Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • hp sura 19 kur. 176-183
  • Wewe Utamwabudu Mungu kwa Njia YAKE?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wewe Utamwabudu Mungu kwa Njia YAKE?
  • Furaha​—Namna ya Kuipata
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUTENDA MAMBO KWA NJIA YA MUNGU
  • KUWA KATI YA WATU WA MUNGU
  • BADILIKO LA MAKUNDI
  • KUABUDU MUNGU KWA NAFSI YOTE
  • Kufanye Kumtumikia Mungu Milele Kuwe Lengo Lako
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Mambo Ambayo Lazima Ufanye Ili Uishi Milele
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Kujiweka Wakf—Kwa Nani? kwa Sababu Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Uchaguzi Unaohakikishia Uzima Katika Amani na Usalama wa Kweli
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
Pata Habari Zaidi
Furaha​—Namna ya Kuipata
hp sura 19 kur. 176-183

Sura ya 19

Wewe Utamwabudu Mungu kwa Njia YAKE?

KATIKA “siku za mwisho,” Biblia inatabiri, watu wangekuwa na “ubinafsi, . . . wenye majivuno, wenye kujiona, . . . kwa nje wataonekana kama watu wenye kumcha Mungu, lakini wataikana nguvu yake.” (2 Timotheo 3:1-5, HNWW) Je! maneno hayo hayaelc zi kwa usahihi matukio tunayoona karibu yetu leo?

2 Ndiyo, katika kila upande wa maisha watu wanatenda kwa njia inayosema, “Mimi kwanza.” Wanafanya hivyo kwa mwenendo wao wanaponunua vitu madukani au wanapoendesha motokaa, kwa kujionyesha namna walivyovaa mavazi na walivyojipamba, na namna ya dansi (ngoma) wanazocheza. Lakini yote hayo hayakuleta furaha ya kweli.

3 Watu wengi hata wanafuata dini ambayo wao wanataka au ile ambayo wao wanajisikia wanahitaji. Lo! ni kosa kubwa namna gani! Sisi sio tunaopaswa kusema namna Mungu anavyopaswa kuabudiwa. Akiwa ndiye Muumba na Mpaji-Uzima, Yehova ndiye wa kuamua namna anavyopaswa kuabudiwa. (Warumi 9:20, 21) Na yale anayotutaka tufanye ni kwa faida yetu. Yanatupa uradhi sasa na kuweka akili na mioyo yetu juu ya mambo mazuri ajabu ambayo ametuwekea katika akiba wakati ujao.—Isaya 48:17.

4 Yehova halemezi Wakristo kwa kuwaagiza waendeshe sherehe zenye mambo mengi yasiyohitajiwa, wala hawawekei vizuizi visivyo na maana. Lakini Mungu anajua kwamba ili watu waendelee kuwa hai inategemea kuwa na uhusiano mwema naye. Tena anajua kwamba tunahitaji kufuata viwango vyake na kuonyesha tunahangaikia wale wengine ndipo tuweze kupata furaha ya kweli maishani. Tunapoabudu Mungu kwa njia ambayo yeye anataka, maisha yanakuwa yenye faida nyingi zaidi na yanakuwa na kusudi.

KUTENDA MAMBO KWA NJIA YA MUNGU

5 Noa ni mfano mwema wa mtu aliyefuata njia ya Mungu. Biblia inasema: “Noa alikuwa mwanamume mwenye uadilifu. Yeye alijithibitisha kuwa bila kikosa miongoni mwa watu wa rika lake. Noa alitembea pamoja na yule Mungu wa kweli.” Mungu alipokwisha kumpa maagizo ya kujenga safina kubwa sana ya kuhifadhia uhai, “Noa akafanya kulingana na yote ambayo Mungu alikuwa amemwamuru yeye. Yeye alifanya ivyo hivyo.” (Mwanzo 6:9, 22, NW) Kutenda mambo kwa njia ya Mungu kuliokoa uhai wa Noa, na pia uhai wa jamaa yake, walioambatana naye akiwa ndiye nabii wa Mungu duniani.—2 Petro 2:5.

6 Mtu mwingine aliyefuata njia ya Mungu alikuwa Abrahamu. Mungu alimwambia aiache nchi alikozaliwa. Kama ingalikuwa ni wewe, je! ungalitii? Abrahamu “alienda ivyo hivyo kama Yehova alivyokuwa amenena,” ingawa “hakuwa anajua ambako yeye alikuwa anaenda.” (Mwanzo 12:4; Waebrania 11:8, NW) Kwa sababu ya kutenda mambo kwa uaminifu kwa njia ya Mungu, Abrahamu alihesabiwa kuwa “rafiki ya Yehova.”—Yakobo 2:23, NW; Warumi 4:11.

KUWA KATI YA WATU WA MUNGU

7 Baada ya muda fulani Mungu akachagua kushughulika na kundi kubwa la watu, lile taifa la Israeli. Wakawa “watu wake, mali ya pekee, kutoka mataifa yote yaliyo juu ya use wa ile ardhi.” (Kumbukumbu la Torati 14:2, NW) Bila shaka, kila Mwisraeli alihitajiwa kutolea Mungu sala na kuwa na uhusiano wa karibu ulio wa kibinafsi pamoja naye. Lakini iliwapasa pia wajue kwamba Mungu alikuwa akielekeza kundi la watu; iliwapasa kuifuata namna ya ibada iliyoonyeshwa na sheria ambayo Mungu aliwapa wakiwa taifa zima. Hivyo wangeweza kufurahia ulinzi na baraka ya Mungu iliyowekwa juu ya lile kundi. (Kumbukumbu la Torati 28:9-14) Ebu fikiri lilikuwa pendeleo kubwa namna gani kuwa sehemu ya wale ambao Mweza Yote aliwaita “watu wangu Israeli.”—2 Samweli 7:8, NW.

8 Namna gani watu wasio Waisraeli waliotaka kumwabudu yule Mungu wa kweli? Watu wa namna hiyo walijumlika wakawa “kundi kubwa la watu waliochangamana” waliochagua kwenda na Israeli wakati Musa alipoliongoza taifa hilo kulitoa Misri. (Kutoka 12:38) Kama ungalikuwako Misri, je! wewe ungaliona kwamba ungaliweza kubaki huko na kumwabudu Mungu peke yako kwa njia yako mwenyewe?

9 Hata wakati Israeli walipokwisha kutulia katika ile Nchi ya Ahadi, wageni waliomkubali Yehova na kutaka kumwabudu waliruhusiwa kufanya hivyo. Walakini, iliwapasa kufahamu kwamba Mungu alikuwa akishughulika na kundi la watu wengi na kwamba ibada Yake ilitegemea hekalu fulani katika Yerusalemu. (1 Wafalme 8:41-43; Hesabu 9:14) Watu wasingeweza kukubalika kwa Mungu ikiwa wangeacha kiburi au roho ya kujitegemea iwaongoze kujitungia njia yao wenyewe ya kuabudu.

BADILIKO LA MAKUNDI

10 Wakati Yesu alipojitia katika huduma yake duniani, Mungu alikuwa angali akishughulika na Israeli wakiwa watu walio wakf kwake. Hivyo haikuwa lazima kila mtu aliyemkubali Masihi akutane kwa ukawaida pamoja na Yesu na kusafiri pamoja naye kama mitume. (Marko 5:18-20; 9:38-40) Lakini lile taifa kwa ujumla lilimkataa Masihi wa Yehova, likamfanya Yesu aseme hivi muda mfupi kabla hajafa: “Ule ufalme wa Mungu utachukuliwa kutoka kwenu wapewe watu ambao watauzalia matunda.”—Mathayo 21:43, Jerusalem Bible.

11 Watu hao wapya wangekuwa akina nani, ile njia ya kuabudu iliyoonyeshwa wazi katika sheria ya Mungu kwa Israeli ikiisha kuwa haitakwi tena? (Wakolosai 2:13, 14; Wagalatia 3:24, 25) Siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33 W.K., kundi la Kikristo lilianzishwa, na Mungu akawaonyesha wazi watazamaji wenye mioyo minyofu kwamba ndiye aliyefanya hivyo. (Matendo 2:1-4, 43-47; Waebrania 2:2-4) Kwanza, Wayahudi na wageni waliokuwa wameikubali dini ya Wayahudi, na, baadaye, Mataifa yale mengine, au watu wa mataifa, walipata kuwa “watu kwa ajili ya jina lake.” Sasa Mungu aliwachukua wao kuwa “jamii iliyochaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa kuwa mali ya pekee.”—Matendo 15:14-18; 1 Petro 2:9, 10, NW.

12 Kama wewe ungaliishi wakati huo na kutaka uwe na uhusiano pamoja na Mungu, ingalikuwa lazima uelekezwe kwenye kundi la Kikristo. Ndivyo alivyoelekezwa yule mwanamume Mwitalia Kornelio, na jamaa yake. (Matendo 10:1-48) Waamini waliokuwa ulimwenguni kote ndio waliokuwa lile kundi la Kikristo. (1 Petro 5:9) Makundi yote ya mahali mahali, yaliyokutana katika nyumba za watu au majengo ya watu wote, yalikuwa sehemu ya kundi moja hilo ambayo sasa Mungu alikuwa analitumia.—Matendo 15:41; Warumi 16:5.

13 Kwa kuwa Yehova ni Mungu wa utaratibu, kwa kadiri fulani alipanga kuwe na mipango mizuri ya kitengenezo makundini. Aliweka wanaume watumikie wakiwa wachungaji au waangalizi ili wawaangalie waabudu mmoja mmoja kama ilivyohitajiwa. Hao walikuwa wanaume wenye ujuzi na sifa za kuwastahilisha, na wangeweza kufundisha watu Neno la Mungu na kuwapa mazoezi washiriki wa lile kundi waweze kugawia wengine kweli ya Biblia, ili wasaidie katika ile kazi ya maana sana ya kuzihubiri “habari njema.”—2 Timotheo 2:1, 2; Waefeso 4:11-15; Mathayo 24:14; Matendo 20:28.

14 Katika njia nyingine nyingi, pia, makundi yangefaidika kutokana na waangalizi hao. Hawakupaswa kushughulika na makundi kwa njia ya kung’ang’ania mno sheria wala kuwagandamiza (kuwaonea). Bali, mgawo wao ulikuwa wa kusaidia Wakristo wenzao kwa upendo ili wautie nguvu uhusiano wao na Mungu. (Matendo 14:21-23; 1 Petro 5:2, 3) Watu wo wote waliokuwa na matatizo wangeweza kuendea wanaume wazee hao wa kiroho wapate msaada wenye fadhili, wa Kimaandiko. (Yakobo 5:13-16; Isaya 32:1, 2) Kwa sababu Wakristo walikuwa bado kukamilika, mara kwa mara ingewezekana magumu yatokee katika makundi. Waangalizi walipaswa kuwa macho kusaidia Wakristo wenzao, na kufungua macho wazuie watu wo wote ambao wangeweza kuharibu hali ya kiroho ya lile kundi.—Wafilipi 4:2, 3; 2 Timotheo 4:2-5.

15 Makundi yalipata maelekezo yaliyohitajiwa kutoka baraza inayoongoza ya Kikristo ya mitume na wanaume wazee wa kundi la Yerusalemu. Wenye kuwa katika baraza hiyo walichunguza na kuamua masuala waliyopelekewa na makundi. Tena baraza inayoongoza ilituma wajumbe wakayatembelee makundi.—Matendo 15:1-3.

16 Yehova Mungu angali anashughulika na watu wake wakiwa kundi la watu wengi. Duniani kote kuna maelfu ya makundi ya Mashahidi wa Yehova. Ikiwa wewe unataka kuwa katika umoja na njia ya Mungu ya kuabudu, kiitikie hiki kipa-moyo chake ukusanyike pamoja na Wakristo wenzako:

“Tujitahidi kushughulikiana kwa ajili ya kuongezeana bidii ya kupendana na kutenda mema. Tusiache ile desturi ya kukutana pamoja . . . bali tunapaswa kusaidiana kwani, kama mwonavyo, Siku i1e ya Bwana inakaribia.”—Waebrania 10:24, 25, HNWW.

KUABUDU MUNGU KWA NAFSI YOTE

17 Ni vema ufikirie mambo yote ambayo Yehova Mungu amekufanyia wewe. Kwake umepata uhai na misaada ya kuendeleza uhai wako kila siku. Juu ya hilo, Mungu alituma Mwana wake duniani afe akiwa dhabihu. Huo ulikuwa wonyesho wa upendo wa Mungu wenye kina kirefu, upendo ulio hakika na usiobadilika-badilika. (Warumi 5:8; 8:32, 38, 39) Kwa njia hiyo Mungu alikuwezesha upate msamaha wa dhambi na lile taraja la kupata uzima wa milele katika furaha.—Yohana 3:17; 17:3.

18 Je! sisi tutauitikiaje upendo wake? Pasipo shaka haitupasi tumpe Mungu wala upendo wake kisogo. Mtume Petro alihimiza hivi:

“Kwa hiyo, tubuni, na kugeuka ili mfutishe dhambi zenu, kwamba majira ya kuburudisha yapate kuja.”—Matendo 3:19, NW.

19 Sote tunahitaji ‘kutubu,’ kwa maana sote tumetenda dhambi, tukapungukiwa na viwango vya Mungu katika mwenendo wetu, usemi na mawazo yetu. (Warumi 2:4; 7:14-21; Yakobo 3:2) Kutubu kwetu kunamaanisha tukubali kwamba sisi ni watenda dhambi na kuona huzuni kwa sababu ya kushindwa kuishi kupatana kabisa na mapenzi ya Yehova. Je! ndivyo wewe unavyoona? Halafu, tunahitaji “kugeuka,” tubadili njia yetu ya maisha na baada ya hapo tujitahidi sana kuonyesha sifa za Yehova na kutenda mambo kwa njia yake. Tukifanya hivyo tunaweza kuwa na hakika kwamba Mungu atatusamehe na kutukubali.—Zaburi 103:8-14; 2 Petro 3:9.

20 Tunapotambua kwamba Yesu aliweka kielelezo ili sisi tuweze kufuata hatua zake katika kumtumikia Mungu, inatupasa tujaribu sana kuiga mfano wake. (1 Petro 2:21) Waebrania 10:7 inatuambia kwamba hii ndiyo iliyokuwa nia ya Yesu: “Tazama, nimekuja . . . niyafanye mapenzi yako, Mungu.” Vivyo hivyo, kumpenda Mungu na kumthamini kunapasa kutuongoze tuweke wakf maisha zetu kwake, tufanye mapenzi yake kwa nafsi yote. Bila shaka, bado tutaendelea kula, kulala, kutunza jamaa zetu na kuzipenda, kupata pumziko lenye kufurahisha na kushiriki kwa njia nyingine nyingi shughuli za kawaida za maisha. Lakini kuweka maisha zetu wakf kwa Mungu kunamaanisha kwamba mapenzi na ibada yake yawe ndiyo mambo ya kwanza, na kwamba, hata tuwe wapi au tuwe tunafanya nini, tutujaribu kwa bidii nyingi kutumia mashauri ya Mungu na kufuata mfano aliouweka Yesu.—Wakolosai 3:23, 24.

21 Maandiko yanaonyesha wazi kwamba mtu anayeweka maisha yake wakf kwa Mungu anapaswa aonyeshe hivyo mbele ya watu wengi kwa kubatizwa. Yesu aliwaambia wafuasi wake:

“Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.”—Mathayo 28:19, 20, NW.

Ikiwa wale wenye kubatizwa walitakwa wawe wamekwisha kujifunza Neno la Mungu na kuwa wanafunzi wa Kristo, ni wazi kwamba hawakuwa vitoto vichanga. Vilevile, ubatizo wao wenye kuonyesha wamejiweka wakf kwa Mungu ungefanywa kwa kuwazamisha kabisa katika maji, kama Yesu alivyobatizwa katika Mto Yordani.—Marko 1:9-11; Matendo 8:36-39.

22 Kuwa mwanafunzi aliyebatizwa wa Kristo kutakuwezesha uwe na maisha kamili yenye furaha ya Ukristo wa kweli. Hayo si maisha yenye kuongozwa na sheria nyingi za kukuambia la kufanya na lisilo la kufanya. Bali, ni maisha yenye ukuzi wa kuridhisha. Unaweza kuzidi kufanya maendeleo katika maoni yako ya kiroho na katika kufuata Neno la Mungu, na hapo uukaribie zaidi na zaidi ule mfano aliouweka Yesu.—Wafilipi 1:9-11; Waefeso 1:15-19.

23 Mfano huo utageuza mawazo na mwenendo wako wa kila siku. Unapoifuata njia ya Kikristo, utazidi kusadiki kwamba karibuni Mungu ataharibu uovu wote ili kuacha nafasi ya ‘mbingu mpya na dunia mpya ambamo uadilifu utakaa.’ Kisha utachochewa zaidi ukuze utu wa Kikristo na kuifuatia njia ya maisha itakayokuwezesha upate ruhusa ya kuwa katika taratibu mpya hiyo inayokuja. (Waefeso 4:17, 22-24) Mtume Petro aliongozwa na Mungu kuandika hivi:

“Fikirini ni namna gani ya watu inawapasa ninyi mwe, ni maisha gani za uchaji wa Mungu na za kujiweka wakf mnazopaswa kuwa nazo! Mkitazamia [taratibu mpya] , fanyeni yote mwezavyo ili mpatikane mkiwa katika amani pamoja naye, bila kutiwa waa na bila suto machoni pake.”—2 Petro 3:11, 14, New English Bible.

24 W Ni baraka kama nini wakati maisha yote ya mtu yanapoonyesha anamwabudu Yehova Mungu! Ingawa leo watu wengi wanaishi wajifurahishe wenyewe tu, kisha wajipatie kwa uchoyo raha zote wanazoweza kujipatia, wewe unaweza kuishi na kumwabudu yule Mungu wa kweli kwa njia yake. Hii ndiyo njia bora zaidi ya maisha. Je! wewe umeweka maisha yako wakf kwa Mungu, na je! unataka kubatizwa?

[Mambo ya Kuzungumziwa]

Watu wengi wanatanguliza nani, na sababu gani hilo si jambo la hekima? (1-4)

Ni kwa njia gani Noa na Abrahamu walikuwa tofauti na watu walio wengi leo? (5, 6)

Katika wakati wa Israeli wa kale, Mungu alishughulikaje na watu? (7-9)

Mungu alifanya badiliko gani la kushughulika kwake na watu? (10-12)

Mungu aliwapanga kitengenezo na kuwaelekezaje Wakristo? (13-15)

Njia ya Mungu ya kushughulika na Wakristo inapasa iwe na maana gani kwako? (16)

Kumpenda Mungu kunapasa kutuongoze tufanye nini? (17-19)

Sababu gani ubatizo ni hatua ya maana, nao unaonyesha nini? (20, 21)

Kufanya hivyo kutakuwa na maana gani kwako? (22-24)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki