Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g99 9/8 uku. 30
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
  • Amkeni!—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—1994
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—1999
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—1999
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—2000
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1999
g99 9/8 uku. 30

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Hawachukii Wayahudi Asanteni kwa sababu ya kukubali makosa yenu. Ijapokuwa ningetaka kusoma ombi la msamaha kwa ajili ya taarifa hii, maelezo yenu juu ya matukio yanayozungumziwa yaliridhisha. Tafadhali endeleeni na kazi yenu bora, mkifahamu kuwa wasomaji wenu wanathamini kina na unyoofu wa Amkeni!

W. H., Marekani

Msomaji anarejezea taarifa zilizo katika “Tangazo la Mambo ya Hakika,” azimio lililokubaliwa mnamo 1933 kwenye mkusanyiko huko Berlin, Ujerumani. (Ona “Mashahidi wa Yehova—Wajasiri Licha ya Hatari ya Wanazi,” katika toleo la “Amkeni!” la Julai 8, 1998.) Kama vile makala hiyo ilivyoonyesha, hakuna jambo lililosemwa katika tangazo la mwaka wa 1933 lililokusudiwa kudhihirisha au kuendeleza uhasama kuelekea Wayahudi, na tunaomba msamaha iwapo kuna taarifa fulani zinazotoa wazo hilo leo. Na ikiwa yeyote aliyekuwako miaka ya 1930 alifasiri lile “Tangazo la Mambo ya Hakika” kumaanisha kuwa Mashahidi wa Yehova waliwachukia Wayahudi, maoni hayo yaliyopotoka yangeweza kurekebishwa kwa urahisi kwa kutazama matendo ya ujasiri na ya huruma ya Shahidi mmoja-mmoja kuelekea Wayahudi. Isitoshe, vichapo vya Watch Tower Society vilikuwa mojawapo ya vichapo vya kwanza kufunua na kushutumu mambo waliyotendewa Wayahudi huko Ulaya.—Mhariri.

Kulea Wana Saba Singeweza kujizuia kutwaa fursa hii kuwashukuru kwa ajili ya makala “Magumu na Baraka za Kulea Wana Saba.” (Januari 8, 1999) Nimegundua kwamba kumlea tineja ni jambo gumu, hasa nikiwa mjane. Makala hii ilipofika ndipo nilipong’amua kwamba ninaweza kufanikiwa kuwalea watoto wangu katika kipindi hiki.

A. R., Marekani

Mimi pia nilizaliwa katika familia yenye watoto saba. Kufikia majuzi, tulikuwa tukimtumikia Yehova kwa umoja. Hata hivyo, yapata miezi sita iliyopita, mmoja wa dada zangu wachanga alitengwa na ushirika. Nilipoona makala hiyo kwa mara ya kwanza, sikutaka kusoma simulizi la familia yenye mafanikio. Nilisali kwamba niweze kunufaika na makala hiyo bila kuwaonea wivu. Nilitiwa moyo sana kujifunza kwamba kuna familia yenye matatizo kama yetu na kwamba Yehova huhangaikia hali yetu. Ningependa kushukuru familia ya Dickman kwa kushiriki nasi simulizi lao. Nina hakika kwamba wazazi wangu na ndugu na dada zangu wachanga walitiwa moyo sana na kufarijiwa na makala hiyo.

W. Y., Japani

Alama Usoni Shukrani nyingi za kutoka moyoni kwa ajili ya makala “Alama Usoni—‘Kitambulisho’ cha Nigeria Kinachotoweka.” (Januari 8, 1999) Mimi na mume wangu tuna marafiki kutoka Afrika walio na makovu usoni, na hatukujua yalikuwa ya nini. Tulipata jibu la swali letu katika makala yenu.

M. V., Italia

Simba Asanteni kwa ajili ya makala “Simba—‘Paka’ Wenye Manyoya na Wenye Fahari wa Afrika.” (Januari 22, 1999) Makala hii ilikuwa muhimu sana kwangu, kwa kuwa nimependezwa na simba kwa miaka mingi. Mimi hupendezwa nao sana kwa sababu ni warembo na wajasiri. Ningependa siku moja kukaa na “mwana-simba.”—Isaya 11:6-9.

E. A. S., Brazili

Mimea Dhidi ya Uchafuzi Ile makala fupi “Mimea Dhidi ya Uchafuzi” (Januari 22, 1999) ilikuwa yenye kutokeza sana. Habari hiyo ilithibitisha bila tashwishi yoyote kwamba lazima kuwe na Muumba mwenye upendo, mwenye kujali, na mwenye akili. Ilionyesha jinsi Yehova alivyoumba dunia ikiwa na uwezo wa kujisafisha yenyewe, hata wakati shughuli za mwanadamu zinapotisha kuiangamiza dunia. Pia makala hiyo iliimarisha tumaini langu la kuishi katika Paradiso iliyoahidiwa na Yesu katika Luka 23:43.

R. J., Marekani

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki