Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yy sura 16 kur. 116-123
  • Michezo na Tafrija

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Michezo na Tafrija
  • Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UONGOZI WA KUONGEZA FURAHA
  • SINEMA NA TELEVISION
  • KUTIMIZA MAHITAJI YA TAFRIJA
  • Kuweka Michezo Mahali Payo Panapofaa
    Amkeni!—1992
  • Ujitoaji Kimungu Una Faida Kuliko Mazoezi ya Kimwili
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2019
  • Vijana Wanataka Nini Maishani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Ninapaswa Kujua Nini Kuhusu Michezo?
    Vijana Huuliza
Pata Habari Zaidi
Kupata Faida Zote za Ujana Wako
yy sura 16 kur. 116-123

Sura ya 16

Michezo na Tafrija

1, 2. (a) Ni michezo gani unayofurahia? (b) Ni kazi gani zilizofanywa na Yehova, zinazoonyesha kwamba anataka tufurahie maisha? (Zaburi 104:14-24).

MICHEZO na namna mbalimbali za tafrija zinapendwa mahali pote ulimwenguni. Kila mwaka mabilioni ya fedha zinatumiwa ili kufurahia michezo na tafrija hizo. Je! wewe pia wafurahia mambo hayo? Kwa mfano, wapenda kucheza mpira? Je! wafurahia kuogelea, kucheza mpira wa vibao, tennis, au kushiriki michezo mingine? Au labda unafurahia kwenda kutazama sinema au kutazama vipindi vya television?

2 Labda watu wengine watasema kwamba anasa hizo ni mbaya. Wewe waonaje? Watu wengine hata wanasema kwamba Biblia yakataza mambo hayo. Lakini kwa wazi, watu hao wamesingizia Biblia na Yehova Mungu aliyeitunga. Neno la Mungu lasema inafaa vijana wapate furaha kutokana na michezo. Kwa mfano, Biblia yasema hivi inaposimulia juu ya watu waliobarikiwa na Mungu: “Na hizo njia za mji zitajaa wavulana, na wasichana, wakicheza katika njia zake.” Inasema vilevile, kwamba kuna “wakati wa kucheza.” (Zekaria 8:5; Mhubiri 3:4) Ni wazi kwamba Mungu alikusudia tufurahie michezo mizuri. Mojawapo la matunda ya roho ya Mungu ni “furaha.” (Wagalatia 5:22) Ni jambo la kawaida na la asili kwetu kufurahia michezo mizuri.

UONGOZI WA KUONGEZA FURAHA

3-8. (a) Ni shauri gani lenye kusawazika linalopatikana katika 1 Timotheo 4:7, 8 juu ya tafrija? (b) “Kujizoeza kupata nguvu za mwili kwafaa” namna gani? (c) Ikiwa mtu anacheza sana michezo ya timu ya shule, anaweza kupata matatizo gani? Ni nini linalopaswa kumsaidia aamue kwa hekima kama ndivyo atakavyofanya?

3 Kwa upendo Mungu ametutayarishia uongozi wa kutusaidia tufurahie michezo hiyo. Kwa mfano, ili tuepuke matokeo mabaya ya ulafi, Neno la Mungu lashauri hivi: “Usiwe miongoni mwao . . . walao nyama kwa pupa.” (Mithali 23:20) Vilevile, yeye anatupa sisi shauri lenye hekima juu ya michezo kwa kutuambia: “Ujizoeze kupata utauwa. Kwa maana kujizoeza kupata nguvu za mwili kwafaa kidogo, lakini utauwa unafaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye.”—1 Timotheo 4:7, 8.

4 Kwa hiyo Biblia yaonyesha kwamba “kujizoeza kupata nguvu za mwili,” kama vile michezoni, kunafaa. Kunatuletea faida; kwaweza kutusaidia tupate usawa wa mwili, kwaweza kusaidia miili kuwa myepesi kukunjika na minofu ya mwili kuwa yenye afya na nguvu. Kwaweza pia kutuburudisha akili, sana sana ikiwa tunatumia wakati mwingi tukijifunza. Lakini fahamu kwamba Biblia yaonya kwamba “kujizoeza kupata nguvu za mwili kwafaa kidogo.” Kwaweza kutokea nini kama shauri hilo la Biblia halifuatwi nawe unacheza sana?

5 Kwanza, kwaweza kuharibu furaha na kufanya michezo iwe jambo la maana sana kuliko kuwa tafrija nzuri. Alipokuwa akieleza juu ya matokeo ya kukazia mno michezo ya kushindana, mganga anayechunguza magonjwa ya akili yanayoletwa na michezo Bruce Ogilvie, alisema: “Siku moja niliwauliza wachezaji wapya katika kambi kubwa 10 za vyama vya mchezo wa mpira wa baseball, nao 87 kwa mia kati yao wakasema ingalikuwa afadhali kama hawakucheza mchezo wa mpira wa baseball wa Little League hata kidogo kwa sababu haukuwa wenye kufurahisha kama walivyodhani.”

6 Vilevile, michezo mingine, kama mpira wa kupigwa kwa miguu, yaweza kuwa hatari, sana sana wakati mwili wako unapoendelea kukua. Gazeti Science Digest laarifu kwamba kabla hawajawa na umri wa miaka kumi na minane, watoto wa Kiamerika wapata 12,000,000 wanalemaa milele kiungo fulani cha mwili kwa sababu ya kushiriki michezo! Mmoja wa wachezaji mashuhuri (anayejulikana) zaidi ambao kazi yao ni kucheza mpira hakutaka wanawe wawili wacheze katika vyama vya watoto vya kucheza mpira. “Wazazi hawafikirii mabaya yote yanayoweza kumpata kijana,” akasema. “Kwanza, aweza kurudi nyumbani akiwa amengoka meno fulani.” Jambo ambalo limefanya michezo fulani iwe hatari sana ni kwa vile mara nyingi watu wanatiwa moyo wawe na nia ya kushindana kupita kiasi—wasikubali kushindwa hata kidogo.

7 Jambo jingine la kufikiria ni vile kucheza michezo inayopangwa na vyama vya michezo kunavyoweza kukutia katika hatari ya ushirika mbaya. Kwa desturi mazungumzo katika chumba cha kuwekea na kuvalia mavazi ya michezo yanakuwa juu ya uasherati. Zaidi ya hayo, wakati timu inapokwenda kucheza na shule nyingine, huenda mtu akashirikiana kwa muda mrefu na watu wasioonyesha uaminifu kwa Mungu. Hilo ni jambo la kufikiria, kwa kuwa Neno la Mungu linakazia ‘kujizoeza ili kupata utauwa.’ Kungekuwa na faida gani kujitia katika jambo ambalo lingeweza kuharibu vyepesi tabia zako njema na uhusiano (urafiki) wako na Muumba wako?

8 Kwa hiyo michezo iko kama mambo mengine ambayo ni mazuri yakifanywa kwa kiasi—ikiwa hayatawali maisha yako hata kuzuia mambo yaliyo ya maana zaidi, au kukuweka katika hatari. Inaweza kufurahisha kama nini kucheza mchezo usiopoteza wakati mwingi na nguvu na kuona raha wakati mwili unapozoea na kutimiza matendo ya uhodari! Inaweza kutoa furaha na uradhi usiosahauliwa upesi. Inaweza kukusaidia umthamini Muumba wetu mkuu aliyetuumba akatupa uwezo wa kufanya mambo hayo.

SINEMA NA TELEVISION

9-14. (a) Inampasa mtu ajihadhari na nini anapochagua vipindi vya, sinema au television? (b) Ikiwa mtu anatazama tafrija ya mambo yenye tabia mbaya atakuwa namna gani? Kwa sababu gani? Ijapokuwa tunajua kwamba matendo hayo ni mabaya, ni kwa sababu gani haitupasi tupuze jambo hilo tukidhani kwamba kuyatazama hakuwezi kutugeuza?

9 Vilevile namna ya sinema na television tunayochagua inaweza kuharibu uhusiano wetu na Mungu. Maonyesho mengine ya sinema na television yanapendeza; mengine yaweza hata kutusaidia tuthamini zaidi kazi za ajabu za Muumba wetu. Lakini bila shaka umepata kuona kwamba maonyesho mengi yametokeza kwa wingi hadithi zinazosimulia uzinzi, uasherati, ngono za wanawake kwa wanawake na ngono za wanaume kwa wanaume, jeuri na mauaji makubwa. Labda mambo hayo yanaonwa kuwa tafrija (kitu cha kufurahisha). Lakini yanamfanya mtu namna gani?

10 Basi, jiulize mwenyewe: Umekuwa mtu wa namna gani leo? Je! si kwa sababu ya hali zinazokuzunguka na elimu yako, kwa sababu ya mambo ambayo umekuwa ukitia katika akili zako, sana sana kupitia kwa macho na masikio yako? Ndiyo, zaidi sana mambo unayotia katika akili zako ndiyo yanayokufanya uwe kama ulivyo. Kadiri unavyozidi kutazama jambo fulani, ndivyo unavyozidi kulizoelea.

11 Bila shaka hungefikiria kula chakula kichafu, sivyo? Basi, namna gani kama ungeendelea kutia mambo machafu katika akili zako? Bila shaka ungekuwa ukifikiri mambo mabaya. Wakati unapotazama sinema, unashirikiana na watu wanaoonyeshwa katika sinema. Nazo sinema zinatungwa kwa makusudi ya kufanya mawazo yako yaambatane na watu wanaoonyeshwa katika sinema, na mara nyingi kukufanya uunge mkono matendo ya mkosaji—mwasherati, mlawiti, hata mwuaji. Je! wewe wataka ujitie sana kwa njia hiyo pamoja na wanaume na wanawake wenye kufanyiana ngono wao kwa wao, waasherati, wazinzi na wahalifu?

12 Tena, unapotazama uasherati au jeuri ikifanywa katika sinema, labda utafikiri hivi: “Hata, mimi singefanya jambo kama lile!” Ni kweli, labda sasa hivi unaweza kuchukia sana ikiwa mtu fulani angekushauri umwibie jirani yako, uwaambie rafiki zako uongo au ufanye uasherati. Lakini namna gani ikiwa ungeendelea kushirikiana kwa muda mrefu na wevi, waasherati na wanaume na wanawake wenye kufanyiana ngono wao kwa wao, ukisikiliza fikira zao zenye kupotoka? Mwishowe, huenda ukaunga mkono matendo yao. Huenda jambo lililoonekana kuwa lenye kuchukiza sana lisionekane hivyo baadaye. Ebu fikiria hili: Je! wanaume na wanawake wengi wanaofanyiana ngono wao kwa wao walipataje kuwa hivyo? Ni kwa kupoteza wakati wakifikiria matendo hayo na kushirikiana na wengine waliokuwa hivyo.

13 Labda unadhani kwamba hungefanya uasherati. Lakini namna gani ikiwa wewe mvulana unakwenda kwenye sinema pamoja na wasichana, au ikiwa wewe msichana unakwenda pamoja na wavulana na kila mara unatazama katika sinema wanaume na wanawake wakibusiana na wakipapasana-papasana kwa mahaba (mapenzi) na kufanya uasherati? Je! baada ya kutazama sinema hizo utaelekea kufanya nini, sana sana vilevile ikiwa unakunywa vileo vinavyoondoa haya? Bila shaka unajua jibu lake. Kwa kweli, sinema nyingi za leo zinatangaza hivi: “Tutafanya mabaya! Tutavunja sheria zote, hata sheria za Mungu!” Je! hayo ndiyo maongozi unayotaka kufuata?

14 Je! kweli unadhani huwezi kuharibiwa na mavutano mabaya? Ebu kumbuka, Wazungu wengi sana ambao wakati mmoja walikuwa wenye tabia njema na wenye bidii ya kufanya kazi waliongozwa na porojo za Wanazi wafanyie wanadamu matendo mabaya sana au wayaunge mkono. Kwa hiyo usipuze ukidhani kwamba huwezi kuvutwa na porojo mbaya zinazoenezwa kupitia kwa sinema za uasherati na jeuri.

KUTIMIZA MAHITAJI YA TAFRIJA

15-19. Ni kazi gani nzuri tunazoweza kufanya ili tutimize uhitaji wetu wa tafrija?

15 Muumba wetu alitufanya ili tuone uhitaji wa kuwa na tafrija. Lakini hakukusudia hata kidogo tafrija ziwe na matendo machafu au jeuri wala kuvunja sheria zake. Ni kweli, ukiacha kutazama sinema na television zinazoonyesha mambo hayo, labda utaona kwamba unakosa vipindi vingi vya sinema na vya television. Lakini bado kuna tafrija nyingi za namna safi unazoweza kufurahia.

16 Ingawaje, tafrija au michezo ina uzuri gani ikiwa ikiisha kumalizika, huoni umeburudika au ikiwa inakuacha katika hali yenye masumbufu au kuudhika na hali ya kuchukizwa sana? Ikiwa mtu angekupa chakula ambacho kingeonekana kuwa kizuri na kitamu lakini baada ya kukila ukawa mgonjwa, je! ungerudia kukila tena? Basi, tumia busara uone namna unavyotumia wakati wako wa kupumzika katika tafrija na michezo. Usipoteze wakati kwa kutazama tafrija ya namna yo yote kwa sababu tu inapatikana, bali tumia wakati wako huo wa kupumzika kwa kufanya kazi fulani itakayokufurahisha na kukuburudisha kweli kweli, kazi ambayo unaweza kufurahia uikumbukapo.

17 Kuna michezo ya namna nyingi unayoweza kucheza nje. Watu wengi wametumia saa zao wakifurahia kutembea misituni, wakicheza mpira au michezo mingine na kukaribisha rafiki zao waje kucheza nao. Ukiwauliza wazazi wako, labda watakubali ufanye hivyo.

18 Labda unaweza vilevile kutembelea nyumba zenye makumbusho au mahali pengine pa kupendeza ambapo unaweza kupata furaha na elimu. Je! umepata kutembelea mahali ambako kuku wanafugwa, kiwanda cha kutengenezea maziwa, siagi na jibini, mahali pa mnada au kiwanda cha kupigia chapa? Ikiwa unaishi mjini, labda kuna idara za serikali zinazoweza kukueleza mahali panapopendeza mjini. Labda watakueleza juu ya viwanda vya kazi vilivyo karibu nawe vinavyokaribisha watu wa kutembelea. Zaidi ya hayo, kutembelea sehemu nzuri kama maziwa (tanganyika), milima na sehemu za pwani kwaweza kuwa tafrija yenye kufurahisha, sana sana ikiwa jamaa zaweza kufurahia mambo hayo pamoja.

19 Bila shaka, kuna uhitaji wa kuangalia tafrija hizo zisije zikawa ndiyo shabaha kuu kuliko zote katika maisha zetu hata tukose kupata faida zake. Hata hivyo jinsi tunavyoweza kushukuru kwa vile Muumba wetu alitufanya tuwe na uwezo wa kushiriki na kufurahia tafrija hizo za namna nyingi! Zaweza kufanya maisha yafae kweli kweli.

[Picha katika ukurasa wa 121]

Je! unageuzwa na mambo unayotazama?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki