Wewe Uliumbwa na Nani?
1 Mungu aliumba mbingu na dunia.—Mwanzo 1:1
2 Mungu ana jina lake. Jina lake ni Yehova.—Zaburi 83:18
Yehova anaishi mbinguni. Yeye ni roho. Wewe huwezi kumwona.—Isaya 66:1; Yohana 1:18; 4:24
3 Yehova Mungu aliumba malaika wengi mbinguni. Wao ni roho pia. Wote walikuwa wazuri. Zamani walikuwa wakijifanya wanadamu ili waonekane na watu.—Waebrania 1:7
4 Yehova aliumba wanyama zamani za kale, kabla ya kuumba wanadamu.—Mwanzo 1:25
5 Pia Yehova aliumba mwanamume jina lake Adamu na mke wake Hawa.—Mwanzo 1:27
Mungu aliwaweka katika bustani (shamba) nzuri sana, au paradiso. Yeye aliumbia Adamu mke mmoja tu. Mwanamume huyo alipaswa kukaa pamoja na mke wake huyo mmoja.—Mwanzo 2:8, 21, 22, 24
6 Mwanadamu ni nafsi.—Mwanzo 2:7
7 Wanyama ni nafsi.—Mwanzo 1:24, tafsiri ya Biblia ya New World