Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • tr sura 1 kur. 4-10
  • Baraka za Ajabu kutoka kwa Mungu Zakaribia Karibu!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Baraka za Ajabu kutoka kwa Mungu Zakaribia Karibu!
  • Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • BADILIKO LA ULIMWENGUNI POTE LAKARIBIA
  • KWELI IONGOZAYO KWENYE UZIMA WA MILELE
  • Kuishi Milele Si Ndoto Tu
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Siku za Mwisho za Taratibu Hii Mbovu ya Mambo
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Je! Mungu Anajali?
    Je! Mungu Anajali?
  • Karibuni Kusudi la Mungu Kutimizwa
    Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
Pata Habari Zaidi
Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
tr sura 1 kur. 4-10

Sura ya 1

Baraka za Ajabu kutoka kwa Mungu Zakaribia Karibu!

1. Kwa sababu ya hali za ulimwengu zinazozidi kuwa mbaya, ni maswali gani huzuka?

JE! WEWE wataka kuishi katika amani na furaha? Je! watamani afya njema na maisha mengi kwako mwenyewe na kwa wapenzi wako? Je! watamani kuona uovu na mateso yakimalizika? Kila mtu mwenye moyo mnyofu ataka mambo haya. Lakini leo, katika sehemu zote za dunia, jeuri, uvunjaji wa sheria, njaa na maradhi vinaongezeka. Kwa nini ulimwengu umejaa sana na taabu? Yote yana maana gani? Je! kuna sababu kamili kwa kusadiki kwamba hali zitakuwa nafuu kweli katika muda wa maisha yetu?

2 (a) Ni kitabu gani kinachotupa sababu kwa tumaini? (b) Kwa nini twaweza kuwa na sababu nzuri kufikiri kwamba Muumba mwenye upendo atakomesha hali zenye kuleta huzuni?

2 Ndiyo, kuna sababu kwa tumaini la namna hiyo, na imeandikwa waziwazi katika kitabu ambacho kimechapwa katika lugha zaidi kuliko kitabu kingine cho chote katika ulimwengu. Kitabu hicho ni Biblia. Kinatuambia juu ya kusudi la Mungu kusimamisha taratibu mpya nzima ya mambo kwa wanadamu. Ikiwa wewe ulikuwa na uwezo wa kufanya hivyo, je! usingezikomesha hali ziletazo huzuni nyingi sana? Bila shaka ungezikomesha! Je! tufikiri kwamba Muumba wa wanadamu atakosa kufanya? Biblia hutuambia kwamba “Mungu ni upendo.” (1 Yohana 4:8) Kwa hakika Baba huyu wa mbinguni mwenye upendo ajua wanadamu wanahitaji nini. Yeye yuna uwezo wa kutimiza mahitaji hayo, naye atafanya hivyo bila shaka, kwa maana Zaburi 145:16 husema kwa habari ya Mungu: “Waufumbua mkono wako, wakishibisha kila kilicho hai matakwa yake.”​—Tazama pia Kumbukumbu la Torati 32:4.

3. (a) Je! bado itakuwa muda mrefu kabla Mungu hajatosheleza tamaa ya wanadamu kwa amani na furaha? (b) Hali za ulimwengu zinazozidi kuwa mbaya ni ushuhuda wa nini?

3 Ni lini Mungu atakapoitosheleza tamaa ya wanadamu kwa amani ya kweli na furaha ya kweli, pamoja na afya na maisha yadumuyo? Je! ni lazima wanadamu wangojee maelfu ya miaka mingine? La! Wakati umekaribia karibu! Lakini hii yaweza kuwaje? Hali katika ulimwengu zinakuwa mbaya zaidi, si nafuu. Kweli, lakini Biblia ilionyesha waziwazi, zamani mbele, kwamba hali hizi hizi zingekuwa ushuhuda wa kwamba tunaishi katika “siku za mwisho” wa taratibu mbovu iliyopo. (2 Tim. 3:1-5) Karibuni Muumba mwenye upendo atakomesha uovu na wale wauletao pia. Lakini Mungu atawabariki kwa wingi watu wenye mioyo minyofu wanaotaka kufanya yaliyo haki, kwa maana yeye ameahidi hivi: “Ulimwengu unatoweka na ndivyo na tamaa yake, lakini yeye ambaye hufanya mapenzi ya Mungu hudumu milele.”​—1 Yohana 2:17, NW.

MAMBO AMBAYO MUNGU ATAWATENDEA WANADAMU

4. (a) Katika taratibu mpya ya Mungu, ni sababu gani ziletazo huzuni zitakazokuwa mambo ya zamani? (b) Mungu atatimizaje ahadi yake ya amani?

4 Lo! dunia hii itapata badiliko namna gani! Hakutakuwapo vita tena, wala hakutakuwapo mateso yo yote yaletwayo na vita. Chuki, choyo, uvunjaji wa sheria na jeuri vyote vitakuwa vitu vya zamani. Badala yake, kutakuwapo amani kamili na usalama duniani. Neno la Mungu mwenyewe hutangaza: “Bado kitambo kidogo asiye haki hatakuwapo; . . . wenye upole watairithi nchi, watajifurahisha kwa wingi wa amani.” (Zab. 37:10, 11) Amani ya namna hiyo haitakuwapo baina ya mataifa tu, bali miongoni mwa majirani na katika kila mtu wa nyumbani. Ebu fikiri hizo zingeweza kuwa baraka za ajabu kwako namna gani! Na inatumainisha namna gani kujua kwamba utimizo wa ahadi hii yenye kuchangamsha moyo haitegemei juu ya wanadamu! Ni Mungu ndiye atakayeitimiza. Jinsi gani? Kwa kuharibu waovu na kwa kuelimisha watu wake katika njia za amani.​—Mithali 2:21, 22; Isaya 54:13.

5. (a) Katika taratibu mpya, jambo gani litatukia kwa maradhi na mauti? (b) Ni maswali gani huzuka juu ya muda mfupi uliopo wa maisha ya wanadamu?

5 Miongoni mwa baraka nyingi ambazo watu watajifurahisha katika taratibu mpya yenye kufanywa na Mungu ni afya njema. Hata mauti, iletayo huzuni nyingi kwetu sote, haitakuwapo tena. Ahadi ya Muumba ni: “Naye [Mungu] atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena. . . . Tazama, nayafanya yote kuwa mapya.” (Ufunuo 21:4, 5) Hilo ni jambo ambalo hakuna mtawala wa kibinadamu, hakuna mtaalamu wa sayansi, hakuna daktari awezaye kulifanya; bali ni jambo ambalo Mungu atalifanya. Je! ni jambo la akili kwamba kusudi pekee la Mungu kwa mwanadamu ni kwamba atumie miaka ishirini akikua, labda miaka mingine ishirini au thelathini akipata maarifa na ujuzi, na upesi baada ya hapo aanze kuzeeka, kupatwa na maradhi na kufa? Kwa nini imempasa mwanadamu aishi kwa muda mfupi sana wakati hata labda kasa huishi kufika umri wa miaka mia mbili na huenda mti ukaishi kwa muda mrefu zaidi kupita? Mungu alimfanya mwanadamu kuishi, si kufa. Muumba huahidi kwamba karibuni itawezekana kujifurahisha uzima milele, apa hapa duniani. (Isaya 25:8) Kuwa na majirani wenye kupenda amani, afya njema na utendaji wenye kutosheleza kuzijaza maisha zetu, lo! hiyo itakuwa raha namna gani!

6. Twawezaje kuwa hakika kwamba taratibu hii mpya itakuja?

6 Wawezaje kuwa hakika kwamba taratibu hii mpya itakuja? Wawezaje kuwa hakika kwamba si ndoto tu? Waweza kutumaini kwa sababu Mungu mwenye Nguvu zote ameiahidi. Yeye aliyeuumba ulimwengu wote na huuendeleza ndiye ametoa uhakikisho wake kwamba itakuja. “Mungu asiyeweza kusema uongo.” (Tito 1:2) Neno lake halikosi kamwe kutimizwa. —Yoshua 23:14.

7. Hata ijapokuwa wanadamu walitumiwa kuandika Biblia, kwa nini twaweza kuikubali kwa kweli kama “neno la Mungu”?

7 Kweli hizi zenye kusisimua hupatikana katika Neno la Mungu, Biblia, Maandiko Matakatifu. Hakuna chanzo kingine cha habari kinachopatikana kwa wanadamu kielezacho katika njia yenye kutosheleza sababu kwa ambayo yametokea duniani na kusudi la Mungu kwa wanadamu. Ijapokuwa wanadamu walitumiwa kuandika Biblia, walifanya hivyo chini ya uongozi wa nguvu ya utendaji yenye uwezo ya Mungu au roho takatifu, hata kwamba “andiko lote liliongozwa na roho ya Mungu.” (2 Tim. 3:16, NW) Kama vile redio iwezavyo kupeleka habari kwako kupitia kwa hewa kwa njia isiyoonekana, ndivyo na nguvu ya utendaji isiyoonekana ya Mungu ilivyowaongoza waandikaji wa Biblia kuandika mambo ambayo yeye alitaka wanadamu wayajue. Ndiyo saba.bu mmojawapo wa waandikaji hao, mtume Paulo, angeweza kusema: “Mlipopata lile neno la ujumbe la Mungu mlilolisikia kwetu, mlilipokea si kama neno la wanadamu, bali kama neno la Mungu; na ndivyo lilivyo kweli kweli.”—1 Wathesalonike 2:13; tazama pia 2 Petro 1:20, 21.

BADILIKO LA ULIMWENGUNI POTE LAKARIBIA

8. Ni baadhi ya matukio gani ambayo Yesu alisema yangeonyesha siku za mwisho wa taratibu hii mbovu?

8 Neno la Mungu la kweli hutuambia waziwazi sana kwamba tunakaribia kwa haraka badiliko la ulimwenguni pote. Linatuonyesha kwamba wakati wetu ndio ule ambao Yesu Kristo alikuwa ameufikiria wakati alipotabiri mwisho wa taratibu hii mbovu. Yesu alitabiri mambo mengi ambayo wafuasi wake wa wakati ujao ingewapasa kutazamia hata wangejua ni lini mwisho ulipokuwa karibu. Yeye alisema kwamba siku za mwisho wa taratibu hii mbovu ungeonyeshwa na mambo kama vita vya ulimwengu, upungufu wa chakula, kuongezeka kwa uvunjaji wa sheria na ukosefu unaoongezeka wa imani katika Mungu. (Mathayo 24:3-12) Alisema kwamba kungekuwapo “huzuni kuu ya mataifa, wasijue njia ya kutokea.” (Luka 21:25, NW) Tumeona utimizo wa unabii huu katika muda wa maisha yetu.

9. Toa mfano au miwili ya ambayo watu wenye kujifunza matukio ya ulimwengu husema juu ya wakati wetu.

9 Watu wengi wajifunzao matukio ya ulimwengu wanasadikishwa kwamba badiliko kubwa linatokea bila shaka. Mwandikaji mashuhuri Walter Lippmann alisema: “Kwetu sisi sote ulimwengu ni wenye kuvurugana na wenye hatari, usiotawalika na kwa wazi usioweza kutawaliwa. Kila mahali kuna hofu kubwa na wasiwasi.” Aliongeza kwamba yote hii “nasadiki, huonyesha uhakika wa historia kwamba tunaishi kupita katika sura za kumalizia za njia ya kawaida ya maisha iliyosimamishwa.”a Pia, kama ilivyoripotiwa katika mwaka wa 1960, Katibu wa zamani wa Serikali ya United States, Dean Acheson, alitangaza kwamba wakati wetu ni “kipindi cha ukosefu wa imara usio na kifani, na jeuri isiyo na kifani.” Na akaonya: “Najua kwa kutosha juu ya mambo yanayotukia kuwahakikishia kwamba, katika miaka kumi na mitano tangu leo, ulimwengu huu utakuwa wenye hatari mno kuishi ndani yake.”b

10. (a) Twajuaje kwamba badiliko la ulimwengu li karibu sana? (b) Badiliko la ulimwengu lijalo linamaanisha uharibifu kwa nini?

10 Mambo mengi yote yaliyotabiriwa katika Neno la Mungu la kweli huonyesha kwamba wakati kwa badiliko la ulimwengu umewadia sasa hivi! Mambo tuyaonayo yakitukia ulimwenguni pote leo katika utimizo wa unabii wa Biblia huonyesha kwamba wakati wetu ndio wakati mtakamotokea uharibifu wa taratibu hii nzima iliyo mbovu. Serikali za kisasa zitaondolewa ili kuacha nafasi kwa utawala wa dunia yote kwa serikali ya Mungu. (Danieli 2:44; Luka 21 : 31, 32) Hakuna kitu kiwezacho kuzuia badiliko hili, kwa sababu Mungu amelikusudia.

KWELI IONGOZAYO KWENYE UZIMA WA MILELE

11. (a) Je! tunaweza kuepuka matokeo ya badiliko lijalo la ulimwengu? (b) Basi, tukitaka kuishi, lazima tufanye nini, kupatana na 1 Timotheo 2:4 na Yohana 17:3?

11 Badiliko la ulimwengu linalokuja litamhusu kila mtu aliye juu ya uso wa dunia, kutia na wewe. Ikiwa waupenda uzima na wataka kuishi, imekupasa ufanye haraka huyatwaa maarifa yaliyo sahihi ya Mungu, makusudi yake na matakwa yake. Hilo ndilo jambo ambalo Mungu ataka ulifanye, kwa maana ni mapenzi yake kwamba “aina yote ya watu ipate kuokolewa na kupata maarifa yaliyo sahihi ya kweli.” (1 Timotheo 2:4, NW) Maarifa yaliyo sahihi kutoka kwa Neno la Mungu la kweli yatawawezesha watu wenye mioyo minyofu kuokoka mwisho wa taratibu mbovu iliyopo. (Sefania 2:3) Yatafunua pia njia ya uzima wa milele katika taratibu mpya ya ajabu ya Mungu. Katika sala kwa Mungu Yesu Kristo alisema: “Hii maana yake n i uzima wa milele, kuyatwaa kwao maarifa yako wewe, Mungu wa kweli peke yako, na ya yeye ambaye ulimtuma, Yesu Kristo.”—Yohana 17: 3, NW; tazama pia Yohana 4:14.

12. Tuna sababu gani zenye nguvu kwa kutaka kujifunza kweli kutoka katika Biblia?

12 Jinsi inatia moyo kujua kwamba karibuni tutaona mwisho wa taabu zote za ulimwengu! Jinsi inasisimua kujua kwamba tunalo tumaini la kuingia upesi katika taratibu mpya ambamo twaweza kujifurahisha milele uzima kwa ukamili! Bila shaka jambo hili litampa kila mtu sababu zenye nguvu za kutaka kujifunza kweli kutokana na Biblia. Kwa kuitafuta kweli hii tunaanza kuweka “msingi mzuri kwa wakati ujao, ili [kupata] uzima ulio kweli kweli,” “uzima wa milele” katika taratibu mpya ya mambo ya Mungu.—1 Timotheo 6:19; AV.

[Maelezo ya chini]

a Newsweek, la Oktoba 9, 1967, ukur. 21

b U.S. News & World Report, la Juni 13 1950, kur. 116, 119.

[Picha katika ukurasa wa 4]

“Mungu . . . atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena.”​—Ufu. 21:3, 4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki