Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 3/15 kur. 20-24
  • Roho Takatifu Yatenda Kazi Katika Makao ya Mbinguni Yasiyoonekana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Roho Takatifu Yatenda Kazi Katika Makao ya Mbinguni Yasiyoonekana
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MAKUSANYIKO YA WATU WA KIROHO MBINGUNI
  • Maono Kuhusu Makao ya Roho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Mungu wa “Mwana-Mfalme wa Amani” Awa “Vitu Vyote kwa Kila Mmoja”
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Ikiwa Mungu Ana Tengenezo, Ni Tengenezo Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Chanzo cha Kimungu cha Roho Takatifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 3/15 kur. 20-24

Roho Takatifu Yatenda Kazi Katika Makao ya Mbinguni Yasiyoonekana

(Funzo la Kitabu)

1. Kwa sababu gani ni jambo la maana kwetu kujua jinsi roho takatifu imetenda kazi katika makao ya mbinguni yasiyoonekana?

HUENDA wanadamu wakawa wanapendezwa zaidi na jinsi roho takatifu ya Mungu inavyotenda kazi katika makao yaonekanayo au katika ulimwengu wote ujulikanao na wanadamu. Lakini, mambo ambayo yametukia katika makao ya mbinguni yasiyoonekana yamehusu sana mambo ya wanadamu. Njia ambayo roho takatifu itatendeshwa kazi karibuni, katika kizazi chetu wenyewe, inahusiana na yanayotukia katika makao yasiyoonekana nayo ni ya maana sana kwa wanadamu. Kwa hiyo yatupasa kufahamu jinsi roho takatifu inavyotenda kazi katika habari hiyo ambayo ni ya maana sana kwetu.

2. Zaburi 104:​29, 30 yaonyeshaje jinsi wanadamu wanavyotegemea makao ya mbinguni yasiyoonekana?

2 Huenda wanadamu wa kisasa wakawa hawataki uhakika wa kwamba wanategemea makao ya mbinguni yasiyoonekana. Kama Mungu Muumba angeacha kutuangalia sisi tuliopo duniani, awe ‘mfu’ kwetu, ingekuwaje? Mtunga zaburi wa Biblia alisema kweli alipomwambia Mungu hivi: “Wewe wauficha uso wako, wao wanafadhaika; waiondoa pumzi yao, wanakufa, na kuyarudia mavumbi yao, waipeleka roho yako, wanaumbwa, nawe waufanya upya uso wa nchi.” (Zaburi 104:​29, 30) Kwa hiyo mwanadamu hapaswi kufanya uchunguzi mkuu juu yake mwenyewe, bali juu ya Muumba, Mungu. Kwa kadiri ambavyo Mungu anapendezwa kutufunulia jinsi makao ya mbinguni yasiyoonekana yalivyo, twapaswa kufanya uchunguzi.

3. Kwa sababu gani ungekuwa upumbavu kwetu kuwaza kwamba Mungu hukaa peke yake na mazingira yake mbinguni hayapendezi?

3 Na tukumbuke nyakati zote kwamba “Mungu ni Roho.” (Yohana 4:​24, na maelezo ya pambizoni) Kwa hiyo, yeye huishi katika makao ya kiroho. Je! yeye huishi peke yake, katika mazingira yasiyopendeza? Hapana! Ungekuwa upumbavu kwetu kuwaza kwamba Mungu ana uwezo wa kuumba vitu vionekanavyo tu na kwamba hakuumba vitu katika makao ya mbinguni yasiyoonekana. Vitu hivyo vya makao ya juu zaidi vingekuwa bora kuliko vile vya uumbaji unaoonekana ambao sisi wanadamu ni sehemu yake.

4. Kwa sababu gani makao ya mbinguni yasiyoonekana hayategemei jua letu ili kupata nuru?

4 Tunapofikiria vitu vyote vya ajabu na vizuri ambavyo Mungu ameweka hapa katika makao yanayoonekana, tunastaajabu tujaribupo kufikiria vitu vyote vya ajabu na vitukufu ambavyo ameumba katika makao ya kiroho. Makao hayo ya juu hayategemei jua letu ili yapate nuru. Hakuna usiku huko! Muumba wa majua yenye kutoa nuru ndiye Jua la mbinguni yeye mwenyewe, chanzo cha nuru. Kwa njia halisi, ya mfano na ya adili, ni kweli kwamba: “Mungu ni nuru, wala giza lo lote hamna ndani yake.” (1 Yohana 1:5) Muda mrefu kabla Yohana mwandikaji wa Biblia hajasema hayo, mtunga zaburi alimweleza Muumba kuwa mwenye kufurahisha kama nuru ya mchana ya jua, alipoandika hivi: “[Yehova], Mungu, ni jua na ngao, [Yehova] atatoa neema na utukufu. Hatawanyima kitu chema hao waendao kwa ukamilifu.”​—⁠Zaburi 84:11.

5. Mungu hukaa pamoja na watu wa namna gani katika makao ya mbinguni yasiyoonekana, nao watofautianaje na wanadamu?

5 Si kwamba ni jambo la akili tu kuamini kwamba Mungu hukaa katika makao ya kiroho yasiyoonekana pamoja na watu kiroho wenye akili, bali pia Biblia Takatifu yenyewe yahakikisha hilo. Anaweza kuonana yeye mwenyewe na watu hao. Wao wanaweza kumwona kama vile yeye anavyowaona. Kwa kuwa wao ni bora na wana nguvu nyingi zaidi kuliko mwanadamu, hawayeyuki, hawavunjiki wala hawaangamii wamwonapo. Wanaweza kumwona kabisa, kutumikia mbele zake mwenyewe. (Luka 1:19) Mungu aliambia wanadamu, si malaika, maneno haya: “Huwezi kuniona uso wangu, maana mwanadamu hataniona akaishi.” (Kutoka 33:20) Ndivyo Mungu alivyomwambia nabii wake Musa.

6. Kulingana na Ufunuo 4:​11, wenzi hao wa kiroho wa Mungu walifikaje huko?

6 Roho hao wenzi wa Mungu walifikaje huko? Naam, wanadamu wawili wa kwanza walifikaje hapa? Tutachukua jibu lililotolewa na wale ambao Yohana mwandikaji wa Biblia aliwaona katika njozi, wakimwabudu Mungu mbinguni. Walisema haya: “Umestahili, Bwana, Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na uwezo, kwani wewe ndiwe uliyeumba vitu vyote; na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwa, vikaumbwa.”​—⁠Ufu. 4:​11, Zaire Swahili Bible.

7, 8. Siku ya kufufuliwa, Yesu alisema roho haina nini, naye alifanya nini na mwili alioonekana nao?

7 Mungu alifanya wanadamu wawili wa kwanza wakawa nyama na damu. Kabla ya hapa, Mungu alikuwa amefanya wenzi wake wa mbinguni wakawa roho. Yesu Kristo alitoa maelezo ya wazi juu ya jambo hilo kwa habari ya kufufuliwa kwake kwa wafu. Aliwatokea wanafunzi wake Yerusalemu katika chumba kilichofungwa kwa kufuli. Alifanya hivyo akiwa na mwili wenye kuonekana kama aliokuwa amekufa nao, walakini wao walidhani waliona roho. Basi, aliwaambiaje? Hivi: “Roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo.”​—⁠Luka 24:​36-39.

8 Baada ya kuzungumza na wanafunzi hao wenye kustaajabu, Yesu aliyefufuliwa alitoweka. Aliuvua au akauyeyusha mwili huo wa kibinadamu aliokuwa amevaa. Hakuingia katika makao ya kiroho akiwa amevaa mwili huo. Kama angaliweza kufanya hivyo, ingalimaanisha kwamba mtu wa kiroho mbinguni ana nyama na mifupa, hasa katika habari ya Yesu Kristo aliyetukuzwa.​—⁠1 Wakorintho 15:50.

9. Mungu aliumba wenzi wake wa mbinguni moja kwa moja kwa vitu gani?

9 Kwa sababu ya mambo yote hayo ya hakika, Bwana Mungu alifanya wenzi wake wa mbinguni wakawa roho moja kwa moja. Hakuhamisha wanadamu wenye nyama, damu na mifupa duniani wakawe pamoja naye katika makao ya mbinguni yasiyoonekana. Mtume Mkristo Paulo ana-eleza namna ya watu ambao Mungu aliumba moja kwa moja mbinguni, anapoandika hivi: “Afanyaye malaika zake kuwa pepo, na watumishi wake kuwa miali ya moto.” (Waebrania 1:7) Hapa mtume Paulo alikuwa akitumia maneno ya mtunga zaburi Daudi amtajapo Yehova Mungu kama ‘akifanya malaika zake kuwa pepo, na watumishi wake kuwa moto wa miali.’ (Zaburi 104:4) Kwa hiyo, Neno la Mungu mwenyewe lililoandikwa lahakikisha kwamba ana uwezo wa kuumba viumbe vya kiroho na vya kibinadamu pia.

10. Mwanzo 1:26 waonyeshaje kwamba watu wa kiroho waliumbwa kabla ya wanadamu?

10 Viumbe vya kiroho viliumbwa kabla ya vya kibinadamu. Maneno ya Mungu mwenyewe tunayoelezwa wazi katika sura ya kwanza ya Biblia yaonyesha hilo. Hapo twasoma: “Mungu akasema, Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.” (Mwanzo 1:26) Sasa, Mungu aliposema, “Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu,” hakuwa akijiambia mwenyewe kama kwamba ni mungu mwenye miungu wawili au watatu ndani yake mwenyewe. Alikuwa akisema na mtu mwingine wa mbinguni aliye tofauti na alikuwa akimkaribisha ajiunge naye kufanya kiumbe wa duniani, mwanadamu.

11. Ayubu 38:​1-7 yaonyeshaje kwamba walikuwako zaidi ya mtu mmoja pamoja na Mungu wakati wa kuumbwa mwanadamu?

11 Lakini, wakati mwanamume na mwanamke walipoumbwa, Mungu alikuwa pamoja na watu wengi wa kiroho. Walikuwa wameumbwa na Mungu hata kabla dunia haijaumbwa. Ayubu mwaminifu wa nchi ya Usi alielezwa hilo, Mungu alipomwambia hivi: “Ulikuwa wapi nilipoiweka misingi ya nchi? Haya! sema, kama ukiwa na ufahamu. Ni nani aliyeamrisha vipimo vyake, kama ukijua . . . au ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni, hapo nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?” (Ayubu 38:​1-7) Hilo lilitukia maelfu mengi ya miaka kabla ya sehemu ya mwisho wa siku ya sita ya Mungu ya kuumba, wakati ambao Mungu aliumba mwanamume na mwanamke. (Mwanzo 1:​27-31) Kwa hiyo hao ‘wana wa Mungu’ hawakuwa viumbe waliokuwa duniani kwanza kama wanadamu kisha wakahamishwa. kupelekwa mbele za Mungu mbinguni. Walikuwa viumbe wa kiroho wa Mungu tangu mwanzo wa kuwako kwao. Mungu hakujaza mbingu na wakaaji wa dunia.

12. Wanadamu na malaika wanalinganaje katika hali ya uhai na uwezo?

12 Hao ‘wana wa Mungu’ wenye mfano wake ni wakuu kuliko wanadamu. Kwa hiyo, baada ya mtunga zaburi Daudi kujua Mungu yuko juu ya mbingu, aliendelea kusema hivi: “Mwanadamu mwenye kufa ni kitu gani hata wamkumbuka, naye mwana wa mwanadamu wa dunia hata wamwangalia? Wewe uliendelea pia kumfanya yeye kuwa mpungufu kidogo kuliko wenye mfano wa Mungu.” (Zaburi 8:​4, 5, NW) Hao “wenye mfano wa Mungu” ni nani? Ni malaika, kwa maana mwandikaji wa Biblia anatumia maneno ya Zaburi 8:5 katika Waebrania 2:​6-9 na kusema: “Umemfanya mdogo punde kuliko malaika.” Kwa hiyo, cheo cha uhai na uwezo wa wanadamu kitaendelea sikuzote kuwa chini kuliko cha hao ‘wana wa Mungu,’ malaika hao wa mbinguni.

MAKUSANYIKO YA WATU WA KIROHO MBINGUNI

13. Twapata wapi maandishi ya kwanza juu ya makusanyiko ya mbinguni, na ni nani aliyeyasimamia?

13 Hao ‘wana wa Mungu’ wanakuwa na makusanyiko mara kwa mara naye Mungu Aliye Juu Zaidi ndiye huyasimamia. Ametufunulia jambo hilo katika Neno lake lililoandikwa. Habari za zamani zaidi zinazotueleza juu ya makusanyiko hayo ya mbinguni ziliandikwa katika sura mbili za kwanza za Ayubu. “Ilikuwa,” katika mwanzo-mwanzo wa maisha ya Ayubu, “siku moja ambayo hao wana wa Mungu wali-kwenda kujihudhurisha mbele za [Yehova], Shetani naye akaenda kati yao. [Yehova] akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu [Yehova], na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na kutembea huku na huku humo.” Katika sura inayofuata, mistari mingine inaeleza kulikuwa na kusanyiko la pili la Yehova pamoja na wana wake wa mbinguni, halafu tena mtu huyo wa kiroho aitwaye Shetani akaja. (Ayubu 1:​6, 7; 2:​1, 2) Makusanyiko hayo, tusiyoweza kuyaona, yana kusudi, naye Mungu Mwenye Nguvu Zote huhakikisha yanakuwa na utaratibu. Wote wanaohudhuria lazima wamjibu walikuwa wapi na wakifanya nini. Hata jamaa aitwaye Shetani lazima aonyeshe heshima, ajapokuwa jinsi jina lake limwonyeshavyo, mpinzani mkuu zaidi wa Yehova Mungu.

14. Ni kusanyiko gani la mbinguni linalotajwa katika Waebrania 12:​22, 23?

14 Twaendelea kusoma habari zifuatazo katika Waebrania 12:​22, 23 juu ya makusanyiko hayo ya ‘wana wa Mungu’ wa kiroho mbinguni: “Ninyi,” Wakristo Waebrania, “mmefikia Mlima Sayuni na mji wa Mungu aishiye, Yerusalemu wa mbinguni, na maelfu ya malaika, katika kusanyiko kuu.” (NW) Maelfu yote hayo ya malaika wanaoendelea kuwa waaminifu kwa Baba yao wa mbinguni na kukataa kumfuata Shetani ni jamaa moja kubwa ya mbinguni ya Mungu.

15. Paulo atajaje jamaa hiyo ya mbinguni katika Waefeso 3:​14, 15, na washiriki wa jamaa hiyo wana uhusiano gani wao kwa wao?

15 Paulo mwandikaji wa Biblia aitaja jamaa hii ya mbinguni. Alipokuwa akiandikia Wakristo wanaomtambua Yehova Mungu kuwa Baba yao wa mbinguni, Paulo alisema: “Kwa hiyo nampigia Baba magoti, ambaye kwa jina lake ubaba wote mbinguni na wa duniani unaitwa.” (Waefeso 3:​14, 15) Kila jamaa inaitwa kwa jina la baba yake, na yapaswa kuishi kulingana na heshima na ustahili wa jina hilo. Kwa kuwa hao ‘wana wa Mungu’ wa mbinguni wana Baba mmoja tu, wote ni ndugu.

16. Nabii Mikaya aliona kusanyiko gani la mbinguni katika njozi mwishoni mwa karne ya kumi K.W.K.?

16 Kusanyiko lilikuwako mbinguni mwishoni mwa karne ya kumi kabla ya Wakati wetu wa Kawaida. Nabii Mikaya Mwisraeli aliona njozi ya kusanyiko hilo. Mikaya aliwaeleza wafalme wawili wenye mwungano habari za kusanyiko hilo, Ahabu na Yehoshafati: “Sikia basi neno la [Yehova]; Nalimwona [Yehova] ameketi katika kiti chake cha enzi, na jeshi lote la mbinguni wamesimama upande wa mkono wake wa kuume na wa kushoto. [Yehova] akasema, Ni nani atakayemdanganya Ahabu, ili akwee Ramoth-Gileadi akaanguke? Basi huyu akasema hivi; na huyu hivi. Akatoka pepo, akasimama mbele za [Yehova], akasema, Mimi nitamdanganya.” -1 Wafalme 22:​19-21.

17. Jeshi lililokuwa karibu na Mungu wakati huo lilikuwa la watu wa namna gani?

17 Na tuangalie kwamba malaika aliyetaja njia yenye kufaulu kumdanganya Mfalme Ahabu mwovu akaangamie katika pigano anaitwa “pepo.” Hiyo yamaanisha kwamba “jeshi” lote hilo lililo mkono wa kuume wa Mungu na wa kushoto ni pepo pia, naam, viumbe vya kiroho vyenye akili. Wanatofautishwa na sisi wanadamu.

18, 19. Danieli aliona baraza gani ya hukumu katika njozi, ambayo inatimizwa karne yetu ya 20?

18 Je! sisi wanadamu wa leo tunajua kwamba zamani za kale kulipangwa kuwe na baraza ya hukumu mbinguni wakati wa kame yetu ya 20? Nabii Danieli alipewa njozi ya baraza hiyo alipokuwa mtumwa Babeli zaidi ya miaka elfu mbili na mia tano iliyopita. Alitoa maelezo akaandika hivi:

19 “Baadaye nikaona katika njozi ya usiku, na tazama, mnyama wa nne, mwenye kutisha, mwenye nguvu, mwenye uwezo mwingi. . . . Nikatazama hata viti vya enzi vikawekwa, na mmoja aliye mzee wa siku ameketi; . . . maelfu elfu wakamtumikia, na elfu kumi mara elfu kumi wakasimama mbele zake; hukumu ikawekwa, na vitabu vikafunuliwa. . . . Nikaona katika njozi za usiku, na tazama, mmoja aliye mfano wa mwanadamu akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia huyo mzee wa siku, wakamleta karibu naye. Naye akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo haitapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.”​—⁠Dan. 7:​7-14.

20. Ni mwana yupi wa Mungu wa mbinguni anayeheshimiwa sana kama anayetajwa kuwa “mwanadamu” katika njozi ya Danieli?

20 Je! yuko mwana wa Mungu ye yote mwingine wa kiroho mbinguni anayeheshimiwa sana hivyo kama huyu anayeonekana katika njozi ya Danieli kama “mwanadamu”? Hapana! Basi yeye ni nani? Mtunga zaburi atujulisha. Katika Zaburi 89:​26, 27 asema hivi: “Yeye ataniita, Wewe baba yangu, Mungu wangu na mwamba wa wokovu wangu. Nami nitamjalia kuwa mzaliwa wangu wa kwanza, kuwa juu sana kuliko wafalme wa dunia.” Maneno hayo ya Yehova hayamhusu Mfalme Daudi, ambaye Mungu alifanya agano na-ye wawe na ufalme wa milele katika jamaa yake ya kifalme, wala hayamhusu mfalme aliyemrithi Daudi, Sulemani. Hakuna ye yote wa wafalme hawa aliyekuwa mwana mzaliwa wa kwanza wa baba yake. (Zaburi 89:​28-37; 2 Samweli 7:​4-17) Mambo yaliyofuata yanaonyesha kwamba Yehova alikuwa akimtaja kwa unabii ‘mzaliwa wa kwanza’ wake mwenyewe katika mbingu, Mwana aliyekuwa amekuwa naye kwa wakati usiojulikana kabla Yehova Mungu hajaumba mwanadamu.

21. Kulingana na Ufunuo 3:​14, je! Mungu alikuwa na mke mbinguni wakati alipomtokeza mwanawe “mzaliwa wa kwanza”?

21 Huenda mtu akauliza, Mungu angewezaje kuwa na ‘mzaliwa wa kwanza,’ na hali Yeye hakuwa na mke mbinguni wakati huo? Yeye ambaye akawa ‘mzaliwa huyo wa kwanza’ ajibu ulizo hilo mwenyewe. Katika kitabu cha mwisho cha Biblia, katika Ufunuo 3:​14, asema: “Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu.” Aliyenena maneno hayo ni Bwana Yesu Kristo aliyefufuliwa na kutukuzwa, ambaye ni “Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli” asiyesema uongo katika habari hiyo. Yeye mwenyewe asema ndiye “mwanzo wa kuumba kwa Mungu.” Kwa hiyo Mungu asingeweza kuwa na mke kabla ya huyo aliyemwumba kwanza.

22. Ingawa Yesu alikuwa kuumba, alimtaja Mungu kuwa nani kwake?

22 Ingawa yeye ni “kuumba” wala si mtoto wa mama fulani, Yesu amtaja Mungu mara nyingi kuwa Baba yake mwenyewe. (Ufunuo 3:21; 14:1) Amtaja Baba yake kuwa Mungu wake mwenyewe pia. Katika Ufunuo 3:12 asema: “Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, . . . nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu.” Hiyo yapatana na maneno aliyosema siku ya kufufuliwa kwake akisema na Mariamu Magdalene karibu na kaburi tupu: “Enenda kwa ndugu zangu ukawaambie, Ninapaa kwenda kwa Baba yangu naye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu naye ni Mungu wenu.” (Yohana 20:17) Hiyo ilikuwa katika Nisani 16, 33 W.K., siku ya tatu alipokuwa amekwisha lia kwa sauti juu ya mti wa mateso alipotundikwa afe kwa kusema: “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?” Na, mwishowe alisema: “Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu”​—⁠Mathayo 27:46; Marko 15:34; Luka 23:46; Zaburi 22:1; 31:5. ​—⁠Kutoka Holy Spirit​—⁠the Force Behind the Goming New Order, Sura ya 2

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki