Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g99 6/22 kur. 26-27
  • Wanawake Wamechangia Sana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wanawake Wamechangia Sana
  • Amkeni!—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Tendo Lililounganishwa kwa Umoja Kufanya Ujenzi Ulimwenguni Pote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Kujenga Pamoja Duniani Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Je, Unaweza Kutoa Wakati na Nguvu Zako?
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
  • Kazi ya Ujenzi Inayomletea Yehova Sifa
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1999
g99 6/22 kur. 26-27

Wanawake Wamechangia Sana

FUNGU la maana la wanawake Wakristo katika kazi ya ujenzi ya ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova ya Zimbabwe lilikaziwa wakati wa programu ya kuwekwa wakfu, iliyofanywa Desemba 12, 1998. Muda wote wa miaka minne ya ujenzi wa mradi huo, wajitoleaji kutoka nchi nyingi—kutia ndani mamia kutoka Zimbabwe—walitumia wakati wao, nishati, stadi, na mali zao ili kujenga majengo haya mazuri unayoona katika picha iliyoandamana na makala hii.

Utaona majengo sita yanayotoshana ya makao huko nyuma. Jengo kubwa mno lililo karibu nayo ni chumba cha kulia, jikoni, na mahali pa kufulia nguo. Majengo ya makao yana vyumba 61 vya kulala, nacho chumba cha kulia chaweza kutoshea watu 200 hivi. Jengo la ofisi liko mbele, upande wa kulia. Katikati kuna sehemu ya mapokezi, na upande wa kulia kuna bohari, ambapo programu ya kuweka wakfu ilifanyiwa.

Jengo hili lenye kupendeza la ofisi ya tawi ya Zimbabwe, kusini mwa Afrika, ni mojawapo tu ya miradi mingi ambayo imekamilishwa tangu programu ya kimataifa ya ujenzi ianzishwe na Mashahidi wa Yehova mnamo Novemba 1985. Gazeti Amkeni! la Agosti 22, 1991 (la Kiingereza), lilifafanua programu hii katika makala yenye kichwa “Jambo Jipya Katika Ujenzi wa Kimataifa.”

Kuhusu fungu la wanawake katika programu hiyo, gazeti Amkeni! liliripoti hivi: “Wengi wamezoezwa kufunga vyuma pamoja na waya, kuweka na kuunganisha vigae, na pia kupiga msasa na kupiga rangi. Wengine hufanya kazi za lazima za kila siku. Hivyo, wote huchangia sana kazi kwenye ujenzi mbalimbali ulimwenguni.”

Wakati wa programu ya kuweka wakfu ya hivi majuzi nchini Zimbabwe, George Evans na James Paulson, waliokuwa wakisimamia ujenzi, walilinganisha fungu la wanawake kwenye ujenzi wa ofisi ya tawi nchini Zimbabwe na fungu la wanawake katika kujenga tabenakulo ya kale ya Israeli. “Wakaja kila mtu ambaye moyo wake ulimhimiza,” yasema Biblia kuhusu Waisraeli, “nao wakaja, waume kwa wake.”—Kutoka 35:21, 22, italiki ni zetu.

Wakitumia simulizi hilo la Biblia, Ndugu Evans na Paulson walikazia ubora wa mchango wa wanawake. Walinukuu simulizi la Biblia: “Wanawake wote waliokuwa na mioyo ya hekima, . . . wanawake wote ambao mioyo yao iliwahimiza katika hekima.” (Italiki ni zetu.) Kwa kweli, wanawake walikuwa miongoni mwa wale waliojitoa wenyewe kwa hiari kufanya kazi. “Wote, waume kwa wake, ambao mioyo yao iliwafanya kuwa wapenda kuleta kwa hiyo kazi, ambayo BWANA aliamuru ifanywe kwa mkono wa Musa.”—Kutoka 35:25, 26, 29, italiki ni zetu.

Kuhusu ujenzi wa ofisi ya tawi ya Zimbabwe, waangalizi hao wa ujenzi walisema hivi: ‘Wanawake walifanya kila kazi ambayo wanaume walifanya.’ Hiyo ilitia ndani kufunga vyuma na kuendesha mashine kubwa-kubwa. Ndugu Paulson alisema kwamba wanawake waliweka malori yao ya kubebea saruji na mashine nyingine kubwa-kubwa zikiwa safi sana, akiliona jambo hilo kuwa tofauti na vile ambavyo wanaume wangelifanya.

Hakika, twashukuru maelfu ya wanawake ambao wameshiriki pamoja na wanaume katika kazi ya ulimwenguni pote ya ujenzi wa ofisi za tawi na Majumba ya Ufalme ya Mashahidi wa Yehova!

[Picha katika ukurasa wa 26]

Ofisi ya tawi ya Zimbabwe

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki