Wao Huamini Nini?
Mashahidi wa Yehova humwamini Mungu Mweza Yote, Yehova, Muumba wa mbingu na dunia. Kuwako kwenyewe kwa maajabu yaliyofanywa kwa ufundi mkubwa katika ulimwengu wote mzima unaotuzunguka kwathibitisha kwa njia ya akili kwamba Muumba mwenye akili na uwezo mkuu aliuumba wote. Kama vile kazi za wanaume na wanawake zinavyoonyesha sifa zao, ndivyo na kazi za Yehova Mungu. Biblia hutuambia kwamba “mambo yake yasiyoonekana tangu kuumbwa ulimwengu yanaonekana, na kufahamika kwa kazi zake.” Pia, bila sauti wala maneno, “mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu.”—Warumi 1:20; Zaburi 19:1-4.
Watu hawafinyangi vyungu vya udongo wala kutengeneza televisheni na kompyuta bila kusudi fulani. Dunia na viumbe vyayo vya mimea na wanyama, ni vitu vya ajabu zaidi sana. Muundo wa mwili wa kibinadamu pamoja na matrilioni yao ya chembechembe, ni jambo tusiloweza kulielewa—hata ubongo tunaotumia kufikiri wastaajabisha kiasi cha kutoweza kuufahamu! Ikiwa wanadamu wana kusudi la kubuni vitu vyao ambavyo ni vidogo sana vikilinganishwa, bila shaka Yehova Mungu alikuwa na kusudi la kuumba viumbe vyake vyenye kutia hofu nyingi! Mithali 16:4 husema ndivyo: “BWANA [Yehova, NW] amefanya kila kitu kwa kusudi lake.”
Yehova aliifanya dunia kwa kusudi, kama alivyowatolea taarifa watu wawili wa kwanza: “Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi . . . , mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.” (Mwanzo 1:28) Kwa sababu hawakutii, jamaa hao wawili walishindwa kuijaza dunia familia zenye uadilifu ambazo zingeitunza kwa upendo dunia na mimea na wanyama waliomo. Lakini kushindwa kwao hakumaanishi kusudi la Yehova limeshindwa. Maelfu ya miaka baadaye iliandikwa hivi: “Mungu; ndiye aliyeiumba dunia na kuifanya . . . hakuiumba ukiwa.” Yeye “aliiumba ili ikaliwe na watu.” Haitaharibiwa, bali “dunia hudumu daima.” (Isaya 45:18; Mhubiri 1:4) Kusudi la Yehova kwa dunia litatimizwa: “Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.”—Isaya 46:10.
Kwa hiyo, Mashahidi wa Yehova huamini kwamba dunia itadumu milele na kwamba watu wote, wanaoishi na waliokufa, watakaopatana na kusudi la Yehova kwa dunia iliyorembwa, yenye kukaliwa wanaweza kuishi milele juu yayo. Ainabinadamu yote ilirithi kutokamilika kutoka kwa Adamu na Hawa, na kwa sababu hiyo ni watenda dhambi. (Warumi 5:12) Biblia hutuambia hivi: “Mshahara wa dhambi ni mauti.” “Walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote.” “Hiyo nafusi . . . ifanyayo dhambi ndiyo itakayokufa.” (Warumi 6:23; Mhubiri 9:5, Union Version; Ezekieli 18:4, 20, The Old Testament in Swahili) Basi wanaweza kuishije tena ili washiriki baraka za kidunia? Ni kupitia dhabihu ya ukombozi ya Kristo Yesu tu, maana alisema: “Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi.” “Watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka.”—Yohana 11:25; 5:28, 29; Mathayo 20:28.
Hayo yatatokeaje? Yameelezwa katika ‘habari njema ya ufalme’ ambayo Yesu alianza kutangaza alipokuwa hapa duniani. (Mathayo 4:17-23) Lakini leo Mashahidi wa Yehova wanazihubiri habari njema kwa njia ya pekee sana.
[Chati katika ukurasa wa 13]
WANAYOAMINI MASHAHIDI WA YEHOVA
IMANI SABABU YA KIMAANDIKO
Biblia ni Neno la Mungu na 2 Tim. 3:16, 17;
ni kweli 2 Pet. 1:20, 21; Yn. 17:17
Jina la Mungu ni Yehova Zab. 83:18; Isa. 26:4;
Kristo alikuwa wa kwanza Kol. 1:15; Ufu. 3:14
wa viumbe vya Mungu
Kristo alikufa mtini, Gal. 3:13; Mdo. 5:30
si msalabani
Uhai wa kibinadamu wa Kristo Mt. 20:28; 1 Tim. 2:5, 6;
ulilipwa uwe ukombozi Tito 2:14; 1 Pet. 2:24
kwa ajili ya wanadamu watiifu
Dhabihu moja ya Kristo ilitosha Rum. 6:10; Ebr. 9:25-28
Kristo alifufuliwa kutoka 1 Pet. 3:18; Rum. 6:9;
kwa wafu akiwa mtu Ufu. 1:17, 18
wa roho asiyeweza kufa
Kuwapo kwa Kristo Yn. 14:19; Mt. 24:3; 2 Kor. 5:16;
ni katika roho Zab. 110:1, 2
Ufalme mikononi mwa Kristo Isa. 9:6, 7; 11:1-5; Dan. 7:13, 14;
utatawala dunia Mt. 6:10
kwa uadilifu na amani
Ufalme utaletea dunia Zab. 72:1-4; Ufu. 7:9, 10, 13-17;
hali bora kabisa za maisha Ufu. 21:3, 4
Dunia haitaharibiwa kamwe Mhu. 1:4; Isa. 45:18; Zab. 78:69
wala kukaa utupu bila watu
Mungu ataharibu mfumo Ufu. 16:14, 16; Sef. 3:8; Dan. 2:44;
wa mambo wa sasa Isa. 34:2
katika pigano la Har–Magedoni
Waovu wataharibiwa milele Mt. 25:41-46; 2 The. 1:6-9
Watu ambao Mungu anakubali Yn. 3:16; 10:27, 28; 17:3;
watapokea uhai wa milele Mk. 10:29, 30
Kuna njia moja tu Mt. 7:13, 14; Efe. 4:4, 5
inayoongoza kwenye uhai
Sasa tumo katika Mt. 24:3-14; 2 Tim. 3:1-5;
‘wakati wa mwisho’ Luka 17:26-30
Nafsi ya kibinadamu inakoma Eze. 18:4, NW; Mhu. 9:10;
kuwapo wakati wa kufa Zab. 6:5; 146:4; Yn. 11:11-14
Helo ni kaburi la jumla Ayu. 14:13, Dy;
la ainabinadamu Ufu. 20:13, 14, AV (pambizo)
Tumaini kwa wafu ni ufufuo 1 Kor. 15:20-22;
Kifo kilichotoka 1 Kor. 15:26; Ufu. 21:4; Isa. 25:8;
kwa Adamu kitakoma 1 Kor. 15:54
Kundi dogo la watu 144,000 Luka 12:32; Ufu. 14:1, 3;
tu ndilo litaenda mbinguni 1 Kor. 15:40-53; Ufu. 5:9, 10
likatawale pamoja na Kristo
Wale 144,000 wanazaliwa tena 1 Pet. 1:23; Yn. 3:3; Ufu. 7:3, 4
kuwa wana wa kiroho wa Mungu
Agano jipya lilifanywa Yer. 31:31; Ebr. 8:10-13
pamoja na Israeli wa kiroho
Kundi la Kristo limejengwa Efe. 2:20; Isa. 28:16; Mt. 21:42
juu yake mwenyewe
Sala lazima zipelekwe Yn. 14:6, 13, 14; 1 Tim. 2:5
kwa Yehova tu kupitia Kristo
Mifano haipasi kutumiwa kamwe Kut. 20:4, 5; Law. 26:1;
katika ibada 1 Kor. 10:14; Zab. 115:4-8
Uasiliani-roho lazima uepukwe Kum. 18:10-12; Gal. 5:19-21;
Shetani ni mtawala 1 Yn. 5:19; 2 Kor. 4:4; Yn. 12:31
wa ulimwengu asiyeonekana
Haimpasi kamwe Mkristo ashiriki 2 Kor. 6:14-17; 11:13-15;
matangamano ya dini mbalimbali Gal. 5:9; Kum. 7:1-5
Ni lazima Mkristo Yak. 4:4; 1 Yn. 2:15;
ajitenge na ulimwengu Yn. 15:19; 17:16
Sheria zote za wanadamu Mt. 22:20, 21; 1 Pet. 2:12; 4:15
zisizopingana na sheria
za Mungu zapasa kutiiwa
Kutia damu mwilini kupitia kinywa Mwa. 9:3, 4; Law. 17:14;
au mishipa huvunja sheria za Mungu Mdo. 15:28, 29
Ni lazima kutii sheria 1 Kor. 6:9, 10; Ebr. 13:4;
za Biblia juu ya maadili 1 Tim. 3:2; Mit. 5:1-23
Ni Wayahudi tu walioagizwa Kum. 5:15; Kut. 31:13;
kushika Sabato na kulikoma Rum. 10:4; Gal. 4:9, 10;
na Sheria ya Musa Kol. 2:16, 17
Jamii ya makasisi na Mt. 23:8-12; 20:25-27;
vyeo vya pekee havifai Ayu. 32:21, 22
Binadamu hakutokea Isa. 45:12; Mwa. 1:27
kwa mageuzi bali aliumbwa
Kristo aliweka kielelezo ambacho 1 Pet. 2:21; Ebr. 10:7;
ni lazima kifuatwe katika Yn. 4:34; 6:38
kumtumikia Mungu
Ubatizo wa uzamisho kamili Mk. 1:9, 10; Yn. 3:23;
hufananisha kujiweka wakfu Mdo. 19:4, 5
Ni lazima Wakristo watoe Rum. 10:10; Ebr. 13:15;
ushuhuda wa peupe juu ya Isa. 43:10-12
kweli ya Kimaandiko
[Picha katika ukurasa wa 12]
DUNIA . . . iliyoumbwa na Yehova . . . itunzwe na mwanadamu . . . itakaliwa milele
[Hisani]
picha ya NASA