Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rs uku. 88-uku. 91
  • Ibada ya Mababu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ibada ya Mababu
  • Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Ibada ya Mababu Waliokufa Yawapasa Wakristo?
    Amkeni!—1990
  • Wazazi Wetu wa Kale Wako Wapi?
    Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?
  • Kuwasiliana na Pepo
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Ni Nini Hali ya Wafu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
rs uku. 88-uku. 91

Ibada ya Mababu

Maana: Zoea la kuwaheshimu na kuwaabudu mababu waliokufa (kwa kufanya sherehe au kwa njia nyingine) kwa sababu wanaamini kwamba mababu hao wanaishi katika makao yasiyoonekana na wanaweza kuwasaidia au kuwadhuru walio hai na kwa hiyo wanapaswa kutulizwa. Hilo si fundisho la Biblia.

Je, mababu waliokufa wanajua mambo ambayo walio hai wanafanya, na je, mababu hao wanaweza kuwasaidia watu walio hai?

Mhu. 9:5: “Walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajui lolote kamwe.”

Ayu. 14:10, 21: “Mtu wa udongo hukata pumzi, naye yuko wapi? Wanawe hupewa heshima, lakini yeye hajui hilo.”

Zab. 49:10, 17-19: “Hata wenye hekima wanakufa, mjinga na asiyetumia akili huangamia wote pamoja, nao hulazimika kuwaachia wengine mali yao. . . . Anapokufa hawezi kuchukua kitu chochote; utukufu wake hautashuka chini pamoja naye. . . . Nafsi yake mwishowe inafikia tu kwenye kizazi cha mababu zake. Hawataona nuru tena kamwe.”

Je, si kweli kwamba chakula kinachowekwa juu ya madhabahu au juu ya kaburi huwa hakiliwi? Je, hilo halionyeshi kwamba wafu hawawezi kukila?

Ona pia kichwa, “Kuwasiliana na Pepo.”

Je, kuna sababu ya kuogopa kwamba mababu zetu waliokufa watatudhuru?

Mhu. 9:5, 6: “Lakini wafu, . . . upendo wao na chuki yao na wivu wao tayari zimepotea, na mpaka wakati usio na kipimo hawana fungu lolote tena katika chochote ambacho kitafanywa chini ya jua.”

Je, mtu ana roho inayoendelea kuishi baada ya mwili kufa?

Eze. 18:4: “Tazama! Nafsi zote—ni zangu. Kama ilivyo nafsi ya baba ndivyo ilivyo nafsi ya mwana—ni zangu. Nafsi inayotenda dhambi—hiyo yenyewe itakufa.” (Ona pia mstari wa 20.)

Zab. 146:3, 4: “Msiweke tegemeo lenu katika watu wenye vyeo, wala katika mtu wa udongo, . . . Roho yake hutoka, naye hurudi kwenye udongo wake; siku hiyo mawazo yake hupotea.”

Wanasayansi na madaktari wa upasuaji hawajaona uthibitisho wa kuwapo kwa sehemu yoyote ya mwanadamu iliyo na ufahamu na inayoendelea kuishi baada ya mwili kufa.

Ona pia ukurasa wa 102-104, chini ya kichwa, “Kifo.”

Je, wewe ungependa watoto wako na wajukuu wako wakuheshimu na kukupenda wakati ungali hai au wafanye matambiko kwenye kaburi lako ukisha kufa?

Efe. 6:2, 3: “‘Mheshimu baba yako na mama yako’; ambayo ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi: ‘Ili mambo yakuendee vema nawe ukae muda mrefu duniani.’” (Watoto waliofundishwa kanuni za Biblia wanaonyesha heshima hiyo inayofurahisha mioyo ya wazazi wao wakiwa wangali hai.)

Met. 23:22: “Msikilize baba yako aliyekuzaa, wala usimdharau mama yako kwa sababu tu amezeeka.”

1 Tim. 5:4: “Ikiwa mjane yeyote ana watoto au wajukuu, acha hao wajifunze kwanza kuzoea ujitoaji-kimungu nyumbani kwao wenyewe na kuendelea kuwalipa wazazi na wazazi wa wazazi wao malipo yanayowastahili, kwa maana hilo linakubalika machoni pa Mungu.”

Watu wanaowasiliana na pepo wanapodai kuleta ujumbe kutoka kwa wafu, ujumbe huo unatoka wapi hasa?

Isa. 8:19: “Nao wakiwaambia ninyi: ‘Toeni maombi kwa wenye kuwasiliana na pepo au kwa wale wenye roho ya kubashiri wanaonong’oneza na kusema maneno kwa sauti za chini,’ je, kundi lolote la watu halipaswi kutoa maombi kwa Mungu wake? Je, maombi yatolewe kwa watu waliokufa kwa ajili ya watu walio hai?” (Je, Mungu angetuonya tujiepushe na zoea hilo ikiwa kwa kweli linatuwezesha kuwasiliana na wapendwa wetu?)

Mdo. 16:16: “Tulipokuwa tukienda pale mahali pa sala, kijakazi fulani mwenye roho, roho mwovu wa uaguzi, akakutana nasi. Yeye alikuwa akiwapatia mabwana zake faida nyingi kwa kufanya ufundi wa kubashiri.”

Ona pia ukurasa wa 140, 141, chini ya kichwa, “Kuwasiliana na Pepo.”

Ni nani tunayepaswa kumwabudu?

Luka 4:8: “Yesu akajibu akamwambia: ‘Imeandikwa, “Yehova Mungu wako ndiye unayepaswa kumwabudu, na yeye peke yake ndiye unayepaswa kumtolea utumishi mtakatifu.”’”

Yoh. 4:23, 24: “Saa inakuja, nayo ipo sasa, wakati ambapo waabudu wa kweli watamwabudu Baba kwa roho na kweli, kwa maana, kwa kweli, Baba anawatafuta watu wa namna hiyo wamwabudu. Mungu ni Roho, na wale wanaomwabudu lazima wamwabudu kwa roho na kweli.”

Je, kuna tumaini kwamba wakati ujao washiriki wa familia, kutia ndani wale waliokufa, wataungana pamoja?

Yoh. 5:28, 29: “Msistaajabie jambo hili, kwa sababu saa inakuja ambayo wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake na kutoka, wale waliotenda mambo mema kwenye ufufuo wa uzima, wale waliokuwa na zoea la kutenda mambo maovu kwenye ufufuo wa hukumu.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki