Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yy sura 2 kur. 9-17
  • Sababu Unaweza Kuutazamia Wakati Ujao Ukiwa na Hakika

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sababu Unaweza Kuutazamia Wakati Ujao Ukiwa na Hakika
  • Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • SAYARI UNAMOKAA
  • KIWANDA CHA AJABU CHA VYAKULA
  • JITAZAME MWENYEWE!
  • UNAWEZA KUSONGA MBELE UKIWA NA HAKIKA
  • Jinsi Tunavyoweza Kujua Kwamba Kuna Mungu
    Je, Kweli Mungu Anatujali?
  • Nani Awezaye Kutuambia?
    Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
  • Je, Unathamini Zawadi Zinazotoka kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Je, Wanadamu Wataiharibu Dunia Kabisa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Kupata Faida Zote za Ujana Wako
yy sura 2 kur. 9-17

Sura ya 2

Sababu Unaweza Kuutazamia Wakati Ujao Ukiwa na Hakika

1-4. Kuwa na hakika kuna sehemu gani katika kushinda au kushindwa kwa mtu? Sababu gani watu wengi hawana hakika sana na wakati ujao?

UMEPATA kujaribu kuruka pao la chuma katika mruko wa juu, au hata kuruka ua au ukuta? Ikiwa ukuta haukuwa mkubwa mno, ukawa na hakika ya kuweza kuuruka, labda uliweza. Lakini ikiwa uliogopa labda ulishindwa ukakasirika.

2 Hivyo ndivyo mambo mengi sana yalivyo. Kwa mfano, ikiwa unaogopa kuingia katika maji, hutajua kuogelea.

3 Ndivyo na kupata faida zote za ujana wako. Uhakika unasaidia sana. Huwezi kuwa na furaha sana wala kufanya maendeleo mazuri katika maisha bila hakika ya mambo yaliyoko mbele. Lakini unaweza kuwa na hakika ya jambo gani leo?

4 Tungeweza kutumia wakati mwingi tukizungumza juu ya sababu zinazofanya tusiwe na hakika. Sayari yetu, Dunia, inazidi kuchafuka, wanyama wake wanamalizwa, tena kuna upungufu wa chakula na magumu mengine mazito. Huenda mambo hayo yakakufanya uone kwamba hakuna tumaini linalofaa. Kwa namna vitu vinavyoharibiwa duniani, vijana wengine wanadhani wakati ujao hauna maana sana kwao. Na pengine iko hivyo. Hata hivyo kuna mambo mengi ambayo watu hawazungumzi sana yanayotupa sababu ya kuutazamia wakati ujao tukiwa na hakika. Ebu fikiria machache.

SAYARI UNAMOKAA

5-8. Taja mambo fulani yanayowezesha uhali uwepo duniani. Mambo yote hayo ya ajabu yalitokeaje?

5 Ni vyepesi kwetu kuiona dunia kama kitu cha kawaida tu. Hata hivyo sayari hii tulimozaliwa na tunamoishi imefanywa kwa njia ya ajabu sana. Kama mpira unaozunguka, dunia inasafiri mamilioni ya maili (kilometres) angani inapolizunguka jua, ikiwa mbali nalo maili milioni 93 (karibu kilometres 150,000,000). Ingekuwaje ikiwa dunia ingekuwa mahali tofauti na pale ilipo sasa? Ikiwa dunia ingekuwa mbali na jua kama zile sayari zinazoitwa Pluto na Neptune, ingekuwa kama barafu kubwa yenye baridi mno isiwezekane kukaliwa na viumbe. Na ikiwa umbali wake na jua ungepungua sehemu ya tatu kwa moja ya maili (kilometres) hizo iwe karibu zaidi na jua kama ilivyo sayari Venus, dunia ingekuwa kama joko (tanuru ya moto), kwa maana joto lingekuwa jingi mno hata maziwa (tanganyika ndogo) na mito ichemke.

6 Au, ijapokuwa umbali wa dunia na jua unafaa kabisa, ingekuwaje ikiwa haingekuwa ikizunguka katika mhimili wake kama inavyozunguka kila saa 24? Namna gani ikiwa ingekuwa ikizunguka mara moja tu, wakati inapokuwa katika safari ya kulizunguka jua kila mwaka kama sayari Mercury? Hapo karibu nusu moja ya dunia ingekuwa mahali penye barafu pasipokaliwa watu, na ile nyingine ingekuwa tanuru ya moto isiyokaliwa watu.

7 Si hayo tu. Kwa sababu gani katika sehemu nyingi za dunia tunaweza kuufurahia uzuri wa masika na maua ya wakati huo, siku za kiangazi zenye jua na umotomoto? Majira hayo yanatokea kwa sababu dunia imeinama kidogo kwa njia inayoufaa mwendo wake wa kulizunguka jua. Majira hayo yanasaidia kufanya sehemu kubwa ya uso wa sayari hii uwe mahali pazuri sana kuishi. Tena yanawezesha sehemu kubwa ya dunia izalie wanadamu na wanyama chakula.

8 Kuna mambo mengine mengi sana yanayoungana pamoja kuwezesha uhai uendelee katika sayari hii. Lakini yote hayo yanatuonyesha nini? Jiulize hivi: Maajabu yote hayo yalitokeaje? Bila shaka yatupasa tufahamu kwamba kuna Fundi fulani aliyeifanya sayari yetu, Dunia. Ndiyo, vitu vingi vinavyowezesha uhai uendelee duniani ni vigumu sana sana kufahamika kuliko chombo cho chote cha angani ambacho wanasayansi wa kibinadamu wamefanya. Vilevile akili yote na kazi yote hiyo inayoonyeshwa na vitu vya dunia ambavyo ni vigumu sana kufahamika inatuambia jambo jinginelo. Kwa wazi, zinatuambia kwamba yule Muumba wa dunia anapendezwa kufanya maisha yafurahishe wale wanaoishi hapa duniani. Wewe ni mmoja wao.

9-12. Ijapokuwa dunia imeharibiwa sana, ni nini kinachoonye-sha kwamba inaweza kurudia hall yake ya kwanza?

9 Ni kweli kwamba watu wengi leo wanaiharibu sana dunia kwa kuichafua na kuitumia vibaya. Lakini wanaweza kuzuiwa wasifanye hivyo. Na uharibifu huo unaweza kumalizika.

10 Kwa mfano, fikiria yaliyotukia katika kisiwa Krakatoa cha Pacific. Kiliteketezwa na mlipuko mkubwa wa mlima wenye kutoa moto. Kama ungalitembelea huko mara baada ya hapo, ungaliona kwamba kisiwa chote kilikuwa majivu matupu. Hakuna kitu kilichobaki hai huko—wala watu, wala wanyama, wala mimea. Kisha ikawaje?

11 Kisiwa hicho kilianza kurudia hali yake ya kwanza bila msaada wa mtu ye yote. Kwa muda wa miaka mitatu, mimea ya namna zipatazo 26 kusitawi tena huko. Minazi, miwa-mwitu na mimea yenye maua mazuri sana ilianza kuota baada ya muda mfupi. Miaka 25 iliyofuata mlipuko huo, kukawako namna 263 za wanyama katika Krakatoa. Ule uharibifu ulioletwa na mlima wenye kutoa moto ulikwisha. Kisiwa kikawa tena kama bustani (shamba).

12 Mageuzo hayo ya ajabu yaliyofanyika katika kisiwa cha Krakatoa yanaweza kufanyika tena duniani pote. Kama tutakavyoona katika kitabu hiki, kuna sababu nzuri ya kusadiki kwamba itakuwa hivyo.

KIWANDA CHA AJABU CHA VYAKULA

13-17. Chakula kinafanyizwaje katika dunia? (Zaburi 104:14) Namna nyingi za chakula kinachofanyizwa na dunia zinasaidiaje mtu afurahie maisha? Basi, Muumba wa vitu hivyo vyote alitaka tuwe na maisha ya namna gani? (Isaya 25:6; Zaburi 67:6)

13 Utakapoanza kula chakula mara nyingine, ngoja kidogo ufikirie hili: Hata ikiwa unakula wali (mchele uliopikwa) mweupe au viazi vyeupe, ngano au maharagwe ya rangi ya kahawa, mahindi au maji ya matunda ya rangi ya manjano, maembe, vyote hivyo vinatokana na mimea yenye majani mabichi. Kwa sababu gani? Kwa sababu ya utaratibu wa ajabu unaoitwa photosynthesis.a

14 Majani ya mimea hiyo yote yana kitu chenye rangi ya kijani kibichi kinachoitwa chlorophyll. Wakati nuru ya jua inapoyapiga majani, kitu hicho kinafanyiza mabadiliko ya namna nyingi sana. Maji na mvuke wa namna ya carbon dioxide (ambayo mmea unapata kutokana na hewa) vinaungana katika visehemu vya mmea na kufanyiza sukari fulani, ambayo ndiyo asili ya vyakula vyote. Ikitumia sukari hiyo, mimea inafanyiza vilevile vitu vingi zaidi vya namna mbalimbali kama sukari na wanga vinavyoitwa carbohydrate, mafuta, protini na vitamini. Akisema juu ya matokeo ya ajabu yanayofanyizwa na utaratibu huu unaoitwa photosynthesis, Frits W. Went, mchunguzi wa miti na mimea, asema hivi:

“Viwanda vya wanadamu ni vidogo mno vikilinganishwa na kiasi cha vitu ambavyo unafanyiza. Kila mwaka mashine za ulimwengu za vyuma vya pua zinafanyiza tani milioni 350 za chuma cha pua, navyo viwanda vya ulimwengu vya udongo-ulaya vinafanyiza tani milioni 325 za udongo-ulaya. Walakini, mimea ya ulimwengu ya kijani kibichi inafanyiza tani milioni elfu 150 za sukari kila mwaka.”

15 Wanasayansi wanajua linalotukia, lakini bado hawawezi kujua namna utaratibu huu photosynthesis unavyofanya kazi. Kama mwandikaji mmoja wa kisayansi anavyosema, mara nyingi wachunguzi wanautaja utaratibu huo kuwa ‘siri.’ Kwa sababu gani? Kwa sababu “wanajua vinavyoingia ndani na vinavyotoka nje lakini hawana hakika na kila jambo linalotendeka ndani.” Wakiwa na uchunguzi wao wote wa dawa na mashine, wanadamu hawawezi kuiga utaratibu huo wa ajabu hata kidogo.

16 Jambo jingine la ajabu ni namna nyingi sana za chakula zinazofanyizwa na dunia. Labda wewe unapenda sana chakula fulani kama maembe. Lakini namna gani ikiwa kila kitu—viazi, wali, mkate, matofaa, machungwa—kingekuwa na ladha kama ya maembe? Ungechoshwa na ladha hiyo, sivyo? Lakini kwa vile kuna matunda mbalimbali, mboga, nafaka, karanga na mazao yanayofanyizwa na kiwanda cha vyakula, yaani, dunia, kuna maelfu ya ladha mbalimbali unazoweza kufurahia.

17 Tena, yote hayo yatuambia nini? Bila shaka, yanatuambia kwamba Yeye aliyeanzisha kiwanda hiki cha ajabu cha vyakula ataka maisha katika dunia hii yawe yenye kufurahika sana. Anataka sana tuwe wenye furaha wakati ujao. Muumba yule yule aliyefanya Dunia iwe makao mazuri sana amehakikisha vilevile kwamba makao hayo yamejazwa kila kitu kinachohitajiwa kufanyia wale wanaoishi humo karamu bora. Tutaona vilevile katika kitabu hiki namna Yeye anavyokusudia kuwezesha wote wanaotaka waishiriki karamu hiyo.

JITAZAME MWENYEWE!

18-23. Ni mambo gani yaliyo katika miili yetu yanayoonyesha kwamba tuliumbwa kuwapita wanyama ubora?

18 Halafu, jifikirie kidogo. Bila shaka, ili ufikiri yakupasa utumie ubongo—basi sababu gani usianze na ubongo? Ni wazi kwamba huwezi kuona ubongo wako, lakini wadhani uko kama nini? ukiisha kukua, ubongo wa mwanadamu una uzito kidogo kuliko ratli tatu (kilo 1.3) Lakini, eneo dogo hilo lina uwezo mkubwa kama nini! Taarifa ya kisayansi katika New York Times yasema hivi:

“Umbo la ubongo . . . ni gumu sana kufahamika hata zile mashine kubwa za umeme za kuhesabia zinakuwa kama vitu tu vya kuchezea watoto zikilinganishwa nao.”

19 Ndiyo, ubongo wako ambao unaweza kutumia, umeelezwa kuwa “kitu kilicho kigumu sana kufahamika kuliko vitu vyote katika ulimwengu wote.” Basi, ikiwa mtu angekupa saa nzuri ya mkono au chombo chenye bei sana cha kupigia picha, au mashine bora sana ya kuhesabia, bila shaka ungeitunza na kujaribu kuitumia vizuri sana, sivyo? Imekupasa uthamini ubongo wako kuliko vitu hivyo.

20 Fikiria mwili wako vilevile. Ni kweli kwamba simba ana nguvu kuliko wewe, tembo ni mkubwa kuliko wewe, papa aweza kuogelea mbio kuliko wewe, nyani aweza kupanda mti au mlima vyepesi kuliko wewe, kisha tai aweza kuruka kwa mabawa yake mwenyewe afike juu sana angani, lakini wewe huwezi kufanya hivyo. Hata hivyo, kati ya viumbe hivyo hakuna kilicho na uwezo wa kufanya mambo yote kama mwanadamu. Simba na tembo hawawezi kuruka kama ndege, papa hawawezi kupanda miti wala milima, wala tai hawawezi kuogelea. Lakini wanadamu wanaweza kufanya yote hayo, ama bila kusaidiwa na vyombo ama kwa kusaidiwa na vyombo walivyounda. Zaidi ya yote, wanadamu wana uwezo wa pekee wa kufanya vitu vya namna nyingi.

21 Sababu moja ni mikono yako. Hakuna chombo cha kufanyia kazi kinachoweza kufanya mambo yote unayoweza kufanya kwa mikono yako—tangu kazi ya kutumia nguvu kuunda mashine au kazi ya mbao, mpaka kazi nyepesi, kama vile kupiga kinanda, kupaka rangi au kuchora ramani ya nyumba.

22 Kwa kweli, mikono yako ni sehemu tu ya vitu vinavyoufanya mwili wako kuwa wa ajabu sana. Ndiyo sababu Dakt. W. W. Akers, fundi wa mitambo anayefanya kazi na madaktari wa kupasua, alisema habari za mwili wa mwanadamu hivi:

“Mwili ndicho kitu kilichofanyiwa ufundi bora kuliko vitu vyote. Karibu mashine yo yote unayoweza kuwazia—hata iwe ngumu sana kufahamika—utaona kwamba ndani ya mwili mna mashine bora kupita hiyo.”

23 Kwa wazi Muumba Mkuu alitaka wanadamu wawapite wanyama ubora, waweze kuifurahia sana dunia. Hilo linatuhakikishia kwamba Yeye anataka tufurahie mambo mema wakati ujao.

UNAWEZA KUSONGA MBELE UKIWA NA HAKIKA

24-28. Sababu gani ni jambo la busara kusadiki kwamba dunia hii iliumbwa? (Warumi 1:20) Muumba amejibu maulizo yetu juu ya uzima wapi? (2 Timotheo 3:16) Twaweza kujuaje kama kufuata maneno ya Biblia kungetusaidia tuutazamie wakati ujao tukiwa na hakika? (2 Petro 3:13; Ufunuo 21:1-4)

24 Tumeona kwamba sayari hii na kila kilichomo, inatoa ushuhuda wa kwamba iliumbwa kwa njia ya akili na kwa ufundi ulio bora sana kupita ule unaoonekana katika nyumba au jengo lo lote ambalo tumepata kuona. Bila shaka unaweza kukubaliana na usemi ulio wazi unaopatikana katika Biblia: “Maana kila nyumba imejengwa na mutu.” (Waebrania 3:4, ZSB) Tuseme ikiwa umekwenda katika nyika kubwa mno ukakuta nyumba lakini usione mtu ye yote karibu. Hungedhani kwamba nyumba hiyo ilijijenga yenyewe, sivyo? Vivyo hivyo, dunia hii ina Muumba aliyeifanya, ijapo hatumwoni. Max Planck, mshindi wa Zawadi ya Nobel alisema:

“Hakuwezi kupatikana maelezo yo yote juu ya namna ulimwengu wote ulivyotokea, isipokuwa kusema kwamba uliumbwa na Mtu Mwenye Akili Kuu ya Uumbaji.”

25 Biblia yatujulisha “Mtu Mwenye Akili Kuu ya Uumbaji” aliyejenga makao yetu, dunia hii. Inatuambia kwamba ni Yehova Mungu, Mfanya mbingu na dunia.

26 Kwa wazi Muumba huyo mkuu ni mwenye nguvu na hekima sana. Anapendezwa sana na sisi sote—kutia na wewe. Ikiwa unaweza kujifunza mambo ambayo wanadamu wengine wanajua, unaweza kujifunza kwake zaidi sana juu ya kupata faida zote za ujana wako.

27 Hapo ndipo Biblia inapohitajiwa. Inajulisha makusudi ya Muumba ya kufanya dunia na wanadamu wote. Inajibu maulizo mengi ya wanadamu. Inaonyesha sababu ya magumu yao na namna yatakavyoondolewa. Biblia haikuambii uzitumaini taratibu za sasa zenye makosa ambazo zimeijaza dunia taabu na hatari nyingi sana. Inakuonyesha taratibu mpya zenye mambo bora zaidi.

28 Ikiwa umeisoma Biblia kidogo au hujaisoma, labda unataka kujua ikiwa maneno yake yaweza kweli kuondoa magumu yako na kujibu maulizo yako. Huwezi kujua usipoichunguza kwa uangalifu. Katika kitabu hiki unachosoma sasa, tutaona mambo ambayo Biblia inasema pamoja na majibu na uongozi inaotoa. Jionee mwenyewe namna Biblia inavyosema mambo yenye busara, yasiyo ya kuwazia tu. Ndiyo, jionee mwenyewe namna Neno la Yehova Mungu, Biblia, linavyoweza kukusaidia uondoe magumu yako. Kisha uutazamie wakati ujao wenye furaha na wenye kufaa ukiwa na hakika.

[Maelezo ya Chini]

a Kutokana na neno photo, maana yake “nuru,” na synthesis, maana yake “kufanyizwa kwa kitu chenye sehemu nyingi kwa kuunganisha vitu vya asili visivyo na sehemu nyingi sana.”

[Picha katika ukurasa wa 11]

Kumjua Muumba wa dunia kunatoa msingi wa kuwa na hakika ya wakati ujao

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki