Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 2/09 kur. 8-9
  • Uandalizi wa Pekee kwa Ajili ya Wanadamu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uandalizi wa Pekee kwa Ajili ya Wanadamu
  • Amkeni!—2009
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ujuzi Unaoongoza Kwenye Uhai
  • Njia ya Kurudia Paradiso
    Amkeni!—1997
  • Kuishi Milele Si Ndoto Tu
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Unaweza Kuwa na Wakati Ujao Wenye Furaha!
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Uhai Una Kusudi Tukufu
    Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2009
g 2/09 kur. 8-9

Uandalizi wa Pekee kwa Ajili ya Wanadamu

WANADAMU wanahitaji mengi zaidi kuliko hewa, chakula, na maji. Ili tuwe na furaha ya kweli, tunahitaji kutosheleza uhitaji wetu wa kiroho. Tunahitaji kujua kusudi la maisha, na kwa nini tuko hapa. Kwa hiyo Yesu Kristo alisema: “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho.”—Mathayo 5:3.

Mungu ametuwezesha kutimiza uhitaji huo wa kiroho kupitia kitabu kitakatifu ambacho kimesambazwa sana duniani, Biblia Takatifu, ambayo inapatikana ikiwa nzima au kwa sehemu katika lugha 2,400 hivi. (2 Timotheo 3:16) Biblia inatuambia kwamba Mungu aliumba ulimwengu na uhai wote duniani. (Mwanzo, sura ya 1 na 2) Vilevile inatuambia kwamba alifanya kazi yake ya uumbaji katika “siku” sita za mfano, au vipindi vya wakati, na mpangilio huo unapatana na maoni ya wanasayansi kuhusu wakati uliotumiwa kutokeza vitu mbalimbali duniani.

Pia, Biblia inafunua kusudi la Mungu kwa wanadamu. Kusudi hilo linaelezwa katika Zaburi 37:29: “Waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake.” Ona kwamba waadilifu, yaani, wale wanaoishi kulingana na viwango vya maadili na kanuni zilizo katika Biblia, wataishi milele duniani si mbinguni. Bila shaka, wakati huo dunia haitakuwa sayari iliyochafuliwa kama ilivyo leo. Badala yake, itakuwa paradiso iliyoenea ulimwenguni pote.—Zaburi 104:5; Luka 23:43.

Ujuzi Unaoongoza Kwenye Uhai

Paradiso hiyo itakuwa mara mbili, yaani, paradiso halisi na ya kiroho. Isaya 11:9 inasema hivi: “Dunia hakika itajawa na kumjua Yehova kama vile maji yanavyoifunika bahari.” Ujuzi huo unapoingia moyoni unawachochea Wakristo wa kweli hata sasa kuishi kwa amani na upatano. Isitoshe, wanachukua kwa uzito maneno ya Yesu aliposali hivi: “Uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo.”—Yohana 17:3.

Ikiwa ungependa kujifunza zaidi kuhusu tumaini linalotajwa katika Biblia, Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia bila malipo yoyote.a

[Maelezo ya Chini]

a Unaweza pia kuwasiliana na Mashahidi wa Yehova kupitia Tovuti yao, www.watchtower.org.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki