Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g99 5/8 uku. 25
  • Wazaliwa wa Amerika na Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wazaliwa wa Amerika na Biblia
  • Amkeni!—1999
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nani Ambao Wameongoza?
  • Wakati Wao Ujao Una Nini?
    Amkeni!—1996
  • Jinsi Ulimwengu Wao Ulivyopotea
    Amkeni!—1996
  • Walitoka Wapi?
    Amkeni!—1996
  • Jina la Mungu Lilibadili Maisha Yangu!
    Amkeni!—2001
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1999
g99 5/8 uku. 25

Wazaliwa wa Amerika na Biblia

TANGU Wazungu wavamie bara la Amerika, wengi wamejaribu kuwafundisha Wazaliwa wa Amerika Biblia.

Tangu karne ya 17, Biblia nzima imetafsiriwa katika lugha sita za Kihindi za Amerika Kaskazini. Biblia ya kwanza ilikuwa ya John Eliot, iliyochapishwa mwaka wa 1663 kwa ajili ya Wahindi wa Massachusett karibu na Boston na Roxbury, Massachusetts. Akiandika katika Encyclopedia of North American Indians, Harvey Markowitz asema hivi: “Ingawa wanahistoria wengi sasa wanatilia shaka unyofu wa wakoloni walio wengi waliojiunga na mkataba [yaani “wa ‘kustaarabisha’ ‘washenzi’ wa Ulimwengu Mpya”], kiwango cha kujitoa kwa Eliot kinathibitishwa na miaka kumi na mitano aliyomenyeka akijifunza lugha ya Massachusett na kutunga tahajia ili kunakili Biblia. Eliot aliona daraka hili gumu kuwa ‘kazi takatifu, inayopasa kuheshimiwa, kufanywa kwa uangalifu, na kustahiwa.’”

Ijapokuwa sehemu za Biblia zilitafsiriwa katika lugha nyingine za Wazaliwa wa Amerika, ilichukuwa muda wa miaka mia mbili kabla ya Biblia nyingine nzima kuchapishwa, tafsiri katika lugha ya Magharibi mwa Cree (1862) na washiriki wa Chama cha Biblia cha Uingereza na cha Kigeni. Upesi tafsiri nyingine zilifuatia: Lugha ya Mashariki mwa Arctic Inuit (1871); Dakota, au Mashariki mwa Sioux (1880); na Gwich’in, lugha ya Amerika ya karibu na aktiki (1898).

Biblia ya karibuni zaidi ni tafsiri ya Navajo, iliyochapishwa mwaka wa 1985 baada ya miaka 41 ya matayarisho na ushirikiano kati ya vyama viwili vya Biblia. Sehemu za Maandiko ya Kiebrania na Kigiriki sasa zinapatikana katika angalau lugha 46 za Kihindi.

Ni Nani Ambao Wameongoza?

Markowitz asema kwamba: “Ni jambo la maana . . . kwamba kazi ya kutafsiri Biblia imekuwa jitihada kubwa sana ya Waprotestanti.” Mwandishi huyohuyo aendelea kusema kwamba kabla ya Baraza la Pili la Vatikani (1962), Kanisa Katoliki “lilipinga kuenezwa kwa Biblia miongoni mwa watu wa kawaida, likisadiki kwamba watu wa kawaida hawakuzoezwa . . . ifaavyo kufasiri vifungu vya Biblia kwa usahihi.”

Kwa sasa vyama mbalimbali vya Biblia vinashughulika na angalau miradi 20 ya kutafsiri katika lugha za Wazaliwa wa Amerika Kaskazini, kutia ndani Cheyenne, Havasupai, Micmac, na Zuni. Tafsiri mpya ya Maandiko ya Kigiriki inatayarishwa kwa ajili ya taifa la Navajo. Tafsiri nyinginezo zinatayarishwa kwa ajili ya Wahindi wa Amerika ya Kati na ya Kusini.

Mashahidi wa Yehova si sehemu ya mashirika yoyote ya Kiprotestanti. Hata hivyo, wanatenda miongoni mwa Wazaliwa wote wa Amerika, na kama tokeo, wengi wa Wazaliwa wa Amerika wanaitikia kweli za Biblia kuhusu “mbingu mpya na dunia mpya,” ambazo katika hizo uadilifu utakaa. (2 Petro 3:13) Mashahidi wanatumia Biblia ambazo zinapatikana sasa katika lugha za wazaliwa wa Amerika. Pia wanatumia fasihi za Biblia zilizotafsiriwa na Watch Tower Society katika lugha kadhaa za Wazaliwa wa Amerika, kutia ndani Amyara, Cree, Dakota, Guarani, Inuktitut, Iroquois, Navajo, Quechua, na lugha nyingine tisa.—Ona Amkeni! la Septemba 8, 1996.

[Picha katika ukurasa wa 25]

Jina “Yehova” linapatikana katika Biblia ya Navajo kwenye Zaburi 68:4

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki