Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 6/15 kur. 281-283
  • Je! Mungu wa Haki Anajali?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Mungu wa Haki Anajali?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MAULIZO HATARINI
  • LAZIMA WANADAMU WATENDE SASA
  • Uovu—Sababu Gani Mungu Anauruhusu?
    Furaha​—Namna ya Kuipata
  • Kwa Nini Mungu Ameruusu Uovu Yetu ya Leo?
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Sababu Gani Mungu Huruhusu Kuteseka?
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Yehova Ni Mpenda-haki
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 6/15 kur. 281-283

Je! Mungu wa Haki Anajali?

KATIKA historia yote wanadamu wametaabika sana. Machozi yametiririshwa kwa uchungu kwa sababu ya kupoteza wapenzi katika kifo. Ugonjwa, uzee, ajali zenye kulemaza na kukosa mahitaji ya maisha vimeleta uchungu mwingi kwa wengi. Zaidi ya haya yote, wanaume, wanawake na watoto wamepatwa na uonezi, udhalimu, uhalifu na jeuri.

Na hali Biblia yasema hivi juu ya Mungu: “Njia zake zote ni haki.” (Kum. 32:4) Je! wewe unaona ugumu kufahamu kwa nini Mungu wa haki angeweza kuachilia uovu kwa karne nyingi? Je! washindwa kujua kama kweli yeye anakujali?

Si wewe peke yako. Hata nyakati za kale watu wanyofu walitatanishwa kwa maana ilielekea kuwa Mungu aliachilia uovu, uonezi na taabu. Walitafuta jibu la kutosheleza kutoka kwa Yehova Mungu, Muumba wao. Mmojawapo wa watu hawa alikuwa nabii wa Kiebrania aliyeitwa Habakuki. Akihuzunikia hali zenye kuogofya, yeye aliuliza hivi: “Ee [Yehova], nilie hata lini, wewe usitake kusikia? Nakulilia kwa sababu ya udhalimu, ila hutaki kuokoa. Mbona wanionyesha uovu, na kunitazamisha ukaidi? Maana uharibifu na udhalimu u mbele yangu; kuna ugomvi, na mashindano yatokea. Kwa sababu hiyo sheria imelegea, wala hukumu haipatikani; kwa maana watu wabaya huwazunguka wenye haki; kwa sababu hiyo hukumu ikipatikana imepotoka.”​—Hab. 1:2-4.

Kwa kujibiwa maulizo yake, nabii Habakuki alipewa njozi iliyomhakikishia kwamba mwishowe Yehova angechukua hatua ya kuondosha uovu. Vile vile Habakuki aliambiwa: “Njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema uongo; ijapokawia, ingojee; kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia.”​—Hab. 2:3.

Hii yatupa matumaini kwamba Yehova Mungu anao “wakati uliowekwa” wa kuchukua hatua. Hata kukielekea kuwapo ‘ukawivu’ kulingana na maoni ya kibinadamu, hii haimaanishi kwamba Mungu hatujali sisi, kwamba ametusahau na kuligeuza kusudi lake. Kwa maana “[Yehova] hupenda haki, . . . hawaachi watauwa wake.” (Zab. 37:28) Neno lake la unabii kutia na ahadi yake kumaliza udhalimu, uonezi na maumivu, linaelekea kasi kwa shauku kwenye utimizo wake. (Ufu. 21:3, 4) Kwa hiyo faraja kutoka katika taratibu ya mambo iliyopo bila shaka itakuja.

Kwa sababu ya muda wetu mfupi wa maisha, sisi wanadamu tungeipenda sana faraja hiyo sasa. Huenda tukafikiri kesho yaweza kuwa ni kuchelewa mno kuanza kuzifurahia faida zitakazotokana na kukoma kwa uovu, maradhi, huzuni na taabu. Kwa hiyo, huenda tukaelekea kuwa wasio na subira, kuona kwamba Mungu ni mkawivu, kuona kwamba yeye ‘anakawia’ katika kuileta faraja iliyotabiriwa.

Lakini, Yehova Mungu hawekewi mipaka na wakati. Yeye ni Mungu “tangu milele hata milele” (Zab. 90:2) “Kwa [Yehova] siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja.” (2 Pet. 3:8) Tofauti na wanadamu wenye maisha mafupi wasioweza kuahirisha mipango yao ikiwa lazima itimilizwe, Yehova Mungu aweza kungojea mpaka mambo katika kipindi cha wakati yamekuwa sawasawa kwa utimizo wa faida bora ziwezazo kutokea.

MAULIZO HATARINI

Akiwa mwenye nguvu zote, Yehova Mungu angaliweza kuwaharibu waovu karne nyingi zilizopita. Lakini kwa kweli hii isingekuwa ni kwa faida bora za mwanadamu. Kwa nini sivyo? Zaidi ni kwa sababu ya maulizo yaliyotokezwa muda mfupi Yehova Mungu alipokwisha kuwaweka wanadamu wawili wa kwanza, Adamu na Hawa, katika makao mazuri ya paradiso.

Aliyeyatokeza maulizo haya alikuwa kiumbe kisichoonekana cha kiroho, aliyeitwa nyumaye “Ibilisi” na “Shetani.” Akitumia nyoka, Ibilisi alidai kwamba kutii sheria ya kimungu kusingeelekeza kwenye mauti kama Mungu alivyokuwa amesema bali kungetokeza faida. (Mwa. 3:4, 5) Dai hili lilitilia mashaka kama kweli matumizi ya Mungu ya utawala juu ya viumbe vyake yalikuwa kwa faida zao bora.

Uhakika wa kwamba Adamu na Hawa walimwunga Shetani katika mwendo wa kutokutii ulitokeza ulizo jingine: Je! viumbe vingine vyote vyenye akili vingekuwa visivyoaminika kwa Mungu wakati ambapo utii usingeleta faida yo yote iliyotazamiwa? Dai la Shetani, lililofanywa nyumaye kwa habari ya Ayubu mwaminifu lilionyesha kwamba​—vikihasirika​—vingeacha kumtumikia Mungu. Shetani alisema: “Ngozi kwa ngozi, naam, yote aliyo nayo mtu atayatoa kwa ajili ya uhai wake. Lakini sasa nyosha mkono wako, uuguse mfupa wake na nyama yake, naye atakukufuru mbele za uso wako.”​—Ayubu 2:4, 5.

Kama Shetani angeharibiwa mara hiyo maulizo haya yaliyotokezwa yasingemalizwa. Wakati ulihitajiwa kuhakikisha kwamba unyenyekevu kwa utawala wa Mungu ni haki na kwa faida bora za uumbaji wote wenye akili. Na wakati ulihitajiwa kuhakikisha kwamba Shetani alikosea kwa kushikilia kauli ya kwamba wote waliomtumikia Mungu walifanya hivyo kwa sababu za kichoyo tu.

Mashtaka yaliyofanywa juu ya Mungu na viumbe vyake vyenye akili huenda yakafananishwa kwa njia ya kibinadamu. Tuseme baba wa jamaa kubwa anachongewa na mmojawapo wa jirani zake. Jirani yule adai kwamba baba hazifikirii faida bora za jamaa naye ni mkali bure tu na mwonezi. Kwa habari ya washiriki wa jamaa, jirani anashikilia kauli ya kwamba hakuna ye yote kati yao ampendaye baba bali wao wakaa nyumbani kwa sababu anawapa chakula na mahitaji mengine.

Baba awezaje kuukanusha uongo? Akiwa mwenye nguvu vya kutosha, aweza kutumia nguvu na kumpiga sana jirani yake, akimlazimisha jirani yake kuyatangua maneno yake ya uchongezi. Lakini je! kweli hii ingelimaliza shauri lile? Je! ingewasadikisha wengine? Je! watazamaji hawatakata maneno kwamba huenda mashtaka yakawa ni kweli kwa sababu baba amejaribu kuyafutilia mbali kwa njia ya jeuri? Kwa hiyo, basi, je! isingekuwa bora kwa baba kuiacha jamaa yake mwenyewe itumikie kama mashahidi juu ya mashtaka ya uongo? Sawasawa! Maneno yao na matendo kwa kipindi cha wakati yangeweza kuonyesha wengine kwamba wao kweli wanampenda baba yao na waliona ubora wa namna alivyoutumia ukichwa wake kwa njia nzuri.

Hivi ndivyo Yehova Mungu alivyofanya. Kwa kuwaacha watu waovu waendelee kuishi kwa muda, amefanya iwezekane kwa wengine kushiriki katika kulikanusha dai la Shetani kwa kuendelea kuwa waaminifu, hata wakiwa chini ya hali zisizofaa na zenye kujaribu. Hii imekuwa ni kupatana na kanuni inayopatikana katika Mithali 27:11: “Mwanangu, uwe na hekima na kunifurahisha moyo wangu; ili nipate kumjibu anilaumuye.”

Kujizuia kwa Mungu asiwaue waovu mara moja vile vile kumewapa watu mmoja mmoja nafasi yenye rehema wageuze njia zao na kuwa watumishi wake watiifu. Ni kama vile mtume Petro alivyowaambia Wakristo wenzake: “[Yehova] hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.” (2 Pet. 3:9) Lo! huu ni ushuhuda mzuri namna gani wa ambavyo Yehova anavyowajali wanadamu! Yeye anataka watu waingie katika hali itakayomaanisha wokovu kwao, naye anawapa wakati wa kufanya hivyo. Kisha, anapotenda, hakuna awezaye kudai kwa haki kwamba Mungu alikuwa dhalimu kwa kutowapa wanadamu wakati wa kutosha wageuke.

Zaidi ya hayo, ushuhuda utakuwa usioweza kukanwa kwamba utawala wa Mungu ni haki na kwamba mamilioni ya viumbe vyake mbinguni na duniani watamtumikia yeye kwa nia safi, kwa sababu ya kumpenda yeye. Ye yote atakayeupinga unyofu, haki na ustahili wa enzi yake nyuma ya hapo hatavumiliwa. Hakutakuwako haja ya kuruhusu wakati kwa wapinzani hao wajaribu kuihakikisha kauli watakayoshikilia, kwa njia hiyo wakiiharibu amani na umoja wa jamaa ya ulimwengu wote ya Mungu. (Linganisha Ufunuo 20:7-9.) Hivyo kuruhusu kwa Mungu wakati wa kutosha ili maulizo yaliyotokezwa na Shetani yapate kumalizwa kutatokeza faida iliyo kuu zaidi kwa wanadamu watiifu. Kumalizwa kwa maulizo haya kwahakikisha kwamba hakuna mtu awaye yote atakayepaswa kuvumilia udhalimu tena, taabu au uonezi kwa ajili ya wale wasiopenda haki.

LAZIMA WANADAMU WATENDE SASA

Zaidi ni jambo la haraka leo tuziitikie fadhili zisizostahiliwa za Yehova Mungu kwa kuwapa wanadamu nafasi ya kuwa watumishi wake waliokubalika. Ushuhuda wa tarehe ya Biblia na unabii wa Biblia bila ya kukosea waelekeza kwenye kizazi kiki hiki kama kile kitakachoushuhudia “wakati uliowekwa” wa kuondolewa kwa hii taratibu mbovu. (Mt. 24:34; 2 Tim. 3:1-5) Mungu wa haki hakuwaacha wanadamu bila ya kuwapa onyo lifaalo juu yake. Katika zaidi ya nchi 200 mashahidi wake wa Kikristo wanautangaza kwa bidii uharibifu wa taratibu mbovu iliyopo na kuletwa haraka kwa taratibu mpya yenye haki. “Tunatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake.” (2 Pet. 3:13) Hii yamaanisha kwamba ufalme wa Mungu kwa njia ya Yesu Kristo utatawala kama “mbingu mpya” juu ya “nchi mpya” ya raia waliojitoa.

Ikiwa wewe watamani kuwamo kati ya raia waaminifu wa ufalme wa Mungu, litii shauri lililoongozwa na roho ya Mungu: “Fanyeni bidii ili mwonekane katika amani kuwa hamna mawaa wala aibu mbele yake.” (2 Pet. 3:14) Ili mtu aweze kupatikana katika hali hiyo, lazima ajue na kutenda kupatana na matakwa ya Yehova Mungu ya uzima kama yalivyoandikwa katika Neno lake Biblia Takatifu. Mashahidi wa Yehova katika eneo lako watafurahi kukusaidia uupate ujuzi huu wa muhimu wa Biblia. Wakati ule mwingine watakapokutembelea wewe, waulize juu ya mpango wao wa funzo la nyumbani la Biblia la bure la kila juma. Au, uwaandikie wachapaji wa gazeti hili nasi tutapanga kwa furaha mtu fulani akutembelee.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki