Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yy sura 24 kur. 187-192
  • Umewekewa Wakati Ujao Ulio Mzuri Ajabu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Umewekewa Wakati Ujao Ulio Mzuri Ajabu
  • Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MAGEUZO YATAKAPOTOKEA
  • MAGEUZO AMBAYO MUNGU ANAKUSUDIA KUIFANYIA JAMAA YA WANADAMU
  • UNAVYOWEZA KUUFURAHIA WAKATI UJAO
  • Je! Mungu Anajali?
    Je! Mungu Anajali?
  • Baraka za Ajabu kutoka kwa Mungu Zakaribia Karibu!
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Kuishi Milele Si Ndoto Tu
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Uhuru wa Kweli Chini ya Utawala wa Ufalme
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Kupata Faida Zote za Ujana Wako
yy sura 24 kur. 187-192

Sura ya 24

Umewekewa Wakati Ujao Ulio Mzuri Ajabu

1-3. (a) Ni kwa sababu gani tunaishi wakati wenye mapenaeleo zaidi katika historia ya wanadamu? (b) Ni mageuzo gani ambayo Mungu atafanyiza kwa faida yetu?

KATIKA njia nyingi unaishi katika wakati wenye mapendeleo zaidi katika historia ya wanadamu. Si kwa vile hali za ulimwengu zilivyo leo, bali kwa sababu ya mambo ambayo Biblia inaonyesha yako karibu kutokea wakati ujao.

2 Yehova Mungu anajua kadiri ya uhitaji wa kufanya mageuzo—mageuzo makubwa ya mambo hapa duniani. Ni Yeye peke yake anayeweza kufanyiza mageuzo hayo. Sasa ulimwengu wa wanadamu umekaa muda wa maelfu ya miaka. Lakini ungali unashindana na magumu yale yale ya kale ambayo yamesumbua jamii ya wanadamu sikuzote: vita, njaa, makao yasiyofaa, uonevu, magumu ya uchumi.

3 Kuna mambo mengi sana yanayotaka kutengenezwa katika taratibu ya sasa ya ulimwengu. Bila shaka kuna jambo ambalo ni bora kuliko hilo. Biblia inaonyesha kwamba Yehova Mungu anafikiria kuletea wale wanaompenda na kumtumikia jambo ambalo ni zuri zaidi. Yeye amekuwa akitumia miaka kama 6,000 akifunua kusudi lake la kutokeza taratibu iliyo mpya kabisa, paradiso ya furaha. Anaahidi kuondoa kabisa katika taratibu hiyo mpya ya mambo yenye kupendeza, hali mbovu na zenye jeuri na choyo zinazofanya maisha yasiwe yenye kufurahisha sana.

MAGEUZO YATAKAPOTOKEA

4-8. (a) Yehova atafanyizaje mageuzo hayo yanayohitajiwa? (b) Ni nini kinachohakikisha kwamba wakati wa kutukia jambo hilo umekaribia sana? (2 Timotheo 3:1-5; Mathayo 24:7, 8, 32, 33)

4 Atafanya hivi namna gani? Kwanza ni kwa kuuondoa utawala wenye fujo na usiofaa, unaoongozwa na mamia ya taratibu za kisiasa. Yeye anatangaza kusudi lake la kuziondoa na pahali pake aweke serikali yake moja, ufalme wake kupitia kwa Mwana wake Yesu Kristo. Mungu alimwongoza nabii Danieli atoe unabii huo, akisema: “Na katika siku za wafalme hao [au tawala hizo] Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele, [na ufalme huo] . . . utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.” (Danieli 2:44) Jambo hilo litatukia wakati gani? Kuna njia ya kujulia wakati litakapokaribia.

5 Ikiwa unaishi katika sehemu ya dunia ambako jua si kali sana wala baridi si kali sana, na kuona majani ya miti yanageuka kuwa rangi ya kahawa na kuanguka, tena unaona kila siku anga zikigeuka kuwa zenye rangi ya kijivu zaidi na hewa inakuwa yenye kuburudisha na baridi nzuri, kisha unaona makundi ya ndege yakiruka kwenda kwenye sehemu ya dunia iliyo na moto zaidi —bila kutazama kalenda, unajua kwamba majira ya baridi yanakaribia, sivyo? Si jambo moja tu la hayo linalokuonyesha hivyo, kwa sababu anga zaweza kuwa zenye rangi ya kijivu hata siku ya kiangazi, au huenda miti ikawa na ugonjwa ikaangusha majani yake. Lakini yote hayo kwa jumla yanafanyiza ishara (alama) hakika ya kukaribia majira ya baridi.

6 Vivyo hivyo, kuna “ishara” iliyo na mambo mengi inayotolewa na Biblia. Na ishara hii inatuonyesha kwamba umekaribia wakati wa ufalme wa Mungu kupitia kwa Kristo Yesu aitawale dunia hii. Leo unaweza kuiona ishara hiyo kwa kusoma magazeti au kupitia kwa taarifa za habari zinazotolewa na radio na television. Ni ishara gani?

7 Yesu alitoa unabii kwamba kungekuja wakati katika kizazi fulani, ambao ungekuwa wenye vita, njaa, magonjwa na matetemeko ya ardhi, pamoja na kuhangaika kwingi na mashaka mengi juu ya mambo yatakayotokea duniani wakati ujao. Je! hayo si mambo yenyewe tunayoyaona sikuzote na kuyasikia katika magazeti, radio na television? Hakuna kizazi kilichotangulia ambacho kimepata kuona yote hayo kwa wingi katika historia ya wanadamu, kama kizazi ambacho kimekuwa kikiishi duniani tangu mwaka 1914. Ndiyo maana watu wa historia wanataja mwaka 1914 kuwa “muda wenye mageuzo” katika historia ya wanadamu.

8 Alipokuwa akisema habari za kizazi kitakachoona “ishara” hiyo, Yesu alisema hivi: “Mwonapo mambo hayo yanaanza kutokea, tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu u karibu. Amin, nawaambieni, Kizazi hiki hakitapita hata hayo yote yatimie.” (Luka 21:31, 32) Hii inamaanisha kwamba taratibu mpya ya Mungu imekaribia. Italeta mageuzo gani?

MAGEUZO AMBAYO MUNGU ANAKUSUDIA KUIFANYIA JAMAA YA WANADAMU

9-13. (a) Ni hali gani zitakazokuwamo katika taratibu mpya ya Mungu kwa faida ya wanadamu wote? (b) Ni nini kinachokusadikisha kwamba bila shaka mambo hayo yanaweza kutukia nayo yatatukia? (Ufunuo 21:5)

9 Kwa kuweka dunia hii na wakaaji wake chini ya utawala wa serikali moja tu ya mbinguni iliyo kamilifu, Mungu anaahidi kumaliza kabisa ugomvi na mapigano ya kisiasa yanayopoteza mali nyingi sana za ulimwengu. Huo utakuwa mwisho wa vita vinavyomaliza vijana bora wa mataifa, kisha wengi wanarudi wakiwa vilema, bila mikono au miguu, labda wakiwa vipofu au hata wakiwa maiti. Wale wote watakaoishi katika taratibu mpya ya Mungu watakuwa watu wenye kupenda amani ambao wametimiza unabii wa Biblia katika Isaya 2:4: “Watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu, taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe.” Amani ikienea duniani pote, ndipo mambo mazuri sana yanaweza kutimizwa kwa ajili ya faida ya watu wote kila mahali.

10 Si mambo ya rushwa peke yake na hasara zinazofanywa na siasa zitakazokwisha. Vilevile taratibu kubwa mno zenye pupa za biashara zitakomeshwa. Taratibu nyingi kati ya hizo zinaichafua dunia, zinachafua hewa, maji, ardhi na kuua wanyama wa duniani. Lakini Biblia inatuambia, katika Ufunuo 11:18, kwamba Mungu anakusudia “kuwaharibu hao waiharibuo nchi.” Kisha, uzuri wa misitu ya dunia, kumetameta kwa mito na maziwa (tanganyika ndogo) yake, usafi na harufu nzuri ya hewa yake, na wingi wa ndege wake wa namna nyingi, samaki na wanyama wa mwitu watarudishwa. Unaweza kuwa mmoja wa wale watakaofurahia mambo hayo yatakayokuja ambayo Mungu amewekea wale wanaoliamini Nano lake.

11 Muumba wetu anaahidi kwamba mazao mengi ya dunia yatafurahiwa na watu wote po pote watakapoishi katika taratibu yake mpya. Hutaona tena hapa duniani watoto wanaokufa njaa wakiwa na matumbo yaliyovimba na mikono iliyokonda sana kama ilivyo leo katika sehemu nyingi za dunia. Mungu aliongoza unabii huu uandikwe katika Isaya 25:6, 8: “[Yehova] wa majeshi atawafanyia mataifa yote karamu ya vitu vinono . . . [Atameza] mauti hata milele; na Bwana [Yehova] atafuta machozi katika nyuso zote.”

12 Ndiyo, zaidi ya yote, Biblia inaonyesha kwamba Mungu atarudishia wanadamu wenye utii afya nzuri kabisa. Huzuni na mateso yote yaliyoletwa na magonjwa na maumivu na mauti yatakwisha milele wakati ufalme wa Mwana wake utakapoponya magonjwa na kutokamilika kwa wanadamu. Ufunuo 21:4 unatuambia hivi: “Atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.”

13 Maana yake utakuja wakati uzee uliotokana na kutokamilika utakapoondolewa. Lo! namna Mungu alivyo mwenye upendo kuleta hali ijayo isiyo na makunyanzi, mvi au upara, mifupa yenye kuvunjika upesi, ukosefu wa nguvu, kupumua kwa taabu na mambo mengine yote yanayotokana sasa na uzee. Ndiyo, Mungu anaweza kutendea watu ambao tayari ni wazee jambo ambalo Ayubu 33:25 anaeleza, akisema: “Nyama ya mwili wake itakuwa laini kuliko ya mtoto; huzirudia siku za ujana wake.” Ndiyo, Yehova Mungu anaweza kuleta afya na nguvu bora kuliko walizo nazo vijana leo, kwa sababu sasa hata vijana wanakuwa wagonjwa na wengine wanakufa ghafula katika umri wa uchanga.

UNAVYOWEZA KUUFURAHIA WAKATI UJAO

14-16. Inakupasa ufanye nini ili uje uufurahie wakati huo ujao ulio mzuri ajabu?

14 Wewe unaweza kuishi wakati huo mzuri ajabu ukifanya kama Biblia inavyosema: “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, kabla hazijaja siku zilizo mbaya, wala haijakaribia miaka utakaposema [kama wazee wanavyosema] , Mimi sina furaha katika hiyo.”—Mhubiri 12:1.

15 Haikupasi umfikirie Muumba wako wakati fulani tu. Inakupasa umkumbuke kila siku na mchana wote kwa kutaka kuishi kwa namna anavyopenda na namna itakayomfanya atake uwe mmojawapo wa wale watakaoishi katika taratibu yake mpya. Yeye hatakulazimisha ufanye hivyo. Inakupasa ufanye kwa kupenda kwako mwenyewe. Unajua kwamba wazazi wako hawafurahi sana wakati wanapoona unafanya jambo fulani wakiisha kukulazimisha tu. Lakini ukilifanya kwa kupenda na kwa furaha kwa sababu unajua wanapendezwa, hapo unawafurahisha sana. Vivyo hivyo, Yehova anakuambla hivi katika Neno lake: “Mwanangu, uwe na hekima na kunifurahisha moyo wangu.”—Mithali 27:11.

16 Ndiyo, ufurahie ujana wako, mwanzo wa maisha yako, na kupata faida zake zote. Sitawisha sifa zitakazokuletea furaha iliyo kubwa zaidi, wakati huu na wakati ujao. Utumie ujana wako uanze vizuri kutembea katika barabara inayokwenda kwenye uzima, si kwenye uzima wa makumi machache ya miaka katika taratibu hii ya mambo inayokufa na kuwa mbovu, bali kwenye uzima wa milele wenye nguvu mpya za ujana katika dunia ya paradiso.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki