Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jt kur. 12-14
  • Wanaamini Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wanaamini Nini?
  • Mashahidi wa Yehova—Wao Ni Nani? Wanaamini Nini?
  • Habari Zinazolingana
  • Wao Huamini Nini?
    Mashahidi wa Yehova Katika Karne ya 20
  • Funzo Namba 10—Biblia Asilia na Kweli
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Kweli Tunazopenda Kufundisha
    Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
  • Sehemu ya 1: Mafundisho ya Kikristo
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
Pata Habari Zaidi
Mashahidi wa Yehova—Wao Ni Nani? Wanaamini Nini?
jt kur. 12-14

Wanaamini Nini?

MASHAHIDI WA YEHOVA huamini kwamba kuna Mungu Mweza Yote, Yehova, Muumba wa mbingu na dunia. Kuwako kwenyewe kwa maajabu yaliyofanywa kwa ufundi mkubwa katika ulimwengu wote mzima unaotuzunguka kwathibitisha kwa njia ya akili kwamba Muumba mwenye akili na uwezo mkuu aliuumba wote. Kama vile kazi za wanaume na wanawake zinavyoonyesha sifa zao, ndivyo na kazi za Yehova Mungu. Biblia hutuambia kwamba “sifa zake zisizoonekana zaonwa waziwazi tangu uumbaji wa ulimwengu na kuendelea, kwa sababu zafahamiwa kwa vitu vilivyofanywa.” Pia, bila sauti wala maneno, “mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu.”—Waroma 1:20; Zaburi 19:1-4.

Watu hawafinyangi vyungu vya udongo wala kutengeneza televisheni na kompyuta bila kusudi fulani. Dunia na mimea na wanyama wake, ni vitu vya ajabu sana. Muundo wa mwili wa kibinadamu pamoja na trilioni zake za chembe, ni jambo tusiloweza kulielewa—hata ubongo tunaotumia kufikiri wastaajabisha kiasi cha kutoweza kuufahamu! Ikiwa wanadamu wana kusudi la kubuni vitu vyao ambavyo ni vidogo sana vikilinganishwa, bila shaka Yehova Mungu alikuwa na kusudi la kuumba viumbe vyake vya ajabu sana! Mithali 16:4 husema hivyo: “BWANA amefanya kila kitu kwa kusudi lake.”

Yehova aliifanya dunia kwa kusudi, kama alivyowaarifu wanadamu wawili wa kwanza: “Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi . . . , mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.” (Mwanzo 1:28) Kwa sababu hawakutii, wanadamu hao wawili walishindwa kuijaza dunia familia zenye uadilifu ambazo zingeitunza kwa upendo dunia na mimea na wanyama walio duniani. Lakini kushindwa kwao hakumaanishi kusudi la Yehova limeshindwa. Maelfu ya miaka baadaye, iliandikwa hivi: “Mungu; ndiye aliyeiumba dunia na kuifanya . . . hakuiumba ukiwa.” “Aliiumba ili ikaliwe na watu.” Haitaharibiwa, bali “dunia hudumu daima.” (Isaya 45:18; Mhubiri 1:4) Kusudi la Yehova kwa dunia litatimizwa: “Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.”—Isaya 46:10.

Kwa hiyo, Mashahidi wa Yehova huamini kwamba dunia itadumu milele na kwamba watu wote, walio hai na wafu, watakaopatana na kusudi la Yehova kwa dunia iliyorembeshwa, yenye kukaliwa wanaweza kuishi milele juu yake. Wanadamu wote walirithi kutokamilika kutoka kwa Adamu na Hawa, na kwa sababu hiyo ni watenda dhambi. (Waroma 5:12) Biblia hutuambia hivi: “Mshahara ambao dhambi hulipa ni kifo.” “Walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote.” “Nafsi inayofanya zambi, itakufa.” (Waroma 6:23; Mhubiri 9:5; Ezekieli 18:4, 20, Zaire Swahili Bible) Basi wanaweza kuishije tena ili washiriki baraka za kidunia? Ni kupitia dhabihu ya ukombozi ya Kristo Yesu tu, maana alisema: “Mimi ndio ufufuo na uhai. Yeye ambaye hudhihirisha imani katika mimi, hata ingawa afa, atakuja kwenye uhai.” “Wote wale waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho watasikia sauti yake na kutoka.”—Yohana 5:28, 29; 11:25; Mathayo 20:28.

Hayo yatatokeaje? Yameelezwa katika “habari njema ya ufalme” ambayo Yesu alianza kutangaza alipokuwa hapa duniani. (Mathayo 4:17-23) Lakini leo Mashahidi wa Yehova wanazihubiri habari njema kwa njia ya pekee sana.

[Chati katika ukurasa wa 13]

WANAYOAMINI MASHAHIDI WA YEHOVA

Imani Sababu ya Kimaandiko

Biblia ni Neno la Mungu 2 Tim. 3:16, 17; 2 Pet.

na ni kweli 1:20, 21; Yn. 17:17

Biblia yategemeka zaidi Mt. 15:3; Kol. 2:8

kuliko mapokeo

Jina la Mungu ni Yehova Zab. 83:18; Isa. 26:4;

42:8, AS; Kut. 6:3

Kristo ni Mwana wa Mungu Mt. 3:17; Yn. 8:42; 14:28; 20:17;

na ni mdogo Kwake 1 Kor. 11:3; 15:28

Kristo alikuwa wa kwanza Kol. 1:15; Ufu. 3:14

wa viumbe wa Mungu

Kristo alikufa mtini, si msalabani Gal. 3:13; Mdo. 5:30

Uhai wa kibinadamu wa Kristo Mt. 20:28; 1 Tim. 2:5, 6;

ulilipwa uwe ukombozi kwa 1 Pet. 2:24

ajili ya wanadamu watiifu

Dhabihu moja ya Rom. 6:10; Ebr. 9:25-28

Kristo ilitosha

Kristo alifufuliwa kutoka kwa 1 Pet. 3:18; Rom. 6:9;

wafu akiwa mtu wa roho Ufu. 1:17, 18

asiyeweza kufa

Kuwapo kwa Kristo ni Yn. 14:19; Mt. 24:3;

katika roho 2 Kor. 5:16; Zab. 110:1, 2

Sasa tumo katika ‘wakati Mt. 24:3-14; 2 Tim. 3:1-5;

wa mwisho’ Luka 17:26-30

Ufalme chini ya Kristo utatawala Isa. 9:6, 7; 11:1-5;

dunia kwa uadilifu na amani Dan. 7:13, 14; Mt. 6:10

Ufalme utaletea dunia hali Zab. 72:1-4; Ufu. 7:9, 10,

bora za kuishi 13-17; 21:3, 4

Dunia haitaharibiwa kamwe Mhu. 1:4; Isa. 45:18;

wala kubaki ukiwa Zab. 78:69

Mungu ataondoa mfumo wa Ufu. 16:14, 16; Sef. 3:8;

mambo wa sasa kwenye Dan. 2:44; Isa. 34:2;

vita ya Har–Magedoni 55:10, 11

Waovu wataharibiwa milele Mt. 25:41-46; 2 The. 1:6-9

Watu ambao Mungu anawakubali Yn. 3:16; 10:27, 28;

watapokea uhai wa milele 17:3; Mk. 10:29, 30

Kuna njia moja tu iendayo Mt. 7:13, 14; Efe. 4:4, 5

kwenye uhai

Wanadamu hufa kwa sababu ya Rom. 5:12; 6:23

dhambi ya Adamu

Nafsi ya mwanadamu haiendelei Eze. 18:4; Mhu. 9:10;

kuishi anapokufa Zab. 6:5; 146:4; Yn. 11:11-14

Helo ni kaburi la ujumla la Ayu. 14:13, Dy;

wanadamu Ufu. 20:13, 14, AV (pambizoni)

Tumaini la wafu ni ufufuo 1 Kor. 15:20-22; Yn. 5:28, 29; 11:25, 26

Kifo kilichotokana na Adamu 1 Kor. 15:26, 54; Ufu. 21:4;

kitakoma Isa. 25:8

Kundi dogo la watu 144,000 Luka 12:32; Ufu. 14:1, 3;

tu ndio watakaoenda mbinguni 1 Kor. 15:40-53; Ufu. 5:9, 10

wakatawale na Kristo

Wale 144,000 wanazaliwa tena 1 Pet. 1:23; Yn. 3:3;

wakiwa wana wa roho wa Mungu Ufu. 7:3, 4

Agano Jipya lilifanywa pamoja Yer. 31:31; Ebr. 8:10-13

na Israeli wa kiroho

Kutaniko la Kristo limejengwa Efe. 2:20; Isa. 28:16;

juu yake mwenyewe Mt. 21:42

Sala zapaswa kupelekwa kwa Yn. 14:6, 13, 14; 1 Tim. 2:5

Yehova tu kupitia Kristo

Mifano haipasi kutumiwa Kut. 20:4, 5; Law. 26:1;

katika ibada 1 Kor. 10:14; Zab. 115:4-8

Uwasiliani-roho lazima uepukwe Kum. 18:10-12;

Gal. 5:19-21; Law. 19:31

Shetani ni mtawala wa ulimwengu 1 Yoh. 5:19; 2 Kor. 4:4;

asiyeonekana Yn. 12:31

Mkristo hapaswi kushiriki katika 2 Kor. 6:14-17; 11:13-15;

harakati zinazochanganya dini Gal. 5:9; Kum. 7:1-5

Ni lazima Mkristo ajitenge na Yak. 4:4; 1 Yoh. 2:15;

ulimwengu Yn. 15:19; 17:16

Tii sheria zote za wanadamu Mt. 22:20, 21;

zisizopingana na sheria 1 Pet. 2:12; 4:15

za Mungu

Kutia damu mwilini kupitia Mwa. 9:3, 4; Law. 17:14;

midomo au mishipa huvunja Mdo. 15:28, 29

sheria za Mungu

Ni lazima kutii sheria za Biblia 1 Kor. 6:9, 10; Ebr. 13:4;

juu ya maadili   1 Tim. 3:2; Mit. 5:1-23

Ni Waisraeli tu walioagizwa Kum. 5:15; Kut. 31:13;

kushika sabato na ilikoma Rom. 10:4; Gal. 4:9, 10;

na Sheria ya Musa Kol. 2:16, 17

Jamii ya makasisi na vyeo vya Mt. 23:8-12; 20:25-27;

kipekee hazifai Ayu. 32:21, 22

Binadamu hakutokea kwa Isa. 45:12; Mwa. 1:27;

mageuzi bali aliumbwa Mt. 19:4

Kristo aliweka mfano ambao 1 Pet. 2:21; Ebr. 10:7;

ni lazima ufuatwe katika Yn. 4:34; 6:38

kumtumikia Mungu

Ubatizo wa kuzamishwa kabisa Mk. 1:9, 10; Yn. 3:23;

huonyesha wakfu Mdo. 19:4, 5

Wakristo hufurahi kutoa ushuhuda Rom. 10:10; Ebr. 13:15;

wa peupe juu ya kweli ya Isa. 43:10-12

Kimaandiko

[Picha katika ukurasa wa 12]

DUNIA . . . iliyoumbwa na Yehova . . . itunzwe na mwanadamu . . . itakaliwa milele

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki