Sura ya 9
Yuko Aliye Juu Zaidi
WEWE umepata kumsikia ye yote akisema, “Kama ningekuwa mtu mzima ningeweza kufanya lo lote nitakalo”?— Wewe umepata kusema hivyo?—
Ni kweli kwamba watu wazima wanaweza kufanya mambo ambayo watoto hawawezi kufanya. Lakini hakuna mmoja wetu awezaye kutufanyia kanuni zetu zote za maisha. Yuko aliye juu zaidi kuliko sisi. Unamjua nani huyo?
Karibu watu wote wanakubali kwamba hakika Mungu yuko juu zaidi kuliko sisi. Lakini haifai kusema hivyo tu. Yatupasa tuonyeshe kwamba tunaamini hivyo kwa mambo ambayo tunafanya.
Hii inaonyeshwa kwa jambo lililowapata Adamu na Hawa. Walikuwa mwanamume na mwanamke wa kwanza. Watu wengine wanasema hadithi juu ya Adamu na Hawa si ya kweli. Lakini Mwalimu Mkuu hakusema hivyo. Yeye alijua ilikuwa ya kweli. Sikiliza, nami nitakuambia jambo lililotukia.
Wakati Mungu alipomfanya Adamu na Hawa, aliwaweka katika bustani nzuri mahali paitwapo Edeni. Ilikuwa shamba la kutembelea, paradiso. Wangaliweza kuishi humo milele. Lakini lilikuwako somo ambalo iliwapasa wajifunze. Nalo ni somo ambalo na sisi yatupasa tuji-funze. Si gumu. Ni jepesi ikiwa kweli twataka tujifunze.
Yehova akamwambia Adamu na Hawa kwamba wangeweza kula matunda yote na karanga ambazo wangetaka kutoka kwa miti katika Edeni. Lakini ulikuwako mti mmoja ambao kwa huo iliwapasa wasile. Yehova alimwambia Adamu: “Walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.”—Mwanzo 2:17.
Kungetukia nini ikiwa wangekula kutoka kwa mti huo mmoja? Wangekufa. Uhai wao ulitegemea kumtii Yehova Mungu. Haikufaa kusema walimwamini Mungu tu. Iliwapasa waonyeshe kwa mambo ambayo walifanya. Hilo ndilo lililokuwa somo. Kwa kweli halikuwa gumu, sivyo? Lakini lilikuwa la maana sana.
Ikiwa Adamu na Hawa wangemtii Mungu, wangekuwa wakionyesha walimpenda na walitaka awe Mtawala wao. Lakini ikiwa wangekula kutoka kwa mti huo, ingeonyesha nini?— Ingeonyesha kweli hawakupiga asante kwa mambo yote ambayo Mungu alikuwa amewapa. Wangekuwa wakisema hivi: “Hakuna mtu awezaye kutuambia sisi jambo Ia kufanya. Sisi tutafanya kadiri tunavyopenda.”
Wewe ungalifanya nini ikiwa ungalikuwako huko? Je! ungalimtii Yehova? Au ungalikula kutoka kwa mti huo?—
Kwanza Adamu na Hawa walimtii Mungu. Lakini ndipo nyoka siku moja akasema kwa Hawa. Kweli, nyoka hawezi kusema mwenyewe. Alikuwa malaika aliyejifanya ionekane kana kwamba ni nyoka aliyekuwa akisema. Malaika huyo alikuwa ameanza kufikiri mambo mabaya. Alitaka Adamu na Hawa wamwabudu yeye. Alitaka wafanye mambo ambayo alisema. Alitaka kuwa pahali pa Mungu.
Basi malaika huyo mbaya akatia mawazo mabaya katika akili za Hawa. Akamwambia: ‘Mungu hakuwaambia ninyi kweli. Hamtakufa mkila kutoka kwa mti ule. Mtakuwa na hekima kama Mungu.’ Je! wewe ungaliamini ambayo sauti hiyo ilisema?—
Hawa hakuwa na haki kuamini aliyosema nyoka. Kila kitu alichokuwa nacho kilitoka kwa Mungu. Lakini sasa akaanza kutaka jambo fulani ambalo Mungu hakuwa amempa. Akala kutoka kwa mti ule. Halafu akampa Adamu sehemu yake.
Adamu hakuamini aliyosema nyoka. Lakini kutaka kwake awe pamoja na Hawa kukawa na nguvu zaidi kuliko kumpenda Mungu. Basi naye akala kutoka kwa mti ule.—Mwanzo 3:1-6.
Matokeo yalikuwa nini?— Mungu hakuwa amesema uongo. Uhai unategemea kumtii yeye. Basi Adamu na Hawa wakafa. Nao wakapeleka kifo kwa wanadamu wote.
Biblia inatuambia kwamba malaika yule aliyesema uongo kwa Hawa anaitwa Shetani Ibilisi. Yeye ni adui wa Mungu. Naye ni adui yetu sisi.—Ufunuo 12:9.
Yeye anataka kila mtu asimtii Yehova. Hivyo anajaribu kuweka mawazo mabaya katika akili zetu. Yeye anasema hakuna mtu kweli anayempenda Yehova. Anasema wewe na mimi hatumpendi Mungu na kwamba kweli hatutaki kufanya ambayo Mungu anasema. Lakini je! anasema kweli? Je! sisi tuko hivyo?—
Mwalimu Mkuu alisema kwamba Ibilisi ni mwongo! Yeye alionyesha wazi kwamba kuna watu wanaompenda Yehova kweli kweli. Yeye hakusema: ‘Hakuna mtu awezaye kuniambia jambo la kufanya.’ Bali, yeye alisema: “Baba ni mkuu kuliko mimi.” Alimtii Yehova. Naye hakufanya ilipokuwa vyepesi tu. Yeye alifanya wakati wote, hata wakati watu wengine walipofanya iwe vigumu kwake. Yeye alikuwa mwaminifu kwa Yehova mpaka kufa. Ndiyo sababu Mungu alimfufua, aishi milele.—Yohana 14:28.
Ndivyo alivyofanya Mwalimu Mkuu. Lakini sisi tutafanya nini?— Tusipomtii Yehova, basi tunafanya analotaka lbilisi tufanye. Lakini ikiwa kweli twampenda Mungu wetu, tutatii amri zake. Tutafanya hivyo kila siku. Nasi tutafanya hivyo kwa sababu kweli ndivyo tunataka.
(Tutamtumikia nani—Yehova au Ibilisi? Soma ambayo Biblia inasema juu ya shauri hili katika Ayubu 1:8-12; 2:1-5; 27:5; Mithali 27:11.)