Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g99 12/8 kur. 10-12
  • Badiliko Muhimu Litakalokuwa Bora

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Badiliko Muhimu Litakalokuwa Bora
  • Amkeni!—1999
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Badiliko la Maadili
  • Twaishi Pamoja Lakini Tukiwa Tumetengana
  • 1914, Mwaka wa Pekee
  • Kutakuwa na Ulimwengu Mpya Kabisa Hivi Karibuni
  • Jinsi Sisi Tujuavyo Kwamba Tumo Katika “Siku za Mwisho”
    Je, Kweli Mungu Anatujali?
  • Karibuni Kusudi la Mungu Kutimizwa
    Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
  • Je, Tunaishi Katika “Siku za Mwisho”?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Habari Njema Wanazotaka Usikie
    Mashahidi wa Yehova—Wao Ni Nani? Wanaamini Nini?
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1999
g99 12/8 kur. 10-12

Badiliko Muhimu Litakalokuwa Bora

“Katika miaka ya 1900 ulimwengu ulikaribia kuingia mojawapo ya vipindi muhimu vya badiliko katika historia ya kibinadamu. Utaratibu mpya ulikuwa ukichukua mahali pa ule wa kale.”—The Times Atlas of the 20th Century.

MAPEMA katika karne ya 20, “ulimwengu uliingia katika muhula wenye maasi na jeuri isiyo na kifani,” chasema kitabu cha ramani kilichonukuliwa juu. Karne hii ingeshuhudia vita zaidi kuliko karne nyingine yoyote, kukiwa na watu zaidi ya milioni 100 waliokufa.

Katika muhula huu, vita vimeua raia wengi kuliko wakati mwingine wowote. Katika Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, asilimia 15 ya watu waliokufa walikuwa raia. Lakini katika Vita ya Ulimwengu ya Pili, katika nchi fulani raia waliokufa walikuwa wengi kuliko wanajeshi. Kati ya mamilioni waliouawa vitani tangu wakati huo, wengi walikuwa raia. Jeuri hiyo yote imetimiza unabii wa Biblia kuhusu mpandaji aliye juu ya “farasi mwenye rangi-moto,” ambaye ‘alipewa ruhusa kuondolea mbali amani katika dunia.’—Ufunuo 6:3, 4; Mathayo 24:3-7.

Badiliko la Maadili

Karne ya 20 imetimiza unabii katika 2 Timotheo 3:1-5, unaosema: “Katika siku za mwisho nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo zitakuwa hapa. Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wapenda-fedha, wenye kujitanguliza, wenye kiburi, wakufuru, wasiotii wazazi, wasio na shukrani, wasio waaminifu-washikamanifu, wasio na shauku ya kiasili, wasiotaka upatano wowote, wachongezi, wasio na hali ya kujidhibiti, wakali, wasio na upendo wa wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kututumuka kwa kiburi, wenye kuzipenda raha badala ya kuwa wapenda-Mungu, wakiwa na namna ya ujitoaji-kimungu lakini wakithibitika kuwa si kweli kwa nguvu ya hiyo.”

Kwa kiwango fulani, wanadamu ambao si wakamilifu wamedhihirisha sifa za namna hiyo sikuzote. Katika karne ya 20, tabia hizo zimeongezeka na kuenea. Watu wanaojiendesha katika njia zilizofafanuliwa juu wakati mmoja walionwa kuwa wanaojitenga na watu—ikiwa si waovu waziwazi. Sasa hata watu ‘walio na namna ya ujitoaji-kimungu’ wanazidi kuona tabia hiyo kuwa ya kawaida.

Wakati mmoja watu wa dini waliliona kuwa jambo lisilofikirika kwa wenzi kuishi pamoja bila kufunga ndoa. Hali ya kuwa mama bila kufunga ndoa ilionwa kuwa yenye kuaibisha, ndivyo na uhusiano wa wagoni-jinsia-moja. Watu wengi waliona utoaji-mimba kuwa jambo lisilokubalika kabisa na ndivyo na talaka. Ukosefu wa ufuatiaji haki katika biashara ulilaumiwa. Lakini leo, kama asemavyo mtu fulani, “jambo lolote linaruhusiwa.” Kwa nini? Sababu moja ni kwamba, “inaridhisha mapenzi ya watu wasiotaka kuambiwa na wengine mambo wasiyopaswa kufanya.”

Kupuuzwa kwa viwango vya juu vya adili katika karne hii kumefanya mambo ya kutangulizwa yabadilike. Kitabu The Times Atlas of the 20th Century chaeleza: “Katika miaka ya 1900 watu na mataifa bado walikuwa wakikadiria thamani yao pasipo kutegemea pesa. . . . Kufikia mwisho wa karne mataifa yalipima mafanikio yao kwa kutegemea pesa karibu katika visa vyote. . . . Mabadiliko kama hayo yalitukia katika njia ambayo watu waliiona mali.” Leo, zoea la kucheza kamari ambalo limeenea pote huchochea upendo wa pesa, huku redio, televisheni, sinema, na vidio zikichochea tamaa ya vitu vya kimwili. Hata maonyesho ya michezo na mashindano ya biashara hutoa wazo la kwamba ikiwa pesa si mambo yote, angalau ndicho kitu kinachokaribia kuwa cha maana zaidi.

Twaishi Pamoja Lakini Tukiwa Tumetengana

Mwanzoni mwa karne ya 20, watu wengi waliishi mashambani. Inasemekana kwamba mapema-mapema mwa karne ya 21, nusu ya idadi ya watu wataishi mijini. Kitabu 5000 Days to Save the Planet chasema: “Kazi ya kuandaa kiwango cha maisha kinachofaa kwa wakazi wa mijini leo, acha vizazi vinavyokuja, yatokeza matatizo yasiyo na kifani.” Gazeti World Health la UM lilisema: “Kiwango cha watu ulimwenguni wanaoishi katika miji kinaongezeka. . . . Mamia ya mamilioni . . . sasa wanaishi katika hali ambazo ni zenye kudhuru afya yao na hata kuhatarisha uhai wao.”

Ni jambo lisilo la kawaida kwamba watu wanapoishi karibu-karibu katika miji, pia wanazidi kutengana! Televisheni, simu, na Internet, pamoja na mfumo wa ununuzi ingawa ni zenye manufaa, zinafanya uhusiano wa ana kwa ana upuuzwe. Kwa hiyo gazeti la Kijerumani Berliner Zeitung lamalizia: “Karne ya 20 si karne ya kuzidi kwa idadi ya watu pekee. Pia ni karne ya upweke.”

Jambo hilo huongoza kwenye misiba kama ule uliotukia Hamburg, Ujerumani, ambapo mwili wa mwanamume mmoja ulipatikana ndani ya chumba chake miaka mitano baada ya kufa! Hakuna aliyemkosa, wala watu wa jamaa wala majirani wala wenye mamlaka,” likasema gazeti Der Spiegel, likiongezea: “Kwa raia wengi kisa hicho chaonyesha kiwango chenye kufadhaisha cha kila siku cha kutojulikana na kukosa kujishughulisha na jamii katika miji mikubwa.”

Makosa kwa hali hizo za kulaumika hayasababishwi tu na sayansi na tekinolojia. Yanasababishwa hasa na watu. Karne hii imetokeza watu wengi kuliko wakati mwingine wowote ambao ni “wenye kujipenda wenyewe, wapenda-fedha, . . . wasio na shukrani, . . . wasio na shauku ya kiasili, wasiotaka upatano wowote, . . . wasio na upendo wa wema, . . . wenye kuzipenda raha badala ya kuwa wapenda-Mungu.”—2 Timotheo 3:1-5.

1914, Mwaka wa Pekee

Kulingana na Winston Churchill, “mwanzo wa karne ya ishirini ulionekana kuwa shwari na wenye matumaini.” Wengi walifikiri kwamba ungeleta muhula wa amani na ufanisi usio na kifani. Lakini, mnamo mwaka wa 1905, Mnara wa Mlinzi, Septemba 1 lilionya: “Baada ya muda mfupi kutakuwa na vita vingi zaidi,” pia ukataja kwamba “msiba mkuu” ungeanza mwaka wa 1914.

Kwa hakika, mapema mwaka wa 1879, kichapo hicho kilitaja mwaka wa 1914 kuwa tarehe muhimu. Katika miaka ya baadaye kilitaja kwamba unabii wa Biblia katika kitabu cha Danieli ulikazia tarehe hiyo kuwa wakati ambapo Ufalme wa Mungu ulisimamishwa huko mbinguni. (Mathayo 6:10) Ingawa mwaka wa 1914 haukuwa wakati wa Ufalme huo kusimamia kabisa mambo duniani, ulikuwa wakati wa kuanza utawala wake.

Unabii wa Biblia ulitabiri: “Katika siku za wafalme hao [walioko katika siku zetu] Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme [huko mbinguni] ambao hautaangamizwa milele.” (Danieli 2:44) Ufalme huo, Kristo akiwa Mfalme wake, ulianza kukusanya watu wenye kumhofu Mungu hapa duniani wanaotamani kuwa raia wake.—Isaya 2:2-4; Mathayo 24:14; Ufunuo 7:9-15.

Kwa kusadifiana na kile kilichotukia mbinguni, mwaka wa 1914 ulikuwa mwanzo wa “siku za mwisho,” mwanzo wa kipindi cha wakati ambacho kingeishia kwenye uharibifu wa umalizio wa mfumo wa mambo uliopo sasa. Yesu alitabiri kwamba mwanzo wa kipindi hiki ungeashiriwa na vita vya ulimwengu, upungufu wa chakula, magonjwa ya mlipuko, matetemeko ya dunia yenye kuleta uharibifu na kuongezeka kwa uasi-sheria na vilevile kupoa kwa upendo wa watu kuelekea Mungu na wanadamu. Mambo hayo yote, alisema, yangeashiria “mwanzo wa maumivu makali ya ghafula.”—Mathayo 24:3-12.

Kutakuwa na Ulimwengu Mpya Kabisa Hivi Karibuni

Sasa tumeishi katika “siku za mwisho” kwa miaka 85, na tunakaribia haraka sana mwisho wa mfumo huu wa mambo usioridhisha. Karibuni Ufalme wa Mungu, chini ya utawala wa Kristo, “utavunja falme hizi zote [zilizoko sasa] vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.”—Danieli 2:44; 2 Petro 3:10-13.

Naam, Mungu ataondoa kabisa uovu duniani na kuingiza watu wenye moyo wa uadilifu kwenye ulimwengu mpya kabisa. “Wanyofu watakaa katika nchi, na wakamilifu watadumu ndani yake. Bali waovu watatengwa na nchi.”—Mithali 2:21, 22.

Ni ujumbe wenye shangwe kama nini—kwa hakika unastahili kutangazwa kila mahali! Hivi karibuni Ufalme wa Mungu utatatua matatizo ambayo yamezidishwa tu na karne ya 20: vita, umaskini, magonjwa, ukosefu wa haki, chuki, kutovumiliana, ukosefu wa kazi ya kuajiriwa, uhalifu, hali ya kutokuwa na furaha, kifo.—Ona Zaburi 37:10, 11; 46:8, 9; 72:12-14, 16; Isaya 2:4; 11:3-5; 25:6, 8; 33:24; 65:21-23; Yohana 5:28, 29; Ufunuo 21:3, 4.

Je, unavutiwa na taraja la kuishi milele katika ulimwengu wenye uadilifu ulio na furaha isiyoelezeka? Waombe Mashahidi wa Yehova wakupe habari zaidi. Kupitia nakala yako mwenyewe ya Biblia watakuonyesha kwamba miaka muhimu ya badiliko iliyoashiria karne ya 20 itaisha hivi karibuni na kwamba baada ya hapo unaweza kufurahia baraka zisizo na kikomo!

[Picha katika ukurasa wa 10]

Kutakuwa na ulimwengu mpya kabisa hivi karibuni

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki