wa utawala wa Kikomunisti. Lakini, gazeti Daily Record la Canon City, Colorado, Marekani, lilisema kwamba watu wengi sasa wapata kwamba kanisa hilo limepungukiwa. Lilikuwa na kichwa hiki cha habari: “Warumania Wapata Kwamba Kanisa Othodoksi Halifai.”

“Alexandru Paleologu, mwandishi na mwana-falsafa,” gazeti hilo likaripoti Oktoba iliyopita, “alitaja ukosefu wa itibari katika mamlaka ya kanisa, na alisema kwamba mtindo na mambo ya msingi ya kanisa hilo yalichangamana. Kwa mfano, watu huvaa misalaba na kufunga katika siku maalum. Lakini utoaji-mimba, jambo ambalo kanisa huliona kuwa ni dhambi, limeenea.”

Gazeti Daily lilisema kwamba wengi wamekuwa Mashahidi wa Yehova, likitaja tokeo ambalo programu ya mafundisho ya Biblia ya Mashahidi ilikuwa nayo juu ya familia moja: “Mume wa Florentina Petrisor alizoea kunywa pombe sana na kumpiga, asema Florentina. Lakini tangu wenzi hao wawe Mashahidi wa Yehova, familia yake imekuwa yenye amani.”

Florentina, fundi cherehani mwenye miaka 38, aliripotiwa kuwa “aliacha kanisa Othodoksi kwa sababu ya ukosefu wa mafundisho ya kiuchungaji na ufuatiaji vitu vya kimwili wa kasisi wa mahali hapo.” Gazeti hilo lilisema: “Baba-mkwe wake alipokufa, Petrisor alisema kwamba familia ililazimika kutumia mali zayo chache kumlipa na kumwandalia chakula kasisi huyo ili kuhakikisha kupata huduma nzuri za maziko kabla hajatumia fedha hizo kununua chakula kwa ajili ya watoto wake. ‘Nilifikiri haikuwa haki,’ alisema.”

Kuhusu kampeni za kanisa za kueneza mawazo yasiyo ya kweli kuhusu Mashahidi, Daily Record lilisema: “Katika Rumania, kanisa Othodoksi, ambalo limepata uvutano tena, lilichochea serikali katika kuhamisha mkusanyiko wa Mashahidi wa Yehova katika kiangazi hiki kutoka jiji kuu la Bucharest kwenda katika miji ya Transylvania ya Brasov na Cluj.”

Gazeti la Amkeni! la Februari 22, 1997, lilisema kuhusu kampeni za kanisa hilo katika kuchochea serikali kufuta mkusanyiko wa kimataifa uliopangwa kufanyika Bucharest Julai 1996. Wewe waweza kusoma gazeti hilo jinsi ambavyo makusanyiko ya badala yalivyoweza kupangwa kwa haraka katika Cluj-Napoca na Brasov na jinsi ambavyo jumla ya watu 34,866 waliyahudhuria. Utangazaji uliofuata na kutukia ulimwenguni pote ulikuwa wenye kustaajabisha. “Mbinu ambayo Kanisa Othodoksi la Rumania ilidhani ingetuzuia,” alisema mwakilishi mmoja Shahidi, “kwa hakika imeeneza habari njema.”

[Picha katika ukurasa wa 31]

Wajumbe wakiimba katika mkusanyiko wa Brasov

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki