MAISHA YA MKRISTO
Ujitoaji-Kimungu Una Faida Kuliko Mazoezi ya Kimwili
Je, mazoezi ya kimwili yana faida? Ndiyo, lakini yana faida ndogo yanapolinganishwa na mazoezi ya kiroho. (1Ti 4:8) Hivyo, Wakristo wanapaswa kuwa na usawaziko wanapojihusisha katika michezo.
TAZAMENI VIDEO YA VIBONZO KWENYE UBAO YENYE KICHWA MAMBO UNAYOPASWA KUJUA KUHUSU MICHEZO, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
1. Tunaweza kujifunza ustadi gani kutokana na michezo?
2. Ni mambo gani matatu yanayoweza kutusaidia kuamua ikiwa mchezo fulani unatufaa au la?
3. Zaburi 11:5 inawezaje kutusaidia kuamua ni michezo gani tunayoweza kutazama na kucheza?
4. Tunawezaje kutumia andiko la Wafilipi 2:3 na Methali 16:18 kuhusu jinsi tunavyocheza?
5. Wafilipi 1:10 inaweza kutusaidiaje kuepuka kutumia muda mwingi sana kutazama au kucheza michezo?