Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 1/11 uku. 3
  • Je, Dini Inachochea Amani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Dini Inachochea Amani?
  • Amkeni!—2011
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Historia Yenye Jeuri
  • Kung’ang’ania Eneo “Takatifu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Je! Dini Imetosheleza Mahitaji Yetu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Sababu kwa Nini Dini ya Kilimwengu Itaisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Je, Dini Inapaswa Kulaumiwa?
    Amkeni!—2011
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2011
g 1/11 uku. 3

Je, Dini Inachochea Amani?

KANISA la Kaburi Takatifu huko Yerusalemu ambalo linasemwa kuwa ndilo kanisa takatifu zaidi la dini zinazodai kuwa za Kikristo, linahusianishwa na mizozo na chuki nyingi ya kidini. Inasemekana kwamba kanisa hilo lilijengwa “mahali ambapo Kristo alizikwa na kufufuliwa.” Hata hivyo, vita vingi vikatili vimepiganwa mahali hapo panapoonwa kuwa patakatifu. Watawa na makasisi kutoka dini sita za “Kikristo” wamekuwa na ugomvi kuhusu ni nani atakayelitumia kanisa hilo na wakati gani. Chuki hiyo imeongezeka katika miaka ya hivi karibuni. Imebidi polisi wa kuzuia fujo wenye bunduki waingilie kati na kulidhibiti kanisa hilo kwa muda.

Historia Yenye Jeuri

Matukio katika Kanisa la Kaburi Takatifu ni sehemu ya historia ndefu ya umwagaji wa damu na mauaji makubwa yanayohusianishwa na ushupavu wa kidini. Kitabu Violence in God’s Name kinasema hivi baada ya kuchunguza mapigano ya hivi karibuni katika sehemu mbalimbali duniani: “Kutoka Indonesia hadi Ireland Kaskazini, Mashariki ya Kati hadi Kashmir, India hadi Nigeria, nchi za Balkani hadi Sri Lanka, Wakristo, Wabudha, Wayahudi, Wahindu, Waislamu na Makalasinga wanajitetea kwamba wanatumia jeuri ili kulinda dini zao na masilahi yao.”

Hata hivyo, amani na upatano ni kati ya mafundisho makuu ya dini nyingi. Kwa miaka mingi, kanuni za kuwajali wengine kama vile kumpenda jirani na utakatifu wa uhai wa mwanadamu zimeendelezwa sana na dini. Kwa hiyo, je, dini hazipaswi kuwa mstari wa mbele kuwachochea watu wawe wenye amani? Waabudu wenye mioyo minyoofu wanapaswa kuchunguza swali hilo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki