Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 7 uku. 24-uku. 25 fu. 1
  • Mnara wa Babeli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mnara wa Babeli
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Watu Wanajenga Mnara Mkubwa
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Je, Lugha Zote Zilianzia Kwenye “Mnara wa Babeli”?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Safina ya Noa
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 7 uku. 24-uku. 25 fu. 1
Baada ya Yehova kuvuruga lugha yao, watu hawakuweza tena kujenga pamoja Mnara wa Babeli

SOMO LA 7

Mnara wa Babeli

Baada ya Gharika, wana wa Noa na wake zao walizaa watoto wengi. Watu waliongezeka na kuenea duniani, kama Yehova alivyokuwa amewaagiza.

Lakini baadhi ya watu hawakumtii Yehova. Walisema: ‘Acheni tujenge jiji na kukaa pamoja. Tutajenga mnara mrefu sana na kilele chake kitafika mbinguni. Kisha, tutakuwa watu mashuhuri.’

Yehova hakupendezwa na mambo ambayo watu hao walifanya, hivyo aliamua kusimamisha ujenzi huo. Je, unajua alifanya hivyo jinsi gani? Yehova alifanya watu hao wazungumze lugha mbalimbali. Kwa kuwa hawakuelewana, ujenzi ulikoma. Jiji walilojenga liliitwa Babeli, jina linalomaanisha “Machafuko.” Watu walitawanyika na kuishi maeneo mbalimbali ya dunia. Hata hivyo, waliendelea kufanya mambo mabaya katika maeneo mapya walioishi. Je, kuna watu walioendelea kumpenda Yehova? Tutajifunza jambo hilo katika somo linalofuata.

“Kila mtu anayejiinua atafedheheshwa, lakini yeyote anayejinyenyekeza atainuliwa.”​—Luka 18:14

Maswali: Watu wa Babeli walifanya nini? Yehova alifanya nini ili kusimamisha mradi wao?

Mwanzo 11:1-9

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki