Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ws sura 13 kur. 106-112
  • “Mwana-Mfalme wa Amani” Aelekeza Fikira kwa Walio Nje ya Agano Jipya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Mwana-Mfalme wa Amani” Aelekeza Fikira kwa Walio Nje ya Agano Jipya
  • Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Kondoo Wengine” Watiwa Katika Kundi Moja
  • Kueneza Ule Mwaliko: “Njoo!”
  • Agano Jipya la Mungu Lakaribia Kutimizwa
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Baada ya Agano Jipya—Ufalme wa Mileani
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Kufaidika Kutokana na “Mpatanishi Mmoja kati ya Mungu na Wanadamu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Mtakuwa “Ufalme wa Makuhani”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
ws sura 13 kur. 106-112

Sura 13

“Mwana-Mfalme wa Amani” Aelekeza Fikira kwa Walio Nje ya Agano Jipya

1. Kwa sababu gani Wayahudi wa leo hawawezi kukana kwamba lile agano ambalo Musa alipatanisha lililofanywa na babu zao halingekoma?

WAYAHUDI wa asili leo, wale ambao ni wazao wa mwili wa Abrahamu mzee wa ukoo, hawawezi kukana kwamba lile agano la kale la Torati ya Musa mahali palo hapangechukuliwa na agano jipya lililo bora zaidi. Hawawezi kufutilia mbali kutoka kwa hati zao za Maandiko ya Kiebrania yale maneno ya Mungu kwenye Yeremia 31:31: “Angalia, siku zinakuja, asema [Yehova], nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.”

2. Lile swali la ni nani angekuwa Mpatanishi wa lile agano jipya mwishowe lilifunuliwaje?

2 Yeremia hakutabiri ni nani angekuwa mpatanishi wa hilo agano jipya. Lakini katika usiku wa Nisani 14, 33 W.K., wakati Yesu Kristo alipowapa wanafunzi wake kikombe cha divai ya Kupitwa, yeye alionyesha kwamba ndiye angekuwa huyo Mpatanishi. (Luka 22:20) Kwenye Waebrania 7:22 tunaambiwa kwamba yeye ndiye “mdhamini,” amana, au uhakikisho, wa hilo “agano” jipya na “lililo bora zaidi.”

3. Yesu Kristo ana cheo gani kingine kuelekea Mungu, na je! cheo hicho ni kulingana na ukoo?

3 Kwa dhabihu yake kwa ajili ya hilo agano jipya, Yesu akawa Kuhani Mkuu wa Yehova. Yeye hakuwa hivyo kwa kuwa mzao wa asili wa Haruni, kuhani mkuu wa kwanza wa Israeli. Yeye aliapishwa kwenye cheo hicho cha kuwa Kuhani Mkuu kwa kiapo cha Mungu Aliye Juu Zaidi, Yehova, Mfanyi-Kuhani. Maneno ya Zaburi 110:4 yanatumika kuhusu Yesu: “[Yehova] ameapa, wala hataghairi, Ndiwe kuhani hata milele, kwa mfano wa Melkizedeki”!—Waebrania 7:20, 21.

4. (a) Yehova alifanya agano jipya lililoahidiwa na “Israeli” wa namna gani, na kwa sababu gani? (b) Wale wanaoingizwa katika agano hilo jipya wanakuwa wana wa wazazi gani?

4 Isipokuwa baki dogo, taifa la Israeli wa asili lilimkataa Yesu Kristo kuwa si Mpatanishi wa lile agano jipya. Hivyo “nyumba ya Israeli” ambayo Mungu alifanya pamoja nayo lile agano jipya lililotabiriwa ilithibitika kuwa Israeli wa kiroho, “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16) Huyo Israeli wa kiroho alizaliwa siku ya Pentekoste, 33 W.K. Akiwa wa kiroho, angeweza kutia ndani ya wenyeji wake waamini wasio Wayahudi, au Mataifa. (Matendo 15:14) Petro alimwita “mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu.” (1 Petro 2:9) Hili “taifa takatifu” washiriki walo ni wana wa kiroho wa yule Abrahamu Mkubwa Zaidi, Yehova, yule Mfanyi na Mtimizaji wa lile agano la Kiabrahamu. Hivyo, wakati ule ule wao ni “wana” wa tengenezo la kimbingu la Yehova lililo mfano wa mke, lililofananishwa na Sara, mke wa Abrahamu. Bila kuepukika, lile agano jipya la yule Abrahamu Mkubwa Zaidi linalihesabu tengenezo hilo la kimbingu kuwa mama ya ule “uzao” ulioahidiwa, uliofananishwa na Isaka.

“Kondoo Wengine” Watiwa Katika Kundi Moja

5. Lile agano jipya lilihitaji nini hapa duniani?

5 Hilo agano jipya lilihitaji wahudumu wenye kutenda hapa duniani, nao washiriki wa mabaki ya wapakwa mafuta wametumika wakiwa “wahudumu” wanaostahili wa “agano jipya” ambalo limechukua mahali pa lile agano la Torati ya Musa. (2 Wakorintho 3:6) Wao si wahudumu viongozi wa kidini ndani ya mamia ya madhehebu ya kidini ya Jumuiya ya Wakristo, ambayo ndiyo sehemu yenye kutokeza zaidi ya Babeli Mkuu wa leo. Wao wametii ule mwito kwenye Ufunuo 18:4 na wametoka katika milki hiyo ya ulimwengu ya dini ya uwongo.

6. (a) Hesabu ya wahudumu wa hilo agano jipya ina kikomo gani? (b) Tunajuaje kwamba yule Mchungaji Mwema angeelekeza fikira zake kwa wale walio nje ya lile agano jipya?

6 Hesabu ya wahudumu hao wa hilo agano jipya ingekuwa na kikomo cha 144,000. (Ufunuo 7:1-8; 14:1-5) Kwa hiyo wakati ulikuwa lazima ufike ambapo Mchungaji Mwema angeelekeza fikira zake kwa wale wasio wahudumu wa agano jipya. Mhudumu Mkuu Zaidi wa Yehova alitangulia kuona hilo na akalitaja wakati aliposema, kwenye Yohana 10:16, kwamba alikuwa na “kondoo wengine,” ambao hawakuwa wa lile “kundi dogo” la 144,000.—Luka 12:32

7. (a) Ni kwa sababu gani washiriki wa jamii ya “kondoo wengine” si wahudumu wa agano jipya? (b) Mabaki ya wale walio katika agano jipya tayari yamekuwaje baraka kwa jamaa na mataifa ya dunia?

7 Ingawa “kondoo wengine” hawangekuwa sehemu ya “kundi dogo,” wangekuwa wahudumu wa Mungu, pia, lakini si wahudumu wa lile agano jipya. Na uhakika wa kwamba hao “kondoo wengine” wangekuwa “kundi moja” pamoja na mabaki ya hao “wahudumu wa agano jipya” ungeonyesha jambo zuri ajabu. Jambo gani? Hili: Kabla ya kutukuzwa katika Ufalme wa kimbingu, mabaki yangeshirikiana kibinafsi pamoja na “kondoo wengine” duniani. Kwa njia hiyo mabaki ya uzao wa kiroho wa Abrahamu yangeanza kuwa baraka kwa jamaa na mataifa yote kabla ya “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” kwenye Har–Magedoni na kabla ya kuanza kwa ile Mileani.—Wagalatia 3:29; Ufunuo 16:14, 16.

8. Ni wakati gani yule Mchungaji Mwema alipoelekeza fikira zake kwa wale walio nje ya agano jipya, na ni hatua gani ya kwanza ambayo hao “kondoo wengine” wamechukua?

8 Kwa kweli hivyo ndivyo imekuwa, sana sana tangu mwaka wa 1935. Tangu hapo, mamilioni ya hao “kondoo wengine” yameshirikiana na makumi ya maelfu ya makundi ya Mashahidi wa Yehova kuzunguka dunia nayo yamejiweka wakfu yenyewe kwa yule Mchungaji Mkuu Zaidi, Yehova Mungu. Hivyo yameingizwa katika lile “kundi moja” la Mchungaji Mwema, Yesu Kristo.

9. Je! Kupanuliwa kwa fikira za Mpatanishi wa lile agano jipya kulimaanisha kwamba ile huduma ya lile agano jipya ilikuwa imekoma duniani?

9 Je! Uhakika wa kwamba yule Mpatanishi wa lile agano jipya alikuwa, tangu hapo, akipanua fikira zake zitie ndani pia wale “kondoo wengine” ulimaanisha kwamba ile huduma ya lile agano jipya ilimalizika mwaka wa 1935? Hapana, kwa kuwa kungali kuna mabaki ya wahudumu wa hilo agano jipya hapa duniani, na ni lazima bado yaimalize huduma hiyo.

10. Ni nani leo wanaofaidika na huduma ya lile agano jipya kama ilivyotolewa na wale waandikaji wanane wa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo?

10 Leo, wote mabaki ya lile “kundi dogo” na “mkutano mkubwa” unaoongezeka wa “kondoo wengine” wa yule Mchungaji Mwema yanafaidika na huduma ya wengine waliowatangulia, kama vile mtume Paulo. Katika kutimiza huduma yake ya lile agano jipya kwa uaminifu mpaka kifo chake huko Roma wakati fulani kabla ya Yerusalemu kuharibiwa 70 W.K., Paulo aliongozwa na Mungu aandike vitabu 14 kati ya vile 27 vya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Mabaki ya wapakwa mafuta na ule “mkutano mkubwa” wa wale “kondoo wengine” wanaweza kuwa na shukrani kama nini kwamba wanaume waaminifu wa karne ya kwanza, kama vile mtume Paulo na wale waandikaji wengine saba wa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, walitimiza huduma yao ya lile agano jipya mpaka mwisho wa maisha zao za kidunia! Na katika wakati wetu, mamilioni ya “kondoo wengine” tayari yanafaidika na huduma ya agano jipya, kama vile inavyotolewa na mabaki yaliyopakwa mafuta chini ya Mpatanishi Yesu Kristo. “Mwana-Mfalme wa Amani” sasa ameelekeza fikira zake kwa hao “kondoo wengine” wapendwa ambao hesabu yao inaongezeka haraka sana.

11. (a) Lile agano jipya limekuwa likitenda kwa muda gani, na hiyo inaonyesha nini? (b) Mabaki ya wahudumu wa lile agano jipya yanatumika yakiwa katika cheo gani leo?

11 Hata hivyo, sasa lazima wakati uwe unakwisha! Lile agano jipya tayari limekuwa likitenda kazi kwa miaka zaidi ya 1,950, miaka zaidi ya 400 kupita lile agano la Torati ya Musa ambalo lilichukua mahali palo, nayo idadi ya wahudumu wa agano jipya inapunguka kadiri washiriki wamalizavyo mwendo wao wa kidunia katika kifo. Lakini mabaki ya leo ya wale wahudumu yanaendelea kutumika yakiwa “mtumwa mwaminifu mwenye akili” ambaye yule Bwana-Mkubwa, Yesu Kristo amemweka “juu ya vitu vyake vyote.”—Mathayo 24:45-47.

Kueneza Ule Mwaliko: “Njoo!”

12. Kulingana na Ufunuo 22:17, ni mwaliko gani unaoenezwa na ile jamii ya “Bibi-arusi,” na kwa nani?

12 Ni utumishi wenye upendo kama nini unaotolewa na hao wahudumu wa agano jipya! Kwa mfano, katika Ufunuo 22:17 tunasoma hivi: “Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure.” Jamii ya “Bibi-arusi,” pamoja na kani ya utendaji ya Yehova, au roho, wanaeneza mwaliko huo kwa wale walio nje ya agano jipya. Mwaliko huo unatolewa, si kwa wale waliokufa katika makaburi ya ukumbusho, ambao watabarikiwa kwa ufufuo kutoka kwa wafu, bali kwa watu wanaoishi sasa wakiwa hatarini kuharibiwa kwenye Har–Magedoni lakini walio na masikio ya kusikia.

13. (a) Je! Ule mwaliko ambao jamii ya “Bibi-arusi” imeeneza umekuwa kazi bure? Eleza. (b) Wale ambao tayari wamekubali mwaliko huo wanafanya nini katika kutii Ufunuo 22:17? (c) Ni lazima iweje kwa habari ya wakati unaobaki wa kueneza mwaliko huo?

13 Kuenezwa ulimwenguni pote kwa mwaliko huu wa upendo sana sana tangu 1935 hakukuwa kazi bure. Zaidi ya milioni tatu tayari wameitikia mwaliko huo wa neema kwa kuja wanywe. Wakiwa wale waliosikia kwa kuthamini, kwa utii bado wanawaambia “Njoo!” mamilioni mengine mengi yaliyo na kiu cha uzima usio na mwisho katika dunia paradiso. Lakini wakati wa kueneza mwaliko huu wa neema kwa “kondoo wengine” una kikomo. Baada ya kuwa ukienezwa kwa zaidi ya nusu karne, wakati unaobaki sasa unapasa uwe mfupi sana, kwa kuwa vita ya Mungu ya Har–Magedoni inaning’inia vya kutisha sana juu ya “kizazi hiki” cha wanadamu.—Mathayo 24:34.

14. Ni kwa ajili ya nini imetupasa tuwe tukimpa Yehova shukrani na sifa?

14 Kwa hiyo, sasa, shukrani zimwendee Yehova kwa kuwa yeye ametoa Mpatanishi mwenye uwezo ambaye kwa kufaulu ametimiza kusudi la lile agano jipya katika kutokeza kikundi cha watu hodari, 144,000, kwa ajili ya jina Lake! Vilevile, sifa imwendee Yehova kwa kuwa Mpatanishi wake akiwa Mchungaji Mwema tayari analeta mamilioni yenye kuongezeka ya “kondoo wengine” katika “kundi moja,” ambamo tayari yameingia kwenye faida za mapema zinazowamiminikia wanadamu kutoka agano jipya!

[Picha katika ukurasa wa 111]

Mamilioni ya “kondoo wengine” wamekuja katika tengenezo la Yehova lionekanalo hizi siku za mwisho

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki