Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rs uku. 351-uku. 355
  • Uovu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uovu
  • Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mtu Akisema—
  • Kwa Nini Mungu Ameruusu Uovu Yetu ya Leo?
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Kwa Nini Uovu Unaendelea
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Je! Mungu wa Haki Anajali?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Siku za Ushetani Zimehesabiwa
    Amkeni!—1994
Pata Habari Zaidi
Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
rs uku. 351-uku. 355

Uovu

Maana: Jambo ambalo ni baya sana kiadili. Mara nyingi humaanisha jambo linalodhuru, lenye nia mbovu, au lenye uvutano unaoharibu.

Kwa nini kuna uovu mwingi sana?

Mungu hapaswi kulaumiwa. Aliwapa wanadamu mwanzo mkamilifu, lakini wanadamu wamechagua kupuuza matakwa ya Mungu nao hujiamulia wenyewe yaliyo mema na yaliyo mabaya. (Kum. 32:4, 5; Mhu. 7:29; Mwa. 3:5, 6) Kwa kufanya hivyo, wanatawaliwa na viumbe waovu wenye nguvu kuliko wanadamu.—Efe. 6:11, 12.

1 Yoh. 5:19: “Ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu.”

Ufu. 12:7-12: “Vita vikatokea ghafula mbinguni . . . joka mkubwa na malaika zake wakapigana lakini hakushinda, wala mahali hapakupatikana mbinguni kwa ajili yao tena. Kwa hiyo yule joka mkubwa akatupwa chini, yule nyoka wa zamani, yeye anayeitwa Ibilisi na Shetani, anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa; akatupwa chini duniani, na malaika zake wakatupwa chini pamoja naye. . . . ‘Kwa sababu hiyo furahini, enyi mbingu nanyi mnaokaa ndani yake! Ole wa dunia na wa bahari, kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu, akiwa na hasira kali, akijua kwamba ana kipindi kifupi cha wakati.’” (Kumekuwa na ongezeko la ole duniani tangu Shetani alipotupwa kutoka mbinguni baada ya kuzaliwa kwa Ufalme. Ona mstari wa 10.)

2 Tim. 3:1-5: “Ujue jambo hili, ya kwamba katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo. Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda pesa, wenye kujidai, wenye majivuno, wakufuru, wasiotii wazazi, wasio na shukrani, wasio washikamanifu, wasio na upendo wa asili, wasiotaka makubaliano yoyote, wachongezi, wasiojizuia, wakali, wasiopenda wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi, wanaopenda raha badala ya kumpenda Mungu wakiwa na namna ya ujitoaji-kimungu lakini wakizikana nguvu zake.” (Hayo ndiyo matokeo ya kuiasi ibada ya kweli kwa karne nyingi. Hali hizo zimesitawi kwa sababu watu wanaodai kuwa wafuasi wa dini wamepuuza mambo ambayo kwa kweli Neno la Mungu linasema. Wamekana nguvu zinazoweza kuwachochea kufanya mambo mazuri, nguvu ambazo zinaweza kutokezwa katika maisha ya mtu anapokuwa na ujitoaji-kimungu wa kweli.)

Kwa nini Mungu anauruhusu?

Nyakati fulani huenda tukaona kwamba jambo bora zaidi ni kumwondolea mbali tu kila mtu mwovu. Tunatamani uovu uishe, ingawa umetupata kwa miaka michache tu ikilinganishwa na muda ambao uovu umekuwako. Basi, Yehova Mungu naye anahisije? Kwa maelfu ya miaka watu wamemlaumu, hata kumlaani, kwa sababu ya hali mbaya ambazo zimewapata. Hata hivyo, si yeye anayesababisha hali hizo, bali ni Shetani na watu waovu. Yehova ana nguvu za kuwaangamiza waovu. Bila shaka, lazima kuna sababu nzuri ambazo zimefanya akajizuia. Ikiwa njia ya Yehova ya kushughulikia hali hiyo ni tofauti na njia ambayo sisi tungependekeza, je, hilo litushangaze? Yeye ana uzoefu mkubwa kuliko mwanadamu, na maoni yake kuhusu hali hiyo ni mapana zaidi kuliko ya mwanadamu yeyote.—Linganisha na Isaya 55:8, 9; Ezekieli 33:17.

Hakungekuwa na uovu ikiwa Mungu hangewapa viumbe wenye akili uhuru wa kuchagua. Lakini Mungu ametupa uwezo wa kuchagua kumtii kwa sababu tunampenda, au kuchagua kutomtii. (Kum. 30:19, 20; Yos. 24:15) Je, tunaona kwamba afadhali haingekuwa hivyo? Ikiwa sisi ni wazazi, ni jambo gani linalotufurahisha zaidi—watoto wetu wanapotutii kwa sababu wanatupenda au tunapowalazimisha watutii? Je, Mungu alipaswa kumlazimisha Adamu atii? Je, kweli tungekuwa na furaha zaidi ikiwa tungeishi katika ulimwengu ambamo tunalazimishwa kumtii Mungu? Kabla ya kuuangamiza mfumo huu mbovu, Mungu anawapa watu nafasi ili waonyeshe kama wao kwa kweli wanataka kuishi kupatana na sheria zake za uadilifu au hawataki. Wakati wake utakapofika, bila shaka atawaharibu waovu.—2 The. 1:9, 10.

Anatumia hekima kuruhusu wakati ili masuala muhimu yatatuliwe: (1) Uadilifu na uhalali wa utawala wa Yehova ulipingwa katika Edeni. (Mwa. 2:16, 17; 3:1-5) (2) Utimilifu wa watumishi wote wa Mungu mbinguni na duniani ulitiliwa shaka. (Ayu. 1:6-11; 2:1-5; Luka 22:31) Mungu angewaharibu mara moja wale waasi (Shetani, Adamu, na Hawa), lakini kufanya hivyo hakungetatua mambo. Mtu akiwa na uwezo wa kutumia nguvu, hilo si lazima lithibitishe kwamba mtu huyo ana haki. Masuala yaliyotokezwa yalikuwa ya kiadili. Kwa kuruhusu wakati upite, Mungu hakutaka kujithibitishia jambo lolote, bali alikuwa akiwaruhusu viumbe wote wenye uhuru wa kuchagua wajionee wenyewe matokeo mabaya yanayotokana na kuuasi utawala wake, na pia kuwapa nafasi ya kuonyesha msimamo wao binafsi kuhusiana na masuala hayo muhimu. Baada ya masuala hayo kutatuliwa, hakuna yeyote ambaye ataruhusiwa tena kamwe kuharibu amani. Utaratibu, amani, na hali njema ya ulimwengu mzima hutegemea kutakaswa kwa jina la Yehova, na viumbe wote wenye akili kumtendea kwa heshima inayotoka moyoni. (Ona pia ukurasa wa 272, 273, chini ya kichwa “Shetani Ibilisi.”)

Mfano: Mtu fulani akikushtaki mbele ya watu kwamba wewe unatumia vibaya cheo chako ukiwa kichwa cha familia, kwamba watoto wako wangekuwa na hali bora zaidi ikiwa wangejifanyia maamuzi yao wenyewe bila kukutegemea, na kwamba wote wanakutii kwa sababu ya faida za kimwili unazowapa wala si kwa sababu ya upendo, ungetumia njia gani bora zaidi ili kutatua jambo hilo? Je, kumpiga risasi mwongo huyo anayekushtaki kutawaridhisha watu kwamba mashtaka hayo si ya kweli? Badala yake, lingekuwa jibu bora kama nini ikiwa ungewapa watoto wako nafasi ya kuwa mashahidi wako kuonyesha kwamba wewe ni kichwa cha familia aliye na haki na upendo na kwamba wanaishi pamoja nawe kwa sababu wanakupenda! Ikiwa baadhi ya watoto wako wangemwamini huyo adui yako, waondoke nyumbani, na kuharibu maisha yao kwa kufuata maisha ya aina nyingine, hilo lingewafanya watazamaji wanyoofu wajue tu kwamba watoto hao wangekuwa na hali bora zaidi ikiwa wangetii mwelekezo wako.

Je, sisi tumefaidika kwa njia yoyote kwa sababu ya Mungu kuruhusu uovu mpaka leo?

2 Pet. 3:9: “Yehova hakawii kuhusiana na ahadi yake, kama watu fulani wanavyoona kukawia, bali yeye ni mwenye subira kwenu kwa sababu hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.” (Kwa sababu subira yake imefika mpaka wakati wetu, sisi tuna nafasi ya kuonyesha kwamba tumetubu na kwamba, badala ya kujifanyia maamuzi yetu wenyewe juu ya mema na mabaya, tunataka kujitiisha chini ya utawala mwadilifu wa Yehova.)

Rom. 9:14-24: “Basi, tuseme nini? Je, Mungu ana ukosefu wa haki? Isiwe hivyo kamwe! . . . Basi, ikiwa Mungu, ingawa alikuwa na nia ya kuonyesha ghadhabu yake na kujulisha nguvu zake, alivumilia kwa ustahimilivu mwingi vyombo vya ghadhabu vilivyofanywa kuwa vyenye kufaa kwa ajili ya uharibifu [yaani, alivumilia kuwepo kwa watu waovu kwa muda fulani], ili ajulishe utajiri wa utukufu wake juu ya vyombo vya rehema, alivyotayarisha kimbele kwa ajili ya utukufu [yaani, angetumia muda huo ili kuwaonyesha rehema watu fulani, kupatana na kusudi lake], yaani, sisi, ambao alituita si kutoka kati ya Wayahudi peke yao bali pia kutoka kati ya mataifa, kuna ubaya gani?” (Kwa hiyo Mungu alikawia kuwaharibu waovu ili aruhusu wakati wa kuchagua watu ambao angewatukuza pamoja na Kristo wakiwa washiriki wa Ufalme wa mbinguni. Kwa sababu Mungu amefanya hivyo, je, hilo limekuwa tendo lisilo la haki kwa yeyote? Hapana; ni sehemu ya mpango wa Yehova kwa ajili ya kuwabariki watu wa namna zote watakaopendelewa kuishi milele katika dunia paradiso. Linganisha na Zaburi 37:10, 11.)

Mtu Akisema—

‘Kwa nini Mungu anaruhusu uovu?’

Unaweza kujibu hivi: ‘Swali lako ni zuri. Watumishi wengi waaminifu wa Mungu wamesumbuliwa na uovu unaowazunguka. (Hab. 1:3, 13)’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Si kwa sababu Mungu hajali. Yeye anatuhakikishia kwamba ameweka wakati ambapo atawatoza waovu hesabu. (Hab. 2:3)’ (2) ‘Lakini tunapaswa kufanya nini ili tuwe kati ya waokokaji wakati huo utakapofika? (Hab. 2:4b; Sef. 2:3)’

Au unaweza kusema: ‘Ninafurahi kwa kuwa umeuliza swali hilo. Swali hilo huwasumbua watu wengi wanyoofu. Hapa nina habari nzuri sana ambazo zinajibu swali lako. (Ndipo someni pamoja baadhi ya habari katika ukurasa wa 352-354.)’

‘Baada ya kupita miaka mingi hivi, mimi siamini kwamba Mungu atafanya lolote ili abadili mambo’

Unaweza kujibu hivi: ‘Ninafurahi kusikia kwamba unamwamini Mungu. Ni kweli kwamba kuna uovu mwingi, nao ulianza zamani sana kabla ya wakati wetu. Lakini umepata kufikiria jambo hili . . . ? (Tumia mawazo yaliyo katika fungu la 1 katika ukurasa wa 352, kuhusu urefu wa wakati ambao Mungu amevumilia uovu.)’

Au unaweza kusema: ‘Bila shaka utakubaliana nami ninaposema kwamba yeyote aliye na uwezo wa kujenga nyumba hakika ana uwezo wa kuisafisha pia. . . . Kwa kuwa Mungu aliiumba dunia, halingekuwa jambo gumu kwake kuisafisha. Kwa nini amengojea muda mrefu sana? Niliona jibu hili linaridhisha sana. Niambie maoni yako. (Ndipo someni pamoja habari iliyo katika ukurasa wa 352-354.)’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki