Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g97 5/22 kur. 4-7
  • Ni Nini Kimepata Vitumbuizo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nini Kimepata Vitumbuizo?
  • Amkeni!—1997
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Uhitaji wa Kutahadhari
  • TV—Ni “Mwalimu Mjanja”
    Amkeni!—2006
  • Kupumbazwa Na Jeuri
    Amkeni!—2012
  • Je! Televisheni Imekubadili Wewe?
    Amkeni!—1991
  • Jinsi ya Kudumisha Mtazamo wa Akili Unaofaa
    Amkeni!—1999
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1997
g97 5/22 kur. 4-7

Ni Nini Kimepata Vitumbuizo?

WAROMA wa kale, ambao walipaswa kuwa kwenye kilele cha kustaarabika, wangewezaje kuona maumivu ya binadamu wenzao kuwa kitumbuizo? “Yaweza kuelezwa tu na tamaa ya kupata visisimuaji vipya vyenye nguvu zaidi,” aandika Gerhard Uhlhorn katika The Conflict of Christianity With Heathenism. “Wakiwa wamekinai ufurahio wote uwezekanao, watu walitafuta . . . msisimko ambao hawakuupata kwingineko kote.”

Watu wengi leo hudhihirisha “tamaa [kama hiyo] ya visisimuaji vipya na vyenye nguvu.” Ni kweli, huenda wasikusanyike kutazama machinjo halisi au uzinifu. Lakini chaguo lao la vitumbuizo hufunua tamaa kama hiyo ya jeuri na ngono. Fikiria baadhi ya vielelezo.

Sinema. Katika miaka ya hivi majuzi watengeneza filamu wamedhihirisha “upendezi kuelekea upotovu,” asisitiza mchambuzi wa sinema Michael Medved. “Wazo kuu katika fungu la sinema,” yeye aongeza, “laonekana kuwa kwamba maonyesho ya ukatili na kichaa yastahili kufikiriwa zaidi, kupokea staha zaidi, kuliko jitihada zozote za kuwasilisha wema au uzuri.”

Kushindana na televisheni kumelazimisha watengeneza filamu wafanye chochote kile ili kushawishi watu waende kwenye majumba ya sinema. “Twahitaji sinema zenye kustaajabisha, zenye ukali, ambazo zinatofautiana sana na programu ambazo watu huona kwenye televisheni,” asema mwenyekiti wa studio moja ya sinema. “Si kwamba tumejitoa kuonyesha umwagikaji wa damu na lugha [chafu], bali hayo ndiyo yanayohitajiwa leo ili kutengeneza filamu.” Kwa hakika, wengi hata hawashtuliwi tena na jeuri nyingi ya waziwazi kabisa ya sinema. “Watu wanakufa ganzi kwa habari ya jeuri ya sinema,” asema mkurugenzi wa sinema Alan J. Pakula. “Kiasi cha wanaouawa kimeongezeka mara nne, nguvu za mlipuko zimeongezeka sana, na watu hawashtuki. Wamesitawisha tamaa kubwa sana ya msisimko wenye ukatili.”

Televisheni. Maonyesho mabaya sana ya ngono kwenye televisheni sasa ni ya kawaida katika sehemu nyingi za ulimwengu, kutia ndani Brazili, Ulaya, na Japani. Mtazamaji wa wastani wa televisheni katika Amerika huona marejezeo ya kingono yapatayo 14,000 kwa mwaka mmoja tu. “Kuongezeka kwa vichwa vikuu kuhusu ngono na maonyesho ya waziwazi hakuonyeshi ishara yoyote ya kukoma,” charipoti kikundi kimoja cha utafiti. “Mambo ambayo wakati mmoja yalikuwa mwiko kama vile ngono ya maharimu, kupata raha kwa kutendea wengine kwa ukatili, na ngono na mnyama yamekuwa njia ya kupata faida ya vipindi vya televisheni vya wakati wa jioni.”

Kulingana na kitabu Watching America, kuna sababu ya kuruhusu kila kitu katika programu zinazoonyeshwa kwenye televisheni. Hicho husema: “Kuonyesha ngono huleta faida nyingi. . . . Kampuni za kutokeza vipindi vya televisheni zilipogundua kwamba zilikuwa zikisisimua watazamaji wengi zaidi ya wale wenye kuchukizwa, zimeongeza hatua kwa hatua uwezekano wa kupata faida kwa vipindi vyao kwa kuruhusu miiko mingi zaidi na zaidi ivunjwe na katika namna ya waziwazi sana.”

Michezo ya Vidio. Muhula ulioonekana kuwa usio mbaya wa michezo ya vidio aina ya Pac-Man na Donkey Kong umeachia nafasi muhula mpya wa michezo yenye ukatili mbaya sana. Profesa Marsha Kinder afafanua michezo hii kuwa “mibaya zaidi kuliko televisheni au sinema. Hiyo huwasilisha ujumbe kwamba njia pekee ya kupata udhibiti na uwezo ni kupitia jeuri.”

Kwa sababu ya hangaiko la umma, kampuni moja mashuhuri ya utengenezaji katika Marekani sasa inatumia mfumo wa kuainisha michezo yayo ya vidio. Kibandiko “MA-17”—kinachoonyesha kwamba mchezo huo wa “waliokomaa” haufai kwa wale walio chini ya umri wa miaka 17—chaweza kuwa na jeuri nyingi mno, habari za kingono, na lugha chafu. Hata hivyo, watu fulani wanahofu kwamba uainishaji wa “waliokomaa” utaongezea uvutio wa mchezo huo. “Kama ningekuwa na umri wa miaka 15 na nione kibandiko MA-17,” asema shabiki mmoja mchanga wa michezo, “ningefanya juu chini kuupata mchezo huo.”

Muziki. Gazeti moja ambalo huchunguza sana yaliyomo katika muziki upendwao sana ladai kwamba mwishoni mwa mwaka 1995, ni rekodi 10 tu katika rekodi bora 40 ambazo hazikuwa na lugha chafu au marejezo ya dawa za kulevya, jeuri, au ngono. “Muziki upatikanao kwa wale hawajafikia ubalehe unashtua sana, mwingi wao unaonyesha waziwazi kwamba maadili ya kidesturi hayana msingi na hayafai,” laripoti St. Louis Post-Dispatch. “[Muziki] unaovutia wabalehe fulani umejaa hasira na hali ya kutokuwa na tumaini nao huchochea hisia za kwamba ulimwengu pamoja na yule anayesikia muziki huo wanaelekea kwenye maangamizi.”

Mdundo wa kifo, roki ambayo gitaa inapigwa kwa mvurugo na muziki kuimbwa kivivu, na rapu ya magenge ya mitaani yaonekana hutukuza sana jeuri. Na kulingana na ripoti ya San Francisco Chronicle, “washiriki wa biashara ya vitumbuizo wanatabiri kwamba vikundi vya kuhofisha zaidi hivi karibuni vitakuwa na mafanikio na umashuhuri.” Nyimbo zenye kutukuza hasira na kifo sasa zimependwa na wengi katika Australia, Ulaya, na Japani. Ni kweli, bendi fulani zimejaribu kuwa na ujumbe ufaao. Hata hivyo, Chronicle laonelea, “Uthibitisho wadokeza kwamba hakuna uwezekano wa kupata faida kwa muziki usio na hatia.”

Kompyuta. Hivi ni vifaa vyenye thamani na vyenye matumizi mengi yafaayo. Hata hivyo, zimetumiwa na watu wengine ili kusambaza habari zenye utovu wa adabu. Kwa kielelezo, gazeti Maclean’s laripoti kwamba hiyo yatia ndani “picha na maandishi kuhusu chochote kuanzia vitu vinavyopendwa na kuheshimiwa mno hadi ukahaba hadi kuvutiwa kingono na watoto—habari ziwezazo kushtua watu wazima wengi, licha ya kushtua watoto wao.”

Habari ya Kusoma. Vitabu vingi vinavyopendwa na wengi vimejaa ngono na jeuri hadi pomoni. Mtindo wa hivi majuzi katika Marekani na Kanada ni ule ambao umeitwa “hadithi ya kubuni ya kushtua”—hadithi zenye kuogofya mno zinazoelekezwa kwa vijana wachanga wa umri wa miaka minane. Diana West, akiandika katika New York Teacher, adai kwamba vitabu hivi “vinatia ganzi watoto, vikizuia uwezo wa kiakili hata kabla ya huo kuanza.”

Vitabu vingi vya ucheshi vinavyochapishwa katika Hong Kong, Japani, na Marekani huonyesha “habari nyingi mno za vita vikatili, ulaji wa nyama ya binadamu, kukatwa kichwa, ibada ya Shetani, ubakaji, na lugha chafu,” waripoti uchunguzi uliofanywa na National Coalition on Television Violence (NCTV). “Wingi wa jeuri na habari zilizopotoka kingono katika magazeti haya unashtua,” asema Dakt. Thomas Radecki, mkurugenzi wa utafiti wa NCTV. “Inaonyesha jinsi tumejiruhusu tufe ganzi.”

Uhitaji wa Kutahadhari

Kwa wazi, katika ulimwengu wa leo kuna hali ya kuvutiwa na ngono na jeuri, na hiyo yaonekana katika biashara ya vitumbuizo. Hali hiyo inafanana na ile iliyofafanuliwa na mtume Mkristo Paulo: “Wakiisha kuishiwa na hisia zote za adili, walijikabidhi wenyewe kwenye mwenendo mlegevu ili wafanye ukosefu wa usafi wa kila namna pamoja na pupa.” (Waefeso 4:19) Wakiwa na sababu ifaayo wengi leo hutafuta kitu bora zaidi. Je, ndivyo ilivyo na wewe? Ikiwa ndivyo, utafurahi kujua kwamba waweza kupata vitumbuizo vifaavyo, kama makala ifuatayo itakavyoonyesha.

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 5]

Televisheni Yaweza Kudhuru

TELEVISHENI ilitokea hadharani mara ya kwanza Marekani kwenye maonyesho ya ulimwengu ya 1939 katika New York. Mwandishi mmoja wa habari aliyekuwapo alieleza tashwishi yake kuhusu wakati ujao wa kifaa hiki kipya. “Tatizo na televisheni,” akaandika, “ni kwamba ni lazima watu wakae na kukaza macho yao kwenye kiwambo; familia ya kawaida ya Marekani haina wakati kwa jambo hilo.”

Alikosea kama nini! Kwa hakika, imesemekana kwamba kufikia wakati Mmarekani wa kawaida amalizapo shule, atakuwa ametumia asilimia 50 zaidi ya wakati mbele ya televisheni kuliko mbele ya mwalimu. “Watoto ambao ni watazamaji wa televisheni wa kupindukia ni wakali zaidi, wasiotazamia mazuri, ni wazito zaidi, hawana uwezo wa mawazo ya kubuni, hawana hisia-mwenzi sana, na ni wanafunzi wasio na uwezo sana kuliko wenzao ambao hawatazami sana televisheni,” adai Dakt. Madeline Levine katika kitabu chake Viewing Violence.

Yeye atoa shauri gani? “Watoto wahitaji kufunzwa kwamba televisheni, kama tu kifaa kingine nyumbani, ina kazi hususa. Hatuachi kikausha nywele kikiendelea kufanya kazi wakati nywele zimekauka, au kioka mkate kikiendelea kufanya kazi wakati kipande cha mkate kimeokwa. Twatambua matumizi hususa ya vifaa hivi na twajua wakati wa kuvizima. Watoto wetu wahitaji kufunzwa vivyohivyo kuhusu televisheni.”

[Sanduku katika ukurasa wa 7]

Vitumbuizo Ulimwenguni

Amkeni! liliomba waleta-habari walo kutoka sehemu kadhaa za ulimwengu wafafanue mielekeo ya vitumbuizo mahali walipo. Yafuatayo ni baadhi ya maelezo yao.

Brazili: “Vipindi vya televisheni vimezidi kupotoka. Hata hivyo, huku wazazi wengi wakifanya kazi mbali na nyumbani, watoto mara nyingi wanaachwa wajitumbuize na televisheni. CD-ROM zilizo na habari kuhusu mambo ya kimafumbo na michezo ya vidio yenye kuonyesha jeuri mbaya zapendwa na wengi.”

Jamhuri ya Cheki: “Tangu kuanguka kwa Ukomunisti, nchi hii imejawa na vitumbuizo ambavyo havijapata kuonwa hapa tena, kutia ndani vipindi vya televisheni kutoka Magharibi na maduka ya ponografia. Vijana huenda kwa ukawaida kwenye majumba ya disko, vilabu vya biliadi, na baa. Matangazo ya kupita kiasi na msongo wa marika mara nyingi huwa na uvutano mkubwa kwao.”

Ujerumani: “Kwa kuhuzunisha, wazazi wengi wamechoka sana kupangia watoto wao vitumbuizo, kwa hiyo vijana wanategemeana ili kupata wakati wa kufurahia. Wengine wanajitenga wakiwa na michezo ya kompyuta. Wengine wanahudhuria vipindi vya usiku kucha vya dansi viitwavyo raves, ambapo dawa za kulevya ni nyingi mno.”

Japani: “Vitabu vya ucheshi ni kipitisha wakati kipendwacho sana na vijana na watu wazima, lakini vimejaa jeuri, ukosefu wa adili, na lugha chafu. Kucheza kamari kumeenea pia. Mwelekeo mwingine wenye kusumbua ni kwamba wasichana fulani wanapiga simu kwenye vilabu vinavyotangazwa sana ambavyo hushughulikia wanaume wenye makusudi yasiyo ya adili. Wengine wanapiga ili kufurahia tu, ilhali wengine wanafikia hatua ya kupeana miadi ya kijinsia ili kulipwa, jambo ambalo katika visa fulani huongoza kwenye ukahaba.”

Nigeria: “Majumba ya vidio yasiyodhibitiwa yanaenea Afrika Magharibi. Vibanda hivi hafifu huruhusu watu wa umri wote kuingia, kutia ndani watoto. Vidio za ponografia na za maogofyo huonyeshwa kwa ukawaida. Kwa kuongezea, filamu zilizotengenezwa hapa zinazoonyeshwa kwenye televisheni kwa kawaida huonyesha uwasiliani-roho.”

Afrika Kusini: “Vipindi vya usiku kucha vya dansi vinasitawi hapa, na dawa za kulevya mara nyingi hupatikana kwa urahisi hapo.”

Sweden: “Baa na vilabu vya usiku vinafanikiwa katika Sweden, na mara nyingi wahalifu na walanguzi wa dawa za kulevya humiminika mahali kama hapo. Vitumbuizo vya televisheni na vidio vimejaa jeuri, uwasiliani-roho, na ukosefu wa adili.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki