Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • te sura 35 kur. 143-146
  • “Furaha Zaidi katika Kutoa”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Furaha Zaidi katika Kutoa”
  • Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya Kuwa Wenye Furaha
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
  • Kupata Furaha ya Kweli kunategemea Wewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Je, Una Roho ya Kutoa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Ni Nini Siri ya Kupata Furaha?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
te sura 35 kur. 143-146

Sura ya 35

“Furaha Zaidi katika Kutoa”

MIMI najua siri. Ungependa kuisikia?— Ni siri ya furaha.

Kuna watu wengi wasio na furaha. Wengine wanategemea mno yale ambayo watu wengine wanafanya. Ikiwa mtu fulani anawapa kitu kizuri, wanafurahi. Ikiwa mtu hawafanyii kitu fulani cha pekee, hawafurahi.

Sasa, hii ndiyo siri. Mwalimu Mkuu alisema: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko zilivyo katika kupokea.” Basi, mwenye furaha kupita wote si mtu anayepokea vitu, bali yeye anayewapa watu wengine. Wewe ulijua hilo?— —Matendo 20:35, NW.

Ebu fikiria maana yake. Je! Yesu alisema kwamba mtu aliyepokea zawadi hangefurahi? Sivyo. Wewe unapenda kupokea zawadi, sivyo?— Hata mimi. Tunafurahi wakati tunapokea vitu vizuri.

Lakini Yesu alisema kwamba kuna furaha hata zaidi wakati tunapotoa. Na sikuzote Yesu alisema kweli, sivyo?

Sasa, kuna nini ambacho twaweza kuwapa watu wengine? Wewe ungesema ni kitu gani?—

Mara nyingine unapotaka kutoa zawadi, inakupotezea fedha. Ikiwa ni zawadi ambayo unapata dukani, itakupasa ulipe. Basi, ikiwa unataka kutoa zawadi ya namna hiyo, itakupasa kuweka akiba ya fedha mpaka upate za kutosha kununua zawadi.

Lakini si zawadi zote zinatoka madukani. Acha nieleze. Siku ya joto hakuna kitu kizuri kuliko bilauri au kikombe cha maji ya baridi. Si lazima uende dukani ukapate huko. Hata hivyo wakati unampa mtu fulani aliye na kiu, unaweza kuwa na furaha inayotokana na kutoa.

Pengine siku moja wewe na mama yako mwaweza kutengeneza maandazi. Hiyo inaweza kuwa furaha. Na wakati ule ule yanapotoka jikoni, yanakuwa matamu sana. Lakini tungeweza kufanya nini na maandazi mengine ambacho kingetufurahisha hata zaidi kuliko kuyala yote sisi peke yetu?—

Ndiyo, furaha kubwa zaidi inatokana na kutoa. Tunaweza sisi kufurahia kuyala mengine peke yetu. Lakini, ikiwa tunataka furaha hata zaidi, basi tunaweza kufunga machache na kutuma kama zawadi kwa mmoja wa rafiki zetu. Je! wewe ungependa kufanya jambo hilo wakati fulani?—

Mtume Paulo alikuwa mtu aliyejua furaha ya kutoa. Yeye aliwapa watu wengine nini?— Yeye alikuwa na kitu cha kutoa kilicho bora kuliko vyote katika ulimwengu. Yeye alijua kweli ya Mungu na juu ya Yesu. Kwa furaha alishiriki pamoja na wengine. Naye alifanya hivyo bila kumwacha mtu ampe fedha kwa msaada wake.

Wakati mmoja mtume Paulo na mwenzi wake Luka walimkuta mwanamke ambaye naye alitaka kuwa na furaha ya kutoa. Walimkuta karibu na mto. Paulo na Luka walikuwa wamekwenda huko kwa sababu walisikia kwamba palikuwa mahali pa kusali. Na kwa hakika, waliwakuta wanawake wengine hapo.

Paulo alianza kuwasimulia wanawake hawa mambo mazuri juu ya Yehova Mungu na ufalme wake. Mmoja wao jina lake Lidia alisikiliza sana. Alipendezwa sana sana na mambo ambayo alisikia. Naye alitaka kufanya jambo fulani ili aonyeshe kushukuru kwake.

Luka anatuambia hivi: ‘Akatuomba: “Kama mmeniona kuwa mwaminifu kwa [Yehova], ingieni nyumbani mwangu mkakae.” Akatushurutisha.’—Matendo 1 6:11-15.

Lidia alifurahi kuwa na watumishi hawa wa Mungu katika nyumba yake. Aliwapenda kwa sababu walikuwa wamemsaidia ajifunze njia ya Mungu kwa watu ya kuishi milele. Ilimfurahisha kuweza kuwapa chakula na mahali pa kulala.

Basi, upaji wa Lidia ulimfurahisha kwa sababu kweli yeye alitaka kutoa. Na hilo ni jambo ambalo imetupasa tukumbuke. Labda mtu fulani atatuambia kutoa zawadi. Lakini ikiwa kweli sisi hatutaki kutoa, hapo upaji hautatufurahisha.

Je! kwa mfano, namna gani ikiwa ungekuwa na peremende ambalo ungetaka kula? Ikiwa ningekuambia kwamba umpe mtoto mwingine, je! ingekufurahisha kumpa? — Lakini labda una peremende wakati unapomkuta rafiki ambaye unapenda sana. Ikiwa ungefikiria wewe mwenyewe kwamba ingekuwa vizuri umgawie rafiki yako peremende, hapo ungefurahia kutoa, sivyo?—

Na, unajua kwamba mara nyingine tunampenda mtu sana sana hata tunataka kumpa kila kitu, na bila kunyima ko kote? Tunapoendelea kuwa na upendo mwingi, ndivyo imetupasa tuone juu ya Mungu.

Mwalimu Mkuu alijua mwanamke aliyeona hivyo. Alimwona katika hekalu katika Yerusalemu. Yeye alikuwa na senti ndogo mbili tu; hizo tu ndizo alikuwa nazo basi. Lakini yeye alizitia zote mbili katika kisanduku kama mchango au zawadi kwa hekalu. Hapana mtu aliyemwambia atoe. Yeye alitoa kwa sababu alitaka, kwa sababu alimpenda Mungu kweli kweli. Ilimfurahisha kuweza kutoa.

Basi, kuna njia nyingi ambazo katika hizo twaweza kutoa, sivyo?— Naye Mwalimu Mkuu anajua kwamba ikiwa tunatoa kwa sababu sisi tunataka, tutakuwa wenye furaha. Ndiyo maana anatuambia hivi: “Jizoezeni upaji.” Ndiyo kusema, fanya yawe mazoea kuwapa watu wengine. Tukifanya hivyo, hatutahuzunika kwa sababu ya kumngojea mtu mwingine atufanyie kitu fulani kizuri. Tutafanya bidii katika kuwafurahisha watu wengine. Na tunapofanya hivyo, sisi ndio wenye furaha zaidi kupita wote!—Luka 6:38, NW.

(Mawazo mazuri zaidi juu ya namna ya upaji unaoleta furaha yanapatikana katika Mathayo 6:1-4, 2 Wakorintho 9:7 na Luka 14: 12-14.)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki