Sura ya 9
Warithi wa Ufalme Washirika Ukamilifu
1. (a) Sababu gani Yesu alirithi jina bora zaidi? (b) Nani wanaweza kufaidika na mfano wake, na jinsi gani?
KWA kuwa mwaminifu mpaka kufa, Yesu alirithi jina ambalo ni bora kuliko lile la malaika. Kati ya viumbe wote wa Mungu wenye akili, Ndiye pekee aliyeonyesha kwamba mwana wa Mungu angeweza kushika ukamilifu kabisa kwa Mungu, aonyeshe hivyo kwamba Shetani ni mwongo. Kwa hiyo, mtume Paulo anaandika: “Akiisha kufanya utakaso wa dhambi [kwa kutoa ukombozi], aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu.” Ni mfano bora kama nini aliowekea wote wanaongojea ‘kuja’ kwa ule Ufalme—wale wa “kundi dogo” watakaorithi ufalme wa kimbingu na pia wale watakaokuwa raia za kidunia za ufalme huo! Kama mtume yule yule anavyoeleza baadaye: “Na tukimbie kwa uvumilivu lile shindano la mbio lililowekwa mbele yetu, wakati tunapokaza macho kwenye yule Wakili Mkuu na Mkamilishaji wa imani yetu, Yesu. Kwa sababu ya ile furaha iliyowekwa mbele yake alivumilia mti wa mateso, akidharau aibu, na ameketi mkono wa kuume wa kile kiti cha enzi cha Mungu.”—Waebrania 1:3, 4, UV; 12:1, 2, NW.
2-4. (a) Yesu alizoeza na kuwapangaje wanafunzi wake hatua kwa hatua ili wafanye utendaji wa kuhubiri? (b) Twajuaje kwamba walizipeleka “habari njema” kwenye nyumba za watu? (c) Utendaji huo ulitoa kifano gani chema kwa watumishi wa Mungu leo?
2 Yesu hakutolea tu wafuasi wake mfano ulio bora bali pia aliwafundisha na kuwazoeza, ili waweze kue ndeleza kazi ya Mungu akiisha kuondoka.
“Akaenda akisafiri mji kwa mji na kwa akihubiri na kutangaza zile habari njema za ufalme wa Mungu. Na wale kumi na wawili walikuwa pamoja naye.”—Luka 8:1, “NW.”
3 Baadaye, Yesu aliwatuma wale 12 wakiwa peke yao ‘wakahubiri ufalme wa Mungu na kuponesha.’ “Wakaenda katika eneo kutoka kijiji kwa kijiji wakitangaza zile habari njema na kufanya maponyo kila mahali.” (Luka 9:2, 6, NW) Katika miji hiyo na walipaswa kutafuta-tafuta wenye kustahili, nao walifanya hivyo kwa kwenda kwenye nyumba za watu. Iliwataka kuendelea kushika ukamilifu kwa ushujaa, kama Mashahidi wa Yehova wanavyotakiwa kufanya katika maeneo mengi leo, kwa sababu ya kupingwa kwa ujumbe huo. Yesu alisema: “Ikiwa nyumba ile inastahili, acheni amani mnayoitakia ije juu yayo; lakini ikiwa haistahili, acheni ile amani kutoka kwenu irudi juu yenu. Mahali po pote ambapo mtu ye yote hawakaribishi ndani wala kusikiliza maneno yenu, mnapotoka katika nyumba hiyo au mji huo yakung’uteni mavumbi yatoke kwenye nyayo zenu.”—Ma-thayo 10:7, 11-14, NW.
4 Baadaye, Yesu alipochagua wanafunzi wengine 70, aliwaambia: “Tazama! Mimi natuma ninyi kama wana-kondoo katikati ya mbwa-mwitu.” Hao, pia, walipaswa kutembelea nyumba za watu, maana Yesu aliendelea kusema: “Mahan po pote ambapo mnaingia ndani ya nyumba semeni kwanza, ‘Nyumba hii na iwe na amani.’ Na ikiwa rafiki ya amani yumo, amani yenu itatua juu yake. Lakini ikiwa hayumo, itarudi kwenu.” Hata ikiwa watu hawakuzisikiliza “habari njema,” walipaswa kuonywa kwamba ufalme wa Mungu ulikuwa umekaribia! (Luka 10:3-11, NW) Hiyo inatoa kifano kizuri cha kazi ya Mashahidi wa Yehova leo, kwa kuwa hao wanaenda nyumba kwa nyumba wakiwa na ujumbe wa Mungu wenye faraja na onyo.—Isaya 61:1, 2.
KUHUBIRI YAJAPOKUWA MATESO
5. Ni katika njia zipi Yesu aliyefufuliwa aliikazia aina ya kazi iliyokuwa mbele ya wafuasi wake?
5 Wakati wa kufa kwa Yesu, wanafunzi hao walitawanyika. Lakini katika pindi nyingi baada ya kufufuliwa kwake katika roho aliwatokea kwa kujivika miili mbalimbali, ili awatumainishe tena na kuwatia nguvu. (1 Wakorintho 15:3-8) Katika moja ya pindi hizo Yesu alimwuliza Petro mara tatu kama kweli alimpenda na kama alikuwa na shauku na yeye. Petro alihuzunikia hilo, lakini mara tatu Yesu akakazia kwamba, ni lazima Petro alishe na kuchunga “wana-kondoo” wake, “kondoo wadogo” wake kuonyesha ni mwenye upendo na shauku. (Yohana 21:15-17, NW) Pindi nyingine Yesu alipotokea, aliwaambia wanafunzi wake waaminifu 11 hivi:
“Mimi nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi. Na, tazama! mimi nipo pamoja na ninyi siku zote mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mathayo 28:18-20, “NW”)
Mbele yao kulikuwa na kazi nyingi ya kufanya.
6. Sababu gani wanafunzi wa Yesu wangefanya ‘kazi zilizo kubwa zaidi’?
6 Yesu alikuwa amewaambia wanafunzi wake hivi: “Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba.” (Yohana 14:12) Wangefanya kazi katika eneo kubwa kuliko yeye, na wangeendesha kazi ya kuhubiri ufalme wa Mungu kwa kipindi kirefu zaidi.
7. Ni mambo gani ya ajabu yaliyofanya ushuhuda kamili kutolewa siku ya Pentekoste, na kukawa na matokeo gani ya kustaajabisha?
7 Baada ya kufika kwenye mkono wa kuume wa Baba yake mbinguni, Yesu alifanya jambo la ajabu. Katika siku ile ya Pentekoste, mwaka wa 33 W.K., alimwaga roho takatifu juu ya wanafunzi wake waliokuwa wakingojea, akawapaka mafuta ili wawe warithi pamoja naye wa ufalme wa kimbingu wa Mungu. Hatimaye, watu 144,000 wangechaguliwa kutoka wanadamu wakawe wafalme na makuhani pamoja na Kristo mbinguni. Kwa sababu ya ule ushuhuda uliotolewa siku hiyo moja tu, Wayahudi 3,000 na waongofu walilikubali lile neno kwa moyo wakabatizwa.—Yohana 14:2, 3; Ufunuo 14:1-5; 20:4, 6; Matendo 2:1-4, 14, 40, 41.
8-11. (a) Ni pambano gani kali ambalo sasa lilitokea kati ya viongozi wa Kiyahudi na mitume? (b) Mitume walijionyeshaje kuwa washika-ukamilifu? (c) Kulingana na Matendo 5:40-42, ni mfano gani ambao mitume hao waliachia watumishi wa Mungu leo?
8 Kazi hiyo ya kuhubiri zile “habari njema” ilienea eneo lote la Yerusalemu kama moto wenye kuteketeza mwitu. Na kupinga ufalme wa Mungu kulienea ivyo hivyo. Upesi wale mitume wakaburutwa mbele ya mahakama ile ya Kiyahudi ya Sanhedrini, wakakatazwa kusema kwa jina la Yesu. Je! wangeshikamana na ukamilifu wao? Petro na Yohana walijibu hivi: “Kwamba ni jambo la uadilifu machoni pa Mungu au sivyo kusikiliza ninyi badala ya Mungu, hukumuni ninyi wenyewe. Lakini sisi, hatuwezi kuacha kusema juu ya yale mambo ambayo tumeona na kusikia.” Katika pindi hii wale mitume wakafunguliwa, na mara hiyo wao pamoja na wenzao wakatoa shukrani kwa Mungu, wakimwomba: “Sasa, Yehova, . . . uwape watumwa wako uwezo wa kuendelea kusema neno lako kwa ujasiri wote.” Hivyo wakaendelea kuhubiri kwa msaada wa roho ya Yehova.—Matendo 4:19, 20, 29, 31, NW.
9 Viongozi wa kidini wakawakamata mitume tena na kuwatia katika jela. Lakini hayakuwa mapenzi y Mungu wakae humo. Usiku huo malaika wa Yehova akawafungua, hivi kwamba mapambazuko yalitokea wakiwa wanafundisha tena katika hekalu la Yerusalemu.—Matendo 5:17-21.
10 Ile Sanhedrin ingeweza kufanya nini izuie kuenezwa kwa zile “habari njema”? Mara tena, wale mitume walipelekwa mahakamani, kuhani akawashtaki hivi: “Sisi tuliwaamuru ninyi kabisa msiendelee kufundisha juu ya msingi wa jina [la Yesu hata hivyo, tazama! mmejaza Yerusalemu kufundisha kwenu, na mmeazimia kuileta ile damu ya mtu huyo juu yetu.” Karne zote 19 lile jibu imara la mitume hao linanguruma hivi:
“Ni lazima nisi tutu Mungu kuwa mtawala badala ya wanadamu”!
Wayahudi wangeweza kufanya nini na hao washika-ukamilifu? Gamalieli mwalimu wa sheria akawapa shauri la hekima: “Msiingilie watu hawa, bali waacheni; (kwa sababu, ikiwa mpango huu na kazi hii imetoka kwa wanadamu, itapinduliwa; lakini ikiwa imetoka kwa Mungu, hamtaweza kuwapindua;) sivyo, huenda labda mkapatikana kuwa wapiganaji hasa dhidi ya Mungu.”—Matendo 5:27-39, NW.
11 Hivyo mitume wakacharazwa viboko, wakaamriwa waache kusema kisha wakafunguliwa. Walitendaje? Walishangilia kwa kuwa walihesabiwa kustahili kuteswa juu ya msingi wa jina la Yesu.
“Na kila siku katika hekalu na nyumba kwa nyumba walindelea bila kuacha wakifundisha na kuzitangaza habari njema juu ya Kristo, Yesu.” (Matendo 5:40-42, “NW”)
Warithi hao wa Ufalme walikuwa wameazimia kuvumilia yaliyokuwa ya lazima ili waendelee kufanya kazi ya Mungu. Kwa njia hiyo waliweka mfano kwa mashahidi wote wa yule Mungu wa kweli ambao wameendelea kuutangaza Ufalme “hadharani na nyumba kwa nyumba” mpaka leo hii.—Matendo 20:20, 21, NW.
“HABARI NJEMA” ZA UFALME ZAENEA
12. Kama inavyoonyeshwa katika Matendo 8:1-4, mara nyingi mateso yanatokezaje kuenezwa zaidi kwa “habari njema”?
12 Yale mateso yaliongezeka sana tena, hivi kwamba wote isipokuwa wale mitume wakatawanyika katika sehemu jirani za Yudea na Samaria. Lakini hiyo ilisaidia tu kupanua ule ushuhuda, kwa maana “wale waliokuwa wametawanyika walienda katika nchi wakizitangaza habari njema za lile neno.” (Matendo 8: 1-4, NW) Inapendeza kwamba jambo lilo hilo limetukia katika nyakati za kisasa. Wakati serikali za kidikteta zimejaribu kuzuia Mashahidi wa Yehova kwa kuwatawanya kwenye maeneo ya mbali mbali, wameendelea kuhubiri huko, na “habari njema” zimeenea.
13, 14. (a) Juma la Mungu la pekee la upendeleo kuelekea Wayahudi lilikwisha wakati gani, na ni nani wakati huo waliokubaliwa kuwa warithi wa Ufalme? (b) Maneno ya Paulo katika Matendo 13 na Warumi 11 yanashuhudiaje hilo?
13 Walakini, huko nyuma katika karne ya kwanza, je! ule ujumbe wa Ufalme ulipasa upelekwe kwa Wayahudi na Wasamaria jirani tu? Je! hesabu kamili ya washiriki wa ufalme wa mbingu ingekuwa ya kutoka kati yao tu? Haikutakiwa hivyo ingawa ushuhuda wa ajabu ulipasa kutolewa. Kwa wazi katika mwaka wa 36 W.K., wakati lile “juma” la pekee la Mungu la kupendelea Wayahudi lilipomalizika, Yehova alimwelekeza Petro atembelee afisa wa kijeshi Mwitalia, Kornelio, nyumbani kwake katika Kaisaria. Petro alipokuwa akihubiria mtu huyo asiye Myahudi na nyumba yake, roho takatifu ikawaangukia, ikawapaka mafuta wawe warithi wa Ufalme. Wakabatizwa wakawa ndio Mataifa wa kwanza wasiotahiriwa kuongoka kuwa Wakristo.—Matendo 10:1-48.
14 Baadaye, mtume Paulo na wenzake walipopatwa na upinzani wenye jeuri kwa Wayahudi katika Antiokia ya Pisidia, Paulo aliwaambia Wayahudi hao hivi: “Ilihitajiwa kabisa neno la Mungu lisemwe kwanza kwenu ninyi. Kwa kuwa mnalisukumia mbali na ninyi na hamjihukumu wenyewe kustahili uzima wa milele, tazama! twawageukia mataifa. Kwa kweli, Yehova ametuamuru kwa maneno haya, ‘Mimi nimekuweka wewe kuwa nuru ya mataifa, ili uwe wokovu kwenye pembe ya dunia.’ ” (Matendo 13:46, 47, NW) Kama Paulo alivyoeleza baadaye katika mfano, Wayahudi hao wasioamini walikuwa kama matawi ya asili yaliyokatwa kutoka mzeituni. Wayahudi hao wangaliweza kutoa ile hesabu kamili ya warithi wa Ufalme. Walakini, badala yao, “watu wa mataifa,” kama matawi ya mzeituni-mwitu, walikuwa wakipandikizwa ndani, na hivyo “Israeli [wa kiroho] wote,” kufikia ukamilifu wa hesabu ya washiriki wa Ufalme, ‘wangeokolewa.’—Warumi 11:13-26; Wagalatia 6:16, NW.
UKAMILIFU CHINI YA “DHIKI” NYINGI
15, 16. (a) Paulo alifanya na kusema nini juu ya “dhiki” nyingi, na hiyo inatupatia kiolezo gani kizuri? (b) Maoni yetu yamepaswa yaweje kuelekea kupingwa na serikali au washiriki wa jamaa, na tunaahidiwa matokeo gani?
15 Yajapokuwa mateso zaidi, huyo mwangalizi-msafiri aliye mwaminifu, yaani, mtume Paulo, akarudi Antiokia, akawatie nguvu na kuwatia moyo wanafunzi na kujenga tengenezo la kundi. Hapo ndipo Paulo aliposema:
“Ni lazima tuingie katika ufalme wa Mungu kupithi dhiki nyingi.”—Matendo 14:21-23, “NW.”
16 Paulo aliendelea kushiriki fungu lake la magumu na majaribu. Lakini alikuwa mfano bora wa kushikamana na ukamilifu. Alitoa kiolezo chema kwa wengi katika nyakati za kisasa wanaolazimika kupiga vita vikali kwa ajili ya ile imani. Baadhi ya hao wamelazimika kukabili mapigo, vifungo vya gereza na hatari kwa uhai wenyewe. Upinzani umetokana na serikali za kidikteta, au hata kutoka kwa watu wa ukoo walio wapendwa sana. Wengine wamekanwa na washiriki wa jamaa kwa sababu ya kukubali na kuchukua kwao hatua ya kuhubiri “habari njema hizi za ufalme.” (Mathayo 24:14, NW) Walakini, watu hao wamefariji-wa sana na maneno haya ya Yesu: “Hakuna mtu ambaye ameacha nyumba au akina ndugu au akina dada au mama au baba au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya zile habari njema ambaye hatapata mara mia sasa katika hiki kipindi cha wakati, nyumba na akina ndugu na akina dada na akina mama na watoto na mashamba, pamoja na mateso, na katika ule mfumo wa mambo unaokuja uzima wa milele.” (Marko 10:29, 30, NW) Wanavuna kweli kweli “mara mia” katika uhusiano wao wa karibu sana na Yehova na Mwanaye na katika kuwa na ushirika wenye furaha pamoja na jamaa ya Yehova ya duniani pote.
17. (a) Wakristo wa kwanza walilazimika pia kupambana na vishawishi gani? (b) Ni mfano na shauri gani bora sana ambalo Paulo alitupatia?
17 Mtume Paulo na wenzake walipaswa pia kupigana na vishawishi vya ulimwengu vya kufanya mambo yasiyo ya adili na vya kupenda mali. Wao walikuwa binadamu tu, kama sisi. Tunapokutana na vishawishi hivyo imetupasa tufanye kama Paulo, aliyesema: “Mimi naupiga-piga ngumi mwili wangu na kuufanya kama mtumwa, ili nikiisha kuhubiri wengine, mimi mwenyewe nisije nikakataliwa kwa njia fulani.” Na kama vile Paulo, sisi, pia, twaweza kupata ulinzi katika kuwaambia jirani zetu habari za ufalme wa Mungu. Kama Paulo alivyosema kuhusu utumishi mtakatifu huo: “Kwa kweli, ole ni wangu ikiwa sikuzitangaza habari njema!”—1 Wakorintho 9:16, 27, NW.
“TUNASHINDA” KABISA
18. Paulo aliachia Wakristo wote wa kweli kitia-moyo gani, na wewe unakiitikiaje?
18 Pia mtume Paulo aliwaambia Wakristo wenzake waliopakwa mafuta hivi: “Kama tu watoto [wa Mungu], basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye tupate na kutukuzwa pamoja naye.” Lakini yale aliyoendelea kusema yanauhusu pia ule “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine,” ambao leo wanajitahidi kufikia ile thawabu tukufu ya uzima wa milele katika dunia-paradiso. (Ufunuo 7:9; Yohana 10:16) Paulo anatia moyo Wakristo wote wa kweli, akisema:
“Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! ni dhiki, au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, an upanga? . . . lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda. Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kingine cho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.” (Warumi 817, 35-39; ona pia 2 Wakorintho 11:22-28.)
Je! wewe unasitawisha uhakika wa aina hiyo juu ya upendo wa Mungu na juu ya kule ‘kuja’ kwa ufalme wa Bwana Yesu? Imekupasa uwe unafanya hivyo!
19. Ni onyo gani ambalo Paulo alitoa juu ya hatari nyingine yenye kufisha?
19 Hatari nyingine unayohitaji kutiwa nguvu ujilinde nayo katika “siku za mwisho” ni mafundisho ya uongo. Paulo alionya juu ya hilo pia. (Matendo 20:29, 30; 2 Timotheo 3:1, 13) Walimu wa uongo wanatoka wapi, na tunaweza kujilindaje nao?