Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • dg seh. ya 11 kur. 28-32
  • Msingi wa Ulimwengu Mpya Sasa Unafanyizwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msingi wa Ulimwengu Mpya Sasa Unafanyizwa
  • Je, Kweli Mungu Anatujali?
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Udugu wa Kimataifa Ulio wa Kweli
  • Kutambua Watu wa Mungu
  • Jambo Jingine la Kutambulisha
  • Kujibu Suala Kuu la Pili
  • Chaguo Lako Ni Nini?
  • Udugu wa Duniani Pote Ni Hakika!
    Amkeni!—1991
  • “Taifa Hodari” la Mungu Lenye Umoja Kujaza Dunia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Mashahidi wa Yehova
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Kumrudia Mungu wa Kweli
    Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu
Pata Habari Zaidi
Je, Kweli Mungu Anatujali?
dg seh. ya 11 kur. 28-32

Sehemu ya 11

Msingi wa Ulimwengu Mpya Sasa Unafanyizwa

1, 2. Katika kutimiza unabii wa Biblia, ni nini kinachotukia mbele tu ya macho yetu?

JAMBO lililo zuri ajabu pia ni uhakika wa kwamba msingi wa ulimwengu mpya wa Mungu unafanyizwa sasa hivi, huku ulimwengu wa kale wa Shetani ukizidi kuharibika. Mbele tu ya macho yetu, Mungu anakusanya watu kutoka mataifa yote na kuwatumia kufanyiza msingi wa jamii mpya ya kidunia ambayo karibuni utakuwa badala ya ulimwengu wa leo uliogawanyika. Katika Biblia, kwenye 2 Petro 3:13, NW, jamii hii mpya huitwa “dunia mpya.”

2 Unabii wa Biblia husema pia: “Katika siku za mwisho [wakati tunamoishi sasa] . . . , mataifa wengi watakwenda na kusema, Njoni, twende juu mlimani kwa BWANA [Yehova, NW] [ibada yake ya kweli], . . . naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake.”—Isaya 2:2, 3.

3. (a) Unabii wa Isaya unatimizwa miongoni mwa nani? (b) Kitabu cha mwisho cha Biblia kinatoa maelezo gani juu ya hilo?

3 Unabii huo sasa unatimizwa miongoni mwa wale wanaotii ‘njia za Mungu na kwenda katika mapito yake.’ Kitabu cha mwisho cha Biblia husema juu ya jamii hii ya kimataifa ya watu wenye kupenda amani kuwa ni “mkutano mkubwa . . . watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha,” udugu wa tufe lote ulio wa kweli wenye kumtumikia Mungu kwa umoja. Na Biblia husema pia: “Hao ndio wanatoka katika dhiki ile iliyo kuu.” Yaani, wataokoka mwisho wa huu mfumo mwovu wa mambo.—Ufunuo 7:9, 14; Mathayo 24:3.

Udugu wa Kimataifa Ulio wa Kweli

4, 5. Kwa nini udugu wa ulimwenguni pote wa Mashahidi wa Yehova unawezekana?

4 Mamilioni ya Mashahidi wa Yehova hujaribu kwa weupe wa moyo kuishi kupatana na maagizo na njia za Mungu. Tumaini lao la uhai wa milele limekazwa katika ulimwengu mpya wa Mungu. Kwa kuendesha maisha zao kila siku kwa kutii sheria za Mungu, wao humwonyesha nia yao ya kutii njia zake za kutawala sasa na katika ulimwengu mpya pia. Kila mahali, bila kujali taifa au jamii yao, wao hutii viwango vilevile vilivyowekwa na Mungu katika Neno lake. Ndiyo sababu wao ni udugu wa kweli wa kimataifa, jamii mpya ya ulimwengu yenye kufanyizwa na Mungu.—Isaya 54:13; Mathayo 22:37, 38; Yohana 15:9, 14.

5 Mashahidi wa Yehova hawajifikirii wenyewe kuwa ndio wenye kusababisha udugu wao wa tufe lote usio na kifani. Wao wajua kwamba hilo ni tokeo la roho ya Mungu yenye nguvu ikitenda kazi juu ya watu ambao hutii sheria zake. (Matendo 5:29, 32; Wagalatia 5:22, 23) Ni kazi ya Mungu. Kama alivyosema Yesu, “yasiyowezekana kwa wanadamu yawezekana kwa Mungu.” (Luka 18:27) Basi yule Mungu aliyewezesha kuwe na ulimwengu wote mzima udumuo ndiye ambaye pia hufanya iwezekane kuwe na jamii ya ulimwengu mpya idumuo.

6. Kwa nini udugu wa Mashahidi wa Yehova waweza kuitwa mwujiza wa ki-siku-hizi?

6 Hivyo, njia ya Yehova ya kutawala katika ulimwengu mpya yaweza tayari kuonwa katika kile anachotokeza katika msingi wa ulimwengu mpya ambao unafanyizwa sasa. Na yale ambayo yeye amefanya na Mashahidi wake, katika maana fulani, ni mwujiza wa ki-siku-hizi. Kwa sababu yeye amejenga Mashahidi wa Yehova kuwa udugu wa kweli wa ulimwenguni pote, ambao hauwezi kuvunjwa kamwe na mapendezi yenye kugawanya ya kitaifa, kijamii, au kidini. Ingawa idadi ya Mashahidi ni mamilioni na wanaishi katika nchi zaidi ya 200, wao wamefungwa pamoja kama mtu mmoja katika kifungo kisichokatika. Udugu huu wa ulimwenguni pote usio na kifani katika historia yote, ni mwujiza kweli kweli wa ki-siku-hizi—kazi ya Mungu.—Isaya 43:10, 11, 21; Matendo 10:34, 35; Wagalatia 3:28.

Kutambua Watu wa Mungu

7. Yesu alisema wafuasi wake wa kweli wangetambuliwaje?

7 Inaweza kujulikanaje zaidi ni watu gani ambao Mungu anatumia wakiwa msingi kwa ajili ya ulimwengu wake mpya? Basi, ni nani ambao hutimiza maneno ya Yesu kwenye Yohana 13:34, 35? Yeye alitaarifu hivi: “Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.” Mashahidi wa Yehova huamini maneno hayo ya Yesu na kutenda kupatana nayo. Kama Neno la Mungu liagizavyo, wao ‘wana juhudi nyingi katika kupendana.’ (1 Petro 4:8) Wao ‘hujivika upendo, maana ndio kifungo cha ukamilifu.’ (Wakolosai 3:14) Hivyo upendo wa kidugu ndio “gundi” ambayo huwashikamanisha pamoja ulimwenguni pote.

8. Andiko la 1 Yohana 3:10-12 hutambulishaje zaidi watu wa Mungu?

8 Pia, 1 Yohana 3:10-12 husema: “Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake. Maana, hii ndiyo habari mliyoisikia tangu mwanzo, kwamba tupendane sisi kwa sisi; si kama Kaini alivyokuwa wa yule mwovu, akamwua ndugu yake. Naye alimwua kwa sababu gani? Kwa sababu matendo yake yalikuwa mabaya, na ya ndugu yake yalikuwa ya haki.” Hivyo, watu wa Mungu ni udugu usio na jeuri, wa tufeni pote.

Jambo Jingine la Kutambulisha

9, 10. (a) Watumishi wa Mungu wangetambuliwa kwa kazi gani katika siku za mwisho? (b) Mashahidi wa Yehova wametimizaje Mathayo 24:14?

9 Kuna njia nyingine ya kuwatambua watumishi wa Mungu. Katika unabii wake juu ya mwisho wa ulimwengu, Yesu alitabiri mambo mengi ambayo yangeonyesha kipindi hiki cha wakati kuwa siku za mwisho. (Ona Sehemu ya 9.) Sehemu ya msingi ya unabii huo inatajwa katika maneno yake kwenye Mathayo 24:14, NW: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa kwa ajili ya ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakuja.”

10 Je! wewe umeona unabii huo ukitimizwa? Ndiyo. Kwa kuwa tangu zilipoanza siku za mwisho katika mwaka 1914, Mashahidi wa Yehova wamehubiri habari njema za Ufalme wa Mungu kotekote ulimwenguni kwa namna ile ambayo Yesu aliagiza, yaani, kwenye nyumba za watu. (Mathayo 10:7, 12; Matendo 20:20) Mamilioni ya Mashahidi hutembelea watu katika kila taifa ili kuongea nao juu ya ulimwengu mpya. Hilo limeongoza katika wewe kupokea broshua hii, kwani kazi ya Mashahidi wa Yehova hutia ndani kuchapa na kugawanya mabilioni ya vipande vya fasihi juu ya Ufalme wa Mungu. Je! wewe wamjua mtu yeyote mwingine ambaye huhubiri juu ya Ufalme wa Mungu nyumba kwa nyumba kotekote ulimwenguni? Na Marko 13:10 huonyesha kwamba kazi hii ya kuhubiri na kufundisha lazima ifanywe “kwanza,” kabla ya mwisho kuja.

Kujibu Suala Kuu la Pili

11. Ni jambo gani jingine wanalotimiza Mashahidi wa Yehova kwa kujitiisha chini ya utawala wa Mungu?

11 Kwa kutii sheria na kanuni za Mungu, Mashahidi wa Yehova hutimiza jambo jingine. Wao huonyesha kwamba Shetani alikuwa mwongo wakati alipodai kwamba wanadamu hawangeweza kuwa waaminifu kwa Mungu chini ya jaribu, hivyo wakijibu suala kuu la pili lihusulo uaminifu-maadili wa kibinadamu. (Ayubu 2:1-5) Wakiwa jamii ya mamilioni ya watu kutoka mataifa yote, Mashahidi huonyesha, wakiwa jamii moja, uaminifu-mshikamanifu kwa utawala wa Mungu. Ijapokuwa wao ni wanadamu wasiokamilika, wao hutegemeza upande wa Mungu wa lile suala la enzi kuu ya ulimwengu wote mzima, ujapokuwa msongo wa kishetani.

12. Kwa imani yao, Mashahidi wa Yehova huiga nani?

12 Leo, mamilioni haya ya Mashahidi wa Yehova wanaongeza ushuhuda wao kwa ule wa mstari mrefu wa mashahidi wengine katika nyakati zilizopita ambao walionyesha uaminifu-mshikamanifu kwa Mungu. Baadhi yao walikuwa Abeli, Noa, Yobu, Abrahamu, Sara, Isaka, Yakobo, Debora, Ruthi, Daudi, na Danieli, kutaja wachache tu. (Waebrania, sura ya 11) Kama vile Biblia husema, wao ni ‘wingu kubwa la mashahidi waaminifu.’ (Waebrania 12:1) Hao, na wengine kutia wanafunzi wa Yesu walidumisha uaminifu-maadili kwa Mungu. Na Yesu mwenyewe aliandaa mfano mkuu zaidi wa kudumisha uaminifu-maadili mkamilifu.

13. Ni maneno gani ya Yesu juu ya Shetani ambayo yamethibitika kuwa kweli?

13 Hiyo huonyesha kwamba yale ambayo Yesu aliwaambia viongozi wa kidini juu ya Shetani ni kweli: “Lakini sasa mnatafuta kuniua mimi, mtu ambaye nimewaambia iliyo kweli, niliyosikia kwa Mungu. . . . Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake.”—Yohana 8:40, 44.

Chaguo Lako Ni Nini?

14. Ni nini kinachotukia kwa msingi wa ulimwengu mpya leo?

14 Msingi wa ulimwengu mpya unaofanyizwa sasa na Mungu katika jamii ya kimataifa ya Mashahidi wa Yehova unazidi kuwa wenye nguvu. Kila mwaka mamia ya maelfu ya watu wanatumia hiari yao, yenye msingi wa maarifa sahihi, kukubali utawala wa Mungu. Wanakuwa sehemu ya hiyo jamii mpya ya ulimwengu, wanategemeza upande wa Mungu wa lile suala la enzi kuu ya ulimwengu wote mzima, na kuthibitisha Shetani kuwa mwongo.

15. Ni kazi gani ya kutenganisha anayotimiza Yesu katika siku zetu?

15 Kwa kuchagua utawala wa Mungu, wao hustahili kuwekwa ‘mkono wa kuume’ wa Kristo huku abaguapo (atenganishapo) “kondoo” na “mbuzi.” Katika unabii wake juu ya siku za mwisho, Yesu alitabiri hivi: “Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake; na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi; atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto.” Kondoo ni watu wanyenyekevu ambao hushirikiana na kuunga mkono ndugu za Kristo, wakijitiisha kwa utawala wa Mungu. Mbuzi ni watu wenye shingo ngumu ambao hukatalia mbali ndugu za Kristo na hawafanyi lolote kuunga mkono utawala wa Mungu. Kwa matokeo gani? Yesu alisema: “Hao [mbuzi] watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki [kondoo] watakwenda katika uzima wa milele.”—Mathayo 25:31-46.

16. Ni lazima ufanye nini ikiwa wataka kuishi katika Paradiso inayokuja?

16 Kweli kweli, Mungu atujali sisi! Karibuni sana yeye ataandaa paradiso ya kidunia yenye kupendeza. Je! wewe wataka kuishi katika Paradiso hiyo? Ikiwa ndivyo, onyesha uthamini wako kwa maandilizi ya Yehova kwa kujifunza juu yake na kutenda juu ya yale unayojifunza. “Mtafuteni BWANA [Yehova, NW], maadamu anapatikana, mwiteni, maadamu yu karibu; mtu mbaya na aache njia yake, na mtu asiye haki aache mawazo yake; na amrudie BWANA [Yehova, NW], naye atamrehemu; na arejee kwa Mungu wetu, naye atamsamehe kabisa.”—Isaya 55:6, 7.

17. Kwa nini hakuna wakati wa kupoteza katika kuchagua ni nani wa kutumikia?

17 Hakuna wakati wa kupoteza. Mwisho wa mfumo huu wa kale u karibu sana. Neno la Mungu hushauri: “Msiwe mkipenda wala ulimwengu wala vitu katika ulimwengu. Ikiwa mtu ye yote anapenda ulimwengu, upendo wa Baba haumo katika yeye. . . . Zaidi, ulimwengu unapitilia mbali na ndivyo na tamaa yao, lakini yeye ambaye hufanya mapenzi ya Mungu hubaki milele.”—1 Yohana 2:15-17, NW.

18. Ni mwendo gani wa tendo utakuwezesha kutazamia kwa uhakika kuishi katika ulimwengu mpya wa Mungu ulio mzuri ajabu?

18 Watu wa Mungu wanazoezwa sasa kwa ajili ya uhai wa milele katika ulimwengu mpya. Wanajifunza stadi za kiroho na nyinginezo zinazohitajiwa ili kusitawisha paradiso. Sisi twakuhimiza uchague Mungu kuwa Mtawala na kuunga mkono kazi ya kuokoa uhai anayofanyiza kotekote duniani leo. Jifunze Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova, upate kujua Mungu ambaye anakujali wewe kweli kweli na ambaye ataleta mwisho wa kuteseka. Kwa njia hiyo wewe pia waweza kuwa sehemu ya msingi wa ulimwengu mpya. Ndipo unapoweza kutazamia kwa uhakika kupata kibali cha Mungu na kuishi milele katika huo ulimwengu mpya mzuri ajabu.

[Picha katika ukurasa wa 31]

Mashahidi wa Yehova wana udugu wa kimataifa ulio wa kweli

[Picha katika ukurasa wa 32]

Msingi wa ulimwengu mpya wa Mungu sasa unafanyizwa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki