‘Mfululizo Ulio Mgumu wa Afya ya Akili’
“Licha ya maendeleo yenye kuvutia katika sehemu mbalimbali za utunzaji wa afya,” yasema makala moja iliyochapishwa katika Synergy, kijarida cha Shirika la Kikanada kwa Afya ya Kimataifa, “twakabili mfululizo ulio mgumu wa tufeni pote wa afya ya akili.”
Uchunguzi mmoja ulikata kauli kwamba 1 kati ya watu 4 ulimwenguni pote ana matatizo ya kiakili, kihisia-moyo, au kitabia. Uchunguzi mwingine ulionyesha kwamba 1 kati ya wagonjwa 3 wanaomwendea daktari hufanya hivyo kwa sababu ya kusumbuliwa na mshuko-moyo au kupatwa na matatizo ya hangaiko. Na bado, wasema wachunguzi, idadi ya watu hao inazidi kuongezeka.
Kwa nini? Uchunguzi uliofanywa na Kitivo cha Tiba ya Kijamii cha Chuo Kikuu cha Harvard wasema kwamba magonjwa kama vile mshuko-moyo unaotambuliwa kitiba, kuchanganyikiwa kiakili, na kurukwa na akili yanaongezeka kwa sababu “watu wengi zaidi huishi kufikia umri wa uzee.” Hata hivyo, kuishi miaka mingi siyo sababu pekee. Matatizo ya kiuchumi na mkazo unaoongezeka wa maisha ya kisasa vinachangia hali hii pia.
Hali mbaya hii yaweza kuondolewaje? Kati ya sehemu nyingi za utunzaji wa afya, wasema wataalamu, afya ya akili yapasa kushughulikiwa kwanza kwa sababu hiyo “inawakilisha sehemu moja ya maeneo mapya yanayohitaji kufanyiwa uchunguzi ili kuboresha hali ya mwanadamu.”