Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w76 6/15 kur. 271-273
  • Ahadi ya Paradiso ya Kiroho

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ahadi ya Paradiso ya Kiroho
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Habari Zinazolingana
  • Ujumbe Wenye Tumaini kwa Mateka Walioshuka Moyo
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
  • Uamuzi wa Hakika Unatakiwa kwa Wale Wanaopata Kimbilio
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Hakuna Kudhuru Wala Kuharibu Katika Paradiso ya Kiroho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Ambayo Kuzaliwa kwa Taifa hilo Kumemaanisha kwa Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
w76 6/15 kur. 271-273

Ahadi ya Paradiso ya Kiroho

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

1. (a) Ni nini linaloonyesha kwamba, hata alipokuwa Yesu. alikuwa akifikiria wanadamu Paradiso? (b) Miaka iliyofuata, Yesu aliliambia nini kundi la Efeso juu ya Paradiso? (c) Je! mitajo yote hii ilikuwa juu ya paradiso ile ile?

MTUMISHI wa Kimasihi wa Yehova Mungu ana sehemu ya maana sana katika kupata kwetu paradiso. Hata usiku ule wenye huzuni karne kumi na tisa zilizopita, wakati Yesu Kristo alipokuwa akihesabiwa pamoja na wakosaji kwa utimizo wa Isaya 53:12, alikuwa akifikiria wanadamu Paradiso. Mmoja wa wanyang’anyi wawili, waliotundikwa kila upande wake, alipomwambia, “Bwana, unikumbuke wakati unapokuya katika ufalme wako,” alijibu hivi: “Kweli ninakuambia, Leo [,] utakuwa pamoya nami katika Paradiso.” (Luka 23:39-43, CSB; Marko 15:25-27) Miaka 63 baadaye, alipokuwa akiliambia kundi la Kikristo katika Efeso, Asia Ndogo, Yesu aliyefufuliwa alisema hivi: “Yeye ashindaye nitamruhusu ale kutokana na mti wa uzima, ulio katika paradiso ya Mungu.” (Ufu. 2:7; NW) Kwa kuwa ahadi hizi waliahidiwa watu wa namna mbalimbali, ya kwanza, wale wasio Wakristo na ya pili, Wakristo wenye kushinda, bila shaka paradiso mbili zinamaanishwa hapa, ya kwanza ni ile ya kidunia, ya pili ile ya kimbinguni. “Mtumishi” wa Yehova anashughulika na zote mbili.

2. Ni Paradiso ya namna gani, iliyotabiriwa na Isaya yaweza kufurahiwa leo, bila kungojea mpaka baada ya kufa na kufufuka kwa mtu?

2 Kila moja ya paradiso hizo ilikuwa ya wakati ujao Yesu alipokuwa akizitaja. Pia, zilikusudiwa zifurahiwe baada ya kufa na kufufuka kwa mtu kutoka kwa wafu katika wakati wa Mungu tu. Lakini kuna paradiso inayofurahiwa na wale wanaoishi duniani sasa. Kwa kuwa mazingira ya kidunia ya wanadamu yanachafuliwa zaidi na zaidi nao uso wa dunia si paradiso leo, paradiso inayofurahiwa sasa duniani na waabudu wa kweli wa Kikristo wa Yehova yapaswa iwe ya mfano, paradiso ya kiroho. Unabii wa Isaya kwa habari ya Mtumishi wa Kimasihi wa Yehova ulitabiri kusimamishwa kwa paradiso hii ya kiroho kwa ajili ya waaminifu wa Yehova.

3. (a) Ni nani aliyetabiriwa na Isaya alipaswa awe na sehemu ya maana katika kufanyizwa kwa paradiso ya kiroho duniani? (b) Kama ‘mwana wa Mungu,’ alikuwa na uhusiano gani na tengenezo lote la kimbinguni?

3 Kulingana na unabii wa Isaya, yule Mtumishi wa Kimasihi anashughulika na kuletwa kwa paradiso ya kiroho duniani. Kabla ya kutimiza sehemu yake duniani kama ilivyotabiriwa katika sura ya 53 ya Isaya, alikuwa mshiriki wa tengenezo la Yehova la kimbinguni la “wana wa Mungu” waaminifu. (Ayubu 1:6; 2:1; 38:7; Dan. 3:25) Tengenezo hilo la kimbinguni la kiroho latenda kama “mke” aliyeolewa na Yehova Muumba, kama vile taifa la kale la Israeli, lilipoingizwa katika agano la Torati pamoja naye kupitia kwa mpatanishi Musa, lilivyokuwa kama limeolewa na Yehova na lilifananishwa kama mke Wake wa kidunia, Basi Yeye anatenda kama Mume wa mwungano huu wa kimbinguni. (Isa. 54:5; 50:1; Yer. 31:31-34) Kwa kuwa “wana wa Mungu” wa kimbinguni walionwa kama watoto wa tengenezo la Mungu la kimbinguni kwa sababu ya kuwa washiriki wake, tengenezo la kimbinguni lilionwa kama mama yao, mke wa Baba yao wa kimbinguni. Hivyo yule Mtumishi anayetajwa katika Isaya 53:11 ni mmojawapo wa wanawe.

4. (a) Tengenezo la Yehova la umama mbinguni lilimtokezaje Masihi aliyeahidiwa? (b) Matokeo yalikuwa nini mbinguni Yesu alipotiwa mafuta, na baadaye alipofufuliwa kutoka kwa wafu?

4 Yehova alichagua mwanawe mkuu wa kimbinguni atumike kama Mtumishi wa Kimasihi duniani. (Isa. 52:13; 53:11) Hivyo tengenezo la Yehova la kimama mbinguni lilimtoa huyu awe mshuhudiaji mkuu wa enzi kuu ya ulimwengu wote ya Mumewe. Huyu alipokwisha kubatizwa na Yohana Mbatizaji katika Mto Yordani wakati alipokuwa duniani, Yehova, Mume, alimmiminia Yesu aliyebatizwa roho Yake takatifu, akimfanya mtiwa mafuta, Kristo. Katika njia hii yule Masihi au Kristo aliyeahidiwa akatokezwa. Lo! yule Mama wa kimbinguni na vile vile Mumewe walifurahi! Kama wana wa Mungu wa kimalaika walikufurahia kuzaliwa kwa kitoto Yesu katika Bethlehemu-Yuda, bila shaka walikuwa wanayo furaha zaidi alipokuwa hivyo Kristo aliyeahidiwa, yule Mtumishi wa Kimasihi wa Mungu wao Yehova. (Luka 2:10, 13, 14; Mt. 3:13-17; Yohana 16:21) Uhai wake ulipoondolewa duniani naye akafufuliwa kutoka kwa wafu, lile tengenezo la kimama mbinguni lilimpokea tena kama “mzaliwa wa kwanza katika wafu.” na kufurahi kuwa naye tena miongoni mwa wanawe wa kimbinguni. (Kol. 1:18; Ufu. 1:5, 17, 18) Furaha yake ilitabiriwa!

5, 6. (a) Ni sababu gani iliyopewa katika Isaya 54:1 kwa kufurahi kwa “mwanamke” huyu wa kimbinguni? (b) Alipaswa awe mama wa kiroho wa “wana” wangapi?

5 “Imba,” asema Isaya 54:1, “wewe uliye tasa, wewe usiyezaa; paza sauti yako kwa kuimba, piga kelele, wewe usiyekuwa na utungu; maana watoto wake aliyeachwa ni wengi kuliko watoto wake yeye aliyeolewa, asema [Yehova].”

6 Mtume wa Kikristo Paulo halitumii andiko hili lililoongozwa na Mungu kwa habari ya taifa la Kiyahudi baada ya kuhamishwa kwalo katika Babeli, bali kwa habari ya tengenezo la Yehova mbinguni lililo kama mke. Kulingana na unabii wa Isaya, tengenezo la Mungu la kimbinguni lilipaswa liwe na watoto zaidi ya Masihi Yesu, ambaye alikuwa amengojea muda mrefu kana kwamba kwa utasa. Kwa hiyo alipaswa awe mama wa kiroho wa washiriki wa Masihi Yesu 144,000. Yeye alipaswa awe Mzaliwa wa Kwanza miongoni mwa wana hawa zaidi wa kiroho wa mama. Furaha ya mama huyo ingeanza wakati alipomzaa Masihi Yesu, mzaliwa wa kwanza, lakini angeendelea kuzaa warithi wote washirika wa Ufalme wa Masihi Yesu. Mtume Paulo alikuwa mmojawapo wa warithi hawa washirika waliotazamiwa wa Kristo, naye ndiye aliyetumia maneno ya Isaya 54:1 kwa kuongozwa na Mungu.

7-9. Anapotofautisha taifa la Kiyahudi na tengenezo la Mungu la kimbinguni, mtume Paulo anatumiaje maneno ya Isaya 54:1?

7 Akitofautisha taifa la Kiyahudi lililokuwa limeolewa na Yehova Mungu kupitia kwa agano la Torati la Musa (lakini lililokuwa limemkana Yesu Kristo) na tengenezo la Mungu la kimbinguni lililo kama mke, mtume Paulo anaandika hivi: “Kwa maana imeandikwa ya kuwa, Ibrahimu alikuwa na wana wawili, mmoja kwa mjakazi [Hajiri Mmisri], na mmoja kwa mwungwana [Sara mkewe]. Lakini yule [aitwaye Ishmaeli] wa mjakazi alizaliwa kwa mwili [kabla Ibrahimu hajakoma kuzaa], yule [aitwaye Isaka] wa mwungwana kwa ahadi [kutoka kwa Mungu]. Mambo haya husemwa kwa mfano; kwa maana hawa [wanawake Hajiri na Sara] ndio kama maagano mawili, moja kutoka mlima Sinai [kupitia kwa Musa], lizaalo kwa utumwa, ambalo ni Hajiri [yule mjakazi]. Maana Hajiri ni kama mlima Sinai ulioko Arabuni, umeiingana na Yerusalemu wa sasa; kwa kuwa anatumika pamoja na watoto. Bali Yerusalemu wa juu ni mwungwana, naye ndiye mama yetu sisi.

8 “Kwa maana imeandikwa [katika Isaya 54:1], Furahi, wewe tasa, [Yerusalemu wa juu] usiyezaa; paza sauti, ulie, wewe usiye na utungu; maana watoto wake aliyeachWa pekee ni wengi kuliko wa huyo aliye na mume. Basi, ndugu zangu, kama Isaka sisi tu watoto wa ahadi. Lakini kama vile siku za yule [Ishmaeli ] aliyezaliwa kwa mwili alivyomwudhi yule aliyezaliwa kwa [roho], ndivyo ilivyo na sasa. Lakini lasemaje andiko? Mfukuze mjakazi na mwanawe, kwa maana mwana wa mjakazi hatarithi kabisa pamoja na mwana wa mwungwana. Ndiposa, ndugu zangu, sisi si watoto wa mjakazi, bali tu watoto wa huyo aliye mwungwana.

9 “Katika ungwana huo Kristo alituandika huru.”​—⁠Gal. 4:22 mpaka 5:1.

10, 11. (a) Isaya 54:13 huonyeshaje kwamba yule “Yerusalemu wa juu” angekuwa na watoto wa kiroho wengi zaidi kuliko Yesu tu? (b) Yesu Kristo alitumia andiko hilo juu ya nani?

10 Ndiyo sababu “Yerusalemu wa juu,” ambaye Muumba wake Mkuu Yehova ndiye mumewe anaambiwa katika Isaya 54:13 kwamba alipaswa awe na Watoto wa kiroho wengi zaidi ya Masihi Yesu, mzaliwa wake wa kwanza: “Na watoto wako wote watafundishwa na [Yehova]; na amani ya watoto wako itakuwa nyingi.”

11 Yesu Kristo alitumia andiko hilo kwa habari ya wanafunzi wake mwenyewe, alipowaambia Wayahudi hivi: “Imeandikwa katika manabii, Na wote watakuwa wamefundishwa na [Yehova]. Basi kila aliyesikia na kujifunza kwa Baba huja kwangu.” (Yohana 6:45) Lilikuwa kusudi la Baba Yesu “awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.” (Rum. 8:29) Yule “Yerusalemu wa juu” ndiye mama pia wa kimbinguni wa ndugu hawa wote wa kiroho wa Yesu Kristo. Basi, badala ya Yerusalemu wa kidunia aliyemkataa Masihi, Yehova, mume wake anamwita kwa sababu nzuri ‘aimbe’ na ‘kupaza sauti kwa kuimba’ kwa sababu ya kuwa mama wa wana wengi sana wa kiroho mwishowe pamoja na Masihi Yesu.​—⁠Isa. 54:1.

12. Isaya sura ya 54 yamalizika kwa kutia moyo gani kwenye nguvu kwa wana hawa wa kiroho?

12 Wana hawa wa kiroho wanahakikishwa ulinzi na kuhifadhiwa kwa kimungu kama kunavyosemwa katika maneno haya anayoambiwa “Yerusalemu wa juu”: “Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa, na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa [Yehova], na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema [Yehova].” Sura ya 54 ya Isaya inayohusu “Yerusalemu wa juu” yamalizika kwa kutia moyo hivyo kwa nguvu.​—⁠Isa. 54:17.​—⁠Kutoka Kitabu Man’s Salvation Out of World Distress at Hand!, sura ya 6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki