Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 12
  • Watu Wanajenga Mnara Mkubwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watu Wanajenga Mnara Mkubwa
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Hawakujifanyia Jina Maarufu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Mnara wa Babeli
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Je, Lugha Zote Zilianzia Kwenye “Mnara wa Babeli”?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Namna Lugha Moja Itakavyoleta Umoja kwa Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 12
Wajenzi wanazungumza lugha mbalimbali na hivyo wanashindwa kuelewana

HADITHI YA 12

Watu Wanajenga Mnara Mkubwa

IKAPITA miaka mingi. Wana wa Nuhu wakazaa watoto wengi. Watoto wao walikua na kuzaa watoto zaidi. Upesi kukawa na watu wengi duniani.

Mmoja wa watu hao alikuwa kijukuu wa Nuhu jina lake Nimrodi. Alikuwa mtu mbaya aliyewinda na kuua wanyama na hata wanadamu. Nimrodi pia alijifanya mfalme atawale watu wengine. Mungu hakumpenda Nimrodi.

Mnara wa Babeli

Wakati huo watu wote walisema lugha moja. Nimrodi alitaka awakusanye wote ili awatawale. Unajua alilofanya? Aliwaambia watu wajenge mji na ndani yake mnara mkubwa. Watazame katika picha hii wakitengeneza matofali.

Yehova Mungu hakupendezwa na jengo hilo. Mungu alitaka watu watawanyike na kukaa pote duniani. Lakini wao walisema: ‘Njoni! Tujenge mji na mnara mrefu sana ufike mbinguni. Ndipo tutasifiwa sana!’ Watu hao walitaka wajiheshimu kuliko Mungu.

Kwa hiyo Mungu aliwaachisha kujenga mnara. Unajua namna alivyofanya? Aliwafanya waanze kusema lugha mbalimbali mara moja. Wajenzi hao hawakufahamiana tena. Ndiyo sababu mji wao ukaitwa Babeli, au Babiloni, maana yake “Mchafuko.”

Basi watu hao walianza kuondoka Babeli. Vikundi vya watu waliosema lugha moja vilikwenda kukaa pamoja sehemu nyingine za dunia.

Mwanzo 10:1, 8-10; 11:1-9.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki