Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • sj kur. 8-11
  • Kanuni za Adili Tunazofuata

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kanuni za Adili Tunazofuata
  • Shule na Mashahidi wa Yehova
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kanuni za Adili Zilizo Timanu
  • Ubora wa Kanuni za Biblia
  • Kuna Ubaya Gani Kufanya Ngono Kabla ya Ndoa?
    Amkeni!—2004
  • Je! Ni Busara Kutofanya Ngono Kabla ya Kufunga Ndoa?
    Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Elekeza Hatua Zako kwa Kufuata Kanuni za Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Je! Inawezekana Kweli Kuwa na Mwenendo Safi Kuhusu Ngono?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
Pata Habari Zaidi
Shule na Mashahidi wa Yehova
sj kur. 8-11

Kanuni za Adili Tunazofuata

Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba badiliko kubwa la maoni juu ya adili limekuwa na matokeo mabaya juu ya vijana. Kama ujuavyo, inayoitwa ati adili mpya imeimarika tangu mwaka wa 1960 na kuendelea. Askofu wa Woolwich, Uingereza, mmojawapo wa watu wa kwanza wenye kuiunga mkono, alidai hivi: “Hakuna jambo ambalo peke yalo laweza kutajwa nyakati zote kuwa ‘baya.’” Sisi hatukubaliani na hilo, lakini twataka kueleza wazi kwamba sisi hatupendi kubishana na wale wanaolikubali. Jambo tunalotaka tu kueleza ni kanuni ya adili tunayofuata na kwa nini tunaifuata.

Joseph Fletcher, profesa mashuhuri wa elimu ya dini katika United States, alisema hivi juu ya adili mpya: “Hakuna jambo kama hilo katika adili hii linalokataza kufanya ngono nje ya mpango wa ndoa, na mara fulani ni vizuri kufanya.” Naye Frederic C. Wood, profesa anayesaidia mambo ya dini katika United States, aliwaeleza wanafunzi hivi: “Hakuna sheria zilizowekwa kukataza kufanya ngono. Narudia kusema: hakuna sheria hata. Hakuna jambo unalopaswa kufanya, wala usilopaswa kufanya.”—Theology Today, Oktoba 1965, ukurasa wa 396.

Ijapokuwa huenda watu wengi wanakubali maoni kama hayo juu ya adili, Mashahidi wa Yehova wanayaona kuwa ni kinyume cha Biblia na kwa hiyo hayafai. Msimamo wetu wenye kutegemea Biblia unaonyeshwa katika kitabu chetu cha mwaka wa 1979 Kupata Faida Zote za Ujana Wako, kinachozungumza jinsi kanuni za adili zinavyogeuza mwenendo. Jambo la kuangaliwa ni kwamba, baada ya kitabu hicho kuchunguzwa na wanafunzi 100 wenye umri wa miaka 12 kufika 19, mchunguzi-habari mmoja aliandika hivi kwa njia yenye kulaumu: “Viwango vya adili kama vile vinavyosemwa katika kitabu chenu labda vingalifaa wakati mmoja, lakini mimi nina shaka kama vingefaa sasa. Kizazi hiki ni chenye elimu zaidi ya cho chote kilichotangulia.”

Hata hivyo, haionekani kwetu kwamba kukubaliwa kwa viwango vipya vya adili kumefanya vijana kuwa wenye “elimu zaidi.” Katika uchunguzi wa hivi majuzi juu ya vijana zaidi ya 160,000 wenye umri wa miaka 13 kufika 15, asilimia 41 ya wavulana na asilimia 21 ya wasichana walikuwa wamefanya ngono. Na kati ya wale wenye umri wa miaka 16 kufika 18, karibu robo tatu ya wavulana na nusu ya wasichana walikuwa wamefanya hivyo. Lakini matokeo yamekuwa nini?

Ni mimba nyingi sana kati ya wabalehe. Karibu mmoja katika wasichana-matineja (jeunnes filles) kumi katika United States anapata mimba kila mwaka—jumla yapata 1,250,000 kwa mwaka. Kati ya hao, karibu wasichana 600,000 wana watoto wao wachanga—wasichana wengine wanatoa mimba. Pia, mamilioni ya vijana wanaambukizwa kila mwaka ugonjwa wa kaswende na kisonono, ikiwa ni pamoja na malengelenge ngozini, ugonjwa wenye kuogopwa. Kwa hiyo, kuna sababu nzuri ya kutokuona hali hizo za kijamii kuwa zao la “elimu zaidi.”

Kanuni za Adili Zilizo Timanu

Kuna mvurugo mwingi juu ya ni kanuni gani za adili wanazopaswa kufundishwa vijana. Mara nyingi walimu wanalalamika juu ya ukosefu wa usadikisho ulio wazi wa kanuni za adili. Tunafahamu kwamba walimu fulani wangependa kuwa na uhuru zaidi wa kufundisha wanafunzi wao kanuni za adili zilizo timamu zinazopatikana katika Biblia. Sisi Mashahidi wa Yehova, tunaamini kwa moyo mnyofu kwamba mafundisho ya Biblia juu ya adili yana matokeo yanayofaa kweli kweli.

Wazazi walio Mashahidi wanaanza mapema kufundisha watoto wao kanuni za adili za Biblia, mara nyingi wakitumia kitabu Kupata Faida Zote za Ujana Wako kuwa msaada wa kufundisha. Kama unataka, mmoja wa wanafunzi wenu walio Mashahidi atafurahi kukuletea nakala moja. Kitakufahamisha kanuni za adili tunazofuata, kikupe maelezo zaidi juu ya maoni yetu juu ya mambo haya yanayofuata.

Ngono Kabla ya Ndoa: Sisi tunaamini kwamba, ngono zote zinazofanywa kabla ya ndoa, ambazo ni uasherati, ni kosa; si za adili. Biblia inaamuru hivi: “Ukimbieni uasherati.” (1 Wakorintho 6:18, New World Translation) “Mwepukane na uasherati.” (1 Wathesalonike 4:3) Maoni yetu ni kwamba ngono kabla ya ndoa ni kumkosea Mungu sana. “Waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu,” ndivyo Maandiko yanavyosema.—Waebrania 13:4; Ufunuo 21:8.

Ngono za Watu wa Jinsia Moja: Tunaamini pia kwamba ni kosa kulingana na adili watu wa jinsia moja kufanya ngono pamoja. Angalia inayosema Biblia juu ya watu wa jinsia moja, wanaume na wanawake, wanaofanya ngono: “Mungu amewaacha wafuate tamaa mbaya. Hata wanawake wanabadili matumizi yanayopatana na maumbile ya miili yao kwa yale yasiyopatana na maumbile. Nao wanaume hali kadhalika, wanaacha kufuata matumizi ya mume na mke wakawakiana tamaa wao kwa wao. Wanaume wanafanyiana mambo ya aibu.”—Waroma 1:26, 27, Habari Njema kwa Watu Wote; 1 Wakorintho 6:9-11.

Pombe: Pombe ni chakula na, ikitumiwa kwa kufaa, inaweza kuwa yenye faida. (Zaburi 104:14, 15; 1 Timotheo 5:23) Hata hivyo pombe inaweza kutumiwa vibaya, na mara nyingi inatumiwa vibaya. Kama Biblia inavyokazia, sisi tunaamini kwamba kulewa pombe au kuitumia kupita kiasi ni kosa zito la adili. (Mithali 20:1; 23:29-35; 1 Wakorintho 6:9, 10) Vilevile tunaheshimu hekima ya wenye mamlaka wanaotunga sheria za kukataza vijana kunywa pombe, na sisi tunazifuata sheria hizo.

Dawa za Kulevya: Sisi hatutumii dawa zenye kufanya iwe mazoea kuzitumia na kugeuza tabia kwa ajili ya kupata raha. Kwa kutaja chache, dawa kama bangi, heroin, cocaine, LSD, tambuu, miraa na tumbaku. Kwa kuwa Biblia inasihi hivi: “Na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili,” Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba ni kosa kuharibu miili yao kwa vitu vinavyoleta mazoea au kugeuza akili kwa ajili ya raha tu ya kichoyo.—2 Wakorintho 7:1.

Usemi Mchafu: Sisi tunaona kuwa jambo lisilofaa kutumia misemo michafu. Haipatani na amri hii ya Biblia: “Uasherati, uchafu wo wote ule au choyo visitajikane kamwe miongoni mwenu . . . [wala] maneno ya aibu, ya upuuzi au ubishi, yote hayo hayafai.”—Waefeso 5:3, 4, Habari Njema kwa Watu Wote.

Kuheshimu Mamlaka: Kupatana na kanuni za Biblia, sisi tunatazamia vijana wetu waheshimu mamlaka yote iliyowekwa, pamoja na walimu wa shuleni. (Warumi 13:1-7; 1 Petro 2:13-17) Yehova Mungu, ambaye watoto wetu wanafundishwa wampe heshima nyingi ya kimungu, anatuambia tuwe wanyofu na wenye kusema ukweli na kuwajali wengine.—Waebrania 13:18; Wakolosai 3:9; Waefeso 4:25; Mathayo 7:12.

Ubora wa Kanuni za Biblia

Sisi tumeona kwamba kufuata kanuni za adili za Biblia kumesaidia maisha ya jamaa zetu yakawa bora. Ijapokuwa sisi pia tuna matatizo kama watu wengine na watoto wetu si wakamilifu, kwa sehemu iliyo kubwa sisi tumeepushwa na maovu kama wivi, kusema uwongo, kupunja na kuumiza wengine. Kwa kadiri sisi na watoto wetu tunavyotii sheria za Mungu, kwa kadiri hiyo hatusumbuliwi na magonjwa ya kuambukiza ya kaswende na kisonono, wanawake kuzaa bila kuolewa, watoto haramu na utoaji wa mimba, wala hatusumbuliwi na masikitiko ya moyo na dhamiri yenye kuumizwa. Sisi tunaamini kwamba alisema kweli John Adams, yule rais wa nyakati za kwanza Mmarekani alipoitaja Biblia kuwa “kitabu kilicho bora kuliko vyote katika ulimwengu.” Pia tunaamini kwamba Abrahamu Lincoln hakukosea katika kusema kwamba kwa kuikubali Biblia “utaishi na kufa ukiwa mtu mwenye furaha zaidi na aliye bora.”

Hata hivyo, kama ujuavyo, watoto wanakazwa sana na watoto wa rika lao wafanye yale ambayo Biblia inashauri wasifanye, yaani ‘kuandamana nao katika hali ya kuishi vibaya.’ Na baadhi yao wasipoandamana nao, wengine ‘wanashangaa, na hivyo wanawatukana.’ (1 Petro 4:4, Habari Njema kwa Watu Wote) Nyakati nyingine watoto wetu wanadhihakiwa na hata kuchekelewa kwa sababu hawashiriki matendo fulani kama kufanya ngono kabla ya ndoa au mambo kama hayo. Hivyo sisi tunathamini wakati walimu wanapounga mkono jitihada za watoto wetu za kushikamana na kanuni za Biblia. Kwa njia hiyo, wanawatia moyo watoto wanaojaribu kufuata kanuni hizo.

Utaona kwamba vijana wetu hawana maoni ya kwamba wananyimwa kitu kwa sababu ya vizuizi vya kiadili vya Biblia. Tofauti na hivyo, Shahidi-kijana mmoja, alipokuwa akilinganisha maisha yake na yale ya wanashule wenzake, alisema: “Jambo tu ambalo nimenyimwa ni taabu nyingi.” Kama sisi tuonavyo, matakwa ya Mungu Mweza Yote ni ya kutulinda sisi, na kwa kuyafuata tunapata faida.—Zaburi 19:7-11.

[Picha na blabu katika ukurasa wa 8]

Kitabu kinachozungumza jinsi kanuni za adili zinavyogeuza mwenendo. Wazazi Mashahidi wanakitumia kufundisha watoto wao

[Blabu katika ukurasa wa 11]

‘Kwa kuikubali Biblia utaishi na kufa ukiwa mtu bora.’—Abraham Lincoln

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki