Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • kc sura 18 kur. 174-185
  • Shangwe ya Ushindi wa Ufalme!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Shangwe ya Ushindi wa Ufalme!
  • “Ufalme Wako Uje”
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KAZI KUBWA MNO
  • “MUNGU . . . WA WALIO HAI”
  • BARAKA KWA ULE “UMATI MKUBWA”
  • JJINA LA YEHOVA LATAKASWA MILELE
  • “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya”
    “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya”
  • Utawala wa Haki Wafanya Dunia kuwa Paradiso
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Wakati Ujuzi Juu ya Mungu Unapoijaa Dunia
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Mamilioni ya Walio Hai Sasa Hawatakufa Kamwe Wamalizike Katika Dunia Yetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Pata Habari Zaidi
“Ufalme Wako Uje”
kc sura 18 kur. 174-185

Sura ya 18

Shangwe ya Ushindi wa Ufalme!

1. (a) Kuna sababu gani ya kuwa na uhakika katika wakati ujao wa wanadamu? (b) Har-Magedoni itawafanya nini wenye kuiharibu dunia?

JE! WANADAMU wataangamizwa wamalizike katika dunia hii? La. Na Ufalme ndiyo sababu ya kuonyesha haitakuwa hivyo. Maana ‘Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana,’ yaani, Yesu aliyetawazwa, ndiye anayechukua hatua wakati wa ‘kuja’ kwa Ufalme ili aponde-ponde tengenezo la kidunia la Shetani na mifumo yenye kuonea watu. Katika Har-Magedoni, wale ambao wangetaka kuiharibu dunia ndio watakaoharibiwa wenyewe.—Ufunuo 11:15, 18; 14:19, 20; 19:11-16.

2, 3. (a) Unabii wa Sefania unatoa onyo gani? (b) Ni jambo gani linalotakwa ili kuokoka?

2 Mungu wetu, Yehova, ametuonya tuzidi kuwa macho kabisa tuone mambo ambayo atatimiza karibuni katika Har-Magedoni.

“ ‘Kwa hiyo jiwekeni ninyi wenyewe katika hali ya kunitazamia mimi,’ ndio usemi wa Yehova, ‘mpaka ile siku ya kuinuka kwangu niende kwenye uporaji, maana uamuzi wangu wa hukumu ni kukusanya mataifa, kukusanya pamoja falme, ili nizimwagie lawama langu, hasira yangu yote yenye kuwaka moto; maana kwa moto wa bidii yangu dunia yote itamezwa.’ ”

Lakini watakuwako wenye kuokoka, nao ni wengi! Na Yehova sasa anawatayarisha, kama maneno haya mengine ya unabii ule ule yanavyosimulia:

“Maana Napo ndipo nitayapa mataifa badiliko la kuwa na lugha safi, ili wote wapate kuita juu ya jina la Yehova, ili wamtumikie bega kwa bega.”—Sefania 3:8, 9, “NW.”

3 Je! wewe utakuwa mmoja wa waokokaji hao? Ndiyo, ikiwa ‘unaita juu ya jina la Yehova.’ Unaweza kufanyaje hivyo? Kwa kufanya badiliko la kuwa na “lugha safi”—kuziingiza katika moyo wako zile habari njema za ufalme wa Mungu zenye kusafisha, na kuchukua hatua. (Marko 13:10) Kwa kuuamini mpango wa Mungu kupitia Kristo, ni lazima ufanye kama Petro alivyowaonya kwa upole watu wake mwenyewe karne 19 zilizopita, akisema: “Kwa hiyo, tubuni, na kugeuka ili mfutishe dhambi zenu, kwamba majira ya kuburudisha yapate kuja kutoka uso wa Yehova.”—Matendo 3:19, NW.

4, 5. (a) Unawezaje kufurahia uhusiano wa karibu sana na Yehova? (b) Unawezaje kuitikia ile “lugha safi”?

4 Kama vile Yesu, ni lazima wewe ujionyeshe kuwa si sehemu ya ulimwengu wa Shetani. (Yohana 17:14, 16, NW) Kwa kujiweka wakf kwa Yehova kupitia Kristo na kubatizwa katika maji kufananisha wakf, huenda ukaingia katika uhusiano ulio wa karibu sana pamoja na Yehova Mungu. (1 Petro 3:21) Imekupasa nyakati zote utafute kusitawisha uhusiano huo wa karibu sana, unapomtumikia Mungu “bega kwa bega” pamoja na watu wake wote waliofanywa tengenezo duniani. Kwa kadiri ya nafasi yako, utataka kushiriki pamoja nao kuwajulisha “habari njema hizi za ufalme” wote watakaosikiliza.—Mathayo 24:14, NW: Warumi 10:10-18; Waebrania 13:15.

5 Je! wewe ni mtu anayeitikia hivyo ile “lugha safi” ya kweli ya Biblia? Basi weka tumaini lako katika Yehova pasipo shaka. “Kwa kuwa Yeye ni Mweza, ataokoa.”—Sefania 3:17, NW; Isaya 12:2-5.

6. Yohana alitoa shauri gani zuri. na limepasa kututia moyo tufanye nini?

6 Unapositawisha kupenda Yehova na uadilifu wake, unahitaji pia kuishi kupatana na kanuni zake za Biblia. Mtume Yohana alitoa shauri hili zuri:

“Msiwe mkiupenda wala ulimwengu wala vitu vilivyomo katika ulimwengu. Mtu ye yote akiupenda ulimwengu, upendo wa Baba haumo katika yeye; kwa sababu kila kitu kilichomo katika ulimwengu—tamaa ya mwili na tamaa ya macho na kujionyesha kwa mtu mali yake—hakitokani na Baba, bali chatokana na ulimwengu. Tena, ulimwengu unapita na ndivyo na tamaa yake, lakini yeye anayefanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.” (1 Yohana 2:15-17, “NW”)

“Milele”! Je! basi haifai kufanya mapenzi ya Mungu kwa bidii nyingi wakati wa siku za kumalizia za mfumo mbovu wa Shetani? Je! haitutii moyo katika hizi “siku za mwisho” kujiweka karibu sana na tengenezo la Yehova, kama linavyowakilishwa duniani na yule “mtumwa mwaminifu mwenye akili”?—Mathayo 24: 45-47.

KAZI KUBWA MNO

7. Baada ya Har-Magedoni, ni nini kitakachosalia?

7 Wakati kivumbi cha Har-Magedoni kitakapokuwa kikiisha, tengenezo lionekanalo la Yehova litakuwapo bado, likiwa tayari kutumia njia yo yote anayoelekeza. Sisi mmoja mmoja na tuhesabiwe kuwa tunastahili kuwapo!—Sefania 2:3; Zaburi 25:8, 9, 20.

8. (a) Ni nini kitakachohitajiwa wakati huo ili kutimiza kazi ya Mungu? (b) Watu wa Mungu watakuwa wametayarishwaje?

8 Watu wa Mungu watahitaji kuendelea kuwa tengenezo chini ya serikali ya Ufalme ili watimize kazi kubwa mno ya kurembesha dunia itakayosafishwa, kuigeuza dunia yetu iwe ‘bustani ya Mungu’ kweli kweli. (Linganisha Ezekieli 31:8.) Je! wewe pia wataka kushiriki kazi hiyo? Roho yenye nia na nishati anazotoa Mungu zitahitajiwa ili kufanya kazi ngumu hiyo—bidii ile ile ambayo Mashahidi wa Yehova wanaonyesha sasa katika ‘kuzihubiri habari njema hizi za ufalme katika dunia yote.’ Wote watahitaji kuwa wa fanya kazi kweli kweli wakifuata mfano wa yule Mfalme, aliyesema: “Baba yangu ameendelea kufanya kazi mpaka sasa, na mimi naendelea kufanya kazi.” —Yohana 5:17; 4:34, NW.

9. (a) Kutakuwako kazi ya aina gani? (b) Ni nini kinachodokeza kwamba haitakuwa kazi yenye kuchosha?

9 Bila shaka mipango ya kujenga nyumba itasitawi duniani pote—si kujengwa kwa nyumba kubwa-kubwa zenye sura mbaya-mbaya za kupangisha mjini, bali kupambwa kwa makao mazuri ya jamaa mbali-mbali katika mazingira ya kiparadiso. Ndiyo, kutakuwako kazi nyingi ya kufanya, lakini itakuwa yenye kufurahisha, kazi yenye kupendeza, kazi yenye kuleta faida ambayo Mfalme Sulemani alisema, “Hakuna jambo lililo bora” kuliko kwamba “kila mwanadamu amepaswa kula na kwa kweli kunywa na kuona mema kwa kazi ngumu yake yote.”—Mhubiri 3:12, 13, NW; linganisha Isaya 65:17, 21-25.

10. Ufunuo 21:1-4 unaonyesha nini kuhusu hali za wakati huo?

10 Wale “kondoo wengine” wa Bwana watatimiza kazi yao wakiwa chini ya hali gani? (Yohana 10:16) Ufunuo sura ya 21 unatuambia tunaloweza kutarajia. Unasimulia juu ya “mbingu mpya na dunia mpya.” Mifumo ya kibinadamu ya serikali yenye upotovu haitawali tena jamii ya watu, maana “mbingu ile ya kwanza na dunia ile ya kwanza” zimekwisha kupita. Pia, yule Ibilisi na uvutano wake wa werevu amekwisha kuondolewa. Hakuna tena “bahari” ya wanadamu wenye kuvurugika, wenye kusukwa-sukwa uku na huku wanapofuatia mambo ya kutomwogopa Mungu. Badala yake, jamii thabiti ya kibinadamu, ile “dunia mpya,” itakuwa msingi imara wa kufanyia mapenzi ya Mungu. Humo unaweza kutii kwa ushikamanifu miongozo ya “mbingu mpya,” ambazo ni yule Mfalme na “bibi arusi” wa washiriki 144,000. Akiwa ana cheo cha kuwa “mji mtakatifu, Yerusalemu mpya,” “bibi arusi” huyo mshikamanifu ‘atashuka chini kutoka mbinguni’ katika maana ya kwamba ataelekeza fikira kwenye kazi ya ujenzi itakayofanywa duniani. Na matokeo yatakuwa ya furaha kama nini! Ni kama Yohana anavyosimulia:

“Tazama! Mungu amefanya makao yake kati ya watu. Atakaa kati yao, nao watakuwa watu wake, naye atakuwa Mungu wao. Yeye atayafuta machozi yao yote; maana hakutakuwako tena na kifo, wala uchungu, wala kilio, wala maumivu; maana ile hali ya kale imepita!”—Ufunuo 21:1-4, “HNWW.”

11. (a) Ni mataraja gani mazuri ajabu yatakayofurahiwa na mamilioni ya waokokaji? (b) Mungu ataijazaje dunia watu?

11 Angalia kwamba ahadi hiyo ina lile taraja zuri ajabu la kwamba “hakutakuwako tena na kifo.” Inatarajiwa kwamba mamilioni wataokoka “dhiki ile iliyo kuu” waingie katika zile baraka za “dunia mpya.” (Ufunuo 7:9, 14) Hata hivyo maelfu ya mamilioni, mabilioni, watafurahia mwishowe uzima apa hapa chini ya ule Ufalme. Kwa nini twasema “mabilioni”? Baada ya gharika ya siku za Noa, Yehova aliwapa wale waokokaji waadilifu agizo, akisema: “Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze [dunia].” Hilo linadokeza taraja lenye furaha la kwamba kutakuwa na ndoa ya kibinadamu, na watoto watazaliwa katika uadilifu angalau kwa muda fulani baada ya Har-Magedoni. (Mwanzo 9:1, 7; 10:1-32; Mathayo 24:37) Walakini, hiyo haitakuwa njia kuu ya ‘kuijaza dunia’ wanadamu wakati huo, Basi, Mungu ataijazaje dunia yetu watu, hivyo atimize kusudi lake la awali? (Mwanzo 1:28; Isaya 45:18) Ni kwa kuufanya mara mabilioni mengi ule mwujiza wake mkubwa wa ufufuo.

“MUNGU . . . WA WALIO HAI”

12. Ni fundisho gani la Yesu lililostaajabisha umati wa watu?

12 Pindi moja, Yesu alijibu wapinzani wake, akisema:

“Kwa habari ya ufufuo wa wafu, je! hamkusoma yaliyosemwa kwenu na Mungu, kwamba, ‘Mimi ndimi Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo’? Yeye ndiye Mungu, si wa wafu, bali wa walio hai.”

Kwa maoni ya Mungu, watu hao waaminifu walikuwa kama wako hai, nao wangefufuliwa. Halaiki ya watu ilistaajabia fundisho hilo.—Mathayo 22:31-33; Luka 20:37, 38, NW.

13. Ni nini linaloweza kutazamiwa kwa habari ya “kondoo wengine” waaminifu ambao wamekufa?

13 Ni jambo la akili kutaraji kwamba waaminifu hao waliovumilia mateso “ili wapate ufufuo ulio bora,” pamoja na washika-ukamilifu wa wale “kondoo wengine” ambao leo huenda wakafa kabla ya Har-Magedoni, watapata ufufuo wa mapema katika ile “dunia mpya.” Labda wewe mwenyewe umefiwa na wapendwa wako, hata watumishi waaminifu wa Mungu. Ni furaha kama nini kuwakaribisha hao wanaporudi kutoka kwa wafu, na kuwasimulia habari ya tendo kuu la Yehova la kujitetea!—Waebrania 11:35.

14. Ni tumaini gani zuri ajabu linaloelezwa katika Yohana 5:28, 29 na Ufunuo 20:11-13?

14 Walakini, namna gani wale wengine kati ya wanadamu ambao wamekuwa wakifa muda wote huo karibu miaka 6,000 ya historia? Yesu anasema: “Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka.” (Yohana 5:28, 29) “Wafu, wakubwa kwa wadogo,” watatoka katika kaburi wasimame mbele ya kiti cha enzi cha hukumu cha Mungu.—Ufunuo 20:11-13.

15. Sababu gani ule wakati wa hukumu hautakuwa wenye kuogopesha?

15 Je! huo utakuwa wakati wenye kuogopesha watakaofufuliwa? Ijapokuwa picha za kidini zinaonyesha Hukumu ya Mwisho kuwa yenye kuogopesha, huo utakuwa wakati wenye furaha nyingi sana. Sababu ni kwamba wale watakaofufuliwa hawatahukumiwa kulingana na matendo yao mabaya ya nyakati za zamani. Watahukumiwa kwa kutegemea kama watapenda au hawatapenda kufuata matakwa yenye uadilifu ya kuishi katika makao ya ufalme wa Mungu. (Linganisha Warumi 6:7.) Na kila jitihada itafanywa kuwasaidia wasonge katika njia ya kuufikia upatanisho kamili pamoja na Mungu. Mpango wa elimu ulio mkubwa kuliko mipango yote ambayo imepata kuwako utaendelezwa chini ya tengenezo lile la Ufalme.

16. (a) Vile “vitabu” ni vitabu gani? (b) Sababu gani elimu katika “dunia mpya” itakuwa bora kupita elimu zote?

16 “Vitabu” vitafunguliwa. Vitakuwa ni maagizo yatakayoandikwa kusaidia wanadamu watakaofufuliwa wayatimize “matendo” yatakayowastahilisha kupata uzima wa milele. (Ufunuo 20:12) Kwa kuwa vifaa na mipango ya elimu itakayokuwa katika “dunia mpya” itaelekezwa na Yehova na Mfalme wake wa Kimasihi, itakuwa bora sana kupita cho chote ambacho ulimwengu wa Shetani umepata kutoa wakati wo wote.

BARAKA KWA ULE “UMATI MKUBWA”

17. Utakapookoka uingie katika “dunia mpya,” utahitaji kufanya ni ni?

17 Walakini, ikiwa wewe ni mmoja wa ule “umati mkubwa” wa waokokaji wa Har-Magedoni, wewe utahusikaje katika mpango huo? Mtume Paulo alisema: “Kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watahuishwa.” (1 Wakorintha 15:22) Wewe, pia, utahitaji ile faida ya ukombozi wa Kristo, ambayo atatumia kuinua wanadamu wafikie ukamilifu wakati wa utawala wake wa miaka 1,000. Wewe, pia, utahitaji kujifaidi na ile elimu itakayokuwa katika vile “vitabu” vya kipindi cha miaka elfu, ili uyatimize kwa ushikamanifu “matendo” yatakayokuongoza uandikwe jina lako katika “kitabu cha uzima.”

18. Ni mpango gani wa Ufalme ambao umepasa ulete furaha ya Pekee?

18 Leo, ubongo wako wa kibinadamu usiokamilika unaweza kuingiza na kutunza sehemu ndogo tu ya uwezo wote ulio nao wa kupokea habari. Labda umepata kupaza sauti na kusema, ‘Laiti ningeweza kukumbuka!’ Imekupasa ushukuru sana kwa sababu ya dhabihu ya Kristo! Kwa maana, sehemu ya ule mpango wa Ufalme wa kuwainua wanadamu haitakuwa kuondoa maumivu na uchungu wa mwili tu, bali pia uumbaji huo wa ajabu, yaani, akili yako ya kibinadamu itakamilishwa uchunguze habari na kuzituma bila kuzisahau, uzifikirie na, zaidi ya yote, uzithamini kwa njia ya sala zile sifa nzuri ajabu za Mungu wetu, Yehova. Vizuizi vya lugha vilivyotokana na kuchafuliwa kwa lugha katika ule mnara wa Babeli vitaondolewa, na wanadamu wote watafundishwa lugha moja ili wamwabudu Yehova kwa umoja, kama inavyodokezwa katika Sefania 3:9.

19. Raia za Ufalme watashiriki furaha gani?

19 Pia, mioyo mikamilifu ya kibinadamu itaongozwa na upendo wa Mungu na jirani. Si ajabu kwamba Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu alisema maneno haya kuhusu watu wake wenye kuthamini:

“Tazama, mimi ninaumba mbingu mpya na dunia mpya, na maneno ya kwanza hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni. Lakini mufurahi, na mushangilie daima, kwa ajili ya hivi ninavyoumba; maana, tazama, ninaumba Yerusalema [Mpya] uwe shangwe, na watu wake wawe furaha. Nami nitashangilia Yerusalema, na nitafurahia watu wangu; na sauti ya kulia haitasikiwa ndani yake tena, wala sauti ya kuomboleza.” (Isaya 65:17-19, “ZSB”)

Furaha na shangwe yenye kuangaza uso ya wale watawala wenzi wa Kristo 144,000 katika ufalme wake itafikia yale mabilioni ya raia za Ufalme hapa duniani watakapokuwa wakisonga mbele kuuelekea ukamilifu wa kibinadamu.

JJINA LA YEHOVA LATAKASWA MILELE

20. (a) Sababu gani ile miaka 1,000 itapita haraka? (b) Daudi alimbarikije Yehova? (c) Je! wewe unaongozwa kutoa maonyesho kama hayo ya sifa?

20 Miaka elfu moja itapita kama siku moja kwa maoni ya Yehova. Na itaonekana pia kuwa muda mfupi sana kwa wanadamu, maana watakuwa na shughuli nyingi za ujenzi! (2 Petro 3:8) Vilevile, tunaweza kutarajia kwamba kutakuwa na wakati wa starehe ilikuwa na mashirika yenye furaha na mazoezi ya mwili yenye kuleta afya, kufurahia muziki na mafaa mengine ya ufundi, na nyakati zote itakuwako mipango ya kumwabudu Muumba Mkuu wetu. Wote watataka kumbariki Yehova, kama alivyofanya Daudi katika kufanya mipango ya ibada ya hekaluni, akisema:

“Wako, 0 Yehova, ni ukuu na uweza na uzuri na ubora kamili na adhama; maana kila kitu katika mbingu na katika dunia ni chako. Wako ni ufalme, 0 Yehova, Wewe unayejiinua juu kuwa kichwa juu ya wote. Mali na utukufu ni kwa ajili yako, nawe unatawala kila kitu; na katika mkono wako mna nguvu na uweza, na katika mkono wako mna uwezo wa kukuza na kuwapa wote nguvu. Na sasa, 0 Mungu wetu, tunakushukuru na kusifu jina lako zuri.”—1 Mambo ya Nyakati 29:11-13, “NW.”

21. (a) Kristo atamaliziaje utawala wake wa miaka elfu? (b) Ufalme huo utakuwa umetimiza nini?

21 Kupatana na wonyesho mtukufu huo wa sifa, Yeye aliye mkubwa zaidi ya Daudi, yaani, Kristo Yesu, atamalizia utawala wake wa miaka elfu wenye amani na ujenzi mpya kwa kufanya yale ambayo mtume Paulo alitabiri:

“Halafu, ndipo ule mwisho, wakati anapomkabidhi Mungu wake na Baba ule ufalme, wakati amekwisha kubatilisha serikali yote na mamlaka na uwezo wote [wenye kupinga].”

Mara moja na kwa wakati wote, utawala wa Mungu utakuwa umeonyeshwa kuwa ndiyo aina inayofaa ya serikali, iliyo na nguvu vya kutosha kuletea waabudu wa Yehova faida za milele. Chini ya utawala wenye fadhili wa Ufalme, kifo kilichotokana na Adamu kitakuwa kimeondolewa na wanadamu wote wakafanywa hai “katika Kristo.”Hivyo, wale mabilioni watakaokuwa wakiishi duniani wakati huo watakuwa ‘wamewekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata waingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.’—Warumi 8:21; 1 Wakorintho 15:22-28, NW.

22. (a) Ni muda gani mfupi wa kujaribiwa utakaofuata? (b) Yesu atatimiza tendo gani la mwisho la kuondoa lawama?

22 Kwa muda mfupi, Shetani ataachiliwa atoke katika lile shimo refu ili aujaribu ulimwengu wa wanadamu utakaokuwa umekamilishwa ionekane kama utaendelea kuwa mshikamanifu kwa uufalme wa Yehova. Huenda idadi fulani isiyojulikana wakachagua kumfuata Ibilisi, lakini hukumu itatekelezwa haraka juu yao. Yule aliye “uzao” wa “mwanamke” wa Mungu, yaani, Kristo Yesu, atatenda tendo lake la mwisho la kuondoa lawama kwa kumponda kichwa yule Nyoka wa kwanza, amwangamize kabisa kabisa pamoja na watoto wake kana kwamba kwa moto unaoendelea “mchana na usiku hata milele na milele.” Lile suala kuu lililotokezwa katika Edeni juu ya kama Yehova ana haki ya kuwa na enzi kuu juu ya viumbe vyake litakuwa limejaribiwa na kukatiwa shauri kwa wakati wote!—Ufunuo 20:7-10; Mwanzo 3:15.

23. (a) Kufikiria ahadi za Mungu kumepasa kutuongoze tufanye nini? (b) Sababu gani imetupasa tutake kuona ‘ufalme wa Mungu ukija’?

23 Tunapozifikiria zile ahadi za ajabu za yule “Mfa-lme wa umilele,” Muumba Mkuu wetu, yule Bwana Yehova Mwenye Enzi Kuu, je! hatuongozwi na shukrani tusifu jina lake kama wengine siku ya Pentekoste, tuseme juu ya “mambo matukufu ya Mungu,” juu ya “Mfalme wa wafalme” ambaye yeye aliweka na Ufalme wa Kimasihi? (Matendo 2: 11; Ufunuo 15:3; 19:16, NW) Je! hatuongozwi tusali kwa Baba yetu wa kimbingu, tukisema “UFALME WAKO UJE”? (Mathayo 6:9, 10) Ndiyo, “UJE,” uharibu kazi na tengenezo la Shetani litoke katika dunia! Ndiyo, “UJE,” uwaandalie wanadamu wote aina nzuri ya serikali! Ndiyo, “UJE,” ulete utawala mtukufu wa miaka elfu ili paradiso irudishwe, wafu wafufuliwe na wanadamu wote wenye moyo wa kupenda wainuliwe wafikie ukamilifu wa kibinadamu! Ndiyo, “UJE,” ili jina la Yehova ambalo hakuna linalolingana nalo lipate kutakaswa kwa umilele wote!

[Picha katika ukurasa wa 180, 181]

Katika dunia mpya, watoto watakaozaliwa katika uadilifu hawatapatwa na ole wo wote unaosumbua jamaa nyingi leo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki