Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g03 9/22 uku. 10
  • Mawasiliano Yanayoongoza Kwenye Uhai

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mawasiliano Yanayoongoza Kwenye Uhai
  • Amkeni!—2003
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Wewe Humsikiliza Mungu?
  • Kuwasiliana Ndani Ya Familia Na Katika Kundi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Je, Unawasiliana na Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Uwasiliano Katika Huduma Ya Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Yehova Na Kristo Wawasilianaji Mashuhuri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2003
g03 9/22 uku. 10

Mawasiliano Yanayoongoza Kwenye Uhai

KATI ya viumbe wote duniani, ni wanadamu peke yao ambao hawatosheki kuwasiliana tu na wanadamu wenzao. Hata iwe wao ni wa taifa gani, tabaka gani, jinsia gani, au wamesoma kadiri gani, wanadamu hutamani kuwasiliana na yule mtu mwenye cheo kikubwa kabisa, yaani, Mungu.

Je, huo ni ushirikina wa kijinga? La hasha! Kama ilivyotajwa katika makala iliyotangulia, Mungu aliwaumba wanadamu kwa mfano wake. Aliwaumba wakiwa na uhitaji wa kiroho. Hiyo inatia ndani tamaa ya kuwasiliana naye akiwa Baba yetu wa mbinguni. (Mwanzo 1:27; Mathayo 5:3) Ama kwa hakika, Mungu anaona mawasiliano yetu pamoja naye kuwa muhimu sana hivi kwamba anaitwa “Msikiaji wa sala.”—Zaburi 65:2, NW.

Ni pendeleo kubwa sana kusali kwa Mweza Yote! Watu wengi huona ni pendeleo kuzungumza faraghani pamoja na mtu mwenye cheo kikubwa, kama vile rais au waziri mkuu. Yehova Mungu ndiye mtu mwenye cheo kikubwa zaidi katika ulimwengu wote mzima! Na hatuhitaji kupanga miadi na yeye ili tuzungumze naye. Tunaweza kusali wakati wowote na mahali popote. Hata tunaweza kuzungumza na Mungu moyoni kimyakimya. (1 Samweli 1:12-15) Hata hivyo, Yehova anataka tuzungumze naye kutoka moyoni na kumsikiliza kwa kumtii. (Mika 6:8; Mathayo 6:5-13) Hayo ndiyo mawasiliano mazuri, kuzungumza na kusikiliza.

Je, Wewe Humsikiliza Mungu?

Mtu anawezaje kumsikiliza Mungu? Kwa kusoma na kutumia mafundisho yaliyo katika Neno lake lililoandikwa, Biblia Takatifu. (2 Timotheo 3:16; 2 Petro 1:20, 21) Yesu alisema hivi: “Binadamu lazima aishi . . . kwa kila tamko linalokuja kupitia kinywa cha Yehova.” (Mathayo 4:4) Je, wewe humsikiliza Mungu kwa kusoma na kutumia yale yaliyo katika Neno lake lililoandikwa?

Wale ambao huwasiliana na Yehova kwa ukawaida hukubaliwa naye na wanapata “amani ya Mungu izidiyo fikira yote kwa ubora.” (Wafilipi 4:6, 7; Mithali 1:33) Pia, wanatumaini kuishi milele katika dunia iliyo paradiso, ambayo haitakuwa na mahangaiko na matatizo tunayoyakabili leo. (Zaburi 37:29; Yohana 17:3) Hizo ni baraka nzuri sana zinazotokana na kutumia vizuri zawadi bora ya mawasiliano!

[Picha katika ukurasa wa 10]

Kusoma Biblia na kusali ni njia za kuwasiliana na Mungu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki