Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • su sura 15 kur. 113-120
  • Kugawanywa kwa Watu kwa Kutegemea Suala la Ufalme

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kugawanywa kwa Watu kwa Kutegemea Suala la Ufalme
  • Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MFALME NA “NDUGU” ZAKE
  • ‘MLIMTENDEA MMOJAWAPO WA HAO NDUGU ZANGU’
  • JE! WEWE ‘UTAURITHI UFALME’?
  • Kuna Wakati Ujao Gani kwa Kondoo na Mbuzi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Raia za Kidunia za Ufalme wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Umati Mkubwa wa Waabudu wa Kweli—Umetoka Wapi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Chukua Hatua Mara Moja Juu ya “Ishara”!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
su sura 15 kur. 113-120

Sura 15

Kugawanywa kwa Watu kwa Kutegemea Suala la Ufalme

1. Kwa nini mgawanyo kwa kutegemea suala la Ufalme ni jambo la maana sana kwa kila mmoja wetu?

KILA MMOJA wetu anakabiliwa na uamuzi wa maana sana. Suala ni juu ya mwelekeo wetu ulivyo kuhusu Ufalme wa Kimasihi wa Yehova ulio mikononi mwa Yesu Kristo. Kugawanywa kwa watu wa mataifa yote kunafanywa kwa kutegemea suala hilo. Kila mtu anawekwa katika kimoja cha vikundi viwili kwa kutegemea utendaji wake mwenyewe. Ni kimoja tu cha vikundi hivyo kitakachookoka uharibifu wa ulimwengu uliokaribia sana.—Mathayo 24:40, 41.

2. (a) Ufalme huo wa Kimasihi unahusianaje na suala la enzi kuu ya Yehova? (b) Karibuni Ufalme huo utakuwa nini, na hivyo imetupasa tuwe tukifikiria nini kwa uzito?

2 Tayari Yehova amemtawaza katika mbingu mpakwa-mafuta, Masihi wake. Mwishoni mwa “nyakati zilizowekwa za mataifa” mwaka wa 1914, Mungu alimpa Yesu Kristo mataifa yawe urithi wake—dunia yote iwe milki yake. (Zaburi 2:6, 8) Serikali ya Kimasihi, yenye Mfalme aliyepakwa mafuta na Yehova akiwa katika kiti cha ufalme, ni njia ya Mungu ya kutimizia kusudi lake mwenyewe lenye hekima na la upendo juu ya dunia hii. Kwa hiyo, mwelekeo wako juu ya Ufalme huo unaonyesha unavyohisi juu ya enzi kuu ya Yehova ya ulimwengu mzima. Karibuni Ufalme wa Kimasihi ‘utavunja vipande vipande na kuuharibu’ mfumo mzima wa kisiasa unaotawala sasa mambo ya kibinadamu na, Ufalme huo, utakuwa serikali moja juu ya dunia yote. (Danieli 2:44; Ufunuo 19:11-21) Utakapoanza kuigeuza dunia iwe Paradiso, wewe utakuwa wapi? Je! utakuwa kati ya wale wanaoongozwa na Ufalme huo wakafurahie uzima mkamilifu? Yesu alieleza msingi ambao juu yake watu wanaoishi sasa wangeweza kushiriki tazamio hilo.

MFALME NA “NDUGU” ZAKE

3. Yesu alisimulia nini katika Mathayo 25:31-33?

3 Alipokuwa akieleza mitume wake juu ya “umalizio wa mfumo wa mambo,” Yesu alitumia mifano kadha. Katika mfano wa mwisho alisema: “Wakati Mwana wa mtu atakapofika katika utukufu wake, na malaika zote wakiwa pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti cha ufalme chake. Na mataifa yote yatakusanywa mbele yake, naye atatenga watu mmoja mmoja, kama vile mchungaji anavyotenga kondoo na mbuzi. Naye ataweka kondoo kwenye mkono wake wa kulia, lakini mbuzi kushoto kwake.”—Mathayo 24:3; 25:31-33, New World Translation.

4. (a) Mfano huo unahusianaje na Danieli 7:13, 14? (b) Ni maulizo gani ambayo ingekuwa faida tukijiuliza?

4 Angalia kwamba hapa Yesu anajisema kuwa “Mwana wa mtu,” kama alivyokuwa ametangulia kufanya mara nyingi katika unabii huu. (Mathayo 24:27, 30, 37, 39, 44) Matumizi yake ya usemi huo yalikuwa kikumbusho cha yale maono ya unabii aliyopewa Danieli karibu karne sita zilizotangulia, kuhusu maono hayo nabii huyo akaandika hivi: “Nikaona katika maono ya usiku, na tazama, pamoja na mawingu ya mbingu alikuja mumoja aliye mufano wa mwana wa watu [Yesu Kristo], akakaribia huyu muzee wa siku [Yehova Mungu], wakamleta karibu naye. Akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wote, mataifa yote, na lugha zote wamutumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, isiyopita kamwe, na ufalme wake ufalme usioweza kuangamizwa.” (Danieli 7:13, 14, Zaïre Swahili Bible; Waebrania 2:5-8) Mamlaka hiyo ya kutawala amekwisha pewa Yesu Kristo. Tangu mwaka wa 1914 yeye anatawala akiwa katika kiti cha ufalme chake cha kimbingu. Wewe binafsi umeitikiaje utawala wake? Je! namna ya maisha yako inatoa ushahidi wa kwamba unamheshimu vya kufaa Huyu ambaye Mungu mwenyewe amefanya kuwa Mtawala wa dunia yote?

5. Kristo anaamuaje ukweli wa dai la mtu kuwa amejitoa kwake yeye akiwa Mfalme?

5 Maneno matupu hayatoshi. Ni rahisi mtu kusema kwamba anauamini Ufalme wa Mungu na kwamba anampenda Yesu Kristo. Lakini katika mfano wake wa kondoo na mbuzi Yesu alionyesha kwamba, kwa kuwa yeye angekuwa asiyeonekana katika mbingu, sababu kuu ambayo angefikiria katika kuamua ukweli wa madai ya mtu ingekuwa ni namna wanavyotendewa wale wanaomwakilisha Kristo duniani, “ndugu” zake.—Mathayo 25:40, 45.

6. “Ndugu” hao wa Kristo ni akina nani?

6 Hao ni nani? Ni wale ambao Mungu amechagua kutoka wanadamu wakawe warithi wa Ufalme wa kimbingu pamoja na Kristo. Hesabu ya hao ni 144,000, na wale ambao bado wapo duniani ni mabaki wachache tu. (Ufunuo 14:1, 4) Kwa sababu ‘wamezaliwa mara ya pili’ kupitia utendaji wa roho ya Mungu, wao ni wana wa Mungu, na kwa sababu hiyo wanasemwa katika Maandiko kuwa “ndugu” za Yesu Kristo. (Yohana 3:3; Waebrania 2:10, 11) Yesu anahesabu yale ambayo watu wanatendea “ndugu” hao, hata “walio wadogo” wao, kuwa ni yeye mwenyewe anatendewa.

7. Kwa nini “ndugu” za Kristo si washiriki wa makanisa ya Jumuiya ya Wakristo?

7 “Ndugu” hao za Kristo wako wapi wakati wetu huu? Je! utawaona kati ya waenda-kanisani wa Jumuiya ya Wakristo? Basi, Yesu alisema nini juu ya wafuasi wake wa kweli? “Wao si sehemu ya ulimwengu, kama vile mimi si sehemu ya ulimwengu.” (Yohana 17:16, New World Translation) Je! hilo linaweza kusemwa hivyo juu ya makanisa ya Jumuiya ya Wakristo na washiriki wayo? Kwa kadiri kubwa, mielekeo yao na mwenendo wao unaonyesha tu walivyo watu wengi walio katika sehemu ya ulimwengu wanamopatikana. Kujiingiza kwa makanisa katika siasa ni jambo linalojulikana sana. Katiba ya Umoja wa Mataifa ilipokuwa ikifanyizwa mwaka wa 1945, wajumbe wa Kiprotestanti, wa Kikatoliki na wa Kiyahudi walikuwapo wakiwa washauri. Miaka ya juzijuzi, mapapa wa Roma wameusifu Umoja wa Mataifa kuwa “ndilo tumaini la mwisho la upatano na amani” na “baraza kuu la amani na haki.” Baraza la Makanisa la Ulimwengu, lenye vikundi vya kidini vilivyo washiriki walo kama 300, hata limetoa fedha ambazo zimetumiwa kulipia mapinduzi ya kisiasa. Lakini, Yesu Kristo alimwambia Pilato, gavana Mroma hivi: “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu.”—Yohana 18:36, New World Translation.

8. (a) Ni nini kimekusaidia uwatambue “ndugu” za Kristo? (b) Kazi ya kuuhubiri Ufalme ni ya maana kwao kadiri gani?

8 Mambo ya hakika yanaonyesha kwamba kikundi kimoja tu ndicho kina msimamo ulio imara upande wa Ufalme. Kinatumia jitihada yenye nguvu ili kutangaza Ufalme huo ulimwenguni pote, huku kikiepuka kujiingiza kwa namna yo yote katika mambo ya kisiasa ya ulimwengu. Kikundi hicho ni Mashahidi wa Yehova. Miongoni mwao wanapatikana mabaki ya “ndugu” za Kristo. Kwa kufuata mfano wa Bwana wao na wa mitume wake, wamejitoa waende mji kwa mji na nyumba kwa nyumba, wakawaambie watu habari njema za Ufalme wa Mungu. (Luka 8:1; Matendo 8:12; 19:8; 20:20, 25) Mwaka wa 1919, kwenye mkusanyiko wa Mashahidi wa Yehova (wakati huo wakijulikana kuwa Wanafunzi wa Biblia wa Mataifa Yote) katika Cedar Point, Ohio, wahudhuriaji wa mkusanyiko walikumbushwa kwamba “kazi yao rasmi wakati huo, na hata sasa, ni kuutangaza Ufalme mtukufu wa Masihi unaokuja.” Kwenye mkusanyiko unaofanana na huo uliofanywa mwaka wa 1922, tena jambo hilo lilitiliwa mkazo, nao walihimizwa hivi: “Mtangazeni, mtangazeni, mtangazeni, Mfalme na ufalme wake.” Kwa kutumia kila njia waliyo nayo, wameendelea kufanya hivyo ulimwenguni pote mpaka leo hii. (Mathayo 24:14) Kwa sababu ya utendaji wao, lile suala la Ufalme limeonyeshwa kwako wewe. Unafanya nini kuhusu suala hilo?

‘MLIMTENDEA MMOJAWAPO WA HAO NDUGU ZANGU’

9. (a) Hali zinazosimuliwa katika Mathayo 25:35-40 zinahusianaje na huduma ya Ufalme? (b) Kwa hiyo watu kila mahali wamekabiliwa na jaribu gani?

9 Kwa sababu ya kuhubiri Ufalme wa Mungu kijasiri, huku wakiendelea kujitenga na ulimwengu, “ndugu” za Kristo wapakwa-mafuta kwa roho wamekuja kuwa chini ya majaribu makali. (Yohana 15:19, 21) Baadhi yao wameona njaa, kiu na ukosefu wa mavazi. Wengi wameacha nyumbani kwao wakaenda kutumikia katika maeneo ambako wakawa wageni. Wanapotimiza huduma yao, wamepatwa na magonjwa na kufungwa gerezani, hata kuuawa na watesi wao. Mambo hayo ambayo yamepata “ndugu” za Kristo yamefanya watu wa mataifa yote wakabiliwe na jaribu. Je! kumpenda Mungu na Kristo kungewafanya waje kusaidia mabalozi hao wa Ufalme wa kimbingu? (Mathayo 25:35-40; linganisha 2 Wakorintho 5:20.) Hasa jambo ambalo Mfalme anahesabu kuwa ni yeye binafsi ametendewa, ni msaada wanaotolewa kwa sababu wao ni watu wa Kristo, si fadhili za kibinadamu zinazoonyeshwa.—Marko 9:41; Mathayo 10:42.

10. (a) Kwa nini kuteta kwa “mbuzi” si kwa halali? (b) Kwa kutofautisha, “kondoo” wamechukua msimamo gani?

10 Wale wanaotoa msaada huo, Yesu anawafananisha na kondoo. Watu wanaoshindwa kuwapa “ndugu” zake msaada wanatajwa katika mfano wa Yesu kuwa mbuzi. Huenda “mbuzi” hao wakateta kwamba hawakumwona Yesu Kristo. Lakini yeye ametuma watumishi wake kwao, na hao wamejitambulisha waziwazi. Huenda si “mbuzi” wote wanaotesa “ndugu” za Kristo, lakini wala hawaongozwi na upendo kwa yule Mfalme wa kimbingu waje kusaidia wawakilishi wake. (Mathayo 25:41-45) Wanang’ang’ania ulimwengu ambao Shetani Ibilisi ndiye mtawala asiyeonekana. Wala “kondoo” hawawezi kumwona Kristo kwa njia halisi. Lakini, tofauti na hao “mbuzi,” hawa wanathibitisha kwamba hawaogopi kujitambulisha kuwa wako pamoja na “ndugu” za Kristo, wakiunga mkono watangazaji hao wa Ufalme wa Mungu. “Kondoo” wanajua wanalofanya, na wanafanya chaguo lililo hakika kwa kupendelea Ufalme wa Mungu kupitia Yesu Kristo. Ndiyo sababu hatua yao ina ustahiki machoni pa Mfalme.

11. (a) Kwa kuwa watu wengi hawajapata kukutana na mmoja wa “ndugu” za Kristo, wanawezaje kuhukumiwa juu ya msingi unaosimuliwa hapa? (b) Ni nini kinachohakikisha kufanikiwa kwa kazi hiyo?

11 Lakini inawezekanaje watu wa mataifa yote wahukumiwe juu ya msingi huo? Je! Yesu hakusema kwamba “ndugu” zake, ambao Baba angewapa Ufalme wa kimbingu, wangekuwa “kundi dogo” tu? (Luka 12:32) Watu wengi hawaonani binafsi kamwe na mmoja wao. Hiyo ni kweli, lakini “ndugu” hao wa Kristo ndio kiini cha tengenezo la mataifa yote la Mashahidi wa Yehova. Kupitia watu hao waliofanywa kuwa tengenezo, suala la maana sana juu ya Ufalme linatolewa kwa watu kila mahali. Yote hayo yanaelekezwa moja kwa moja na Kristo mwenyewe kutoka kiti cha ufalme chake cha kimbingu, kwa kusaidiwa na malaika. Katika nchi na visiwa fulani 200 kuzunguka dunia—hata kule ambako kazi ya kuhubiri Ufalme wa Mungu imepigwa marufuku na serikali—kazi ya kugawanya watu inasonga mbele pasipo kuzuiwa, na umati mkubwa wa watu wanasimama upande wa Ufalme wa Mungu.

12. (a) “Kondoo” wanaonyeshaje wazi msimamo ambao wamechukua? (b) Kwa nini wanafanya hivyo?

12 Wanaonyeshaje hivyo? Kwa kufanya kazi wakiandamana na wapakwa-mafuta, wakitangaza kwa bidii kwamba Ufalme unatawala na kwamba karibuni utaukomesha mfumo wa kilimwengu. Kwa njia hiyo wanajitambulisha kuwa wamechukua msimamo wa kuunga mkono Ufalme wa Kimasihi wa Yehova na kwa upendo wanawahimiza wengine wafanye vivyo hivyo. Kuna zaidi kinachosukuma watu hao wenye mioyo mizuri kuliko tamaa ya kuokolewa. Wanapenda Yehova kweli kweli na njia zake. Mwandalio wa Ufalme wake pamoja na Kristo akiwa Mfalme unajaza mioyo yao shukrani, na wanataka wengine nao wafaidike nao. Hivyo wanashiriki kutoa ushuhuda wa Ufalme kwa kadiri iliyo kamili zaidi sana wawezavyo. Kama Yesu alivyoagiza wanafunzi wake, ‘wanatafuta kwanza ufalme,’ bila kuruhusu kuhangaikia mahitaji ya kimwili kuusukumie mahali pa pili. Kwa njia hiyo wanajiweka katika hali ya kuja kupokea baraka kubwa sana.—Mathayo 6:31-33.

JE! WEWE ‘UTAURITHI UFALME’?

13. (a) Ni tangu wakati gani Yehova amekuwa akifikiria zawadi ya kuwapa hao walio mfano wa kondoo? (b) ‘Kuurithi ufalme’ kunamaanisha nini kwao?

13 Walichowekewa akiba wale wanaothibitisha kuwa “kondoo” wa mfano wa Yesu ni kizuri ajabu. Akiwa katika kiti cha ufalme chake cha kimbingu, anawaambia hivi: “Njoni, ninyi ambao mmebarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme uliotayarishwa kwa ajili yenu tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu.” (Mathayo 25:34, New World Translation) “Tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu,” wakati ule Adamu na Hawa walipoanza kuzaa watoto ambao wangeweza kufaidika na mwandalio wa Mungu wa kukomboa wanadamu, kulingana na Mwanzo 3:15, 16, Yehova alikuwa akifikiria zawadi ya kuwapa “kondoo” hao. (Linganisha Luka 11:50, 51.) Wana nafasi ya kufurahia katika Paradiso itakayorudishwa ule ukamilifu wa uhai wa kibinadamu ambao Adamu alipoteza. ‘Kurithi kwao ufalme’ hakumaanishi kwamba wataenda mbinguni, kwa sababu mfano huo unaonyesha kwamba “kondoo” hao si sawa na “ndugu” za Mfalme, ambao ni warithi wa Ufalme wa kimbingu. Hivyo “kondoo” hao bila shaka ni raia za kidunia za serikali ya kimbingu. Kamusi Greek-English Lexicon ya Liddell na Scott inaeleza kwamba neno hili la Kigiriki basileiʹa, ambalo hapa limetafsiriwa “ufalme,” laweza kufahamika katika maana ya usemi wa kutendewa, kumaanisha “kutawalwa na mfalme.” Kwa wazi maana hiyo ndiyo inayohusika hapa.

14. Hukumu wanayopewa “mbuzi” itatofautianaje na urithi wa wale “kondoo”?

14 “Mbuzi” watakapoondoka wakaingie katika “kukatiliwa mbali kwa milele,” katika uangamivu ulio kamili kama kwamba ni kuangamizwa kwa moto, “kondoo” watalindwa na Mfalme wa Kimasihi. (Mathayo 25:41, 46, New World Translation; linganisha Ufunuo 21:8.) Pasipo kuhitaji kufa, watahifadhiwa katika ile dhiki kubwa waingie katika “dunia mpya” yenye utukufu ambayo haitakuwa na uvutano mbaya sana wa Shetani na mfumo wa mambo wake ulio mbovu. Watakuwa na baraka hiyo kwa sababu wanafanya sasa uamuzi unaofaa kwa kutegemea suala la Ufalme.

15. (a) Twajuaje kwamba mfano huo unahusu sasa? (b) Hivyo, ni kazi gani yenye umaana sana?

15 Lingekuwa kosa kubwa kuwaza kwamba, kwa sababu kuangamizwa kwa “mbuzi” hao ni kwa milele, mfano huo utahusu baadaye, labda wakati wa Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo, wala haungehusu sasa. Tofauti na hivyo, Yesu alitoa mfano huo kuwa sehemu ya ile ishara ya “umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mathayo 24:3, New World Translation) Mambo anayosimulia yanatukia baada ya yeye kutawazwa lakini pia wakati “ndugu” zake wangali katika mwili na wanapata shida anazozitaja. Tunaishi katika wakati huo, nao unamalizika haraka sana. Kwa hiyo, ni jambo la maana kama nini sisi tuweke uhakika wote katika Ufalme, na pia tuwasaidie wengine waone umaana wa kufanya hivyo sasa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki