Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g21 Na. 2 kur. 10-12
  • Teknolojia Inaathirije Ndoa Yako?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Teknolojia Inaathirije Ndoa Yako?
  • Amkeni!—2021
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UNACHOPASWA KUJUA
  • UNACHOWEZA KUFANYA
  • Jinsi ya Kutumia Teknolojia kwa Usawaziko
    Msaada kwa Ajili ya Familia
  • Jinsi ya Kuacha Kazi “Ibaki Kazini”
    Msaada kwa Ajili ya Familia
  • Tumieni Muda Mwingi Pamoja
    Msaada kwa Ajili ya Familia
  • Jinsi ya Kuepuka “Talaka ya Uzeeni”
    Msaada kwa Ajili ya Familia
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2021
g21 Na. 2 kur. 10-12
Mwanamume akiwa uwanja wa ndege anazungumza na mke wake aliye nyumbani kwa njia ya video.

Teknolojia Inaathirije Ndoa Yako?

Inapotumiwa vizuri, teknolojia inaweza kuimarisha uhusiano kati ya mume na mke. Kwa mfano, inaweza kuwasaidia wawasiliane siku nzima.

Hata hivyo, baadhi ya wenzi wa ndoa wameruhusu matumizi mabaya ya teknolojia . . .

  • yawanyang’anye wakati wanaotumia pamoja.

  • yawachochee kufanya kazi za ofisini wakiwa nyumbani isivyo lazima.

  • yafanye wasiaminiane.

UNACHOPASWA KUJUA

Mume na mke, kila mmoja akitumia simu yake usiku wa manane.

KUTUMIA WAKATI PAMOJA

Mume anayeitwa Michael anasema hivi: “Wakati mwingine mimi na mke wangu tunakuwa pamoja, lakini hanikazii uangalifu. Anajishughulisha tu na simu yake, na ananiambia kwamba hakupata nafasi ya kuangalia jumbe na mambo mengine hadi sasa.” Mume anayeitwa Jonathan anasema kwamba katika hali kama hizo “wenzi wa ndoa wanaweza kuwa pamoja lakini kiakili kila mmoja yuko mbali sana na mwenzake.”

JAMBO LA KUFIKIRIA: Ni mara ngapi unaruhusu simu, ujumbe mfupi, au taarifa fulani kwenye simu iingilie muda ambao ungetumia pamoja na mwenzi wako?​—WAEFESO 5:33.

KAZI

Baadhi ya watu wanafanya kazi ambazo zinawalazimu wajibu simu au barua pepe hata wakiwa nyumbani. Lakini si rahisi kwa watu wengine kuacha kazi zao kazini, hata ikiwa hawalazimiki kufanyia kazi nyumbani. Mwanamume anayeitwa Lee anakiri hivi: “Si rahisi kwangu kutojibu simu au ujumbe unaohusiana na kazi hata ikiwa utatumwa wakati ambao nilipanga niutumie pamoja na mke wangu.” Mwanamke anayeitwa Joy anasema hivi: “Ninafanyia kazi nyumbani, hivyo si rahisi kwangu kujua muda wa kuacha kufanya kazi. Ninajitahidi sana ili niwe na usawaziko.”

JAMBO LA KUFIKIRIA: Je, unamsikiliza kwa makini mume au mke wako anapozungumza nawe?​—LUKA 8:18.

UAMINIFU

Utafiti mmoja ulisema kwamba ugomvi mwingi kwenye ndoa unatokana na kutilia shaka matumizi ya mitandao ya kijamii. Asilimia kumi ya waliofanyiwa utafiti walikiri kwamba waliweka mtandaoni vitu ambavyo hawataki wenzi wao wajue.

Watu wengi wanaamini kwamba mitandao ya kijamii ina mitego mingi hatari inayoweza kuvunja ndoa au hata kufanya iwe rahisi kwa wenzi wa ndoa kuwa wazinzi. Haishangazi mawakili wengi wanaoshughulikia mambo ya talaka wanasema kwamba mitandao ya kijamii imechangia kuvunjika kwa ndoa nyingi.

JAMBO LA KUFIKIRIA: Je, unamficha mwenzi wako mawasiliano unayofanya na mtu wa jinsia tofauti?​—METHALI 4:23.

UNACHOWEZA KUFANYA

AMUA MAMBO YA KUTANGULIZA

Mtu anayepuuza kula chakula atakuwa na afya mbaya. Vivyo hivyo, si rahisi kwa mtu anayepuuza kutumia wakati pamoja na mume au mke wake, kuwa na ndoa nzuri.​—Waefeso 5:28, 29.

KANUNI YA BIBLIA: “Mhakikishe mambo muhimu zaidi.”​—WAFILIPI 1:10.

Weka alama kwenye mapendekezo ambayo ungependa kutumia, au andika mawazo yako kwenye sehemu iliyoachwa wazi yatakayosaidia ndoa yako isiathiriwe na teknolojia.

  • Kula angalau mlo mmoja pamoja kila siku

  • Kutenga muda hususa ambao hatutatumia vifaa vyetu

  • Kupanga muda au siku ya kufanya jambo lenye kufurahisha pamoja

  • Kuzima simu zetu usiku na kuziweka mbali na kitanda

  • Kutenga angalau dakika 15 kila siku za kuzungumza pamoja bila kuwa na vifaa vyetu vya kielektroni

  • Kupanga muda wa kuzima Intaneti

MASWALI AMBAYO WENZI WA NDOA WANAWEZA KUZUNGUMZIA

Baada ya wewe na mwenzi wako kuchunguza maswali haya kibinafsi, zungumzieni majibu pamoja.

  • Unaweza kutumia teknolojia kwa njia gani ili uimarishe ndoa yako?

  • Ni kwa kiwango gani teknolojia inaingilia muda mnaotumia pamoja?

  • Mngependa kufanya mabadiliko gani?

  • Je, ni rahisi kwako kuacha kazi ibaki kazini? Mwenzi wako anakubaliana na jibu lako?

  • Unawezaje kuwa na usawaziko inapohusu muda unaotarajia mwenzi wako atumie pamoja nawe?

    KANUNI YA BIBLIA: “Kila mmoja na aendelee kutafuta, si faida yake mwenyewe, bali faida ya yule mtu mwingine.”​—1 WAKORINTHO 10:24.

Jason na Alexandra.

“Ninafanyia kazi nyumbani, hivyo, muda wa kazi unapokwisha, ninajitahidi kuacha kufanya kazi. Pia, ninazima taarifa za barua pepe baada ya muda fulani ili niweze kutumia simu yangu kwa ajili ya mambo mengine kama vile kuangalia wakati bila kukengeushwa na kazi.”​—JASON, NA MKE WAKE, ALEXANDRA

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki